Suluhisho la Kudumu la Mgogoro wa Maziwa Makuu (Rwanda, Congo et al) ni kutenga na kupata nchi ya hao waliopo hapo sasa (North Kivu)

Suluhisho la Kudumu la Mgogoro wa Maziwa Makuu (Rwanda, Congo et al) ni kutenga na kupata nchi ya hao waliopo hapo sasa (North Kivu)

Logikos

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
15,460
Reaction score
24,233
Kwanza kabisa mimi sio Mtaalamu na baada ya kuangalia kwa haraka matakwa ya pande tofauti nimeona ni vigumu sana kwa upande mmoja kukubaliana na matakwa ya upande mwingine kutokana na usalama wao na kutokuaminiana; Hivyo Suluhisho pekee ni hapo katikati kuwepo na nchi ya hao waliomo. Kwa kufahamu vizuri ugumu wa mgogoro huu ni vema ukauangalia katika mtizamo (perspective) ya watu Husika;

Watutsi ambao ni Wakongo (Ambao Watu wa Congo wanasema ni Wanyarwanda na warudi Kwao):
  • Kumbuka hawa kabla ya wakoloni kuweka mipaka yao baadhi yao walikuwepo hapo, kwahio kuwepo kwao Congo sasa hivi sio kwamba wote walikuja bali walijikuta wamewekwa Congo; Kwahio hawa kwa mtizamo wao ni Wakongo
  • Hawa watu wananyanyaswa kwamba sio Wakongo na warudi kwao, Sasa kwao wapi sababu ukiwafukuza je unawafukuza na ardhi ?
  • Hawa watu wanachotaka wao ni kuwa na haki sawa kama wakongo na uwezo wa kupiga kura n.k, jambo ambalo wakongo hawataki kuwapa (na wana hoja sababu kwa macho yao hawa ni mamluki)
  • Hao askari wa M23 nao wanataka wawe assimilited kwenye jeshi la Congo (jambo ambalo sidhani kama Congo watakubali)

Nchi ya Congo
  • Wao wanaona hawa sio raia wala wakongo na kwao wanaweza kuwa hatari kwa usalama wa nchi kama mapandikizi, na pia wanaona wanatumika kama nyenzo ya kuwaibia na pia kikundi cha M23 ambacho kinasema kinawalinda watutsi hao kwa Congo kundi hili ni magaidi.
  • Kwa Rais wa Congo kukubali hawa watu waingizwe nchini na kupewa kila haki hata yeye akikubali kuna watu wa Congo ambao watamuona kama msaliti, na vilevile kwa macho yake hii ni hatari ya kuleta mamluki (watu ambao wewe unaona sio Watu wako katika nchi yako).
  • Congo wanaona M23 ni kama nyenzo ya Rwanda kuwaingilia na ukizingatia hata Kabila alivyochukua nchi alipata msaada wa hawa watu na wakitokea Uganda na kumuondoa Mobutu utaona kwamba Rais wa Congo ana hoja za msingi za kutokukubaliana na assimilation ya hawa watu Congo.

Nchi ya Rwanda:
Kumbuka nchi ya Rwanda Kagame alivyochukua nchi kuna wale watu ambao inasemekana ndio walihusika na mauaji ya Kimbari pamoja na Waliokuwa ndio wanaongoza nchi walikimbilia Congo na kupokelewa Congo, na Ufaransa pamoja na Mobutu kuwafundisha zaidi ili waweze kurudi Rwanda na kumpindua Kagame; Ingawa Kagame na yeye kuona hivyo akatumia Watutsi waliopo Congo kuwafundisha ili kuweza kuwakabili hao anaowaona ni waasi (hivyo matatizo ya Rwanda ni kama yakahamia Congo).

Kwahio ni ngumu kwa Kagame kuona kuna Watutsi wanaonyanyaswa Congo wakati yeye aliingia kwenye madaraka kwa kuonyesha kwamba anamaliza manyanyaso hayo; Na Tukisema hao Watutsi warudi Rwanda, je warudi wapi ukizingatia wengine wapo hapo tangia enzi na enzi ? Pia Kagame lazima jicho lake litakuwa Congo sababu anaona kuna uwezekano wa kuvamiwa kutokea Congo

Uganda:
Uganda pia na yeye yupo macho sababu kunaweza kutokea waasi wowote kutokea Congo kuleta machafuko Uganda ukizingatia community hizi kuna watu ambao walikimbia kutoka Congo kwenda Uganda na wanaweza kurudi wakati wowote na vice versa

Tanzania:
Shida yoyote ya jirani yako pia ni ya kwako mfarakano wowote utakaotokea huko lazima na wewe utakufikia; Pia kuna ndugu zetu Wanyarwanda na Warundi wengi zaidi ambao walikuja huko baada ya shida za huko kwao, shida zinazotokea huko huenda zikaanza kupelekea hawa ndugu zetu kutengwa na kunyanyaswa kama vile watusi wa Congo wanavyoonekana ni matatizo na waleta shida.

Hitimisho
Hitimisho pekee na la kudumu, ni hawa watu waliopo sasa hapo North Kivu (Jamii zote) waweze kupata nchi yao hapo hapo na nchi zote za maziwa makuu na kwa kushirikiana zinaweza zikawa na Base ya kuangalia Amani hapo, na kuhakikisha vinatokomeza vikundi vyote vya Kuasi (Magaidi hata kama wanajiita Freedom Fighters) na vya aina yoyote kwa kuwa assimiliate katika nchi yao hii mpya. Na kuhakikisha hakuna masalia ambayo yanaweza kuanzia hapo na kuleta shida yoyote au kutishia Amani katika nchi Jirani.

Suala hili inabidi sisi kama Waafrika tusaidiane kulimaliza na kabla ya Afrika sisi majirani kwanza (Maziwa Makuu)
 
Hakuna kugawa ardhi, nchi ya wacongo sio wahutu au watusi
Nani kasema ugawe Ardhi ? Waliopo hapo ndio wataendelea kuwapo hapo, sababu alternative ni kwamba watusi waliopo hapo wanataka haki sawa kama raia ya hapo waliopo sababu kabla wakoloni hawajapagawa walikuwepo hapo hapo.., sasa je unadhani Congo itakubali kuwa assimilate kwenye Taifa lao na kutambulika mpaka Kinshasha na bila kuwanyanyasa (sababu hio ndio alternative) ukisema waondoke Je waondoke na Ardhi iliyopo chini ya Miguu yao ?
 
Yani hao wanyamulenge waliokimbia vita Rwanda na kulowea hapo kivu ndo wasababishe nchi igawiwe?? Hiyo hapana.,, kivu ni ya wakongo hao wakishindwa kukaa hapo warudi kwao Rwanda
Hivi unajua kuna watu ambao sio kwamba walikimbilia hapo bali walijikuta wamegawiwa kwenda Congo baada ya wakoloni kujigawia Africa ? Sasa kipi bora uwatenge sasa hivi na wajitegemee au uendelee kutegemea kuongezeka na wengine ambao hawakuwepo tangia mwanzo, sababu kwao ni rahisi kwenda sehemu ambapo culturally kuna watu kama wao...

Issue kama hii ni kama ukisema wamasai wa Kenya au Tanzania waondoke, Je waondoke kwenda wapi ?
 
Kabla hujafika hapo jiulize hao Jamaa ni asilimia ngapi ya Congo?

Population yao ni laki 4 kwenye watu Million 100 hawafiki hata Asilimia 1 ya nchi.

Ugawe nchi uwape kipande kikubwa Asilimia 0.5 ya watu kilichobakia wapewe Asilimia 99.5? Ni ujinga kiwango cha lami.

Na ukiona matakwa ya M23 ndio utaona hawana time na Amani ni vitu visivyomake sense kabis.
 
Hawaridhiki wale, wanataka kutwaa nchi nzima ya congo. Hata ukimega nchi ya congo mashariki na kuwapa watataka kujitanua kwenye nchi zingine kama Tanzania, kigoma, katavi, kagera na tabora watataka iwe yao washenzi wale
 
Hivi unajua kuna watu ambao sio kwamba walikimbilia hapo bali walijikuta wamegawiwa kwenda Congo baada ya wakoloni kujigawia Africa ? Sasa kipi bora uwatenge sasa hivi na wajitegemee au uendelee kutegemea kuongezeka na wengine ambao hawakuwepo tangia mwanzo, sababu kwao ni rahisi kwenda sehemu ambapo culturally kuna watu kama wao...

Issue kama hii ni kama ukisema wamasai wa Kenya au Tanzania waondoke, Je waondoke kwenda wapi ?
Wamsai Wana demand ya kupewa nusu ama robo ya nchi? Hawana so mfano sio sahihi.
 
For those interested haya matakwa ya M23



M23’s Demands in the DRC – Are They Justified for Peace?​

The M23 rebel group, which has been fighting the Democratic Republic of Congo (DRC) for years, has made a list of demands to the Congolese government in exchange for peace. These demands would significantly alter the country’s governance, military structure, and territorial administration, particularly in the eastern DRC, where conflicts have raged for decades.
Here’s what they are asking for:
  1. Military control: The government would give 43% of command positions in North Kivu and 39% in South Kivu to the Tutsi community.
  2. Border security: A new M23-controlled police force would handle security along DRC’s borders with Rwanda and Uganda.
  3. Special autonomy for Eastern DRC: The provinces of North Kivu, South Kivu, Ituri, Maniema, Haut-Uele, and Tanganyika (which cover 23.3% of the DRC’s total land area of 2,345,409 km²) would get special status, financial autonomy, and security under M23 control.
  4. Political control: M23 would be allowed to appoint administrators, mayors, and local leaders in certain areas.
  5. Integration into government institutions: M23 members would be placed in the Presidency, Parliament, Judiciary, and other top government bodies.
  6. Recognition of M23 military ranks: Their fighters would be formally integrated into the Congolese army and police.
  7. Return of Tutsi refugees: The Congolese government would be responsible for bringing back Congolese Tutsi refugees from Rwanda, Uganda, Kenya, and Tanzania.
 
Wamsai Wana demand ya kupewa nusu ama robo ya nchi? Hawana so mfano sio sahihi.
Sio kila demand mtu unapewa na lazima mwisho wa siku unaangalia implications hao watusi wanataka kupewa Haki kamili kama wakongo; kuna ambao hapo ni kwao na hawajawahi kwenda hata Rwanda hio ni haki yao; ila pia ni shida kwa Congo kukubali sababu huenda ukiwaachia hawa wachache kesho na kesho kutwa wakazidi wengine na bila kuwa na Uhamiaji wa uhakika hilo ni tatizo la kesho na kesho kutwa; Sasa kipi ni bora kuwaachia hapo walipo pawe kwao na wajinafasi wanavyotaka au undelee kuwa nao wakati wote hamuaminiani na mnashutumiana

Under the rule of Mobutu Sese Seko, the Banyarwanda were not considered citizens of Congo despite many of them having lived in Kivu since long before Congoan independence, and even colonization. In 1972, they were granted citizenship rights. However, this was rescinded in 1981, though it was never made into law. In practice, they have had no voting rights and no representation. Since the takeover of Congo by Laurent Kabila in May 1997, there has been no formal change of policy. As of 2003, the issue of citizenship for the Bayarwnada has been left to the Transitional Government, created in June of 2003.
 
Una hoja ya msingi,
Congo igwanywe tu kwa sababu imeshindwa kutawalika kutokea Kinshasa, DRC Mashariki wapewe nchi yao.
 
Kabla hujafika hapo jiulize hao Jamaa ni asilimia ngapi ya Congo?

Population yao ni laki 4 kwenye watu Million 100 hawafiki hata Asilimia 1 ya nchi.

Ugawe nchi uwape kipande kikubwa Asilimia 0.5 ya watu kilichobakia wapewe Asilimia 99.5? Ni ujinga kiwango cha lami.

Na ukiona matakwa ya M23 ndio utaona hawana time na Amani ni vitu visivyomake sense kabis.
Haijalishi, hata kama wangekuwa wawili tu mume na mke, suluhisho ni kuwapa haki zote za raia wa Congo au kwapa nchi yao wajitawale.
 
For those interested haya matakwa ya M23



M23’s Demands in the DRC – Are They Justified for Peace?​

The M23 rebel group, which has been fighting the Democratic Republic of Congo (DRC) for years, has made a list of demands to the Congolese government in exchange for peace. These demands would significantly alter the country’s governance, military structure, and territorial administration, particularly in the eastern DRC, where conflicts have raged for decades.
Here’s what they are asking for:
  1. Military control: The government would give 43% of command positions in North Kivu and 39% in South Kivu to the Tutsi community.
  2. Border security: A new M23-controlled police force would handle security along DRC’s borders with Rwanda and Uganda.
  3. Special autonomy for Eastern DRC: The provinces of North Kivu, South Kivu, Ituri, Maniema, Haut-Uele, and Tanganyika (which cover 23.3% of the DRC’s total land area of 2,345,409 km²) would get special status, financial autonomy, and security under M23 control.
  4. Political control: M23 would be allowed to appoint administrators, mayors, and local leaders in certain areas.
  5. Integration into government institutions: M23 members would be placed in the Presidency, Parliament, Judiciary, and other top government bodies.
  6. Recognition of M23 military ranks: Their fighters would be formally integrated into the Congolese army and police.
  7. Return of Tutsi refugees: The Congolese government would be responsible for bringing back Congolese Tutsi refugees from Rwanda, Uganda, Kenya, and Tanzania.
Kama hao watusi wataacha kunyanyaswa au kupewa uraia kama raia wengine (jambo ambalo ni gumu kupewa) hivyo hapo walipo wakiwa na nchi yao tofauti basi hakuna haja ya kuwa na M23 labda liwepo jesho la hio nchi kama nchi na vikundi vyote vya waasi na likiwemo hilo liweze kuondolewa hayo madai ni unrealistic
 
Kongo unatakiwa kuimarisha jeshi lake,kwenye hayo maeneo wawe na base kubwa ya kijeshi.wanatakiwa wawe na vifaa kama drones vya kumonitor mpaka wao wa mAshariki wajue ni nini kinachoingia kwenye ardhi yao.pia wanatakiwa kuimarisha mfumo wao wa kiintelijensia kwa kuongeza idadi ya watu kwenye idara hizo.na kama wataweza basi wahamishe watu kwenye hayo maeneo
 
Haijalishi, hata kama wangekuwa wawili tu mume na mke, suluhisho ni kuwapa haki zote za raia wa Congo au kwapa nchi yao wajitawale.
Kwa hio upo tayari kutoa 23% ya Nchi kwa watu wawili?

Assume tu leo waarabu ama wahindi wadai Znz ama Dar ama wairan wadai Kilwa huo mtiti wake utakaotokea hapa,

Hakuna mtu anaekataa watu kudai Haki zao, ila tunajua Fika Kagame na Genge lake wanadai Madini na Sio haki za raia. Kutaka 23% ya nchi igawanywe na viongozi wawe watusi ni demand za kipuuzi.
 
Kwanza kabisa mimi sio Mtaalamu na baada ya kuangalia kwa haraka matakwa ya pande tofauti nimeona ni vigumu sana kwa upande mmoja kukubaliana na matakwa ya upande mwingine kutokana na usalama wao na kutokuaminiana; Hivyo Suluhisho pekee ni hapo katikati kuwepo na nchi ya hao waliomo. Kwa kufahamu vizuri ugumu wa mgogoro huu ni vema ukauangalia katika mtizamo (perspective) ya watu Husika;

Watutsi ambao ni Wakongo (Ambao Watu wa Congo wanasema ni Wanyarwanda na warudi Kwao):
  • Kumbuka hawa kabla ya wakoloni kuweka mipaka yao baadhi yao walikuwepo hapo, kwahio kuwepo kwao Congo sasa hivi sio kwamba wote walikuja bali walijikuta wamewekwa Congo; Kwahio hawa kwa mtizamo wao ni Wakongo
  • Hawa watu wananyanyaswa kwamba sio Wakongo na warudi kwao, Sasa kwao wapi sababu ukiwafukuza je unawafukuza na ardhi ?
  • Hawa watu wanachotaka wao ni kuwa na haki sawa kama wakongo na uwezo wa kupiga kura n.k, jambo ambalo wakongo hawataki kuwapa (na wana hoja sababu kwa macho yao hawa ni mamluki)
  • Hao askari wa M23 nao wanataka wawe assimilited kwenye jeshi la Congo (jambo ambalo sidhani kama Congo watakubali)

Nchi ya Congo
  • Wao wanaona hawa sio raia wala wakongo na kwao wanaweza kuwa hatari kwa usalama wa nchi kama mapandikizi, na pia wanaona wanatumika kama nyenzo ya kuwaibia na pia kikundi cha M23 ambacho kinasema kinawalinda watutsi hao kwa Congo kundi hili ni magaidi.
  • Kwa Rais wa Congo kukubali hawa watu waingizwe nchini na kupewa kila haki hata yeye akikubali kuna watu wa Congo ambao watamuona kama msaliti, na vilevile kwa macho yake hii ni hatari ya kuleta mamluki (watu ambao wewe unaona sio Watu wako katika nchi yako).
  • Congo wanaona M23 ni kama nyenzo ya Rwanda kuwaingilia na ukizingatia hata Kabila alivyochukua nchi alipata msaada wa hawa watu na wakitokea Uganda na kumuondoa Mobutu utaona kwamba Rais wa Congo ana hoja za msingi za kutokukubaliana na assimilation ya hawa watu Congo.

Nchi ya Rwanda:
Kumbuka nchi ya Rwanda Kagame alivyochukua nchi kuna wale watu ambao inasemekana ndio walihusika na mauaji ya Kimbari pamoja na Waliokuwa ndio wanaongoza nchi walikimbilia Congo na kupokelewa Congo, na Ufaransa pamoja na Mobutu kuwafundisha zaidi ili waweze kurudi Rwanda na kumpindua Kagame; Ingawa Kagame na yeye kuona hivyo akatumia Watutsi waliopo Congo kuwafundisha ili kuweza kuwakabili hao anaowaona ni waasi (hivyo matatizo ya Rwanda ni kama yakahamia Congo).

Kwahio ni ngumu kwa Kagame kuona kuna Watutsi wanaonyanyaswa Congo wakati yeye aliingia kwenye madaraka kwa kuonyesha kwamba anamaliza manyanyaso hayo; Na Tukisema hao Watutsi warudi Rwanda, je warudi wapi ukizingatia wengine wapo hapo tangia enzi na enzi ? Pia Kagame lazima jicho lake litakuwa Congo sababu anaona kuna uwezekano wa kuvamiwa kutokea Congo

Uganda:
Uganda pia na yeye yupo macho sababu kunaweza kutokea waasi wowote kutokea Congo kuleta machafuko Uganda ukizingatia community hizi kuna watu ambao walikimbia kutoka Congo kwenda Uganda na wanaweza kurudi wakati wowote na vice versa

Tanzania:
Shida yoyote ya jirani yako pia ni ya kwako mfarakano wowote utakaotokea huko lazima na wewe utakufikia; Pia kuna ndugu zetu Wanyarwanda na Warundi wengi zaidi ambao walikuja huko baada ya shida za huko kwao, shida zinazotokea huko huenda zikaanza kupelekea hawa ndugu zetu kutengwa na kunyanyaswa kama vile watusi wa Congo wanavyoonekana ni matatizo na waleta shida.

Hitimisho
Hitimisho pekee na la kudumu, ni hawa watu waliopo sasa hapo North Kivu (Jamii zote) waweze kupata nchi yao hapo hapo na nchi zote za maziwa makuu na kwa kushirikiana zinaweza zikawa na Base ya kuangalia Amani hapo, na kuhakikisha vinatokomeza vikundi vyote vya Kuasi (Magaidi hata kama wanajiita Freedom Fighters) na vya aina yoyote kwa kuwa assimiliate katika nchi yao hii mpya. Na kuhakikisha hakuna masalia ambayo yanaweza kuanzia hapo na kuleta shida yoyote au kutishia Amani katika nchi Jirani.

Suala hili inabidi sisi kama Waafrika tusaidiane kulimaliza na kabla ya Afrika sisi majirani kwanza (Maziwa Makuu)
Iyo kivu ina madini muhimu sana so kuifanya iwe nchi Congo hawezi kukubali Kupoteza Rasilimali kirahisi ivo.
Hao Banyamulenge wakubali kutulia apo Congo na wapewe haki zao ila sio Ardhi.
 
Nchi ibaki kwa wenye nayo, wakongo na hao wengine wabaki huko walipotokea, Rwanda, Burundi, Uganda n.k
Haya mambo ya watusi na wahutu yakifumbiwa macho siku za usoni itatokea balaa kubwa.
Kwa sasa hapa Tanzania hao jamaa wamejaa kule Karagwe na Kyelwa,na wanaishi bila shida.
Najua ipo siku watataka utawala wao rasmi na hapo ndipo tz itakuwa kama Congo.
 
Yani nyie Watusi mnacho taka ule Mkataba wa lemera utimie.
Ili mfaidike na Matunda ya Ardhi ya Wakongomani,mlimsaidia Raisi kabila akawatosa sasa Mishipa ya shingo inawatoka mnakuja kutafuta huruma uku Tz.
“Kwa Mtego huo uwe wa kutumwa au wa bahati mbaya hatutouwingia kamwe”
 

Attachments

  • 61E019F5-CECD-4ED3-908D-F68741AAA803.MOV
    160.6 KB
Kabla hujafika hapo jiulize hao Jamaa ni asilimia ngapi ya Congo?

Population yao ni laki 4 kwenye watu Million 100 hawafiki hata Asilimia 1 ya nchi.

Ugawe nchi uwape kipande kikubwa Asilimia 0.5 ya watu kilichobakia wapewe Asilimia 99.5? Ni ujinga kiwango cha lami.

Na ukiona matakwa ya M23 ndio utaona hawana time na Amani ni vitu visivyomake sense kabis.
Hapo walipo sasa hivi ndio kwao sasa wanapewa kiasi gani hilo ndio swali la msingi, ila alternative ni hao so called wachache either wabakie hapo (wakati hao so called wengi wanaogopa kwamba ni mamluki) au wawagawie kipandi hicho no matter ni kidogo kiasi gani ili wajitawale)..

Kumbuka hawa kama ukisema waendelee kama kawaida basi wakubalini kama wenzenu (yaani raia wenzenu); alternative kama mnakata kuwafukuza wafukuzeni na hio ardhi. Hao M23 mwisho wa siku hao watu huko north Kivu watakuwa na taifa lao Na sio wao tu bali na jamii nyingine ambazo zipo sasa hivi hapo Kivu; hao M23 watakuwa hawana maana ya kuendelea kuwepo. Yaani itabidi wafe kifo cha kawaida au nchi zote ziwatokomeze (sababu watasema wanamtetea nani)?
 
Back
Top Bottom