Pre GE2025 Sumaye: Hakuna anayeweza kuongoza hii nchi zaidi ya Rais Samia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hata ambaye hakupaswa kujikomba anajikomba umri ule anataka nini awam hii?

Warioba huwa namuelewa sana hajui kusifia walio juu

..wote wanafiki.

..Warioba ana ndimi mbili.

..anawapumbaza wapinzani kwamba anawatetea, ukifika wakati wa uchaguzi anapigia kampeni ma-Cc-mu.
 
EEEEeeeeNHEEeeeeee! Nchi hii tumekuwa na wana sanaa wengi (Comedian) mno sasa! Huyu naye sasa anatafuta njia ya kuambatana na Samia (mfadhli mkuu wa fani hii) huko ughaibuni?

Huyu jamaa nilidhani alishatangulia mbele, kumbe bado yupo?

Sasa niulize swali muhimu kutaka kujuwa: huyu alipo ondoka CCM, aliwahi kusamehewa kama alivyo samehewa Lowassa na kurudi ndani ya chama hicho; au yeye hakufukuzwa, bali alikuwa ametumwa kufanya kazi maalum huko CHADEMA?

Ngoja nieleze kwa kifupi nilivyo mwelewa kwa haya aliyozungumzia hapa. Ni kwamba, alipoingia CHADEMA alivutiwa na mienendo ya Mwenyekiti wa chama hicho cha upinzani. Kwa hiyo tuseme alikuwa anakwenda kuongeza nguvu kwa yale aliyoyasimamia Mwenyekiti wa chama.

Sasa hivi, inambidi ajitokeze tena, yeye na Mwenyekiti wakiwa upande ule ule mmoja wa kusafisha njia ya Samia. Hivyo ndivyo nilivyo mwelewa. Kama ndani ya CHADEMA kuna makundi, na kagusia kidogo hilo, basi yeye anajitambulisha kuwa na Mwenyekiti, kama alivyokuwa toka mwanzo. Sasa wote wawili wanampambania Mwenyekiti wa CCM kwa sababu wazijuazo wenyewe.
 
Tatizo la wanasiasa ni kuwa ni waongo na wanafiki!
 
Bila uchawa hii nchi hutoboi,

Somo la uchawa lingeongezwa mashuleni na vyuoni ili na vijana wetu wafundishwe namna ya kujikomba kwa viongozi ili kujinasua kwenye lindi la umaskini.
Kinyume chake mm nimewapiga narufuku watoto wangu kuangalia Taarifa za Habari za Tanzania ! Lengo ni kupunguza uharibifu wa unongo Kwa sababu asilimia kubwa ya hdbari ni za siasa za propaganda!
 
Huyu Mbulula alishindwa hadi na Mary Nagu hana base hapo Hanang.
 
Namtakia njozi njema kamanda wa zamani.
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…