Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Nani kakataa uwepo wa hao watu na siasa zao? AA na TAA zilikuwepo nini cha kubisha hapo. Watu unaowataja walikuwepo, nini cha kubisha hapo?

Kinachogomba ni kuwa unarudia makosa unayosema unayasahihisha.

Sijawahi kusoma wala kutilia maanani historia ya Kivukoni! Hilo tu linasababisha nijielimishe mwenyewe kuliko kusubiri hotuba , tamthilia, ngano au hekaya za wananchi wengine

Mohamed, kupitia kavazi la Mwalimu Nyerere na kavazi la Kleist hadi Abdul, unaweza kutuonyesha katiba za AA au TAA. Hili naliluliza kwenu mabingwa, nimekwama nisaidie
Nguruvi 3,
Hijasoma kitabu cha Kivukoni kuhusu historia ya TANU lakini umesoma kitabu cha Mohamed Said na unafanya mjadala wa historia ya TANU kwa miaka 9.
 
Laki...
Haya umeyapata wapi?
Unaweza kuweka hapa kama ushahidi?
mkuu, wewe si umetueleza Nyerere alipewa chumba cha kuishi nyumbani kwa akina Sykes? Wewe si ndio umetueleza kila siku mama Daisy alikuwa anampelekea chakula Mama Maria na watoto wake kwenye kiduka chake cha kuuza mafuta ya taa? hizi habari zote nimezipata kutoka kwako
 
Unajitahidi! ningeshauri uendelee kusoma ...
Nguruvi,

Hapo chini ni moja ya Nyaraka za Sykes ambazo sasa zinahifadhiwa katika Kavazi la Mwalimu Nyerere.

Kavazi limeeleza hii nyaraka wamepata kutoka kwangu nami nikawaandikia kuwafahamisha kuwa nyaraka zote nilizowapa mimi nimezipata kutoka kwa wenyewe.

 
Nguruvi,

Hapo chini ni moja ya Nyaraka za Sykes ambazo sasa zinahifadhiwa katika Kavazi la Mwalimu Nyerere.

Kavazi limeeleza hii nyaraka wamepata kutoka kwangu nami nikawaandikia kuwafahamisha kuwa nyaraka zote nilizowapa mimi nimezipata kutoka kwa wenyewe.

 
umesahau ulishatuletea kisa cha Nyerere kwenda sokoni kuhemea chakula cha watoto wake wakati mfukoni hana hata senti tano?
 
umesahau ulishatuletea kisa cha Nyerere kwenda sokoni kuhemea chakula cha watoto wake wakati mfukoni hana hata senti tano?
Laki...
Rejea kusoma upya ukiwa umetulia ukimaliza nifahamishe nikuletee historia nzuri kushinda hiyo.
 
Tafadhali nakuomba tuandikie vitabu maana kuna mengi yanatufungua fahamu ambayo umefanya juhudi kutafiti na kutuletea


Tukubali kwamba kama Waafrika na Watanzania tuna haki ya kuandika historia yetu.

Tumepotoshwa sana
Mag 3,
Ninachokushindia ni kuwa mwenzangu ghadhabu zimekujaa sana katika historia hii ungependa sana tubaki na ile ''official history,'' iliyowafuta wazee wangu.

Hii ndiyo sababu ghadhabu zako unazielekeza kwangu kwa maneno makali ya ''ngano,'' ''uongo,'' na lugha za kejeli kama ''ngumi na ''mateke,'' nk.

Mimi sitakuita muongo kwa haya uliyosema kuhusu Nyerere.
Nachukulia kuwa historia ya Nyerere huijui kwa kuwa hujaitafiti kama nilivyofanya mimi.

Nyerere hakuwa kiongozi wa TAA Tabora 1945.

Tarehe 3 Machi, 1945 African Association mjini Tabora ilifungua ofisi yake ikiwa na na viongozi wafuatao: Hamisi Simbe (Rais), Ramadhani Nasibu (Makamu wa Rais), M. K. Hemed (Katibu), Chamng'anda Usingizi (Mwenyekiti), Fimbo Mtwana (Mweka Hazina) na Rashidi Mussa (Mkaguzi wa Hesabu).

Unaliona jina la Nyerere hapo?

Julius Nyerere, wakati huo akifundisha St. Mary's School, alishuhudia sherehe za uzinduzi wa African Association.

Mwaka 1946 wasomi wa Makerere ndipo walianza kujishughulisha na African Association pale Hamza Mwapachu na Julius Nyerere walipochaguliwa Katibu na Katibu Msaidizi.

Baada ya uhamisho wa Mwapachu kutoka Tabora, Nyerere akashika nafasi yake na kuwa Katibu.

Angalia rejea hizi: Barua ya M.K. Hemed kwa Secretary, African Association, Dar es Salaam, 11 th January 1945, TAA Tabora Party Archives File 741. Angalia Iliffe, A Modern History of Tanganyika, uk 430-431.

Angalia pia E. A. M. Mang'enya, Discipline and Tears, Dar es Salaam University Press, 1984, uk. 173.

Haya niliyokueleza na rejea hizi naamini zinatosha kukufahamisha kuwa historia hii mimi naijua vizuri sana wala sibahatishi kwa hiyo hayo mengine wala sina haja ya kuyasemea kwa kuwa hayana maana.

Nakuuliza kati yetu mimi na wewe nani mwandishi wa ngano na nani anaeandika kwa ushahidi?
 
Mzee wetu Mohamed Said najua wengi wetu tuna kasumba ya kumpinga mjumbe badala ya ujumbe,wengi tunafikiri kwamba kwa sababu hatukubaliani na mjumbe basi tunaweza kutumia kigezo hicho hicho kukataa ujumbe,jambo ambalo si kweli.

Ujumbe wako naamini uko wazi kwamba kuna mengi tunapaswa kuyafahamu kuhusu historia ya nchi yetu sio kwa sababu ya ubaya ila ni kwa faida ya nchi yetu na vizazi vijavyo.

Najua kwamba historia yetu rasmi inaweza kuwa inakosa baadhi ya madini ambayo wewe unatuambia kwamba umeyafanyia utafiti na yenye vielelezo thatbiti.

Najua pia kwamba sio jambo rahisi kubadili historia rasmi hasa ukilinganisha kwamba mengi ya mambo uliyonayo kimsingi yanaonekana kuwa (errors of omission)mfano kutowataja kwa majina wahusika katika hao wazee wa Dar es Salaam) au kutokuelezea kwa kina mchango wao katika historia ya nchi yetu.

BInafsi nafikiri sasa ni wakati wa wanazuoni kama wewe na wengine wengi kuandika kuhusu historia katika mtazamo tofauti.Cha msingi ni kuhakikisha kwamba katika kufanya utafiti wako usiatafute kuichalenge official historia ispokuwa tu pale ambapo kuna reliable facts ambazo zinaweza kusaidia zaidi watu kuelewa historia yetu bila kuwa upotoshaji,uongo au chuki.

Biinafsi naamini hio ndio njia muafaka katika kuhakikisha kwamba historia ya nchi yetu inakuwa tajiri.Haijalishi hata tukiwa na aina sita za historia ya nchi yetu cha muhimu ni kuhakikisha kwamba tunakuwa na utajiri wa taarifa utakaowezesha vizazi vijavyovyo kufurahi urithi huu wa historia.
 
Haya yanahusiana vipi na bandiko #31

Pascal Mayalla alisema yapo ya kweli na yapo ya ''urongo'' a.k.a ngano
Mkuu, Nguruvi 3, kwanza asante kuni tag hapa, Mkuu Maalim Mohammed Said kila anapoleta urongo humu, ukishutukiwa, hukwepa ama kwa kutoka baru, kwa kunyamaza, ama kwa kuzunguka zunguka, yuko vizuri sana kwenye kupiga chenga. Mfano mzuri ni hilo swali lako la kwenye bandiko No. 31 kumhusu Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, kamwe hatalijibu maana litamuumbua urongo wake kuwa Mwalimu katambulishwa mjini na babu zake tuu. Babu zake pekee ndio walimtambulisha Mwalimu kwa Wazee wa Dar es Salaam in 1950s, hivyo data zozote kuwa Mwalimu Nyerere alifika Dar 1948 na kuhudhuria mkutano Mkuu wa TAA, is not a good news!.

Kuna siku humu yule Bidada wake alileta bandiko humu la urongo mtupu wa mchana kweupe akidai

ndani ya bandiko hilo akaweka voice clip ya Mkuu Maalim Mohammed Said akitema urongo fulani kwa kudai ndani ya Bunge la JMT, wabunge asilimia 76% ni Wakristu Wakatoliki, Asilimia 18% ni Wakristu wa madhehebu mengine, na Waislamu ni asilimia 6% tuu!.

Nilipokosoa bandiko hilo, na kuanzisha bandiko hili,

Kwanza ile sound clip ya maurongo ya Mkuu Maalim Mohammed Said, ilifutwa from the source, pili Mkuu Maalim Mohammed Said mwenyewe akaingia front with an excuse kuwa hizo data za urongo na yeye alizisoma tuu kutoka sources fulani.

Hivyo Mkuu Maalim Mohammed Said akileta urongo humu, akishtukiwa, kamwe hawezi kukiri urongo wake, atazuga kwa kuzunguka zunguka hadi watu wasahau kama lilivyo bandiko lako No. 31, Mkuu Maalim Mohammed Said hawezi jibu hilo ataumbuka.

P
 
Mzee wetu Mohamed Said najua wengi wetu tuna kasumba ya kumpinga mjumbe badala ya ujumbe,wengi tunafikiri kwamba kwa sababu hatukubaliani na mjumbe basi tunaweza kutumia kigezo hicho hicho kukataa ujumbe,jambo ambalo si kweli.

Ujumbe wako naamini uko wazi kwamba kuna mengi tunapaswa kuyafahamu kuhusu historia ya nchi yetu sio kwa sababu ya ubaya ila ni kwa faida ya nchi yetu na vizazi vijavyo.

Najua kwamba historia yetu rasmi inaweza kuwa inakosa baadhi ya madini ambayo wewe unatuambia kwamba umeyafanyia utafiti na yenye vielelezo thatbiti.

Najua pia kwamba sio jambo rahisi kubadili historia rasmi hasa ukilinganisha kwamba mengi ya mambo uliyonayo kimsingi yanaonekana kuwa (errors of omission)mfano kutowataja kwa majina wahusika katika hao wazee wa Dar es Salaam) au kutokuelezea kwa kina mchango wao katika historia ya nchi yetu.

BInafsi nafikiri sasa ni wakati wa wanazuoni kama wewe na wengine wengi kuandika kuhusu historia katika mtazamo tofauti.Cha msingi ni kuhakikisha kwamba katika kufanya utafiti wako usiatafute kuichalenge official historia ispokuwa tu pale ambapo kuna reliable facts ambazo zinaweza kusaidia zaidi watu kuelewa historia yetu bila kuwa upotoshaji,uongo au chuki.

Biinafsi naamini hio ndio njia muafaka katika kuhakikisha kwamba historia ya nchi yetu inakuwa tajiri.Haijalishi hata tukiwa na aina sita za historia ya nchi yetu cha muhimu ni kuhakikisha kwamba tunakuwa na utajiri wa taarifa utakaowezesha vizazi vijavyovyo kufurahi urithi huu wa historia.
Ondoza,
Kama kuandika nitaandika mengine lakini si kurudia upya historia ya TANU.

Hii historia nimeshaiandika miongo mwiwili iliyopita.

Hivi sasa kitabu kinakwenda toleo la nne.

 
Mkuu, Nguruvi 3, kwanza asante kuni tag hapa, Mkuu Maalim Mohammed Said kila anapoleta urongo humu, ukishutukiwa, hukwepa ama kwa kutoka baru, kwa kunyamaza, ama kwa kuzunguka zunguka, yuko vizuri sana kwenye kupiga chenga. Mfano mzuri ni hilo swali lako la kwenye bandiko No. 31 kumhusu Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, kamwe hatalijibu maana litamuumbua urongo wake kuwa Mwalimu katambulishwa mjini na babu zake tuu. Babu zake pekee ndio walimtambulisha Mwalimu kwa Wazee wa Dar es Salaam in 1950s, hivyo data zozote kuwa Mwalimu Nyerere alifika Dar 1948 na kuhudhuria mkutano Mkuu wa TAA, is not a good news!.

Kuna siku humu yule Bidada wake alileta bandiko humu la urongo mtupu wa mchana kweupe akidai

ndani ya bandiko hilo akaweka voice clip ya Mkuu Maalim Mohammed Said akitema urongo fulani kwa kudai ndani ya Bunge la JMT, wabunge asilimia 76% ni Wakristu Wakatoliki, Asilimia 18% ni Wakristu wa madhehebu mengine, na Waislamu ni asilimia 6% tuu!.

Nilipokosoa bandiko hilo, na kuanzisha bandiko hili,

Kwanza ile sound clip ya maurongo ya Mkuu Maalim Mohammed Said, ilifutwa from the source, pili Mkuu Maalim Mohammed Said mwenyewe akaingia front with an excuse kuwa hizo data za urongo na yeye alizisoma tuu kutoka sources fulani.

Hivyo Mkuu Maalim Mohammed Said akileta urongo humu, akishtukiwa, kamwe hawezi kukiri urongo wake, atazuga kwa kuzunguka zunguka hadi watu wasahau kama lilivyo bandiko lako No. 31, Mkuu Maalim Mohammed Said hawezi jibu hilo ataumbuka.

P
Pascal,

Mmeshindwa kuungana mkaandika kitabu kunijibu?

 
Pascal,
Mmeshindwa kuungana mkaandika kitabu kunijibu?

Mkuu Maalim Mohammed Said, uandishi wa kitabu ni kipaji, sio kila mtu anacho, wewe mwenzetu umejaaliwa kipaji hicho na unaandika, tunakusoma na inatosha, ila unapoandika urongo, na kuna wanaojua ukweli, ni haki yao kukukosoa na kukuambia hoja hii ni urongo, kama alivyofanya hapa Mkuu Nguruvi3, wewe unaongopa Mwalimu Nyerere katambulishwa jijini Dar es Salaam na wazee wako miaka ya early 1950s, Nguruvi3 kakuuliza aliyehudhuria mkutano Mkuu wa TAA 1948 kutokea Tabora ni nani?, unakimbia kimbia. Ukweli ni kuwa Mwalimu Nyerere aliwafahamu wazee wa Dar es Salaam miaka mingi kabla ya hao wazee wako, ila hii haiondoi ukweli kuwa wazee wako walikuwa ni ma Al watan mjini hapa hivyo walipomtambulisha Mwalimu Nyerere, walimuongezea tuu umaarufu, they are just amongst but not the only ones.

P
 
Mkuu Maalim Mohammed Said, uandishi wa kitabu ni kipaji, sio kila mtu anacho, wewe mwenzetu umejaaliwa kipaji hicho na unaandika, tunakusoma na inatosha, ila unapoandika urongo, na kuna wanaojua ukweli, ni haki yao kukukosoa na kukuambia hoja hii ni urongo, kama alivyofanya hapa Mkuu Nguruvi3, wewe unaongopa Mwalimu Nyerere katambulishwa jijini Dar es Salaam na wazee wako miaka ya early 1950s, Nguruvi3 kakuuliza aliyehudhuria mkutano Mkuu wa TAA 1948 kutokea Tabora ni nani?, unakimbia kimbia. Ukweli ni kuwa Mwalimu Nyerere aliwafahamu wazee wa Dar es Salaam miaka mingi kabla ya hao wazee wako, ila hii haiondoi ukweli kuwa wazee wako walikuwa ni ma Al watan mjini hapa hivyo walipomtambulisha Mwalimu Nyerere, walimuongezea tuu umaarufu, they are just amongst but not the only ones.

P
Pascal,
Hapana neno.
Ni yale yale ya simba wa Agip ana miguu mingapi?

Sasa mbona historia ya Kivukoni haikuandika haya usemayo?
 
Mmi binafsi najiuliza kwanini serikali inahofia kuwataja wazee hao kama tafiti zote zinawathibitisha kuwa walianza harakat za Uhuru hata kabla ya hayati baba wa taifa,,au kwani kutawagharim nni kuwatambua na kuwapa héshma yao?!.au kama serikali haijui au haizïamini kwéli hizi watumie vyombo vyake vinavyohusika kujirdhisha..ugumu uko wapi au sielewi Mimi
Heshima ya Nyerere kama ndio kila kitu ktk historia ya uhuru itapungua,historia ya wazee walio wengi waislam itapanda,huku wajukuu zao wakifia magerezani sababu tu ni waislam,hii ni hatari wacha mambo yawe yalivyo.
Nadhani ktk nchi yetu uislam ni tatizo kila wanapoulizwa kuhusu Zanzibar kuwa na serikali yake wanajibu sababu ni waislam wapo 99% ,wakiambiwa kipengele cha dini kwenye sensa wanajibu itakuwaje kama waislam wakiwa majority?
Hili suala la dini hili ni bomu!
 
Ndugu Mzee Said,hapa kwa taarifa hii inaondoa vipi ukweli kwamba Mwalimu alianza siasa/harakati kabla ya kukutana na kina Sykes na timu yao?

Au inakanusha vipi kwamba Mwalimu alikuwa anawasiliana na watu wa Dar kuhusu siasa/harakati za uhuru?

Nadhani tunapopishana ni hivi unavyoegemea sana kwenye nyaraka za Sykes au maelezo ya kundi moja. Hivi ni nani mwingine aliandika tofauti na Sykes?

Hakuna anayebeza mchango au nafasi ya kina Sykes na wenzake, ila bado kuna wengine nyuma waliokuwa na mchango na labda hawakupata nafasi ya kuandika kama Bw sykes, na hawa ndio wamekuwa mara kwa mara wakitajwa kama Wazee wa Dar, huenda hawakuwa na nafasi/uwezo kama kina Sykes ila sidhani kama ni sawa kuwapuuza na kung'ang'ana na kina Sykes na timu yao pekee.

Mwalimu alikuja Dar tayari akiwa anajua anataka nini, kutambulishwa kwa kina Sykes labda ilikuwa ni bahati tu na sidhani kama bila hivyo ingemzuia Mwalimu kuendelea na mission zake. Sasa kwa kuwa sykes haonyeshi/hakusema kama Mwalimu alikuwa na mawasiliano kabla ndio uitake na jamii yote iamini hivyo...kuna Wazee waliokuwa wanawasiliana na Mwalimu na sio kina Sykes.

Kingine kisichoeleweka kutoka kwako na nyaraka za Sykes ni hivi unavyoonyesha kana kwamba Mwalimu alitafutwa tu na kupewa kazi lakini huonyeshi yeye Mwalimu alikuja na nini hata kama Dar alikuwa mgeni, ugeni wa Dar sio ugeni wa siasa au mipango.
Hawa Wazee wa pwani wakitafuta mtu wa bara waunganishe nguvu kumtoa mkoloni wakijua kama waislam hawawezi kuwapa kirahisi,ndipo walipomfuata Chief Makwaia akakataa,ndipo wakamgeukia Nyerere,kama Chief angekubali basi historia ya Nyerere isingekuwa hivi ilivyo.
 
Heshima ya Nyerere kama ndio kila kitu ktk historia ya uhuru itapungua,historia ya wazee walio wengi waislam itapanda,huku wajukuu zao wakifia magerezani sababu tu ni waislam,hii ni hatari wacha mambo yawe yalivyo.
Nadhani ktk nchi yetu uislam ni tatizo kila wanapoulizwa kuhusu Zanzibar kuwa na serikali yake wanajibu sababu ni waislam wapo 99% ,wakiambiwa kipengele cha dini kwenye sensa wanajibu itakuwaje kama waislam wakiwa majority?
Hili suala la dini hili ni bomu!
Ngozimbili,
Ngoja niingie Maktaba nikuwekee link ya makala kuhusu dini.

 
Hawa Wazee wa pwani wakitafuta mtu wa bara waunganishe nguvu kumtoa mkoloni wakijua kama waislam hawawezi kuwapa kirahisi,ndipo walipomfuata Chief Makwaia akakataa,ndipo wakamgeukia Nyerere,kama Chief angekubali basi historia ya Nyerere isingekuwa hivi ilivyo.
Ngozimbili,
Waliokuwa wamesimama kutaka kuunda chama cha siasa hawakuwa wazee.
Uongozi wa wazee katika TAA ulishapinduliwa mwaka wa 1950.

Mwaka wa 1950 Abdul Sykes alikuwa na miaka 26.
Sijui hii historia ya wazee wapigania uhuru kabla ya TANU kuundwa imeanzishwa na nani.

Chief David Kidaha Makwaia hakufatwa na mzee yeyote.

Nyumba ya Abdul Sykes wakati akiwa kiongozi wa TAA ilikuwa inatembelewa na machifu wengi na mmoja wao alikuwa Chief Kidaha.

Chief Kidaha hadi taarifa za Special Branch yumo kuwa alikuwa akifika nyumbani kwa Abdul Sykes.

1574679781790.png

Nyumba ya Mwinjuma Mwinyikambi Mwananyama imewekwa kibao kinasema TANU iliasisiwa ndani ya nyumba hii.
Hawa wanaofanya upotoshaji huu hakika walikuwa ''very desparate,'' taharuki yao ya kufuta jina la Abdul Sykes katika TANU ilikuwa imewaelemea sana kupita kiasi.

1574680322858.png

Kuna kitu kimoja bahati mbaya sana hakifahamiki kwa wengi na sababu yake Abdul alikichukua kama jambo binafsi nje ya uhusiano wake na Nyerere katika siasa.

Abdul alikwenda mbali sana katika uhusiano wake na familia ya Nyerere.

Yeye alimchukua Nyerere kama ndugu yake na akaunganisha familia hizi mbili zikawa moja.


Marafiki hawa wawili walikuwa kama ndugu na hivi ndivyo watu wa Dar es Salaam walivyowachukulia na kuwajua baba yangu akiwa mmoja wao.
 
Mohamed Said, huu ni mchango wangu wa mwisho katika santuri hii yako ambayo imechuja lakini bado wapo watu wanaomeza tu ngano zako bila takafuri yoyote.

Wakati wote unapodai unaandika historia ya Waislaam ukweli ni kuwa unaandika historia ya wazee wako, Wazulu na Wamanyema.

Unapodai unaandika historia ya Watanganyika ukweli ni kuwa unaandika historia ya wazazi wako na babu zako,Wamanyema na Wazulu.

Kwa kukufahamisha Watanganyika walikuwepo sana tu ingawa huwapi kipaumbele stahiki katika hizi ngano zako.

Huwezi kuongelea AA bila kumtaja muasisi na Kiongozi wake Mkuu wakati inaanzishwa mwaka 1929 na huyo si mwingine bali Mtanganyika Myao na Msomi Hayati Mwalimu Cecil Matola.

Baada ya Matola kufariki, AA ilikosa uongozi madhubuti hali iliyoifanya AA kuwa kama chombo kilichokosa dira hadi Zanzibar ilipojitoa mwaka 1948 na kuzaliwa TAA.

Lakini hata ilipozaliwa TAA, uongozi thabiti ulikuja kupatikana mwaka 1950, Mtanganyika Mhaya Dr. Vedasto Kyaruzi alipochaguliwa kuwa Raisi wake wa kwanza.

Baada ya Wakoloni kumpa uhamisho wa nguvu Raisi wa TAA, shughuli za TAA zilizorota kwa sababu kiongozi mkuu hakuwepo.

Kumbuka kwamba Dr. Kyaruzi alipopewa uhamisho wa kwanza hakupelekwa mbali na hivyo aliweza kuendelea kuwasiliana na wasaidizi wake mojawapo akiwa Abduwahid Sykes.

Wakoloni walipogundua hilo ilibidi wamhamishe tena wampeleke mbali zaidi ili mawasiliano na wasaidizi wake yawe magumu zaidi na hivyo kupelekea TAA kuzorota hadi ujio wa Mwalimu Nyerere mwaka 1952.

Hivyo nafasi ya Abdulwahid Sykes ndani ya TAA wakati Mwalimu Nyerere yuko Makerere ni kwamba wakati huo TAA haikuwapo, ilikuwepo AA iliyoasisiwa na Cecil Matola mwaka 1929.

Huyu Abdulwahid Sykes unamtajataja sana na bila shaka kwa sababu unazozijua wewe mwenyewe lakini ukweli ni kwamba hakuwahi kuwa kiongozi Mkuu wa TAA wala TANU wakati wowote ule.

Dai la kuwa ndiye alipendekeza jina la TANU ni kweli kwa kiasi Fulani kwani alichofanya ni kwamba jina alilopendekeza awali Mwalimu Nyerere lilikuwa gumu kidogo kutamkwa kwa haraka ingawa maneno yalikuwa yale yale.

Mwalimu Nyerere alitaka maneno manne yasikosekane nayo ni AFRICAN, TANGANYIKA, NATIONAL na UNION yawepo na iliyobakia ni namna tu ya kuyapanga na ndipo Abdulwahid Sykes kupendekeza Tanganyika African National Union (TANU)
 
Mohamed Said, huu ni mchango wangu wa mwisho katika santuri hii yako ambayo imechuja lakini bado wapo watu wanaomeza tu ngano zako bila takafuri yoyote.

Wakati wote unapodai unaandika historia ya Waislaam ukweli ni kuwa unaandika historia ya wazee wako, Wazulu na Wamanyema.

Unapodai unaandika historia ya Watanganyika ukweli ni kuwa unaandika historia ya wazazi wako na babu zako,Wamanyema na Wazulu.

Kwa kukufahamisha Watanganyika walikuwepo sana tu ingawa huwapi kipaumbele stahiki katika hizi ngano zako.

Huwezi kuongelea AA bila kumtaja muasisi na Kiongozi wake Mkuu wakati inaanzishwa mwaka 1929 na huyo si mwingine bali Mtanganyika Myao na Msomi Hayati Mwalimu Cecil Matola.

Baada ya Matola kufariki, AA ilikosa uongozi madhubuti hali iliyoifanya AA kuwa kama chombo kilichokosa dira hadi Zanzibar ilipojitoa mwaka 1948 na kuzaliwa TAA.

Lakini hata ilipozaliwa TAA, uongozi thabiti ulikuja kupatikana mwaka 1950, Mtanganyika Mhaya Dr. Vedasto Kyaruzi alipochaguliwa kuwa Raisi wake wa kwanza.

Baada ya Wakoloni kumpa uhamisho wa nguvu Raisi wa TAA, shughuli za TAA zilizorota kwa sababu kiongozi mkuu hakuwepo.

Kumbuka kwamba Dr. Kyaruzi alipopewa uhamisho wa kwanza hakupelekwa mbali na hivyo aliweza kuendelea kuwasiliana na wasaidizi wake mojawapo akiwa Abduwahid Sykes.

Wakoloni walipogundua hilo ilibidi wamhamishe tena wampeleke mbali zaidi ili mawasiliano na wasaidizi wake yawe magumu zaidi na hivyo kupelekea TAA kuzorota hadi ujio wa Mwalimu Nyerere mwaka 1952.

Hivyo nafasi ya Abdulwahid Sykes ndani ya TAA wakati Mwalimu Nyerere yuko Makerere ni kwamba wakati huo TAA haikuwapo, ilikuwepo AA iliyoasisiwa na Cecil Matola mwaka 1929.

Huyu Abdulwahid Sykes unamtajataja sana na bila shaka kwa sababu unazozijua wewe mwenyewe lakini ukweli ni kwamba hakuwahi kuwa kiongozi Mkuu wa TAA wala TANU wakati wowote ule.

Dai la kuwa ndiye alipendekeza jina la TANU ni kweli kwa kiasi Fulani kwani alichofanya ni kwamba jina alilopendekeza awali Mwalimu Nyerere lilikuwa gumu kidogo kutamkwa kwa haraka ingawa maneno yalikuwa yale yale.

Mwalimu Nyerere alitaka maneno manne yasikosekane nayo ni AFRICAN, TANGANYIKA, NATIONAL na UNION yawepo na iliyobakia ni namna tu ya kuyapanga na ndipo Abdulwahid Sykes kupendekeza Tanganyika African National Union (TANU)
Mkuu mag3 asante kwa historia nzuri .nafatilia kwa karibu huu mnakasha
 
Lakini mbn huyu mzee huwa anapenda sana hizi habari ni madai ya kutaka wazee wake watambulike tu au kuna jambo liko nyuma ya pazia.

Huenda kuna jambo maana kuna wengine humu jf wameomba ikulu irejeshwe kwa waislam. Madai ambayo ni ya ajabu kabisa kama kila aliyefanya jambo fulani arejeshewe kutakuwa na kubakia na nini, taifa litagawanyika.

Huyu mzee anadai kila siku watambuliwe watambuliwe kivipi sasa hao walishapita wakajenga kwa sehemu yao imepita wakumbukweje basi. Kila mmoja wetu hufanya kwa sehemu yao na yote waliyofanya watalipwa na MUNGU huko mbele ya haki.

Tukianza kutafuta nani alihusika na nini tutafika wapi haya mpewe Ikulu ya Dar mkakae hapo sijui mnaitaka mukaishi pale sijui Mhimbili nayo watoto wa Mwaisela sijui wauze majengo wagawane. Kumbukeni hao wazee wenu walianzisha wengine wakaendeleza. Kumbukeni hata hao walioendeleza ndiyo wa maana zaidi. Maana hao ndiyo waliofanya yaliyopo leo na tunajivunia kilichopo kwa faida ya sisi sote.
Jengo la ikulu halikuwa hivyo jengo la mhimbili halikuwa vile chama chenu cha TAA hakikuwa hivyo waliojenga juu yake ndiyo wa maana zaidi.

Huyu mzee kila kukicha ya nyuma tuuu ndiyo kukua huko haya basi eee tumekusikia tuwafanyie nini hao wazee wako.
Hao wazee wako hawawezi kukumbukwa kwa kupewa sijui majengo au madaraka kwa vitukuu wao ambao hawakuweza kuendeleza chochote juu yake na wakaishia kukimbilia ubaharia na kuterekeza harakati za wazazi wao, au hawakuweza kuonesha vipaji sawa na wazazi wao katika nyazifa mbalimbali na kwa uhitaji wa nyakati hizo wakawepo wengine kuendeleza kazi zao hao wazee.
 
Back
Top Bottom