Swali Gomvi: Korona 2.0 kwani Rais Magufuli ni mbia wa maisha yenu?

Swali Gomvi: Korona 2.0 kwani Rais Magufuli ni mbia wa maisha yenu?

Serikali ilichukua hatua kwa kufuata miongozo ya WHO ili kumlinda Rais wa nchi hivyo idara za usalama zilimpeleka Rais Chato kwa lock down isiyo rasmi kwa miezi mitatu, huku msisitizo ukitolewa wa tahadhari kubwa na njia mbadala yakupambana na Covid 19.
Eeenh.
Kumbe yeye yupo "lockdown", huku akiwatangazia waTanzania kinyume chake?
 
Akiri zimekurudia Leo? Magu anajfanya Nabii! Anapingana na kila kitu utadhani yuko dunia ya pekee yake, za kuambiwa changanyaga na zako
 
Kujikinga na Corona Personally bila national policy haisaidii kitu... see

Yes kuna weza tusiwe na lock down lakini..
1.Tukakubali kuwa huo ugonjwa upo Nchini
2. Tusisitize follow up ya WHO guideline kama ilivo kwa Ukimwi na Malaria etc
3. Kuendelea kutoka elim kwa umma... bado tuna population kubwa ya watu wanaotegemea information kutoka serikalin...
4. Kuzuia kabisa mikusanyiko isio na lazima
5. Kuwakinga wahudum wa Afya
6 Tu acknowledge juhudi za wengine na tusiwabeze kwenye kupambana na ugonjwa huu.... yes some agenda might be there, ila lazima tujiridhishe kweli ni hype kias gan...

That's simple... sasa wengi watu hatujui lipi ni lipi...
 
Maoni aina hii nimeyasikia sehemu nyingi sana kutoka kwa watetezi wa mfumo! Mnachoshau ni kwamba, maoni yenu ni applicable kwa watu wa mitandaoni hususani JF na Twitter ndio ambao wana access to mass information ya kile kinachoendelea duniani kote! Wale wenzangu mimi hata huo muda wa kusikiliza redio hawana! Halaiki hii hawana taaqrifa za kitaalamu kwa sabbabu wataalamu wetu hawawezi kwenda kinyume na matamko ya rais! Matokeo yake, kauli kama chanjo zawazungu ni uongo mtupu ndizo zinazowafikia wananchi wengi kwa sababu ndizo taarifa zinazosambazwa na traditional media! Taarifa kutoka kwa wana mamlaka kwamba hakuna korona ndizo zinawafikia wananchi walio wengi! Sasa hao huwezi kuwaambia eti watumie hizo suggestions zako wakati taarifa wanazopata wao ni kwamba mambo ni shwari, na hao mabeberu ni wivu wao tu wa kutaka kupigana nasi kiuchumi ndo maana wanasema kuna korona ukweli lakini ukweli ni kwamba WANAWATISHA TU, korona HAKUNA!!
Mkuu BonT, umetusemea wengi kwa ufasaha kabisa.
 
Siwaoni Ccm wakimpinga ccm mwezao hhapa, wako wapi?
 
Sisi wengine tunaamini baada ya Mungu ni Magufuli, huyu ameweza yasiyowezekana, ametuomba Watanzania tumuondolee magunzi (Wapinzani) tumeyaondowa yote tumempa safu ya kijani tupu, bunge la kijani.

Tuna imani kubwa na jemedari wetu na tumekubali kumkabidhi maisha yetu awe na ubia nayo.

Je vipi wewe shabiki wake? Unashabikia lipi mpaka uwe na mawazo mbadala badala ya kuandika mapambio?

Hypocrite.
 
Basi kifuatacho nadhani kusiwe na Rais kabisa nchi hii.

Kwasababu mnakwepa majukumu ya dhahiri kwa vijisababu vya kijinga tu wakati mnatumbua kodi za walalahoi kwa kazi hiyo.

Yaani pesa na treatment za kifahari zinazotokana na kodi za walalahoi mnataka ila majukumu yake HAMTAKI.

Mtanzania akipigwa marufuku kwenda nchi za ng'ambo anaweza kutatua vipi hali hiyo peke yake ?

( Je, Raia wa kawaida anaweza kurejesha confidence ya nchi kwa watu wa mataifa mengine )
Tunawalaumu China kwa kutodhibiti ugonjwa mpaka unausumbua dunia, leo tena wengine wanapambana, halafu sisi tupo tupo tu tumekaa, tunasubiri wakimaliza, tuwapelekee.

Je, mikusanyiko mikubwa kama shule raia wa kawaida ana nafasi gani hapo bila Mwongozo ??

Je, ukubwa wa Tatizo ukoje hizi taarifa mwananchi wa kawaida anazipataje ili ajilinde. Knowledge is power.

Wewe Jamaa ni mwehu. Magu huyo anaetandika watu risasi 36 na kutaka wakazikwe haraka haraka ndio mwenye imani ya Petro. Yuko wapi Azory Gwanda, Kanguye, Ben Saanane, enyi wacha mungu ??

Sasa kama imani ndio imekuwa kimbilio la Magufuli, hao maaskari wenye mabunduki na helkopter za ulinzi anatembeatembea nazo za nini ??

Anyway, sasa tuanze kutibu MARALIA, TYPHOID, KIPINDU PINDU, UKIMWI, kwa imani ya Petro.

Kila kitu cha wazungu ni kibaya na hakifai isipokuwa pesa zao, mabomu ya machozi, vifaru vya kijeshi, mabunduki, magari ya washa washa, , vx-v8
Nimekuelewa vizuri tu, sijui hao washauri kama wamepita hapa.
 
Haya, mshabiki wa wa Magufuli unayeishi Chato. Labda huko chato hiyo kovidi 19 ya ajabu ajabu mtaishinda kwa kujifukiza tena. Yetu macho.
 
Wapinzani wanataka tufungiwe ndani kama kuku wa kisasa
 
Mfano wa Petro umenichekesha saaana 😃😃😃 kwamba wenzake walimtoa chambo kwanza

Mfano ni mzuri sana, hauchekeshi na wala wenzake wala hawakumtoa chambo...

Petro yeye mwenyewe alijitoa na akafanikiwa japo alipoona wimbi kubwa la maji mbele yake "wasiwasi na mashaka vikamwingia", akaanza kuzama na alipoita jina la Yesu Kristo kuomba msaada, aliokolewa...

Mwandishi kasema vizuri sana. Anayeweza kwenda sambamba na imani ya Magufuli, atembee juu ya maji ya bahari (Covid 19) kwa imani, asione shaka atashinda...

Huna imani hiyo, baki mtumbwini, subiri chanjo na chukua tahadhari nyingine zote...
 
Ni kweli mkuu.
Mlinzi wa maisha yako wa kwanza ni wewe mwenyewe.
Ndio maana kuna wamarekani waliokimbia ukandamizaji huko Ulaya na kukimbilia Marekani ii kulinda nafsi zao miaka mingi tuiliyopita.
Leo mtu ukiona maisha yako yakuwa taken for granted, unaamua unavyoona inakufaa!
 
Hapo ndipo uone ubinafsi wa wana siasa
Samahani mkuu 'Sem2708' naomba nikuulize swali:

Hivi kila aliyepo kwenye uongozi na katika vyama vinavyojitambilsha kuwa vya siasa ni lazima ajulikane kuwa ni "Mwanasiasa"?

Hakuna vigezo maalum vinavyohitajika kuwa navyo mhusika kutambulika kuwa yeye ni 'mwanasiasa'?

Akina Amin Dada, Bokassa, Mobutu, n.k., wote hawa wanajulikana kuwa walikuwa 'wanasiasa', kwa sifa tu ya kuwa kwenye nafasi ya uongozi wa nchi?

Hili neno "Mwanasiasa" ninaliona kuwa lina utata mkubwa. Mi nadhani kuna vigezo vinavyompambanua mhusika kuwa ni mwanasiasa, mbali ya yeye kuwa tu kwenye madaraka ya juu nchini.

Simwoni Magufuli kuwa ni mwanasiasa, kwa sababu haonyeshi dalili yoyote ya kuwa mwanasiasa.
 
Watu wanadeka sana... Wanasubiri Rais aseme ndio wachukue hatua, sasa ni kuwaacha waendelee kulalama. Na pia chanjo kama wanaitaka wasafiri huko nje hata malawi wakaipate.

Suala la afya linaanza na mtu binafsi, kama huwezi kulinda familia yako basi mtaangamia na kulalamika ambapo pia itakua ni dua la kuku kwa mwewe.
 
Rais Magufuli anajua anachokifanya, pia anajua kuna Covid19 phase II. Ila ameona athari za kuruhusu lockdown ya Nchi nzima kama wengine wanavyofanya itaathiri Sana Raia wake kuliko kutoweka lockdown.

Watanzania ni maskini wa kutupwa, tusije kufa kwa njaa kabla ya Corona.

Muhimu alichosema ni kuchukua tahadhali za kujikinga. Tahadhari ulizosema hapo juu ni muhimu zikachukuliwa na kila mwananchi,

Ila kulikuwa na haja yeye Kama Amiri jeshi Mkuu aseme kwa kusisitiza kuhusu hilo.
Ninachoamini ni kwamba ikitokea Corona umechanganya (Mola apishie mbali) watu wakaanza kudondoka kila kona, watu watajifungia wenyewe bila shuruti...
 
Back
Top Bottom