Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Nguruvi3,
Hiyo si lugha ya ghadhabu hata kidogo.
Nimekualika au nimekutaja?

Jina la Abdulwahid Kleist Sykes ndiyo hilo sasa mmefahamu na Mwalimu alikisoma kitabu tena alipelekewa na kijana aliyeoa katika familia yake ambae mimi ni rafiki yangu.

Baada ya kukisoma Mwalimu alizungumza na huyu rafiki yangu.

Prof. Haroub Othman aliomba miadi na Mwalimu wazungumze kuhusu kitabu changu na cha Ali Muhsin Barwani, "Conflict and Harmony in Zanzibar."

Prof. kamuomba Mwalimu na yeye aandike kutujibu.

Hivi sasa rafiki zangu wananiweka katika shinikizo niandike kitabu kingine kuhusu haya na mengine yaliyotokea kutoka kitabu cha Abdul Sykes na mihadhara niliyofanya kueleza upya historia ya TANU.

Wewe unanirudisha nyuma nimjadili Mwalimu Nyerere ambae tayari nimeshaandika historia yake.

Mwaka jana radio, televisheni na magazeti walinipa uwanja kuadhimisha miaka 50 ya kifo cha Abdul Sykes naamini ulibahatika kusoma mfululizo wa makala zilizochapwa na Raia Mwema alizoandika bint yake Aisha "Daisy"Sykes.

Daisy aliwaeleza vizuri sana Abdul Sykes, Hamza Mwapachu na Julius Nyerere alivyokuwa akiwaona nyumbani kwao wakati ule 1950s yeye bint mdogo akisikiliza mazungumzo yao.

Kila wafikapo wageni kwangu haya ndiyo wanayoshinikiza niandike.
Wewe unanirejesha kwenye kitabu kinachokwenda toleo la nne tena unataka tufanye mjadala.
Haya yanahusiana vipi na bandiko #31

Mag3 unaona? Hii ndiyo ngano anayozomesha mzee wetu.

Pascal Mayalla alisema yapo ya kweli na yapo ya ''urongo'' a.k.a ngano

Mohamed, ukinialika uwe tayari mvumilivu na mwenye stara, mimi sikai juu ya jamvi kusikiliza tu na kumeza kila kinachotupwa!

Kwa Taarifa yako lile bandiko la Kleist alivyokuja Pangani lina makosa pitia usahihishe!

Mag3 , Mkubwa narudi mtoni kuchutama...
 
Haya yanahusiana vipi na bandiko #31

Mag3 unaona? Hii ndiyo ngano anayozomesha mzee wetu.

Pascal Mayalla alisema yapo ya kweli na yapo ya ''urongo'' a.k.a ngano

Mohamed, ukinialika uwe tayari mvumilivu na mwenye stara, mimi sikai juu ya jamvi kusikiliza tu na kumeza kila kinachotupwa!

Kwa Taarifa yako lile bandiko la Kleist alivyokuja Pangani lina makosa pitia usahihishe!

Mag3 , Mkubwa narudi mtoni kuchutama...
Nguruvi3,
Mimi sina tatizo na yeyote ambae hakubaliani na kitabu cha Abdul Sykes kwani hiyo ni haki yao achilia mbali kuwa tuna historia ya TANU iliyoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni ambayo ndiyo inayotambuliwa kama historia rasmi ingawa ina makosa mengi.

Narudia tena kuwa sijapatapo kukualika popote pale.

Aliyeshuka Pangani kutoka manowari ya Kijerumani hakuwa Kleist Sykes bali baba yake Sykes Mbuwane.

Ikiwa bado unaona juu ya kosa hili bado ipo haja ya kufanya masahihisho hili litakuwa jambo zuri ila ningependa kukufahamisha kuwa historia hiyo ya safari ya Wazulu kutoka Kwa Likunyi, Imhambane kuja Pangani wakitokea Laurenco Marquis, Kleist Sykes alielezwa na Affande Plantan baba yake mlezi na yeye Kleist akaandika historia hii kwenye mswada wa maisha yake kabla hajafariki mwaka wa 1949.

Mswada huu sasa ni kitabu kilichohaririwa na John Iliffe, ''Modern Tanzanians,'' (1973) na mswada wenyewe (seminar paper) kama ilivyoandikwa na Aisha ''Daisy'' Sykes uko Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, East Africana toka mwaka wa 1968.

Hunisahihishi mimi utakuwa unasahihisha nyaraka za wenyewe akina Sykes na hili ni jambo nalisubiri kwa hamu kubwa.
 
Haya yanahusiana vipi na bandiko #31

Mag3 unaona? Hii ndiyo ngano anayozomesha mzee wetu.

Pascal Mayalla alisema yapo ya kweli na yapo ya ''urongo'' a.k.a ngano

Mohamed, ukinialika uwe tayari mvumilivu na mwenye stara, mimi sikai juu ya jamvi kusikiliza tu na kumeza kila kinachotupwa!

Kwa Taarifa yako lile bandiko la Kleist alivyokuja Pangani lina makosa pitia usahihishe!

Mag3 , Mkubwa narudi mtoni kuchutama...
Wewe unauliza maswali kutokana na uliyoyasoma kwa Allama Mohamed Said ambayo hujapatapo kuyaandika wala kuyasoma kwa mwengine kabla yake.

Huo sisi huuita ujanja wa sungura, zabibu za watu alipozikosa akasema hizo mbichi!

Mbichi, zako?
 
Wewe unauliza maswali kutokana na uliyoyasoma kwa Alama Mohamed Said ambayo hujapatapo kuyaandija wala kuyasoma kwa mwengine kabla yake.

Huo sisi huuita ujanja wa sungura, zabibu za watu alipozikosa akasema hizo mbichi!

Mbichi zako?
Ah Kumbe Alama ndiye mmiliki wa Historia! hili nalo geni nalijua leo
Unajua kwanini tunamuuliza? Kwasababu between the lines kuna ngano.

Huwa hapendi kuulizwa anajua lazima atakwama,si kwasababu anachoandika si kweli! la hasha ! ila kuna upotoshaji, ushehereshaji ambao hataki uwekwe sawa!
Makosa yale yale ya historia ya kivukoni, akificha maeneo asiyotaka yasomeke

Wewe unaamini Nyerere alikuja Dar kwa mara ya kwanza mwaka 1950!
Mkutano Mkuu wa 1948 alikuja Dar akitokea Tabora, Tawi kubwa sana lakini Abdul hakumjua!

Mohamed anasisitiza mtu wa kwanza kujulishwa kwake ni Abdul mwaka 1950! wapi na wapi

Tunamuuliza Abdul Sykes aliwatimua vipi wazee wake ofisini! hataki kusema

Haaijulikani kama aliwakaripia,chapa viboko,dunda ngumi na mateke au kuwasota madole ya macho wazee wake. Mohamed hapo haendi kabisa atakwambia hana nyaraka!

Atakwambia visa vyoote, asichosema ni kuwa Abdul ndiye mwasisi wa AMNUT iliyofeli

Hata wazee wetu wa Dar walimgomea, pengine kwa kujua alivyowatimua waliotangulia

Tulipo kaa kimya tuliona ni heri ''kuchutama mtoni....'' Katualika tumeitikia wito! la hau anaghadhabika tena!

Msaidie kujibu bandiko# 31
 
Ah Kumbe Alama ndiye mmiliki wa Historia! hili nalo geni nalijua leo
Unajua kwanini tunamuuliza? Kwasababu between the lines kuna ngano.

Huwa hapendi kuulizwa anajua lazima atakwama,si kwasababu anachoandika si kweli! la hasha ! ila kuna upotoshaji, ushehereshaji ambao hataki uwekwe sawa!
Makosa yale yale ya historia ya kivukoni, akificha maeneo asiyotaka yasomeke

Wewe unaamini Nyerere alikuja Dar kwa mara ya kwanza mwaka 1950!
Mkutano Mkuu wa 1948 alikuja Dar akitokea Tabora, Tawi kubwa sana lakini Abdul hakumjua!

Mohamed anasisitiza mtu wa kwanza kujulishwa kwake ni Abdul mwaka 1950! wapi na wapi

Tunamuuliza Abdul Sykes aliwatimua vipi wazee wake ofisini! hataki kusema

Haaijulikani kama aliwakaripia,chapa viboko,dunda ngumi na mateke au kuwasota madole ya macho wazee wake. Mohamed hapo haendi kabisa atakwambia hana nyaraka!

Atakwambia visa vyoote, asichosema ni kuwa Abdul ndiye mwasisi wa AMNUT iliyofeli

Hata wazee wetu wa Dar walimgomea, pengine kwa kujua alivyowatimua waliotangulia

Tulipo kaa kimya tuliona ni heri ''kuchutama mtoni....'' Katualika tumeitikia wito! la hau anaghadhabika tena!

Msaidie kujibu bandiko# 31
Na hayo uliyasoma wapi? "citation please".

Ngano unazisoma mwaka wa 9 sasa?

Ukishajibu nna maswali mengine.
 
Umejitahidi kujitutumua ELIMU YAKO USIWARITHISHE WANAO.

Kama unalipenda taifa la TANZANIA.
Hizi ngano zako sasa zinachosha…! Najua wazee wa Dar es Salaam walikuwa wazee wako na ungependa sana uwainue. Najua unavyohangaika na ngano zile zile kila mara lakini utake usitake kwa ufupi sana ni hivi...

Ni uongo uliopitiliza kudai kwamba AA iliyoanzishwa mwaka 1929 na Gavana wa wakati huo Cameroun kama klabu ya starehe kwa wasomi weusi ilikuwa na malengo ya kudai uhuru.

Hilo la kwanza na pili ni ukweli kuwa wakati Nyerere anahudhuria mkutano mkuu wa AA akiwakilisha jimbo la Tabora wewe ulikuwa hujazaliwa. Na kwamba viongozi wa AA walikuwa hawamjui Mwalimu Nyerere kabla ya mwaka 1953 alipohamia Dar es Salaam pia ni uongo.

Mtu ambaye yawezekana hakumjua Mwalimu Nyerere labda ni Abdul Sykes peke yake kwa sababu nyakati hizo hakuwepo...tunaanza kumsikia tu pale alipoongoza uvamizi wa ofisi za AA kuwatoa wazee wake!

Mwalimu Nyerere tayari alikuwa kiongozi wa AA mwaka 1945 akiwa Tabora na mwaka huo huo alifika Dar es Salaam na kukutana na viongozi na wanachama wa AA mojawapo akiwa Dossa Aziz.

Sasa, kama Mwalimu Nyerere na Abdul hawakukutana ni wazi kumbe Abdul Sykes hakuwa kati ya vinara wa AA mjini Dar es Salaam...swali la kujiuliza ni je, Abdul alikuwa nani ndani ya AA kabla ya kuvamia ofisi za TAA mwaka 1948 kwa ngumi na mateke?

cc: Nguruvi3, Yericko Nyerere, JokaKuu
 
Na hayo uliyasoma wapi? "citation please".

Ngano unazisoma mwaka wa 9 sasa?

Ukishajibu nna maswali mengine.
Hivi unaweza kufanya ''citation ya maswali'' (Bandiko#31)
Hata hivyo kwa kukusaidia tu soma '' The life and times of Abdul Sykes (1924-1968)

Ngano miaka 9! Nilishakaa kimya, wewe na Alama Mohamed mkanialika, kuchungulia ninaona ushereheshaji wa historia unaendelea, nikaona nijisogeze si kulala jamvini bali kutafakari

Mimi si wale wa hewala, hongera, ahsante! hapana, nyote mnaelewa hilo

Jibu bandiko # 31 please
 
Ah Kumbe Alama ndiye mmiliki wa Historia! hili nalo geni nalijua leo
Unajua kwanini tunamuuliza? Kwasababu between the lines kuna ngano.

Huwa hapendi kuulizwa anajua lazima atakwama,si kwasababu anachoandika si kweli! la hasha ! ila kuna upotoshaji, ushehereshaji ambao hataki uwekwe sawa!
Makosa yale yale ya historia ya kivukoni, akificha maeneo asiyotaka yasomeke

Wewe unaamini Nyerere alikuja Dar kwa mara ya kwanza mwaka 1950!
Mkutano Mkuu wa 1948 alikuja Dar akitokea Tabora, Tawi kubwa sana lakini Abdul hakumjua!

Mohamed anasisitiza mtu wa kwanza kujulishwa kwake ni Abdul mwaka 1950! wapi na wapi

Tunamuuliza Abdul Sykes aliwatimua vipi wazee wake ofisini! hataki kusema

Haaijulikani kama aliwakaripia,chapa viboko,dunda ngumi na mateke au kuwasota madole ya macho wazee wake. Mohamed hapo haendi kabisa atakwambia hana nyaraka!

Atakwambia visa vyoote, asichosema ni kuwa Abdul ndiye mwasisi wa AMNUT iliyofeli

Hata wazee wetu wa Dar walimgomea, pengine kwa kujua alivyowatimua waliotangulia

Tulipo kaa kimya tuliona ni heri ''kuchutama mtoni....'' Katualika tumeitikia wito! la hau anaghadhabika tena!

Msaidie kujibu bandiko# 31
Nguruvi 3,
Unanifurahisha sana.

Niwekee nukuu ninayosema nimesema Nyerere kaja Dar es Salaam mwaka wa 1950.
Unatumia lugha za kejeli ati Abdul Sykes ''aliwatimua,'' wazee.

Historia hii ipo katika kitabu cha Kivukoni?
Jibu ni haipo wewe kwa mara ya kwanza umeisikia kutoka kwa Mohamed Said.

Je, unajua sababu ya kutokuwepo?

Tunaweza tukasema mengi lakini jibu lepesi lisilo na matatizo ni kusema Chuo Cha CCM Kivukoni walikuwa hawaijui historia hii.

Tunaweza tukasema si Hassan Upeka aliwaletea ''notes,'' za Abdul Sykes wakazikataa?
Kwa nini walizikataa?

Tuseme walikuwa hawajui uhusiano wa Abdul Sykes na TAA na TANU na Nyerere?

Ndipo ninaposema unanipa starehe kubwa sana kwani haya ningeyaelezaje?
Wenye kutusikiliza wanajua baina yangu na wewe nani bingwa wa historia hii.

Wewe unauliza maswali mimi natoa majibu na wasikilizaji wananufaika na hii ''Elimu bila Khiyana,'' chembelecho Maalim Faiza.

Historia ya kuwatoa Thomas Saudtz Plantan na Clement Mohamed Mtamila mwaka wa 1950 ni ''mile stone,'' katika historia ya kuundwa kwa TANU kwa sababu hapo ndipo harakati za kubadili mbinu dhidi ya Waingereza zilipoanza na waliofanya mapinduzi haya walikuwa Schneider Abdillah Plantan, Hamza Mwapachu na Abdulwahid Kleist Sykes.

Kilichofuatia baada ya mapinduzi haya ni kuingia madarakani Dr. Vedasto Kyaruzi kama Rais na Abdul Sykes Katibu kisha ikaundwa TAA Political Subcommittee wajumbe wake: Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, Dr. Kyaruzi, Abdul Sykes, Steven Mhando na John Rupia (mjumbe ambae hatajwi ni Earle Seaton).

Earle Seaton alikuwa wakili na rafiki ya Abdul Sykes kutoka Bermuda akifanya shughuli zake Moshi.

Huyu nimemsoma historia yake katika Nyaraka za Sykes na ndiye akiisaidia TAA katika mambo ya sheria.

Kwa miaka mingi nimekuwa na mswada wa Dr. Kyaruzi, ''Muhaya Doctor,'' kwenye Maktaba yangu.

Bado haujachapwa kitabu.
Dr. Kyaruzi anaeleza historia hii katika sura inayoitwa, ''Action Group.''

Katika sura hii anamweleza vizuri Abdul Sykes na Schneider Platana na anasema kuwa Schneider ni mmoja wa baba zake Abdul.

Unauona uzi unavyojitunga katika sindano?

Mnadhani mnaweza mkafuta historia hii kwa kumbebesha Mwalimu Nyerere mizigo isiyomuhusu kwa ujanja ujanja na vitisho?

Bado hujaamini kuwa Mohamed Said anaijua historia ya TANU?
 
Hivi unaweza kufanya ''citation ya maswali'' (Bandiko#31)
Hata hivyo kwa kukusaidia tu soma '' The life and times of Abdul Sykes (1924-1968)

Ngano miaka 9! Nilishakaa kimya, wewe na Alama Mohamed mkanialika, kuchungulia ninaona ushereheshaji wa historia unaendelea, nikaona nijisogeze si kulala jamvini bali kutafakari

Mimi si wale wa hewala, hongera, ahsante! hapana, nyote mnaelewa hilo

Jibu bandiko # 31 please
Nguruvi 3,
Wala mimi hainipi shida kwa kitabu changu kukiita ''ngano.''

Naamini ungekuwa una kitu cha maana miaka 21 ingekutosha sana kuandika hata ''paper,'' kujieleza.

Miaka 9 unauliza maswali na unapewa majibu.
Hivi unataarifa kuwa nimeandika vitabu 3 kusherehesha zaidi historia ya uhuru wa Tanganyika?:

Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No.1 (2019).
Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No.2 (2019).
Dar es Salaam na Wazalendo Wake Mashujaa Katika Kupigania Uhuru wa Tanganyika (2019).

Wewe bado uko na The Life and Times of Abdulwahid Sykes...(1998) na swali no. 31.

AMNUT,
Majina yote ya waasisi wa AMNUT na historia yake yote nimeieleza katika kitabu cha Abdul Sykes.

Abdul hakuwemo ila mmoja wa baba zake Ramadhani Mashado Plantan ni mmojawapo wa waasisi na alitoa nyumba yake Mtaa wa Kirk Street na Nyamwezi kuwa ofisi.

Bado unabisha kuwa mimi bingwa wa historia hii?
 
"Mohamed Said, post: 33574772, member: 12431"
Niwekee nukuu ninayosema nimesema Nyerere kaja Dar es Salaam mwaka wa 1950.
Moddy amakweli umri umesonga! Siyo wewe uliyewahi kueleza Nyerere kutambulishwa kwa Abdul mwaka 1950. Na hili tulilijadili sana huko nyuma tukakueleza si Kweli!
Unataka nukuu zako kwamba aliyemwingiza Nyerere katika siasa ni Abdul?
Unatumia lugha za kejeli ati Abdul Sykes ''aliwatimua,'' wazee.
Mapinduzi ni kitu gani kama si kutimua! Kuna mapinduzi ya mapenzi? Mapinduzi, kuwaondoa kwa nguvu au kuwapiga mateke ni kitu kile kile! hili sitajadili tena maana huna jibu
Tunaweza tukasema mengi lakini jibu lepesi lisilo na matatizo ni kusema Chuo Cha CCM Kivukoni walikuwa hawaijui historia hii.
Hapana, walijua historia, walichokifanya ni kusherehesha kwa makusudi ili ku 'fit narrative'' . Na hilo nililifahamu kabla hujaandika

Ndiyo maana nakuasa uandike historia kama ilivyotokea, usishereheshe maana itakuwa kivukoni part 2. Utuambie Nyerere kaingizwa katika siasa na Abdul tukae kimya!
Utueleze Nyerere kaja Dar hakumjua mtu wakati tunajua alikuja kabla tukae kimya!
Utueleze mapinduzi na sub committee bla bla wakati wazee walitimuliwa kwa mateke!
Hutuelezi AMNUT ilifia wapi unatueleza Bakwata ilivyoanzishwa, tukae kimya
Tafadhali bwana !
Wenye kutusikiliza wanajua baina yangu na wewe nani bingwa wa historia hii.
Sina ubingwa wowote na wala sitawania popote! kilimo cha minazi hapa Tanga kinanitosha. Hilo halinifanyi nikae kimya wakati unaifanyanga historia kwa mtindo wa ngano.
Wewe unauliza maswali mimi natoa majibu na wasikilizaji wananufaika na hii elimu bila khiyana chembelecho Maalim Faiza.
Hapana, unajua maswali yangu yanaelekea wapi ndiyo maana unajaribu kuyakwepa. Moja ya maswali hayo ni hili
Tawi la Tabora lilizinduliwa 3/3/1945. Nyerere alichukua madaraka lini, na katika wazee uliowataja nani alihudhuria mkutano wa Dar wa mwaka 1948

Historia ya kuwatoa Thomas Saudtz Plantan na Clement Mohamed Mtamila mwaka wa 1950 ni ''mile stone,'' katika historia ya kuundwa kwa TANU kwa sababu hapo ndipo harakati za kubadili mbinu dhidi ya Waingereza zilipoanza na waliofanya mapinduzi haya walikuwa Schneider Abdillah Plantan, Hamza Mwapachu na Abdulwahid Kleist Sykes.
Anachronism
Earle Seaton alikuwa wakili na rafiki ya Abdul Sykes kutoka Bermuda akifanya shughuli zake Moshi.
Irrelevant
Huyu nimemsoma historia yake katika Nyaraka za Sykes.
so what!
Mnadhani mnaweza mkafuta historia hii kwa kumbebesha Mwalimu Nyerere mizigo isiyomuhusu kwa ujanja ujanja na vitisho?
Na wala hawezi kufutika katika Historia kwa njia za ngano
Bado hujaamini kuwa Mohamed Said anaijua historia ya TANU?
Inakusaidia wewe
 
Nguruvi 3,
Wala mimi hainipi shida kwa kitabu changu kukiita ''ngano.''

Naamini ungekuwa una kitu cha maana miaka 21 ingekutosha sana kuandika hata ''paper,'' kujieleza.

Miaka 9 unauliza maswali na unapewa majibu.
Hivi unataarifa kuwa nimeandika vitabu 3 kusherehesha zaidi historia ya uhuru wa Tanganyika?:

Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No.1 (2019).
Watu Mashuhuri Katika Uhuru wa Tanganyika No.2 (2019).
Dar es Salaam na Wazalendo Wake Mashujaa Katika Kupigania Uhuru wa Tanganyika (2019).

Wewe bado uko na The Life and Times of Abdulwahid Sykes...(1998) na swali no. 31.
Na wala sina mpango wa kuandika kuhusu familia za wat.
Kuuliza si ujinga,unafahamu hilo.Na kupitia maswali hayo mara nyingi sana umejichanganya!

Mohamed suala hapa si kuwa unachoandika hakipo! la hasha.

Hoja kubwa ni kuwa unajaribu kusherehesha historia! kuipaka rangi n.k. hapana hilo si sahihi

Ukiambiwa kabla ya Nyerere vyama vilikuwa vya starehe, haina maana vilabu vya Pombe
Vilikuwa vijiwe vya siasa, na ushahidi unao wewe.
Tuonyeshe katiba ya AA au TAA kabla ya katiba ya TANU!

Mohamed huhitaji kuandika wewe ni nani! Mbona watu wanakufahamu
Itapendeza zaidi kazi zako zikukueleza wewe ni nani.
 
Na wala sina mpango wa kuandika kuhusu familia za wat.
Kuuliza si ujinga,unafahamu hilo.Na kupitia maswali hayo mara nyingi sana umejichanganya!

Mohamed suala hapa si kuwa unachoandika hakipo! la hasha.

Hoja kubwa ni kuwa unajaribu kusherehesha historia! kuipaka rangi n.k. hapana hilo si sahihi

Ukiambiwa kabla ya Nyerere vyama vilikuwa vya starehe, haina maana vilabu vya Pombe
Vilikuwa vijiwe vya siasa, na ushahidi unao wewe.
Tuonyeshe katiba ya AA au TAA kabla ya katiba ya TANU!

Mohamed huhitaji kuandika wewe ni nani! Mbona watu wanakufahamu
Itapendeza zaidi kazi zako zikukueleza wewe ni nani.
Nguruvi 3,
Nitakujibu katika hayo yote moja tu.

Mwanzo wa kitabu naanza kueleza historia ya familia tatu maarufu Dar es Salaam ambazo ndiyo zilitawala siasa - Sykes, Plantan na Aziz Ali Dossa.

Huwezi kuandika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika bila ya kuwataja hawa.

Kivukoni wamejaribu na matokeo yake ndiyo haya miaka 9 unauliza maswali.

Miaka 21 kitabu cha Abdul Sykes kinajadiliwa.

Hii sijaona popote katika uzoefu wangu wa vitabu.
 
Hivi unaweza kufanya ''citation ya maswali'' (Bandiko#31)
Hata hivyo kwa kukusaidia tu soma '' The life and times of Abdul Sykes (1924-1968)

Ngano miaka 9! Nilishakaa kimya, wewe na Alama Mohamed mkanialika, kuchungulia ninaona ushereheshaji wa historia unaendelea, nikaona nijisogeze si kulala jamvini bali kutafakari

Mimi si wale wa hewala, hongera, ahsante! hapana, nyote mnaelewa hilo

Jibu bandiko # 31 please
"Citation" ya uliposoma hayo uliyojengea maswali yako.. Maana si swali tu umekuja na hekaya ya 1948. Nayo haihitaji "citation"? Umeitoa wapi hiyo?

Basi tuchukulie siku 9 kama miaka 9 imekukera!

Huwa sikisii. Kumbuka hilo.
 
Nguruvi,
Nitakujibu katika hayo yote moja tu.

Mwanzo wa kitabu naanza kueleza historia ya familia tatu maarufu Dar es Salaam ambazo ndiyo zilitawala siasa - Sykes, Plantan na Aziz Ali Dossa.

Huwezi kuandika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika bila ya kuwataja hawa.

Kivukoni wamejaribu na matokeo yake ndiyo haya miaka 9 unauliza maswali.

Miaka 21 kitabu cha Abdul Sykes kinajadiliwa.

Hii sijaona popote katika uzoefu wangu wa vitabu.
Nani kakataa uwepo wa hao watu na siasa zao? AA na TAA zilikuwepo nini cha kubisha hapo. Watu unaowataja walikuwepo, nini cha kubisha hapo?

Kinachogomba ni kuwa unarudia makosa unayosema unayasahihisha.

Sijawahi kusoma wala kutilia maanani historia ya Kivukoni! Hilo tu linasababisha nijielimishe mwenyewe kuliko kusubiri hotuba , tamthilia, ngano au hekaya za wananchi wengine

Mohamed, kupitia kavazi la Mwalimu Nyerere na kavazi la Kleist hadi Abdul, unaweza kutuonyesha katiba za AA au TAA. Hili naliluliza kwenu mabingwa, nimekwama nisaidie
 
"Citation" ya uliposoma hayo uliyoukiza maswali. Maana si swali tu umekuja na hekaya ya 1948. Nayo haihitaji "citation"? Umeitoa wapi hiyo?

Huwa sikisii. Kumbuka hilo.
Unajitahidi! ningeshauri uendelee kusoma ...
 
Nani kakataa uwepo wa hao watu na siasa zao? AA na TAA zilikuwepo nini cha kubisha hapo. Watu unaowataja walikuwepo, nini cha kubisha hapo?

Kinachogomba ni kuwa unarudia makosa unayosema unayasahihisha.

Sijawahi kusoma wala kutilia maanani historia ya Kivukoni! Hilo tu linasababisha nijielimishe mwenyewe kuliko kusubiri hotuba , tamthilia, ngano au hekaya za wananchi wengine

Mohamed, kupitia kavazi la Mwalimu Nyerere na kavazi la Kleist hadi Abdul, unaweza kutuonyesha katiba za AA au TAA. Hili naliluliza kwenu mabingwa, nimekwama nisaidie
Utajielimisha bila nyaraka za akina Sykes? Utayatoa wapi? Hewani?

Hilo kavazi unàlolitaja limemuhusisha nani kuliandika?


Unauliza kuhusu katiba wakati wewe unasema kuwa "nijielimishe mwenyewe"? Sasa kinakushinda nini kujielimisha mwenyewe mpaka uje kumuuliza mtoa ngano? Angalia, ngano nyingi utavimbiwa.

Nje ya nyaraka za akina Sykes huna pengine pa kujielimisha kuhusu AA, TAA, TANU. Kama unapo tuoneshe na sisi tujielimishe.

Hapo sasa.
 
Habari za Mzee Said ni za kusoma kwa tahadhari.
kweli kabisa inabidi kusoma kwa tahadhari, Mohamed Saidi anamuelezea Nyerere kama mtu hohe hahe , mshamba ambae alipokewa dar na Abdul Sykes(alwatan wa mji) na abdul akamtambulisha Nyerere kwa wazee wa dar. Nyerere alivyoingia dar es salaam alikuwa hana sehemu ya kukaa, ikabidi akina Sykes wamuhifadhi nyumbani kwao kariakoo, Alikuwa hana hata senti tano ikabidi mke wa Abdul Sykes mama Daisy amfundishe mama Maria Nyerere kupika vitumbua ili aikimu familia yake,
 
kweli kabisa inabidi kusoma kwa tahadhari, Mohamed Saidi anamuelezea Nyerere kama mtu hohe hahe , mshamba ambae alipokewa dar na Abdul Sykes(alwatan wa mji) na abdul akamtambulisha Nyerere kwa wazee wa dar. Nyerere alivyoingia dar es salaam alikuwa hana sehemu ya kukaa, ikabidi akina Sykes wamuhifadhi nyumbani kwao kariakoo, Alikuwa hana hata senti tano ikabidi mke wa Abdul Sykes mama Daisy amfundishe mama Maria Nyerere kupika vitumbua ili aikimu familia yake,
Tuwekee nukuu wapi Allama Mohamed Said kamuelezea hivyo marehemu mzee Nyerere?

Au unajaribu kutusomesha ujinga?
 
kweli kabisa inabidi kusoma kwa tahadhari, Mohamed Saidi anamuelezea Nyerere kama mtu hohe hahe , mshamba ambae alipokewa dar na Abdul Sykes(alwatan wa mji) na abdul akamtambulisha Nyerere kwa wazee wa dar. Nyerere alivyoingia dar es salaam alikuwa hana sehemu ya kukaa, ikabidi akina Sykes wamuhifadhi nyumbani kwao kariakoo, Alikuwa hana hata senti tano ikabidi mke wa Abdul Sykes mama Daisy amfundishe mama Maria Nyerere kupika vitumbua ili aikimu familia yake,
Laki...
Haya umeyapata wapi?
Unaweza kuweka hapa kama ushahidi?
 
Back
Top Bottom