Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Abdul Sykes alichukua uongozi wa AA kwa kutumia vurugu na ubabe, hakukuwa na uchaguzi uliomuweka madarakani, nadhani hii ndio sababu iliyomfanya ashindwe kirahisi na Nyerere kwenye uchaguzi wa TAA. Abdul alikuwa kijana sana hakuwa na busara za uongozi
Laki...
Kabla ya mimi kueleza jinsi Schneider Abdillah Plantan alivyosimama kidete kumtoa kaka yake Thomas Saudtz Plantan katika uongozi wa TAA mwaka wa 1950 ili vijana Abdul na Dr. Kyaruzi wachukue uongozi kuna yeyote alikuwa anaijua historia hii?
 
Laki...
Kabla ya mimi kueleza jinsi Schneider Abdillah Plantan alivyosimama kidete kumtoa kaka yake Thomas Saudtz Plantan katika uongozi wa TAA mwaka wa 1950 ili vijana Abdul na Dr. Kyaruzi wachukue uongozi kuna yeyote alikuwa anaijua historia hii?
Kiukweli hii historia sikuwa naijua wewe ndio umenifungua mambo mengi, lakini pale kwenye mapungufu ndio na sisi tunarekebisha, mfano ni Abdul Sykes alipochukua madaraka kwa wapinduzi ya vurugu na ubabe, hukutujulisha, hapa ndio tunarekebisha.
 
kiukweli hii historia sikuwa naijua wewe ndio umenifungua mambo mengi, lakini pale kwenye mapungufu ndio na sisi tunarekebisha, mfano ni Abdul Sykes alipochukua madaraka kwa wapinduzi ya vurugu na ubabe, hukutujulisha, hapa ndio tunarekebisha
Laki...
Hii ni mara nyingine tena nakusisitizia usome kitabu cha Abdul Sykes kwani haya mapinduzi ya kuwatoa viongozi wa TAA Thomas Plantan na Clement Mtamila nimeeleza kwenye kitabu hicho na waliokwenda pale ofisini kuwatoa wazee hawa kwa nguvu walikuwa Hamza Mwapachu na Abdul Sykes.

Sasa unarekebisha nini ilhali historia hii ya mapinduzi mimi ndiyo niliyotafiti na kuandika.
Wewe unadai ati sikukujulisheni.

1574519862836.png

Thomas Plantan


 
May Day,

Unazijua Nyaraka za Sykes?

Mimi zimeniwezesha kuandika kitabu kizima kuhusu historia ya TAA na TANU na uhuru wa Tanganyika.

Kubwa zaidi zimeniwezesha kumjua Nyerere kuanzia siku ya kwanza anafika nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Aggrey na Sikukukuu mwaka wa 1952 akiongozana na Joseph Kasella Bantu.

Nyaraka hizi na kumbukumbu za Sykes zimeniwezesha kujua historia ya Chief David Kidaha Makwaia na Abdul Sykes katika juhudi ya kumpata kiongozi wa kuongoza TAA na kuunda TANU kati ya mwaka wa 1951 na 1953.

Ungejuaje kama Chief Kidaha alimtangulia Nyerere katika kufikiriwa kuongoza TANU kama si kumbukumbu hizi?

Ulikuwa unajua kuwa baada ya juhudi hizi kushindwa ndiyo Hamza akamtaka Abdul amsaidie Nyerere kuingia katika uongozi wa TAA 1953 katika kikao kilichofanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu Nansio na kuhudhuriwa na Abdul na Ali Mwinyi Tambwe?

1574527276077.png

Hamza Mwapachu na Abdul Sykes

Wazalendo hao wawili hapo juu wana historia ya kusisimua ukiisikia kwani hawa wawili ndiyo waliomleta Julius Nyerere katika ulingo wa siasa za TAA Dar es Salaam.

Ukijua historia za wazalendo hawa utakuwa umefungua mlango mpya katika historia ya Mwalimu Nyerere, TANU na historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hivi ushajiuliza kama nisingefunguliwa nyaraka hizi historia ya uhuru ingekuwaje si ingejaa nusu ukweli kama ilivyo katika kitabu kilichoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni?

Naamini unajua kuwa Nyaraka za Sykes hivi sasa zinaonyeshwa katika Kavazi la Mwalimu Nyerere kama nyaraka za kuaminika kuhusu historia ya Mwalimu Nyerere.

Angalia na jaribu kusoma hiyo barua ya mwaka wa 1953 na angalia ni nani walikuwa viongozi wa TAA kuelekea kuunda TANU:

 
May Day,
Unazijua Nyaraka za Sykes?

Mimi zimeniwezesha kuandika kitabu kizima kuhusu historia ya TAA na TANU na uhuru wa Tanganyika.

Kubwa zaidi zimeniwezesha kumjua Nyerere kuanzia siku ya kwanza anafika nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Aggrey na Sikukukuu mwaka wa 1952 akiongozana na Joseph Kasella Bantu.

Nyaraka hizi na kumbukumbu za Sykes zimeniwezesha kujua historia ya Chief David Kidaha Makwaia na Abdul Sykes katika juhudi ya kumpata kiongozi wa kuongoza TAA na kuunda TANU kati ya mwaka wa 1951 na 1953.

Ungejuaje kama Chief Kidaha alimtangulia Nyerere katika kufikiriwa kuongoza TANU kama si kumbukumbu hizi?

Ulikuwa unajua kuwa baada ya juhudi hizi kushindwa ndiyo Hamza akamtaka Abdul amsaidie Nyerere kuingia katika uongozi wa TAA 1953 katika kikao kilichofanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu Nansio na kuhudhuriwa na Abdul na Ali Mwinyi Tambwe?

View attachment 1270463
Hamza Mwapachu na Abdul Sykes

Wazalendo hao wawili hapo juu wana historia ya kusisimua ukiisikia kwani hawa wawili ndiyo waliomleta Julius Nyerere katika ulingo wa siasa za TAA Dar es Salaam.

Ukijua historia za wazalendo hawa utakuwa umefungua mlango mpya katika historia ya Mwalimu Nyerere, TANU na historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hivi ushaiuliza kama nisingefunguliwa nyaraka hizi historia ya uhuru ingekuwaje si ingejaa nusu ukweli kama ilivyo katika kitabu kilichoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni?

Naamini unajua kuwa Nyaraka za Sykes hivi sasa zinaonyeshwa katika Kavazi la Mwalimu Nyerere kama nyaraka za kuaminika kuhusu historia ya Mwalimu Nyerere.

Angalia na jaribu kusoma hiyo barua ya mwaka wa 1953 na angalia ni nani walikuwa viongozi wa TAA kuelekea kuunda TANU:

Ndugu Mzee Said,hapa kwa taarifa hii inaondoa vipi ukweli kwamba Mwalimu alianza siasa/harakati kabla ya kukutana na kina Sykes na timu yao?

Au inakanusha vipi kwamba Mwalimu alikuwa anawasiliana na watu wa Dar kuhusu siasa/harakati za uhuru?

Nadhani tunapopishana ni hivi unavyoegemea sana kwenye nyaraka za Sykes au maelezo ya kundi fulani. Hivi ni nani mwingine aliandika tofauti na Sykes na wachache?

Hakuna anayebeza mchango au nafasi ya kina Sykes na wenzake, ila bado kuna wengine nyuma waliokuwa na mchango na labda hawakupata nafasi ya kuandika kama Bw sykes, na hawa ndio wamekuwa mara kwa mara wakitajwa kama Wazee wa Dar, huenda hawakuwa na nafasi/uwezo kama kina Sykes ila sidhani kama ni sawa kuwapuuza na kung'ang'ana na kina Sykes na timu yao pekee.

Mwalimu alikuja Dar tayari akiwa anajua anataka nini, kutambulishwa kwa kina Sykes labda ilikuwa ni bahati tu na sidhani kama bila hivyo ingemzuia Mwalimu kuendelea na mission zake. Sasa kwa kuwa sykes haonyeshi/hakusema kama Mwalimu alikuwa na mawasiliano kabla ndio uitake na jamii yote iamini hivyo...kuna Wazee waliokuwa wanawasiliana na Mwalimu na sio kina Sykes.

Kingine kisichoeleweka kutoka kwako na nyaraka za Sykes ni hivi unavyoonyesha kana kwamba Mwalimu alitafutwa tu na kupewa kazi lakini huonyeshi yeye Mwalimu alikuja na nini hata kama Dar alikuwa mgeni, ugeni wa Dar sio ugeni wa siasa au mipango.
 
Ndugu Mzee Said,hapa kwa taarifa hii inaondoa vipi ukweli kwamba Mwalimu alianza siasa/harakati kabla ya kukutana na kina Sykes na timu yao?

Au inakanusha vipi kwamba Mwalimu alikuwa anawasiliana na watu wa Dar kuhusu siasa/harakati za uhuru?

Nadhani tunapopishana ni hivi unavyoegemea sana kwenye nyaraka za Sykes au maelezo ya kundi moja. Hivi ni nani mwingine aliandika tofauti na Sykes?

Hakuna anayebeza mchango au nafasi ya kina Sykes na wenzake, ila bado kuna wengine nyuma waliokuwa na mchango na labda hawakupata nafasi ya kuandika kama Bw sykes, na hawa ndio wamekuwa mara kwa mara wakitajwa kama Wazee wa Dar, huenda hawakuwa na nafasi/uwezo kama kina Sykes ila sidhani kama ni sawa kuwapuuza na kung'ang'ana na kina Sykes na timu yao pekee.

Mwalimu alikuja Dar tayari akiwa anajua anataka nini, kutambulishwa kwa kina Sykes labda ilikuwa ni bahati tu na sidhani kama bila hivyo ingemzuia Mwalimu kuendelea na mission zake. Sasa kwa kuwa sykes haonyeshi/hakusema kama Mwalimu alikuwa na mawasiliano kabla ndio uitake na jamii yote iamini hivyo...kuna Wazee waliokuwa wanawasiliana na Mwalimu na sio kina Sykes.

Kingine kisichoeleweka kutoka kwako na nyaraka za Sykes ni hivi unavyoonyesha kana kwamba Mwalimu alitafutwa tu na kupewa kazi lakini huonyeshi yeye Mwalimu alikuja na nini hata kama Dar alikuwa mgeni, ugeni wa Dar sio ugeni wa siasa au mipango.
May Day,
Sasa kama historia ni hiyo uliyoandika hapo juu nini kimesababisha kufutwa kwa mchango wa Sykes katika historia ya TANU?
 
Ni dhahiri wazee wa TAA walimuandaa Nyerere kuwa kiongozi wao toka yuko Tabora baada ya kuridhishwa na uwezo wake wa kiuongozi, wakamuita dar na kupokewa na familia ya Sykes, Hata akina Sykes walivyompokea Nyerere Dar walikuwa wanajua ndio kiongozi wao ajae wa TAA.
 
ni dhahiri wazee wa TAA walimuandaa Nyerere kuwa kiongozi wao toka yuko Tabora baada ya kuridhishwa na uwezo wake wa kiuongozi, wakamuita dar na kupokewa na familia ya Sykes, Hata akina Sykes walivyompokea Nyerere Dar walikuwa wanajua ndio kiongozi wao ajae wa TAA,
Mwalimu aliitwa au alikuja kufundisha Pugu?
 
ni dhahiri wazee wa TAA walimuandaa Nyerere kuwa kiongozi wao toka yuko Tabora baada ya kuridhishwa na uwezo wake wa kiuongozi, wakamuita dar na kupokewa na familia ya Sykes, Hata akina Sykes walivyompokea Nyerere Dar walikuwa wanajua ndio kiongozi wao ajae wa TAA,
Laki...
Unafanya maskhara.
 
Mag3 kulikoni? Wengine ''tulichutama mtoni kujisetiri, tukichelea kukimbizana ''
Sisi watu wa Pwani adabu zetu ni kuitika mwito tunapoitwa na Wakubwa kama wewe

Mohamed, utaweza kuwa na stara tuongee kidogo? Ni muda ati
Mwito wako niliupata, niliuitika kwa ukimya kwani wito ulijaa indhara

Naomba tuongee kwa point kwa maana ya hoja kwa hoja bila kuleta hadithi nje ya point
"Mohamed Said, post: 33552747, member: 12431"]
Hii ndiyo sababu ghadhabu zako unazielekeza kwangu kwa maneno makali ya ''ngano,'' ''uongo,'' na lugha za kejeli kama ''ngumi na ''mateke,'' nk.
Mohamed,ngano ni tamthilia iliyosadifu(series). Uongo ni neno linaloonyesha kinyume cha ukweli, si tusi

''Ngumi na mateke'' inaturudisha katika kitabu chako (Nyakati za Abdulwahid Sykes) ambako umeeleza Abdul na wenzie kuvamia ofisi na kuchukua madaraka kwa nguvu.

Hapakuwepo na kanuni wala Katiba na kwa mantiki yako maneno nguvu na kuvamia hujafafanua ikiwa waliwachapa wazee wao viboko, waliwatia madole ya macho ama...

Hadi hapo utakapofafanua, sioni matumizi ya 'ngumi na mateke'' ya Mag3 kama yana matatizo. Mag3 amekuwa specific hadi utakapomthibitisha vinginevyo, wewe umetumia lugha laini, mantiki yenu ni ile ile, Abdulwahid Sykes Kleist Mbuwane aliwatimua wazee wetu wa Dar es Salaam kwa nguvu
Nyerere hakuwa kiongozi wa TAA Tabora 1945.
Tarehe 3 Machi, 1945 African Association mjini Tabora ilifungua ofisi yake ikiwa na na viongozi wafuatao: Hamisi Simbe (Rais), Ramadhani Nasibu (Makamu wa Rais), M. K. Hemed (Katibu), Chamng'anda Usingizi (Mwenyekiti), Fimbo Mtwana (Mweka Hazina) na Rashidi Mussa (Mkaguzi wa Hesabu).
Tarehe 3/3/1945 ni siku ofisi ipofunguliwa, fair enough!
1. Hao viongozi walidumu katika madaraka kwa muda gani?
2. Mwalimu aliingia katika uongozi lini na kwa utaratibu gani
Julius Nyerere, wakati huo akifundisha St. Mary's School, alishuhudia sherehe za uzinduzi wa African Association.
Rejea # 2 hapo juu
3. Mwaka 1945 kulikuwa a matawi mangapi ya chama wakati huo Tanganyika
4. Mkutano mkuu wa mwaka 1948 Dar es Salaam nani alihudhuria kutoka tawi jipya Tabora(3/3/1945) miongoni mwa Waanzilishi uliowataka hapo juu.

Tuanzie hapa halafu tutaendelea kuteta jamvini.
 
Mag3 kulikoni? Wengine ''tulichutama mtoni kujisetiri, tukichelea kukimbizana ''
Sisi watu wa Pwani adabu zetu ni kuitika mwito tunapoitwa na Wakubwa kama wewe

Mohamed, utaweza kuwa na stara tuongee kidogo? Ni muda ati
Mwito wako niliupata, niliuitika kwa ukimya kwani wito ulijaa indhara

Naomba tuongee kwa point kwa maana ya hoja kwa hoja bila kuleta hadithi nje ya point
Mohamed,ngano ni tamthilia iliyosadifu(series). Uongo ni neno linaloonyesha kinyume cha ukweli, si tusi

''Ngumi na mateke'' inaturudisha katika kitabu chako (Nyakati za Abdulwahid Sykes) ambako umeeleza Abdul na wenzie kuvamia ofisi na kuchukua madaraka kwa nguvu.
Hakukuwepo na kanuni wala Katiba na kwa mantiki yako maneno nguvu na kuvamia hujafafanua ikiwa waliwachapa wazee wao viboko, waliwatia madole ya macho ama...

Hadi hapo utakapofafanua, sioni matumizi ya 'ngumi na mateke'' ya Mag3 kama yana matatizo. Mag3 amekuwa specific wewe umetumia lugha laini, mantiki yenu ni ile ile Tarehe 3/3/1945 ni siku ofisi ipofunguliwa, fair enough!
1. Hao viongozi walidumu katika madaraka kwa muda gani?
2. Mwalimu aliingia katika uongozi lini na kwa utaratibu gani
Rejea # 2 hapo juu
3. Mwaka 1945 kulikuwa a matawi mangapi ya chama wakati huo Tanganyika
4. Mkutano mkuu wa mwaka 1948 Dar es Salaam nani alihudhuria kutoka tawi jipya Tabora(3/3/1945) miongoni mwa Waanzilishi uliowataka hapo juu.

Tuanzie hapa halafu tutaendelea kuteta jamvini.
Nguruvi3,
Unaniita tujadili kitabu kilichochapwa miaka 21 iliyopita?

Mbona mlikuwa kimya hamkujadili kitabu cha historia ya TANU (1981)kilichoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni kilichowafuta wazalendo waasisi wa TANU?

Unataka tujadili historia ya TANU leo baada ya miongo miwili tena tujadili historia ambayo nyote nyie hamkuijua ila baada ya kuandikwa na mimi?

Mimi nawasihi mbakie na ile historia yenu iliyomfuta Abdul Sykes.

Hiyo ndiyo historia rasmi lazima tuiheshimu.
 
Nguruvi3,
Unaniita tujadili kitabu kilichochapwa miaka 21 iliyopita?

Mbona mlikuwa kimya hamkujadili kitabu cha historia ya TANU (1981)kilichoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni kilichowafuta wazalendo waasisi wa TANU?

Unataka tujadili historia ya TANU leo baada ya miongo miwili tena tujadili historia ambayo nyote nyie hamkuijua ila baada ya kuandikwa na mimi?

Mimi nawasihi mbakie na ile historia yenu iliyomfuta Abdul Sykes.

Hiyo ndiyo historia rasmi lazima tuiheshimu.
Ah Mohamed, ghadhabu za nini asbuhi hii Sheikh. Pata funda la maji muungwana

Majuzi si ulinialika hapa kwa indhara, kipi kimebadilika tena

Kwani tumeanza leo mimi na wewe! Kuanzia 2010 tupo kitako jamvini na kwa maneno yako mwenyewe! Wiki mbili zilizopita ukanialika. Mbona hamaki?

Mzee Said, tukae kitako watu wazima tuyazungumze kwa stara

Turejee bandiko #31 sheikh!
 
kweli mkuu, Nyerere alivyotoka Tabora, alikuja Dar kufundisha Pugu, tatizo Mohamed Said anatuambia alikuja dar kwa ajili ya kuingizwa TAA, hapo ndio nikachanganya,
Habari za Mzee Said ni za kusoma kwa tahadhari.
 
Ah Mohamed, ghadhabu za nini asbuhi hii Sheikh. Pata funda la maji muungwana

Majuzi si ulinialika hapa kwa indhara, kipi kimebadilika tena

Kwani tumeanza leo mimi na wewe! Kuanzia 2010 tupo kitako jamvini na kwa maneno yako mwenyewe! Wiki mbili zilizopita ukanialika. Mbona hamaki?

Mzee Said, tukae kitako watu wazima tuyazungumze kwa stara

Turejee bandiko #31 sheikh!
Nguruvi3,
Hiyo si lugha ya ghadhabu hata kidogo.
Nimekualika au nimekutaja?

Jina la Abdulwahid Kleist Sykes ndiyo hilo sasa mmefahamu na Mwalimu alikisoma kitabu tena alipelekewa na kijana aliyeoa katika familia yake ambae mimi ni rafiki yangu.

Baada ya kukisoma Mwalimu alizungumza na huyu rafiki yangu.

Prof. Haroub Othman aliomba miadi na Mwalimu wazungumze kuhusu kitabu changu na cha Ali Muhsin Barwani, "Conflict and Harmony in Zanzibar."

Prof. kamuomba Mwalimu na yeye aandike kutujibu.

Hivi sasa rafiki zangu wananiweka katika shinikizo niandike kitabu kingine kuhusu haya na mengine yaliyotokea kutoka kitabu cha Abdul Sykes na mihadhara niliyofanya kueleza upya historia ya TANU.

Wewe unanirudisha nyuma nimjadili Mwalimu Nyerere ambae tayari nimeshaandika historia yake.

Mwaka jana radio, televisheni na magazeti walinipa uwanja kuadhimisha miaka 50 ya kifo cha Abdul Sykes naamini ulibahatika kusoma mfululizo wa makala zilizochapwa na Raia Mwema alizoandika bint yake Aisha "Daisy"Sykes.

Daisy aliwaeleza vizuri sana Abdul Sykes, Hamza Mwapachu na Julius Nyerere alivyokuwa akiwaona nyumbani kwao wakati ule 1950s yeye bint mdogo akisikiliza mazungumzo yao.

Kila wafikapo wageni kwangu haya ndiyo wanayoshinikiza niandike.
Wewe unanirejesha kwenye kitabu kinachokwenda toleo la nne tena unataka tufanye mjadala.
 

Attachments

  • SYKES BOOK ALL EDITIONS.jpg
    SYKES BOOK ALL EDITIONS.jpg
    54.1 KB · Views: 2
  • SHEIKH ALI MUHSIN BARWANI.JPG
    SHEIKH ALI MUHSIN BARWANI.JPG
    23.2 KB · Views: 2
  • DAISY POTRAIT.jpg
    DAISY POTRAIT.jpg
    4.3 KB · Views: 2
  • HAMZA MWAPACHU NA ABDUL SYKES.png
    HAMZA MWAPACHU NA ABDUL SYKES.png
    24.8 KB · Views: 2
kweli mkuu, Nyerere alivyotoka Tabora, alikuja Dar kufundisha Pugu, tatizo Mohamed Said anatuambia alikuja dar kwa ajili ya kuingizwa TAA, hapo ndio nikachanganya,
Laki,
Sijasema maneno hayo.
 
Habari za Mzee Said ni za kusoma kwa tahadhari.
May Day,
Umenifurahisha sana kwa kusema nahitaji tahadhari kusomwa.

Kuna rafiki yangu yeye anapenda sana kunisoma nami namuheshimu sana kwa akili zake.

Yeye huniambia maneno haya, ''Mohamed kalamu yako inakata kama upanga wa Sayyidna Ali.''

Haya May Day nini tena kimezidi?''

Ikiwa kusema kuwa nimesema kuwa Nyerere aliitwa Dar es Salaam kuingizwa TAA hilo nimekanusha kuwa sijasema kitu kama hicho na kama ushahidi upo na uletwe tuusome.
 
Laki,
Sijasema maneno hayo.
Mohamed Said, uko hapa kwa ajili ya kutupa darsa kuhusu wapigania uhuru wa tanganyika waliosahaulika, umebadili fikra za watu wengi sana kwa elimu yako, wengine ndio tumeujua mchango wa akina Sykes kupitia wewe, kwa heshima uliyojijengea naomba ujibu maswali ya nguruvi3 hapo juu ili tuendelee kupata elimu hii adhimu, inawezekana ukawa mkombozi kwa kutupa historia ya kweli na siku moja kitabu cha Sykes kikaja kutumika kwenye mitaala ya elimu mashuleni, tafadhali usikwepe maswali tupe majibu tuendelee kujifunza
 
Mohamed Said, uko hapa kwa ajili ya kutupa darsa kuhusu wapigania uhuru wa tanganyika waliosahaulika, umebadili fikra za watu wengi sana kwa elimu yako, wengine ndio tumeujua mchango wa akina Sykes kupitia wewe, kwa heshima uliyojijengea naomba ujibu maswali ya nguruvi3 hapo juu ili tuendelee kupata elimu hii adhimu, inawezekana ukawa mkombozi kwa kutupa historia ya kweli na siku moja kitabu cha Sykes kikaja kutumika kwenye mitaala ya elimu mashuleni, tafadhali usikwepe maswali tupe majibu tuendelee kujifunza
Laki...
Mimi nikwepe maswali!
Hayo si maswali bali ni ubishi.

Mmanyema mmoja anabishana na mwenzake anamuuliza yule simba wa Agip katika nembo ana miguu mingapi?

Mwenzake akamtajia.
''Muongo wewe hujui hesabu yake.''

Mwisho wakaamua waende kituo cha Agip wakahesabu miguu ya simba wamalize ubishi.
Sasa kweli natakiwa nitoe jibu la matawi ya African Association Tanganyika nzima!

Nimemjibu kila swali alilopatapo kuniuliza.
Umesoma anasema yeye na mimi tuko katika mjadala huu sasa mwaka wa 9.

Nguruvi 3 ndugu yangu anateseka na kile ambacho hakukijua toka awali kama alivyoteseka mwalimu wangu Prof. Haroub Othman.

Abdul Sykes na historia yake katika uhuru wa Tanganyika na uhusiano wake na Mwalimu Nyerere imewashangaza watu wengi hata wasomi wa African History Ulaya na Marekani kiasi wamemtia baba yake katika Dictionary of African History (DAB).

Prof. Haroub yeye alichofanya kwanza ilikuwa ni kupata kauli ya Mwalimu kuhusu historia yake katika kuunda TANU na kutaka kujua kutoka kinywa cha Mwalimu kuhusu Abdul Sykes.

Hakuishia hapo alimfata Ahmed Rashad Ali rafiki kipenzi wa Abdul Sykes kutaka kusikia historia ya Abdul Sykes.

Prof. hakuweza kuamini yale niliyoandika katika kitabu alitaka ushahidi zaidi.
Mwalimu wangu hapa ndipo alipozidi kuchanganyikiwa zaidi bora angebakia na yale yangu.

Ahmed Rashad Ali alisema, ''Unastaajabishwa na Abdul kuunda TANU 1954 kwa nini hustaajabishwi na baba yake kuasisi African Association 1929?''

Ikiwa hii ndiyo historia ya Abdul Sykes sasa mimi nijibu nini?
Umesikia nini kasema Ahmed Rashad.

Kaulizwa swali karejesha swali kwa muulizaji.

Ahmed Rashad anatoka katika nyumba ya masultani wa Zanzibar na yeye na Abdul walikuwa marafiki toka mwaka wa 1939 Abdul akiwa na umri miaka 15 na Rashad 22.
 

Attachments

  • PROF. HAROUB OTHMAN, AHMED RASHAD NA SHEIKH AHMED ISLAM.jpg
    PROF. HAROUB OTHMAN, AHMED RASHAD NA SHEIKH AHMED ISLAM.jpg
    18.7 KB · Views: 2
Back
Top Bottom