Swali Gomvi: Korona 2.0 kwani Rais Magufuli ni mbia wa maisha yenu?

Swali Gomvi: Korona 2.0 kwani Rais Magufuli ni mbia wa maisha yenu?

Hapo ndio serikali imetangaza kuna corona na inachukua hatua za kupunguza maambukizi ila wananchi wenye sasa walichokuwa wanafanya.
download.jpg
download%20(1).jpg
 
Uko sawa kabisa, Mimi wasiwasi wangu ni uwezo wa Mwananchi kumudu kula yake ya kila siku akiwa locked ndani.

Watanzania wengi wetu ni maskini Sana, ukitaka kujua hili Jaribu kuwa na shida ya 20M hivi then jaribu kuwapigia jamaa wakukope. Unaweza kuta unatafuta na usipate, hadi uende Benki kukopa.

Sasa vipi wale wa kule vijijini ambao unakuta wanategemea kilimo wavune ndiyo wale.

Kwa kweli Mungu atusaidie
Siyo lazima kuwe na lockdown wala curfew kwa kila mtu. Serikali inaweza kuruhusu hata, upimaji, 'community awareness' na kuweka restrictions mipakani.
 
Siyo lazima kuwe na lockdown wala curfew kwa kila mtu. Serikali inaweza kuruhusu hata, upimaji, 'community awareness' na kuweka restrictions mipakani.
Uko sahihi, nadhani tukifanya hivyo itasaidia mno kuenea.

Swali ni Je, Waziri wa Afya haoni umuhimu wa haya uliyosema na akamshauri boss wake??

Hata Waziri mpendwa wa JPM bwana Kabudi haoni hilo na kumshauri wakati wa vikao vyao
 
Uko sahihi, nadhani tukifanya hivyo itasaidia mno kuenea.

Swali ni Je, Waziri wa Afya haoni umuhimu wa haya uliyosema na akamshauri boss wake??

Hata Waziri mpendwa wa JPM bwana Kabudi haoni hilo na kumshauri wakati wa vikao vyao
Magufuli HASHAURIKI na ameshakuwa sugu kutomsikiliza yeyote.

Kuwa mpendwa wa Magufuli maana yake ni kufanya kila anachotaka, au kufanya kile utakachoona kitamfurahisha.
 
Magufuli HASHAURIKI na ameshakuwa sugu kutomsikiliza yeyote.

Kuwa mpendwa wa Magufuli maana yake ni kufanya kila anachotaka, au kufanya kile utakachoona kitamfurahisha.
Basi ni hatari

Nakumbuka kwenye kitabu cha Yona kwenye agano la Kale tuliona adhabu ya Mungu kwa watu ambao wanashindwa kutii maagizo ya Mungu.

Ingekuwa enzi zile kwenye ugonjwa wa hatari kama huu wa Covid19, ilikuwa Mfalme anauguliwa na mpendwa wake mmoja au yeye mwenyewe, hapo ingemlazimu kubadilisha maamuzi na kuangalia Utaalamu.

Bahati Mbaya Jiwe huwa haliugui kwa sababu ni Non organism
 
Basi kifuatacho nadhani kusiwe na Rais kabisa nchi hii.

Kwasababu mnakwepa majukumu ya dhahiri kwa vijisababu vya kijinga tu wakati mnatumbua kodi za walalahoi kwa kazi hiyo.

Yaani pesa na treatment za kifahari zinazotokana na kodi za walalahoi mnataka ila majukumu yake HAMTAKI.

Mtanzania akipigwa marufuku kwenda nchi za ng'ambo anaweza kutatua vipi hali hiyo peke yake ?

( Je, Raia wa kawaida anaweza kurejesha confidence ya nchi kwa watu wa mataifa mengine )
Tunawalaumu China kwa kutodhibiti ugonjwa mpaka unausumbua dunia, leo tena wengine wanapambana, halafu sisi tupo tupo tu tumekaa, tunasubiri wakimaliza, tuwapelekee.

Je, mikusanyiko mikubwa kama shule raia wa kawaida ana nafasi gani hapo bila Mwongozo ??

Je, ukubwa wa Tatizo ukoje hizi taarifa mwananchi wa kawaida anazipataje ili ajilinde. Knowledge is power.

Wewe Jamaa ni mwehu. Magu huyo anaetandika watu risasi 36 na kutaka wakazikwe haraka haraka ndio mwenye imani ya Petro. Yuko wapi Azory Gwanda, Kanguye, Ben Saanane, enyi wacha mungu ??

Sasa kama imani ndio imekuwa kimbilio la Magufuli, hao maaskari wenye mabunduki na helkopter za ulinzi anatembeatembea nazo za nini ??

Anyway, sasa tuanze kutibu MARALIA, TYPHOID, KIPINDU PINDU, UKIMWI, kwa imani ya Petro.

Kila kitu cha wazungu ni kibaya na hakifai isipokuwa pesa zao, mabomu ya machozi, vifaru vya kijeshi, mabunduki, magari ya washa washa, , vx-v8
Hujui kuna Toba?
 
Hujui kuna Toba?
Kikristo Toba haifanywi hivyo Mkuu.

Kwanza unapaswa kukiri kosa, kufanya toba na kuomba msamaha kwa uliowakosea na mwishowe ukubali kutorudia makosa.
 
Korona 2.0 Kwani Rais ana Ubia na Maisha Yenu?

Na. M. M. Mwanakijiji
Naandika kama shabiki wa Magufuli; naandika kama mtu ambaye nimeelewa malengo yake na mitazamo yake, na ninaandika kama mtu ambaye sijaegesha akili yangu mahali mwenyewe nikaondoka. Nimesoma na kufuatilia mijadala ya kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili (2.0) la maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) ambayo yanasemekana yanaendelea nchini mwetu. Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya na kwa kiasi kikubwa wanafanya hivyo kwa sababu Rais ndio kiongozi mkuu wa serikali na nchi.

Neno la Rais lina uzito wake, hofu za Rais zina uzito wake na ikumbukwe kuwa wengi wanachukulia kuwa kwa vile Rais ana watu wengi wanaomzunguka basi ana taarifa za mambo mengi ambayo labda watu nje ya serikali hawana. Aliposema watu wajifukize, mamilioni walijifukiza, aliposema watu wafunge na kuomba, watu walifunga na kuomba, aliposema watu waiage korona watu walifanya na send off! Na alipotangaza kuwa korona hakuna Tanzania na kuwa imekwisha watu waliamini hivyo.

Sasa hili wimbi la pili ni kweli? Kama ni kweli je Watanzania wafanye nini? Je, watu wanaokufa ni kweli wote wanakufa kwa korona au magonjwa mengine? Na kama wimbi hili kweli lipo kama nchi tufanye nini na kama mtu mmoja mmoja tufanye nini? Ni wazi msimamo wa serikali umetolewa na Rais jana huko Chato na kuwa hakuna mtendaji wa serikali atakayepingana na Rais kwenye hili isipokuwa kama yuko tayari kujiuzulu akipinga (resigning in protest). Kwa vile msimamo wa serikali unajulikana na kuwa serikali haitaleta lock down, na kuwa hata chanjo watu wafikirie mara mbilimbili basi sehemu ya nini kila mtu afanye ndio swali linalohitaji kujibiwa.

Ndugu zangu naandika kama shabiki; Watanzania msijitoe ufahamu na mkajifanya nyie fyatu! Rais si mbia wa maisha yenu, ya mababa na mama zenu, na wala si mbia wa maisha ya watoto wenu! Mnapougua, kuuguza na kuuguliwa yote hayo ni yenu; mauti yakiwafikia vilio ni kwenye nyumba zenu, jamaa, ndugu na marafiki zenu. Sasa kama hili ni kweli, kwanini watu wengine wafikiri wanaweza kuifanyia ibada imani ya mtu mwingine? Hivi, mnajua kwanini mitume wengine hawakuungana na Petro kujaribu kutembea juu ya maji japo wote walimuona Yesu akitembea juu ya maji na walimsikia Yesu akimwambia Petro atembee? (Mathayo 14:22-33).
View attachment 1687880

Rais Magufuli anaweza kuwa na imani kubwa kabisa hata ya kutembea juu ya maji na akatembea; lakini wangapi wanaamini kama yeye? Kama imani yako haijafikia ile ya Magufuli sasa unakanyaga maji ya nini?

Ndugu zangu kuna njia tatu/nne kubwa na za haraka za kupunguza maambukizi ya corona:

1. Vaa barakoa iliyotengenezwa na kitambaa cha pamba (siyo hariri). Kuvaa barakoa kuna kulinda wewe na kinamlinda mwingine. Ukivaa barakoa funika pua na mdomo (korona inaingia zaidi kupitia puani!)

2. Osha mikono kwa sabuni mara kwa mara; epuka kusalimiana na watu kwa kushikana mikono. Ikitokea hivyo hakikisha huingiza vidole midomoni au puani (jitahidi kuosha kabla ya kufanya hivyo na baada).

3. Jiweke umbali wa karibu mita moja kutoka kwa mtu mwingine ambaye si wa nyumbani mwako. Na hii inaendana na kuepuka misongamano isiyo ya lazima hasa mahali ambapo watu hawavai barakoa. Na wale wenye ndugu (wazazi, mababu wazee) waambieni wasiende makanisani au misikitini kwa wakati huu au makanisa na misikiti iweke taratibu za kuhakikisha watu wanakaa mbalimbali na wanavaa barakoa!

4. Jifukize nyungu; sijui ni kwa namna gani hii ilisaidie kuzuia wimbi la kwanza lakini kama watu watafanya tena na kwa wingi wao mnaweza kujikuta mnazuia tena wimbi hili la pili maana kama ni chanjo msijipe matumaini saini.

Njia hizo tatu ndio njia zitakazokinga maisha yako na maisha ya wale uwapendeo. Lakini kama unafikiria Rais ana ubia na maisha yako haya we. Kwa sababu lile swali la bahati nasibu ya Magufuli kama italipa bado linasimama.
Mwanakijiji you're talking nonsense, Magufuli should be made responsible for the majority of covid deaths in TZ because of his attitude towards the desease.
 
Korona 2.0 Kwani Rais ana Ubia na Maisha Yenu?

Na. M. M. Mwanakijiji
Naandika kama shabiki wa Magufuli; naandika kama mtu ambaye nimeelewa malengo yake na mitazamo yake, na ninaandika kama mtu ambaye sijaegesha akili yangu mahali mwenyewe nikaondoka. Nimesoma na kufuatilia mijadala ya kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili (2.0) la maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) ambayo yanasemekana yanaendelea nchini mwetu. Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya na kwa kiasi kikubwa wanafanya hivyo kwa sababu Rais ndio kiongozi mkuu wa serikali na nchi.

Neno la Rais lina uzito wake, hofu za Rais zina uzito wake na ikumbukwe kuwa wengi wanachukulia kuwa kwa vile Rais ana watu wengi wanaomzunguka basi ana taarifa za mambo mengi ambayo labda watu nje ya serikali hawana. Aliposema watu wajifukize, mamilioni walijifukiza, aliposema watu wafunge na kuomba, watu walifunga na kuomba, aliposema watu waiage korona watu walifanya na send off! Na alipotangaza kuwa korona hakuna Tanzania na kuwa imekwisha watu waliamini hivyo.

Sasa hili wimbi la pili ni kweli? Kama ni kweli je Watanzania wafanye nini? Je, watu wanaokufa ni kweli wote wanakufa kwa korona au magonjwa mengine? Na kama wimbi hili kweli lipo kama nchi tufanye nini na kama mtu mmoja mmoja tufanye nini? Ni wazi msimamo wa serikali umetolewa na Rais jana huko Chato na kuwa hakuna mtendaji wa serikali atakayepingana na Rais kwenye hili isipokuwa kama yuko tayari kujiuzulu akipinga (resigning in protest). Kwa vile msimamo wa serikali unajulikana na kuwa serikali haitaleta lock down, na kuwa hata chanjo watu wafikirie mara mbilimbili basi sehemu ya nini kila mtu afanye ndio swali linalohitaji kujibiwa.

Ndugu zangu naandika kama shabiki; Watanzania msijitoe ufahamu na mkajifanya nyie fyatu! Rais si mbia wa maisha yenu, ya mababa na mama zenu, na wala si mbia wa maisha ya watoto wenu! Mnapougua, kuuguza na kuuguliwa yote hayo ni yenu; mauti yakiwafikia vilio ni kwenye nyumba zenu, jamaa, ndugu na marafiki zenu. Sasa kama hili ni kweli, kwanini watu wengine wafikiri wanaweza kuifanyia ibada imani ya mtu mwingine? Hivi, mnajua kwanini mitume wengine hawakuungana na Petro kujaribu kutembea juu ya maji japo wote walimuona Yesu akitembea juu ya maji na walimsikia Yesu akimwambia Petro atembee? (Mathayo 14:22-33).
View attachment 1687880

Rais Magufuli anaweza kuwa na imani kubwa kabisa hata ya kutembea juu ya maji na akatembea; lakini wangapi wanaamini kama yeye? Kama imani yako haijafikia ile ya Magufuli sasa unakanyaga maji ya nini?

Ndugu zangu kuna njia tatu/nne kubwa na za haraka za kupunguza maambukizi ya corona:

1. Vaa barakoa iliyotengenezwa na kitambaa cha pamba (siyo hariri). Kuvaa barakoa kuna kulinda wewe na kinamlinda mwingine. Ukivaa barakoa funika pua na mdomo (korona inaingia zaidi kupitia puani!)

2. Osha mikono kwa sabuni mara kwa mara; epuka kusalimiana na watu kwa kushikana mikono. Ikitokea hivyo hakikisha huingiza vidole midomoni au puani (jitahidi kuosha kabla ya kufanya hivyo na baada).

3. Jiweke umbali wa karibu mita moja kutoka kwa mtu mwingine ambaye si wa nyumbani mwako. Na hii inaendana na kuepuka misongamano isiyo ya lazima hasa mahali ambapo watu hawavai barakoa. Na wale wenye ndugu (wazazi, mababu wazee) waambieni wasiende makanisani au misikitini kwa wakati huu au makanisa na misikiti iweke taratibu za kuhakikisha watu wanakaa mbalimbali na wanavaa barakoa!

4. Jifukize nyungu; sijui ni kwa namna gani hii ilisaidie kuzuia wimbi la kwanza lakini kama watu watafanya tena na kwa wingi wao mnaweza kujikuta mnazuia tena wimbi hili la pili maana kama ni chanjo msijipe matumaini saini.

Njia hizo tatu ndio njia zitakazokinga maisha yako na maisha ya wale uwapendeo. Lakini kama unafikiria Rais ana ubia na maisha yako haya we. Kwa sababu lile swali la bahati nasibu ya Magufuli kama italipa bado linasimama.
Ndugu Mwanakijiji,

Kwanza, nadhani hujamtendea haki Magufuli kwa kujiita SHABIKI wake. Shabiki wa kweli huwa mkweli kwa anachoshabikia. Shabiki wa kweli wa Simba, kwa mfano, hawezi kushangilia timu hiyo ikitaka kusajili mchezaji mbovu bali atajitahidi kupaza sauti ili wahusika wachukue hatua stahili.

Kwa mantiki hiyohiyo, laiti ungekuwa shabiki wa kweli wa Magufuli, mada yako isingelenga "kuwazodoa" wananchi anaowaongoza na badala yake ungejikita kwenye kauli za huyo unayedai kumshabikia.

Lakini pengine si vibaya kukumbushia kwamba mie na wewe tulikuwa "njia moja" mwaka 2015 kumnadi Magufuli kwa sababu zilizokuwa wazi kwa wakati huo. Hata hivyo, baada ya kumnadi mwanasiasa wakati wa kampeni hakumaanishi ubaki mfungwa wake milele hata anapokosea, baadhi yetu tulijiweka kando baada ya kubaini mwenendo usioridhisha wa mwanasiasa tuliemnadi kwenye kampeni. Lakini baadhi ya wenzetu sio tu mmebaki wafuasi watiifu wa Magufuli - na hili si kosa - bali pia mmejitoa ufahamu na kuwa kwenye "campaign mode" indefinitely. Nachomaanisha hapa ni kwamba wakati wa kampeni si mwafaka kumkosoa mgombea wako, lakini ni hujuma dhidi yake endapo mfuasi atakalia kimya "utopolo" wa mwanasiasa anayemuunga mkono.

Turejee kwenye bandiko lako. Usingejitoa ufahamu, usingekimbilia kuongelea watendewa (objects) badala ya mtendaji (subject). Wananchi "unaowalaumu" hawajatoa hotuba kudai kwamba "Rais Magufuli anatukwaza kwenye vita dhidi ya korona." Sote twafahamu - ikiwa ni pamoja na wenzetu mliojitoa ufahamu - kuwa Ni Rais Magufuli anayejibidiisha kuwavunja moyo wale wote wanaojaribu kuichukulia korona kama janga hatari. Na sasa ni kama amewaambukiza ninyi wafuasi wake, maana Mwanakijiji nayemjua mie si mtu wa kujifanya haelewi hali ya korona ikoje nchini Tanzania. Lakini hata kama angekuwa haelewi, ukaazi wake nchini Marekani ambako korona inatafuna uhai kama moto mkali kwenye nyasi ungempa uzalendo wa "kumtolea jicho" kila COVIDIOT, iwe huko Marekani au kwetu Tanzania.

Mnaweza kuendelea kuwa mashabiki wa Magufuli lakini pia mkamshauri, kama si kumkemea, bali anapokwenda ndivyo sivyo. Na position yake katika korona imekuwa na athari zaidi kuliko faida. Athari hizo hazifahamiki kwa sababu hakuna chombo cha habari kinachoruhusiwa kuripoti, kwa mfano, watu wangapi hadi sasa wana maambukizi ya korona au kutaja idadi ya vifo. Serikali inayoficha idadi ya vifo isivyohusika navyo haiwezi kuwa wazi kwa vifo vilivyosababishwa na serikali hiyo. Hii sio sayansi ya roketi. Serikali inayohadaa wananchi wake kwa janga ambalo sio kosa lake, haiwezi kuwa mkweli kwenye janga ilililosababisha.

Kwahiyo badala ya kuwazodoa wananchi kwamba Magufuli hana ubia na maisha ya Watanzania - kana kwamba sio Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - ulipaswa kumshauri huyo unayedai kumshabikia kuwa kukaa kimya nako ni busara. Lakini pia ungeweza kumkosoa kwenye kauli yake fyongo kuhusu CHANJO. Kudai chanjo si salama, ilhali takriban kila Mtanzania - ikiwa ni pamoja na Magufuli mwenyewe - alichanjwa udogoni sio tu ni suala linaloweza kuzua taharuki bali pia laweza kuwa na athari kubwa kwa mamilioni ya watoto na akinamama. Najua mtamtetea kuwa "alimaanisha chanjo ya korona," lakini yeye kama si mdau wa uhai wa Watanzania -kama bandiko lako linavyojaribu kutushawishi - kwanini basi awashikie akili Watanzania wenzake zaidi ya milioni 59?

Nihitimishe kwa kuwashauri wapambe kindakindaki kuwa mwaweza kuwa na msaada zaidi kwa huyo mnayemshabikia endapo mtampongeza pale anapostahili na kummosoa pale inapobidi. Katika hili la korona, ushauri wenu unahitajika sana ili Magufuli aongozwe sio tu na busara bali pia kama mwanasayansi azingatie sayansi pia.

Niwie radhi endapo nitakuwa nimekukwaza.
 
Korona 2.0 Kwani Rais ana Ubia na Maisha Yenu?

Na. M. M. Mwanakijiji
Naandika kama shabiki wa Magufuli; naandika kama mtu ambaye nimeelewa malengo yake na mitazamo yake, na ninaandika kama mtu ambaye sijaegesha akili yangu mahali mwenyewe nikaondoka. Nimesoma na kufuatilia mijadala ya kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili (2.0) la maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) ambayo yanasemekana yanaendelea nchini mwetu. Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya na kwa kiasi kikubwa wanafanya hivyo kwa sababu Rais ndio kiongozi mkuu wa serikali na nchi.

Neno la Rais lina uzito wake, hofu za Rais zina uzito wake na ikumbukwe kuwa wengi wanachukulia kuwa kwa vile Rais ana watu wengi wanaomzunguka basi ana taarifa za mambo mengi ambayo labda watu nje ya serikali hawana. Aliposema watu wajifukize, mamilioni walijifukiza, aliposema watu wafunge na kuomba, watu walifunga na kuomba, aliposema watu waiage korona watu walifanya na send off! Na alipotangaza kuwa korona hakuna Tanzania na kuwa imekwisha watu waliamini hivyo.

Sasa hili wimbi la pili ni kweli? Kama ni kweli je Watanzania wafanye nini? Je, watu wanaokufa ni kweli wote wanakufa kwa korona au magonjwa mengine? Na kama wimbi hili kweli lipo kama nchi tufanye nini na kama mtu mmoja mmoja tufanye nini? Ni wazi msimamo wa serikali umetolewa na Rais jana huko Chato na kuwa hakuna mtendaji wa serikali atakayepingana na Rais kwenye hili isipokuwa kama yuko tayari kujiuzulu akipinga (resigning in protest). Kwa vile msimamo wa serikali unajulikana na kuwa serikali haitaleta lock down, na kuwa hata chanjo watu wafikirie mara mbilimbili basi sehemu ya nini kila mtu afanye ndio swali linalohitaji kujibiwa.

Ndugu zangu naandika kama shabiki; Watanzania msijitoe ufahamu na mkajifanya nyie fyatu! Rais si mbia wa maisha yenu, ya mababa na mama zenu, na wala si mbia wa maisha ya watoto wenu! Mnapougua, kuuguza na kuuguliwa yote hayo ni yenu; mauti yakiwafikia vilio ni kwenye nyumba zenu, jamaa, ndugu na marafiki zenu. Sasa kama hili ni kweli, kwanini watu wengine wafikiri wanaweza kuifanyia ibada imani ya mtu mwingine? Hivi, mnajua kwanini mitume wengine hawakuungana na Petro kujaribu kutembea juu ya maji japo wote walimuona Yesu akitembea juu ya maji na walimsikia Yesu akimwambia Petro atembee? (Mathayo 14:22-33).
View attachment 1687880

Rais Magufuli anaweza kuwa na imani kubwa kabisa hata ya kutembea juu ya maji na akatembea; lakini wangapi wanaamini kama yeye? Kama imani yako haijafikia ile ya Magufuli sasa unakanyaga maji ya nini?

Ndugu zangu kuna njia tatu/nne kubwa na za haraka za kupunguza maambukizi ya corona:

1. Vaa barakoa iliyotengenezwa na kitambaa cha pamba (siyo hariri). Kuvaa barakoa kuna kulinda wewe na kinamlinda mwingine. Ukivaa barakoa funika pua na mdomo (korona inaingia zaidi kupitia puani!)

2. Osha mikono kwa sabuni mara kwa mara; epuka kusalimiana na watu kwa kushikana mikono. Ikitokea hivyo hakikisha huingiza vidole midomoni au puani (jitahidi kuosha kabla ya kufanya hivyo na baada).

3. Jiweke umbali wa karibu mita moja kutoka kwa mtu mwingine ambaye si wa nyumbani mwako. Na hii inaendana na kuepuka misongamano isiyo ya lazima hasa mahali ambapo watu hawavai barakoa. Na wale wenye ndugu (wazazi, mababu wazee) waambieni wasiende makanisani au misikitini kwa wakati huu au makanisa na misikiti iweke taratibu za kuhakikisha watu wanakaa mbalimbali na wanavaa barakoa!

4. Jifukize nyungu; sijui ni kwa namna gani hii ilisaidie kuzuia wimbi la kwanza lakini kama watu watafanya tena na kwa wingi wao mnaweza kujikuta mnazuia tena wimbi hili la pili maana kama ni chanjo msijipe matumaini saini.

Njia hizo tatu ndio njia zitakazokinga maisha yako na maisha ya wale uwapendeo. Lakini kama unafikiria Rais ana ubia na maisha yako haya we. Kwa sababu lile swali la bahati nasibu ya Magufuli kama italipa bado linasimama.
Ahsante shabiki wa Magufuli
 
Korona 2.0 Kwani Rais ana Ubia na Maisha Yenu?

Na. M. M. Mwanakijiji
Naandika kama shabiki wa Magufuli; naandika kama mtu ambaye nimeelewa malengo yake na mitazamo yake, na ninaandika kama mtu ambaye sijaegesha akili yangu mahali mwenyewe nikaondoka. Nimesoma na kufuatilia mijadala ya kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili (2.0) la maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) ambayo yanasemekana yanaendelea nchini mwetu. Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya na kwa kiasi kikubwa wanafanya hivyo kwa sababu Rais ndio kiongozi mkuu wa serikali na nchi.

Neno la Rais lina uzito wake, hofu za Rais zina uzito wake na ikumbukwe kuwa wengi wanachukulia kuwa kwa vile Rais ana watu wengi wanaomzunguka basi ana taarifa za mambo mengi ambayo labda watu nje ya serikali hawana. Aliposema watu wajifukize, mamilioni walijifukiza, aliposema watu wafunge na kuomba, watu walifunga na kuomba, aliposema watu waiage korona watu walifanya na send off! Na alipotangaza kuwa korona hakuna Tanzania na kuwa imekwisha watu waliamini hivyo.

Sasa hili wimbi la pili ni kweli? Kama ni kweli je Watanzania wafanye nini? Je, watu wanaokufa ni kweli wote wanakufa kwa korona au magonjwa mengine? Na kama wimbi hili kweli lipo kama nchi tufanye nini na kama mtu mmoja mmoja tufanye nini? Ni wazi msimamo wa serikali umetolewa na Rais jana huko Chato na kuwa hakuna mtendaji wa serikali atakayepingana na Rais kwenye hili isipokuwa kama yuko tayari kujiuzulu akipinga (resigning in protest). Kwa vile msimamo wa serikali unajulikana na kuwa serikali haitaleta lock down, na kuwa hata chanjo watu wafikirie mara mbilimbili basi sehemu ya nini kila mtu afanye ndio swali linalohitaji kujibiwa.

Ndugu zangu naandika kama shabiki; Watanzania msijitoe ufahamu na mkajifanya nyie fyatu! Rais si mbia wa maisha yenu, ya mababa na mama zenu, na wala si mbia wa maisha ya watoto wenu! Mnapougua, kuuguza na kuuguliwa yote hayo ni yenu; mauti yakiwafikia vilio ni kwenye nyumba zenu, jamaa, ndugu na marafiki zenu. Sasa kama hili ni kweli, kwanini watu wengine wafikiri wanaweza kuifanyia ibada imani ya mtu mwingine? Hivi, mnajua kwanini mitume wengine hawakuungana na Petro kujaribu kutembea juu ya maji japo wote walimuona Yesu akitembea juu ya maji na walimsikia Yesu akimwambia Petro atembee? (Mathayo 14:22-33).
View attachment 1687880

Rais Magufuli anaweza kuwa na imani kubwa kabisa hata ya kutembea juu ya maji na akatembea; lakini wangapi wanaamini kama yeye? Kama imani yako haijafikia ile ya Magufuli sasa unakanyaga maji ya nini?

Ndugu zangu kuna njia tatu/nne kubwa na za haraka za kupunguza maambukizi ya corona:

1. Vaa barakoa iliyotengenezwa na kitambaa cha pamba (siyo hariri). Kuvaa barakoa kuna kulinda wewe na kinamlinda mwingine. Ukivaa barakoa funika pua na mdomo (korona inaingia zaidi kupitia puani!)

2. Osha mikono kwa sabuni mara kwa mara; epuka kusalimiana na watu kwa kushikana mikono. Ikitokea hivyo hakikisha huingiza vidole midomoni au puani (jitahidi kuosha kabla ya kufanya hivyo na baada).

3. Jiweke umbali wa karibu mita moja kutoka kwa mtu mwingine ambaye si wa nyumbani mwako. Na hii inaendana na kuepuka misongamano isiyo ya lazima hasa mahali ambapo watu hawavai barakoa. Na wale wenye ndugu (wazazi, mababu wazee) waambieni wasiende makanisani au misikitini kwa wakati huu au makanisa na misikiti iweke taratibu za kuhakikisha watu wanakaa mbalimbali na wanavaa barakoa!

4. Jifukize nyungu; sijui ni kwa namna gani hii ilisaidie kuzuia wimbi la kwanza lakini kama watu watafanya tena na kwa wingi wao mnaweza kujikuta mnazuia tena wimbi hili la pili maana kama ni chanjo msijipe matumaini saini.

Njia hizo tatu ndio njia zitakazokinga maisha yako na maisha ya wale uwapendeo. Lakini kama unafikiria Rais ana ubia na maisha yako haya we. Kwa sababu lile swali la bahati nasibu ya Magufuli kama italipa bado linasimama.

Mkuu ni haki yako kuwa shabiki wa Magufuli lakini si vyema kutaka kuhalalisha (rationalize) ubovu na mkanganyiko wa uongozi wake kwa kutuchokoza (provoke) kuwa Magufuli hana ubia na sisi wananchi wake katika afya zetu. Yaani unamaanisha hawajibiki kwa lolote kuhusu afya za wananchi wake! Tunachokiona ni leadership failure. Period.

Si Watanzania wengi wenye elimu na uelewa mkubwa kama tulio nao sisi wachache tunaosoma na kuchambua taarifa za media mitandaoni kimataifa. Watanzania hawa wanasikiliza sana na kuzingatia kauli za viongozi wao hasa za Mheshimiwa Rais wa wanyonge. Anapowasisitizia kuwa dawa kubwa ya corona ni maombi na kujifukiza; Tanzania tumeishinda corona haipo/ipo kidogo sana; barakoa hazizuii corona tena za kutoka nje zinaweza kuja na vidudu; anabeza wavaa barakoa na kuweka total blackout kuzuia taarifa za uwepo wa corona nchini zisitolewe wala kuzungumzwa, huo si uongozi.

Unapochaguliwa kuwa Rais wa nchi basi automatically una ubia na maisha ya wananchi wako. Wanatarajia uongozi makini dhidi ya majanga makuu ya kitaifa. You have to show leadership.

Mimi Drifter kama mtu binafsi nina nyenzo kibao za kupambanua na kupambana na matatizo yangu. Naweza hata kwenda nchi za mbali kutafuta masuluhisho ya matatizo yangu ikibidi. Lakini mimi si kielelezo cha Mtanzania wa kawaida ambaye kwake maendeleo ni kuwa na bomba la maji la kijiji, shule ya kata, umeme wa REA, nk. Anayetegemea sana kuwasilisha masuala yake binafsi kwa Mwenyekiti wa kijiji/mtaa.

It’s futile to attempt rationalising incoherence for the sake of justifying leadership failure. Huhitaji kututishia “ubia” ili tusihoji mambo muhimu ya kitaifa. We are intelligent sufficiently.
 
Rais Magufuli anajua anachokifanya, pia anajua kuna Covid19 phase II. Ila ameona athari za kuruhusu lockdown ya Nchi nzima kama wengine wanavyofanya itaathiri Sana Raia wake kuliko kutoweka lockdown.

Watanzania ni maskini wa kutupwa, tusije kufa kwa njaa kabla ya Corona.

Muhimu alichosema ni kuchukua tahadhali za kujikinga. Tahadhari ulizosema hapo juu ni muhimu zikachukuliwa na kila mwananchi,

Ila kulikuwa na haja yeye Kama Amiri jeshi Mkuu aseme kwa kusisitiza kuhusu hilo.
Nafikiri hapa swala siyo lock down bali ni conspiracy theories anazokuja nazo kila kukicha.
 
Watu wanadeka sana... Wanasubiri Rais aseme ndio wachukue hatua, sasa ni kuwaacha waendelee kulalama. Na pia chanjo kama wanaitaka wasafiri huko nje hata malawi wakaipate.

Suala la afya linaanza na mtu binafsi, kama huwezi kulinda familia yako basi mtaangamia na kulalamika ambapo pia itakua ni dua la kuku kwa mwewe.
Hakuna anayedeka! Ni jukumu la serikali kupitia kwa waziri wa afya kuwaambia umma juu ya hali halisi na nn kifanyike. Siyo lazima lock down km Rais anavyojitetea kuwa watu baadhi wanalazimisha lockdown.
Itoshe kukiri kuwa kuna tatizo lenye ukubwa kidogo na mbinu za kushinda ni 1,2,3 nk. Kusema “Siyo kubwa, haipo ni chache sana” nikukanganya umma
 
Mkuu ni haki yako kuwa shabiki wa Magufuli lakini si vyema kutaka kuhalalisha (rationalize) ubovu na mkanganyiko wa uongozi wake kwa kutuchokoza (provoke) kuwa Magufuli hana ubia na sisi wananchi wake katika afya zetu. Yaani unamaanisha hawajibiki kwa lolote kuhusu afya za wananchi wake! Tunachokiona ni leadership failure. Period.

Si Watanzania wengi wenye elimu na uelewa mkubwa kama tulio nao sisi wachache tunaosoma na kuchambua taarifa za media mitandaoni kimataifa. Watanzania hawa wanasikiliza sana na kuzingatia kauli za viongozi wao hasa za Mheshimiwa Rais wa wanyonge. Anapowasisitizia kuwa dawa kubwa ya corona ni maombi na kujifukiza; Tanzania tumeishinda corona haipo/ipo kidogo sana; barakoa hazizuii corona tena za kutoka nje zinaweza kuja na vidudu; anabeza wavaa barakoa na kuweka total blackout kuzuia taarifa za uwepo wa corona nchini zisitolewe wala kuzungumzwa, huo si uongozi.

Unapochaguliwa kuwa Rais wa nchi basi automatically una ubia na maisha ya wananchi wako. Wanatarajia uongozi makini dhidi ya majanga makuu ya kitaifa. You have to show leadership.

Mimi Drifter kama mtu binafsi nina nyenzo kibao za kupambanua na kupambana na matatizo yangu. Naweza hata kwenda nchi za mbali kutafuta masuluhisho ya matatizo yangu ikibidi. Lakini mimi si kielelezo cha Mtanzania wa kawaida ambaye kwake maendeleo ni kuwa na bomba la maji la kijiji, shule ya kata, umeme wa REA, nk. Anayetegemea sana kuwasilisha masuala yake binafsi kwa Mwenyekiti wa kijiji/mtaa.

It’s futile to attempt rationalising incoherence for the sake of justifying leadership failure. Huhitaji kututishia “ubia” ili tusihoji mambo muhimu ya kitaifa. We are intelligent sufficiently.
Long lives Great Thinkers, long lives JF...
 
Rais Magufuli anajua anachokifanya, pia anajua kuna Covid19 phase II. Ila ameona athari za kuruhusu lockdown ya Nchi nzima kama wengine wanavyofanya itaathiri Sana Raia wake kuliko kutoweka lockdown.

Watanzania ni maskini wa kutupwa, tusije kufa kwa njaa kabla ya Corona.

Muhimu alichosema ni kuchukua tahadhali za kujikinga. Tahadhari ulizosema hapo juu ni muhimu zikachukuliwa na kila mwananchi,

Ila kulikuwa na haja yeye Kama Amiri jeshi Mkuu aseme kwa kusisitiza kuhusu hilo.
Erythrocyte huyu ndiye mwenye akili kuliko alilosema mbowe! Acha kushabikia watoa upupu kama Tundu Lissu
 
Rais Magufuli anajua anachokifanya, pia anajua kuna Covid19 phase II. Ila ameona athari za kuruhusu lockdown ya Nchi nzima kama wengine wanavyofanya itaathiri Sana Raia wake kuliko kutoweka lockdown.

Watanzania ni maskini wa kutupwa, tusije kufa kwa njaa kabla ya Corona.

Muhimu alichosema ni kuchukua tahadhali za kujikinga. Tahadhari ulizosema hapo juu ni muhimu zikachukuliwa na kila mwananchi,

Ila kulikuwa na haja yeye Kama Amiri jeshi Mkuu aseme kwa kusisitiza kuhusu hilo.
Kwanza hakuna anaetaka Lock down pia usisahau umaskini huo wao ndio wamewatengenezea watanganyika!

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Huwa naandika Mara kwa Mara hapa ...mitachukua muda mrafu MzeeMwanakjiji kurudi katika ubora wake...kupitia andiko hili Leo nasems ...itachukua muda mrefu saana kwa MM kurudi katika ubora wake!
 
Back
Top Bottom