Swali Gomvi: Korona 2.0 kwani Rais Magufuli ni mbia wa maisha yenu?

Swali Gomvi: Korona 2.0 kwani Rais Magufuli ni mbia wa maisha yenu?

Sijasoma hadi huko mwisho wa bandiko refu.

Hii hapa inatosha kabisa kujua umeandika nini huko.

1. Mstari wa kwanza unajitambulisha kuwa wewe ni "shabiki", hii ina maana unawapotezea muda wasomaji wako wasiokuwa "mashabiki" kama wewe kuendelea kupoteza muda wao kwa kusoma mambo ya 'kishabiki'.

2. Una hakika "unaelewa malengo yake na mitizamo yake"? Huwezi kuwa umepofushwa na "ushabiki" tu ulioutangaza hapa?

3. Unajuaje kwamba hili ni "wimbi la pili la corona" na sio wimbi lile lile la kwanza kutokana na kusitisha juhudi zote za kupambana na corona huko nyuma kwa madai kwamba haipo nchini bila ya ushahidi wowote wa madai hayo.

4. Unaandika kuwa "...kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili la maambukizi..., ambayo 'yanasemekana'; kwa nini watu wajadili mambo ambayo huna uhakika nayo wewe mwenyewe. Hii ni sehemu ya kuwavuruga na kuwachanganya akili waTanzania kama anavyofanya huyo unayemshabikia?

5. Mwisho unaandika, kama mtu aliyezinduka toka kwenye ndoto mbaya: "Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya..." Kwani wewe ungependa wamwangalie kiongozi wao kama "mpotoshaji" kama anavyojipambanua sasa hivi kuwa ndiyo lengo lake hasa kwa haya anayoyasemea juu ya ugonjwa huu na kutaka waTanzania waamini kuwa 'wazungu' kwa ujumla wao lengo lao ni kuwaangamiza watu weusi?

Naona hii itakuwa ni 'awamu ya pili' ya mkataba ulioingia na huyo mtu wako kwa kzai hii chafu ya kuwavuruga akili waTanzania.

Nchi inaingia vitani, nyinyi mnasema watu wafanye ya kwao wasimsikilize Jemadari mkuu; hiyo itakuwa vita ya namna gani.
Mwanzo unasema... "sijasoma hadi huko mwisho wa bandiko refu"... Lakini kwenye point na. 5 unasema mwisho amesema..... Sasa ikiwa wewe mwenyewe unajidanganya (halafu kwa akili yako unadhani unatudanganya sisi), nani atakayekyamini hapa??
 
Sisi wengine tunaamini baada ya Mungu ni Magufuli, huyu ameweza yasiyowezekana, ametuomba Watanzania tumuondolee magunzi (Wapinzani) tumeyaondowa yote tumempa safu ya kijani tupu, bunge la kijani.

Tuna imani kubwa na jemedari wetu na tumekubali kumkabidhi maisha yetu awe na ubia nayo.

Je vipi wewe shabiki wake? Unashabikia lipi mpaka uwe na mawazo mbadala badala ya kuandika mapambio?

Hypocrite.
Kuna wengine wanamuona ni mungu kabisa.
 
Ninachoamini ni kwamba ikitokea Corona umechanganya (Mola apishie mbali) watu wakaanza kudondoka kila kona, watu watajifungia wenyewe bila shuruti...
Uko sawa kabisa, Mimi wasiwasi wangu ni uwezo wa Mwananchi kumudu kula yake ya kila siku akiwa locked ndani.

Watanzania wengi wetu ni maskini Sana, ukitaka kujua hili Jaribu kuwa na shida ya 20M hivi then jaribu kuwapigia jamaa wakukope. Unaweza kuta unatafuta na usipate, hadi uende Benki kukopa.

Sasa vipi wale wa kule vijijini ambao unakuta wanategemea kilimo wavune ndiyo wale.

Kwa kweli Mungu atusaidie
 
"Watanzania ni matajiri sana na tunapaswa kutembea vifua mbele" In Magu voice [emoji16][emoji16][emoji16]
Hiyo ilikuwa ni kauli ya Kisiasa tu, hakuna lolote. Watanzania ni Maskini wa Kutupwa.

Ikitokea tumefanya lockdown tu, basi wapo Watanzania ambao watachinja hadi Paka/Mbwa kula.

Nimewahi kuhadithiwa kuwa wakati wa Vita ya Kagera Watanzania walikuwa Wanatumia sijui majani gani kufulia nguo badala ya Sabuni.

Ikija hiyo lockdown sipati picha 🙆
 
Yes that is fine, ulichoacha ni hiki:
Angekuwa JK (Kikwete) anasema maneno kama anayosema Magufuli; ingekuwa kinyume kabisa kwa comment zako. Ungeaapiza mengi sana. Ushabiki ni kweli huwa haujifichi. Hata Udini na Ukabila. Mambo yale yale aliyafanya KIKWETE anayafanya Magufuli, mnasema ati sawa kabisa. Hypocricy never hide. Ukweli ni kuwa Corona ikichachamaa hapa mtakuja na sabbabu nyingine, na wa Tanzania washazoea kudanganywa, watalia watasahau
 
Korona 2.0 Kwani Rais ana Ubia na Maisha Yenu?

Na. M. M. Mwanakijiji
Naandika kama shabiki wa Magufuli; naandika kama mtu ambaye nimeelewa malengo yake na mitazamo yake, na ninaandika kama mtu ambaye sijaegesha akili yangu mahali mwenyewe nikaondoka. Nimesoma na kufuatilia mijadala ya kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili (2.0) la maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) ambayo yanasemekana yanaendelea nchini mwetu. Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya na kwa kiasi kikubwa wanafanya hivyo kwa sababu Rais ndio kiongozi mkuu wa serikali na nchi.

Neno la Rais lina uzito wake, hofu za Rais zina uzito wake na ikumbukwe kuwa wengi wanachukulia kuwa kwa vile Rais ana watu wengi wanaomzunguka basi ana taarifa za mambo mengi ambayo labda watu nje ya serikali hawana. Aliposema watu wajifukize, mamilioni walijifukiza, aliposema watu wafunge na kuomba, watu walifunga na kuomba, aliposema watu waiage korona watu walifanya na send off! Na alipotangaza kuwa korona hakuna Tanzania na kuwa imekwisha watu waliamini hivyo.

Sasa hili wimbi la pili ni kweli? Kama ni kweli je Watanzania wafanye nini? Je, watu wanaokufa ni kweli wote wanakufa kwa korona au magonjwa mengine? Na kama wimbi hili kweli lipo kama nchi tufanye nini na kama mtu mmoja mmoja tufanye nini? Ni wazi msimamo wa serikali umetolewa na Rais jana huko Chato na kuwa hakuna mtendaji wa serikali atakayepingana na Rais kwenye hili isipokuwa kama yuko tayari kujiuzulu akipinga (resigning in protest). Kwa vile msimamo wa serikali unajulikana na kuwa serikali haitaleta lock down, na kuwa hata chanjo watu wafikirie mara mbilimbili basi sehemu ya nini kila mtu afanye ndio swali linalohitaji kujibiwa.

Ndugu zangu naandika kama shabiki; Watanzania msijitoe ufahamu na mkajifanya nyie fyatu! Rais si mbia wa maisha yenu, ya mababa na mama zenu, na wala si mbia wa maisha ya watoto wenu! Mnapougua, kuuguza na kuuguliwa yote hayo ni yenu; mauti yakiwafikia vilio ni kwenye nyumba zenu, jamaa, ndugu na marafiki zenu. Sasa kama hili ni kweli, kwanini watu wengine wafikiri wanaweza kuifanyia ibada imani ya mtu mwingine? Hivi, mnajua kwanini mitume wengine hawakuungana na Petro kujaribu kutembea juu ya maji japo wote walimuona Yesu akitembea juu ya maji na walimsikia Yesu akimwambia Petro atembee? (Mathayo 14:22-33).
View attachment 1687880

Rais Magufuli anaweza kuwa na imani kubwa kabisa hata ya kutembea juu ya maji na akatembea; lakini wangapi wanaamini kama yeye? Kama imani yako haijafikia ile ya Magufuli sasa unakanyaga maji ya nini?

Ndugu zangu kuna njia tatu/nne kubwa na za haraka za kupunguza maambukizi ya corona:

1. Vaa barakoa iliyotengenezwa na kitambaa cha pamba (siyo hariri). Kuvaa barakoa kuna kulinda wewe na kinamlinda mwingine. Ukivaa barakoa funika pua na mdomo (korona inaingia zaidi kupitia puani!)

2. Osha mikono kwa sabuni mara kwa mara; epuka kusalimiana na watu kwa kushikana mikono. Ikitokea hivyo hakikisha huingiza vidole midomoni au puani (jitahidi kuosha kabla ya kufanya hivyo na baada).

3. Jiweke umbali wa karibu mita moja kutoka kwa mtu mwingine ambaye si wa nyumbani mwako. Na hii inaendana na kuepuka misongamano isiyo ya lazima hasa mahali ambapo watu hawavai barakoa. Na wale wenye ndugu (wazazi, mababu wazee) waambieni wasiende makanisani au misikitini kwa wakati huu au makanisa na misikiti iweke taratibu za kuhakikisha watu wanakaa mbalimbali na wanavaa barakoa!

4. Jifukize nyungu; sijui ni kwa namna gani hii ilisaidie kuzuia wimbi la kwanza lakini kama watu watafanya tena na kwa wingi wao mnaweza kujikuta mnazuia tena wimbi hili la pili maana kama ni chanjo msijipe matumaini saini.

Njia hizo tatu ndio njia zitakazokinga maisha yako na maisha ya wale uwapendeo. Lakini kama unafikiria Rais ana ubia na maisha yako haya we. Kwa sababu lile swali la bahati nasibu ya Magufuli kama italipa bado linasimama.
Wewe nawe anti-vaxxer kama Magufuli?

Magufuli akiwaambia watu wajipige risasi utasema sio mbia wa maisha yao au utasema he is abdicating his responsibility in a criminally responsible way?
 
Mwanzo unasema... "sijasoma hadi huko mwisho wa bandiko refu"... Lakini kwenye point na. 5 unasema mwisho amesema..... Sasa ikiwa wewe mwenyewe unajidanganya (halafu kwa akili yako unadhani unatudanganya sisi), nani atakayekyamini hapa??
Hiyo "mwisho" umeelewa maana yake?
Maana yake ni kwamba namalizia ninayoandika katika kipande hicho nilichoki'quote'. Hopeless kabisa!

Lakini nikuulize. Kakutuma uje hapa kutetea aliyoandika?
 
PLEASE SEND THIS MSG TWICE TO ANY GROUP. ONCE TODAY AND ONCE TOMORROW.


Important Message for all

The hot water you
drink is good for your throat.

But this corona
virus is hidden behind the
paranasal sinus of your nose for 3 to 4 days.

The hot water we
drink does not reach there.

After 4 to 5 days
this virus that
was hidden behind the
paranasal sinus reaches your lungs.

Then you have trouble breathing.

That's why it is very important to take steam,

which reaches the
back of your paranasal sinus.

You have to kill this
virus in the nose with steam.

At 50°C, this virus becomes disabled i.e. paralyzed.

At 60°C this virus
becomes so weak that any
human immunity
system can fight against it.

At 70°C this virus dies completely.

This is what steam does.

The entire public
health department knows this.

But everyone wants to take
advantage of this pandemic.

So they don't share this information openly.

One who stays at home should take steam once a day.

If you go to the market to buy
vegetables,
take it twice a day.

Anyone who meets
some people or goes to office
should take steam 3 times a day.

Steam week

According to doctors,
Covid -19 can be killed by
inhaling steam from the nose and mouth,
eliminating the Coronavirus.

If all the people
started a steam drive campaign for a week,

the pandemic will soon end.

So here is a suggestion:

* Start the process for a week from
morning and evening, for
just 5 minutes
each time,
to inhale steam.

If we all adopt this practice for a week the deadly

Covid-19 will be erased.

This practice has no side effects either.

So please send this message to all your relatives,
friends and neighbours,
so that we all can kill this
corona virus together and live and walk freely
in this beautiful world.

Thank you
 
Unataka tu tuendeleze majibishano yasiyokuwa na tija.

Hao wanaoitaka wataipata wapi iwapo mwenye nchi yake kaikataa?
Mbona mkuu amesha kuambia, wale wa kwenda wameenda na baada ya kuchanjwa walikokwenda wamerudi na covid21( waliikwepa covid19).
 
Umesema unaandika kama shabiki wa Magufuli , huku ukijifanya hukuegesha akili yako mahali , hapa unadanganya , Wizara ya afya ambayo iko chini ya Serikali ya magufuli ndio yenye dhamana ya kutoa mwongozo kuhusu corona , kuitenga kwenye kampeni hii ni kujaribu kuunga mkono ujinga .

Nchini Tanzania yametolewa matangazo ya kudhibiti na kuwachukulia hatua wale wote wanaosambaza taarifa za corona , hii imetolewa na TCRA , kama watu wanaweza kujiamlia kuchukua hatua za kudhibiti corona hivyo vitisho vinatoka wapi ?

Hata hivyo kwa taarifa yako wewe Mzee Mwanakijiji na Mataga wengine wanaothamini matumbo yao kupitia serikali ya awamu hii na kusifia kila ushuzi ili kujikimu , hakuna kipindi ambapo viongozi wa Tanzania wamedharauliwa na wananchi kama kipindi hiki cha corona
 
Samahani mkuu 'Sem2708' naomba nikuulize swali:

Hivi kila aliyepo kwenye uongozi na katika vyama vinavyojitambilsha kuwa vya siasa ni lazima ajulikane kuwa ni "Mwanasiasa"?

Hakuna vigezo maalum vinavyohitajika kuwa navyo mhusika kutambulika kuwa yeye ni 'mwanasiasa'?

Akina Amin Dada, Bokassa, Mobutu, n.k., wote hawa wanajulikana kuwa walikuwa 'wanasiasa', kwa sifa tu ya kuwa kwenye nafasi ya uongozi wa nchi?

Hili neno "Mwanasiasa" ninaliona kuwa lina utata mkubwa. Mi nadhani kuna vigezo vinavyompambanua mhusika kuwa ni mwanasiasa, mbali ya yeye kuwa tu kwenye madaraka ya juu nchini.

Simwoni Magufuli kuwa ni mwanasiasa, kwa sababu haonyeshi dalili yoyote ya kuwa mwanasiasa.
Sawa mkuu ila mimi naamanisha hawa viongozi wetu ...
 
Back
Top Bottom