Swali Fyatu la Mwezi: Wakimpa Sifa Zake, Watapunguza za Kwao?

Mimi nakubaliana nawe kwa kiasi fulani kuwa mwendazake John P. Magufuli alikuwa na mapungufu yake mengi kiuongozi hususani katika eneo la UTU, DEMOKRASIA, HESHIMA na ni mtu ambaye hakuwa na SUBIRA wala UVUMILIVU na HAKUAMINI KTK KUSHUGHULIKIA MAMBO KWA KUFUATA UTARATIBU WA KISHERIA NA KIKATIBA kwa watu wake...

Aliamini kuwa yeye ndiye MWANZO na MWISHO wa kila kitu katika nchi hii. Kwa sababu ya imani yake hii, John P. Magufuli akawa na kiburi na kuanza ku - abuse madaraka na mamlaka yake ya u - Rais. Hii ilikuwa ni kasoro kubwa kwa kiongozi huyu na ubaya wake huu unafunika mazuri mengi aliyofanya..!!

Lakini pia it's not fair at all kutompa sifa katika maeneo aliyofanya vizuri. Mojawapo ni uamuzi wake wa kuuweka ktk vitendo uamuzi wa kuhamishia makao makuu (ikulu) ya serikali Dodoma ulioshindikana kwa miaka takribani 55 ya uhuru. Huu ulikuwa uamuzi sahihi na mzuri sana..

Yako mengine mengi mazuri ambayo serikali aliyoiongoza wakati wake ilichukua maamuzi ya kuyatekeleza. Mfano ujenzi wa reli ya SGR. Hili Mimi nampongeza sana huko alipo. It was a bold and good decision..

Yako maamuzi mengine mabaya sana aliyofanya.

Mfano;
✓ Kuminya uhuru wa watu wa kujiamulia mambo yao, kukusanyika na kujieleza yaani DEMOKRASIA. That was a grave mistake..!

✓ Kuua au kuwaumiza watu waliokuwa wanakosoa mbinu na style ya utawala/uongozi wake Kwa kutumia njia mbalimbali..

✓ Kupuuza taratinu, sheria na katiba ya nchi katika serikali yake kuanzia ma - DCs, RCs, mawaziri na hadi yeye mwenyewe Rais walipokuwa wakitenda majukumu yao ya kiutawala...

Ubaguzi wa kikabila na kieneo na wa kiitikadi za kisiasa katika kuwahudumia watu. Mathalani kwenye hili aliwahi kusema akiwa maeneo mbalimbali ya nchi kuwa kama watu wa eneo hilo watakuwa na kiongozi asiyetokana na chama chake cha CCM, basi yeye kama Rais wa nchi hangewapelekea huduma bora za kijamii kama Maji, umeme, elimu nk nk.. This was too bad indeed..!

✓ Si tu ubaguzi, Rais Magufuli alikuwa hulka ya upendeleo kwa misingi ya ukabila na urafiki na kama ungependa kumwabudu..

## Hayo☝️☝️☝️☝️yote na mengine yaliharibu kabisa upande wote wa sifa njema ya ujasiri katika kufanya maamuzi aliokuwa. Na whether tunapenda au hatupendi, mtu yeyote achilia mbali kiongozi kama Rais akiwa na tabia hizo, asitegemee kufika mbali..

Huyu ndiye alikuwa John P. Magufuli. Alikuwa na UZURI na pia UBAYA wake.

🙏🙏🙏🙏🙏
 
Nyie ndo mnalazimisha tumsifie wakati kuna mambo ya kijinga yalifanyika kwenye utawala wake. Uwanja wa ndege wa Chato una faida gani kwa taifa? Hata hiyo ikulu ya Dodoma ni kuongeza tu gharama kwa Taifa wakati ya Dar ipo. Marais waliopita hawakuwa wajinga kuendelea kuwepo Dar. Waziri wa fedha enzi za mwalimu Amir Jamal alitahadharisha sana kuhusu gharama za kuhamia Dodoma na zoezi akasikilizwa... enzi zile kulikuwa na unafuu kuliko sasa hivi lakini bado ikaonekana ni gharama... sasa from nowhere anajitokeza mtu anakomba hazina kwa mambo ambayo hayakuwa kwenye mipango ya nchi. SUKUMA GANG KAENI KIMYA
 


Mimi binafsi sina kingine zaidi ya heshima kuu kwa Mwalimu JK Nyelele,

yeye ndio Rais bora kabisa kwangu then anakuja JPM,

hapo nilikuwa nazungumzia marais waliofuata baada ya Mwalimu......vile vile sikuwa na lengo la kudharau mambo mengine mazuri yaliyofanywa na marais wengine ila nilikuwa namuweka tu sawa huyo jamaa aliyesema kwamba mwisho wa siku kodi za wananchi ndio zinazitumika kufanya hiyo miradi..... ndio nikamjibu hivyo



Na Mwisho kabisa,umeme wa gas kwetu hauwezi kuwa nafuu kufananisha na umeme wa maji kwa kuwa hiyo gas ingawa ipo ndani ya nchi yetu lakini si mali yetu tena ....yaani ni kama unavyoona mchango wa madini kwenye maendeleo ya Taifa hili ulivyo mdogo pamoja na madini yote tuliyonayo
 
Najaribu kujiuliza hizi sifa mnazolazimisha nyerere angelazimisha ingekuaje????? Hivi vitu vipo kwa ajili ya watanzania na vimejengwa kwa kidi zetu. Mbaya zqidi tunazihudumia kwa kodi sasa cha ajabu nn??
 
Uamuzi wa kuhamia Dodoma ni hasara kwa taifa. Fedha zinapotea bure kufanya jambo ambalo halina tija kwa sasa. Enzi za Nyerere kulikuwa na umuhimu wa makao makuu kuwa Dodoma lkn siyo ktk zama hz ambazo usafiri upo wa anga, reli na barabara nzuri.

SGR ni nzuri lkn alikuwa na pupa na papara nyingi. Kulikuwa hakuna haja ya kuanzisha miradi mingi mikubwa kwa pamoja:-SGR, JNHPP, kuhamia Dodoma , daraja la Busisi n.k.

Mm simkubali hata ktk angle moja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…