Mohamed Said, huu ni mchango wangu wa mwisho katika santuri hii yako ambayo imechuja lakini bado wapo watu wanaomeza tu ngano zako bila takafuri yoyote.
Wakati wote unapodai unaandika historia ya Waislaam ukweli ni kuwa unaandika historia ya wazee wako, Wazulu na Wamanyema.
Unapodai unaandika historia ya Watanganyika ukweli ni kuwa unaandika historia ya wazazi wako na babu zako,Wamanyema na Wazulu.
Kwa kukufahamisha Watanganyika walikuwepo sana tu ingawa huwapi kipaumbele stahiki katika hizi ngano zako.
Huwezi kuongelea AA bila kumtaja muasisi na Kiongozi wake Mkuu wakati inaanzishwa mwaka 1929 na huyo si mwingine bali Mtanganyika Myao na Msomi Hayati Mwalimu Cecil Matola.
Baada ya Matola kufariki, AA ilikosa uongozi madhubuti hali iliyoifanya AA kuwa kama chombo kilichokosa dira hadi Zanzibar ilipojitoa mwaka 1948 na kuzaliwa TAA.
Lakini hata ilipozaliwa TAA, uongozi thabiti ulikuja kupatikana mwaka 1950, Mtanganyika Mhaya Dr. Vedasto Kyaruzi alipochaguliwa kuwa Raisi wake wa kwanza.
Baada ya Wakoloni kumpa uhamisho wa nguvu Raisi wa TAA, shughuli za TAA zilizorota kwa sababu kiongozi mkuu hakuwepo.
Kumbuka kwamba Dr. Kyaruzi alipopewa uhamisho wa kwanza hakupelekwa mbali na hivyo aliweza kuendelea kuwasiliana na wasaidizi wake mojawapo akiwa Abduwahid Sykes.
Wakoloni walipogundua hilo ilibidi wamhamishe tena wampeleke mbali zaidi ili mawasiliano na wasaidizi wake yawe magumu zaidi na hivyo kupelekea TAA kuzorota hadi ujio wa Mwalimu Nyerere mwaka 1952.
Hivyo nafasi ya Abdulwahid Sykes ndani ya TAA wakati Mwalimu Nyerere yuko Makerere ni kwamba wakati huo TAA haikuwapo, ilikuwepo AA iliyoasisiwa na Cecil Matola mwaka 1929.
Huyu Abdulwahid Sykes unamtajataja sana na bila shaka kwa sababu unazozijua wewe mwenyewe lakini ukweli ni kwamba hakuwahi kuwa kiongozi Mkuu wa TAA wala TANU wakati wowote ule.
Dai la kuwa ndiye alipendekeza jina la TANU ni kweli kwa kiasi Fulani kwani alichofanya ni kwamba jina alilopendekeza awali Mwalimu Nyerere lilikuwa gumu kidogo kutamkwa kwa haraka ingawa maneno yalikuwa yale yale.
Mwalimu Nyerere alitaka maneno manne yasikosekane nayo ni
AFRICAN, TANGANYIKA, NATIONAL na
UNION yawepo na iliyobakia ni namna tu ya kuyapanga na ndipo Abdulwahid Sykes kupendekeza
Tanganyika African National Union (TANU)