Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?

Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?

Duniani hapa kama una Technology na Leadership lazima tu utaendelea na hivyo ndivyo vitu ambavyo sisi kwa masikitiko makubwa hatuna.

Sisi kabla ya vita na Uganda tulikuwa na uchumi mzuri ktk ukanda wote huu lkn baada ya tu ya vita tuliambiwa tufunge mikanda kwa miezi 18 lkn hadi leo hiyo miezi 18 haijaisha...!!!

Kwa nchi za wenzetu wanasiasa wanawaheshimu sana wataalam na hawawaingilii ktk utendaji wao wa kazi na haya yanayoongelewa humu ni matokeo ya kuheshimu fikra za wataalam.

Sisi tunafanya mambo tukilenga kupata sifa za kisiasa ili iwe mtaji ktk uchaguzi na watalaam wetu wamekuwa heavily brainwashed politically na wenyewe kwa kuendekeza njaa wamekuwa hawawezi ku-practise kile wanachokiamini hasa hilo likiwa tofauti na anachoamini mwanasiasa.

Tumeona mengi kwa akina Mwakyembe, Kabudi na wengine wengi tu. Angalia miradi mingi inayoanzishwa ktk nchi hii ni ile inayochochewa kisiasa pasipo kuangalia Economic Benefits / Viability au hata Environmental Impact zake.

Nchi kama Russia ktk elimu yao wameangalia nini wanahitaji kama taifa na waka-design curriculum yao mahsusi kulenga hicho na ndio maana wana bajeti kubwa sana inayotengwa kwa ajili ya Research kwani pasipo Research hakuna Innovation.

Russia wana kila sababu ya kuendelea na watazidi tu kuendelea kwani wanawekeza ktk maendeleo na wana sera thabiti zinazolenga ktk dhana nzima ya maendeleo. Sisi ngoja tuendelee kuwawinda wale wapinzani wanaokataa sera yetu ya kuunga juhudi.

Duniani hapa kama una Technology na Leadership lazima tu utaendelea na hivyo ndivyo vitu ambavyo sisi kwa masikitiko makubwa hatuna.

Sisi kabla ya vita na Uganda tulikuwa na uchumi mzuri ktk ukanda wote huu lkn baada ya tu ya vita tuliambiwa tufunge mikanda kwa miezi 18 lkn hadi leo hiyo miezi 18 haijaisha...!!!

Kwa nchi za wenzetu wanasiasa wanawaheshimu sana wataalam na hawawaingilii ktk utendaji wao wa kazi na haya yanayoongelewa humu ni matokeo ya kuheshimu fikra za wataalam.

Sisi tunafanya mambo tukilenga kupata sifa za kisiasa ili iwe mtaji ktk uchaguzi na watalaam wetu wamekuwa heavily brainwashed politically na wenyewe kwa kuendekeza njaa wamekuwa hawawezi ku-practise kile wanachokiamini hasa hilo likiwa tofauti na anachoamini mwanasiasa.

Tumeona mengi kwa akina Mwakyembe, Kabudi na wengine wengi tu. Angalia miradi mingi inayoanzishwa ktk nchi hii ni ile inayochochewa kisiasa pasipo kuangalia Economic Benefits / Viability au hata Environmental Impact zake.

Nchi kama Russia ktk elimu yao wameangalia nini wanahitaji kama taifa na waka-design curriculum yao mahsusi kulenga hicho na ndio maana wana bajeti kubwa sana inayotengwa kwa ajili ya Research kwani pasipo Research hakuna Innovation.

Russia wana kila sababu ya kuendelea na watazidi tu kuendelea kwani wanawekeza ktk maendeleo na wana sera thabiti zinazolenga ktk dhana nzima ya maendeleo. Sisi ngoja tuendelee kuwawinda wale wapinzani wanaokataa sera yetu ya

Duniani hapa kama una Technology na Leadership lazima tu utaendelea na hivyo ndivyo vitu ambavyo sisi kwa masikitiko makubwa hatuna.

Sisi kabla ya vita na Uganda tulikuwa na uchumi mzuri ktk ukanda wote huu lkn baada ya tu ya vita tuliambiwa tufunge mikanda kwa miezi 18 lkn hadi leo hiyo miezi 18 haijaisha...!!!

Kwa nchi za wenzetu wanasiasa wanawaheshimu sana wataalam na hawawaingilii ktk utendaji wao wa kazi na haya yanayoongelewa humu ni matokeo ya kuheshimu fikra za wataalam.

Sisi tunafanya mambo tukilenga kupata sifa za kisiasa ili iwe mtaji ktk uchaguzi na watalaam wetu wamekuwa heavily brainwashed politically na wenyewe kwa kuendekeza njaa wamekuwa hawawezi ku-practise kile wanachokiamini hasa hilo likiwa tofauti na anachoamini mwanasiasa.

Tumeona mengi kwa akina Mwakyembe, Kabudi na wengine wengi tu. Angalia miradi mingi inayoanzishwa ktk nchi hii ni ile inayochochewa kisiasa pasipo kuangalia Economic Benefits / Viability au hata Environmental Impact zake.

Nchi kama Russia ktk elimu yao wameangalia nini wanahitaji kama taifa na waka-design curriculum yao mahsusi kulenga hicho na ndio maana wana bajeti kubwa sana inayotengwa kwa ajili ya Research kwani pasipo Research hakuna Innovation.

Russia wana kila sababu ya kuendelea na watazidi tu kuendelea kwani wanawekeza ktk maendeleo na wana sera thabiti zinazolenga ktk dhana nzima ya maendeleo. Sisi ngoja tuendelee kuwawinda wale wapinzani wanaokataa sera yetu ya kuunga juhudi.
Imeloa kabla ya kulogwa😂😂
 
Hakuna anayesumbuliwa na Russia wewe sijui upo dunia gani, juzi Russia ameenda kuomba msaada wa kuunga na North Korea kuunganisha nguvu ya pamoja mana US peke yake haiwezi na hata North Korea haikutosha kaenda tena Vietnum ni russia anatapa tapa alijinata yeye ni superpower Ukrean tu imemtoa mavi sasa mwaka 3
Kweli umekataa kutumia akili.ukraine huku akisaidiwa na NATO nzima wameshindwa kuwapiga Russia Ukraine.hizo nchi Amekwenda kuimarisha mahusiano hana sababu ya kuomba silaha kwa sababu anatengeneza mara 3 ya NATO
 
Ni ukweli kwamba hatua ya kimaendeleo iliyokwisha fanyika nchini Russia ukilinganisha na kiwango cha elimu waliyonayo na raslimali walizonazo haziendani kabisa.

Katika nchi tano zenye wasomi wengi duniani Russia ni moja wao na Russia ndio nchi inayoongoza duniani kwa kuwa na raslimali lukuki lakini bado ukienda ktk vijiji vyao huko ndani ndani bado unakuta wanahangaika kupata maji safi na salama ya uhakika na unakuta bado kuna kaya zingine zenye vyoo vya shimo (Pit Latrines) kama Afrika...!!!
Kwa ukubwa wa Russia, geographically haishangazi sana kuona baadhi ya vijiji vina changamoto mbalimbali katika maendeleo. Lakini sidhani kama ni Russia pekee wana changamoto kama hizo ulizozitaja.
Lakini pia mkongwe, Russia inaishi kwa vikwazo lukuki, hauoni kama walipo kama taifa wanastahili pongezi pamoja na vikwazo vya kiuchumi walivyonavyo?
 
Kwa ukubwa wa Russia, geographically haishangazi sana kuona baadhi ya vijiji vina changamoto mbalimbali katika maendeleo. Lakini sidhani kama ni Russia pekee wana changamoto kama hizo ulizozitaja.
Lakini pia mkongwe, Russia inaishi kwa vikwazo lukuki, hauoni kama walipo kama taifa wanastahili pongezi pamoja na vikwazo vya kiuchumi walivyonavyo?
Ukubwa au udogo sio sababu, Burundi/Rwanda ni mataifa madogo madogo sana lakini wenyewe pia wana changamoto hizo hizo.

Russia pamoja na kwamba waliharibiwa na akina Vladmir Lenin kwa kuwaletea mfumo wa hovyo wa kikomunisti lakini kutokutambua vipa umbele vyao kama taifa ni sababu nyingine kubwa inayosababisha iwe hapo ilipo.

Pia hiyo inasababishwa na utawala wa kiimla ambapo rais ndiye anayeamua kipa umbele kiwe nini na kwa rais wao wa sasa kipa umbele chake ni Russia yenye nguvu kijeshi tofauti na maendeleo ya kiuchumi.
 
Sawa kabisa,

Lakini kuhusu hiyo sera ya Revanchism nadhani iko kwa kila taifa kubwa hapa duniani (Inherent to any Global and Regional Power) sema kwasababu wengi huwa hamuipendi Urusi kwasababu ambazo mnazifahamu wenyewe na hata kushindwa kukubali kwamba kinachofanywa na Urusi hufanywa na mataifa yote makubwa duniani, tena huenda vibaya zaidi kupita Urusi.

Hicho unachokiita Revanchism, kikawaida ni Imperialism tu sema tumeamua kutumia neno jingine. Haya hebu zingatia haya yafuatayo:
  • Kule Urusi inaitwa Revanchism ambapo kweli Urusi anavunja sheria za kimataifa na kuvamia mataifa halali kijeshi na kujimegea vipande vya nchi, akisingizia analinda usalama wake. Kuhusu Russian Revanchism hili ni kweli kabisa, kila taifa linatakiwa liheshimu Political Independence, Territorial Integrity and Sovereignty of other nations.

  • Kule Israeli wanaiita The Right to Return (Aliya) ambayo inasindikizwa na Genocide kabisa. Tena hiki wengi humu ndani mmekuwa mkikishabikia kwa nguvu kweli kwasababu za kidini na kisiasa. Wazungu wa Ulaya waliotokea Urusi, Poland na Ukraine wanaamini kabisa wana haki ya kuishi kwenye eneo linaloitwa Palestina kuliko jamii za Kiyahudi na kiarabu ambazo zimeishi pale kwa miaka zaidi ya 2000. Hili ni hatari kuliko hata anachokifanya Urusi. Kituko ni ule mfano anaoutoa mwanahistoria wa Israel Illan Pappe kwamba "Most Zionists don't believe in God, yet they believe that he has given them land in the Middle-East". Kituko kingine ni hiki, Hii Revanchism ya Israeli inaungwa mkono na mataifa makubwa kama Marekani, Uingereza na Ufaransa ambayo hayaungi mkono Revanchism ya Urusi kule Ulaya Mashariki. (Hakuna utofauti wowote na anachofanya Urusi)

  • Kule Marekani wanaiita Manifest Destiny/The Munroe Doctrine na wote tunajua nini kinazikuta nchi za Western Hermisphere pindi wanaenda kinyume na Marekani. Haijapita hata miaka 50, tangu serikali ya Ronald Reagan ifanye ambacho Vladmir Putin anakifanya leo kule Ulaya Mashariki. Mwaka 1983 alivamia Grenada na kumtoa Waziri Mkuu halali wa nchi Maurice Bishop na kuweka kibaraka wao. Ila zaidi ya hapo, Marekani alituma magaidi kuvamia Nicaragua hadi kupelekea The Contra-Affair. Yote hayo viongozi waandamizi wa Marekani kama William Casey walisema ni kwa ajili ya kulinda maslahi na usalama wa Marekani unaohatarishwa na nchi jirani. (Hakuna utofauti wowote na anachofanya Urusi)

  • Kule Uingereza wameipa jina zuri The Commonwealth of Nations ila malengo ni yaleyale, Restoration of the Influence of the British Empire through the backdoor. Ndiyo maana kipindi cha harakati za kupigania uhuru wa Northern Ireland almaarufu kama The Troubles, Uingereza inayojiita nchi ya kidemokrasia ilifanya mauaji ya kutisha ili Northern Ireland isijitoe kwenye The Commonwealth of Nations. Sababu hiihii ya kuamini katika Old Glory ndiyo inazuia harakati za Scotland na Australia kujipatia uhuru wao zenyewe bila kukutwa na mkono wa chuma wa mabwanyenye ya Downing Street. Gough Whitlam waziri mkuu wa Australia alipinduliwa kimabavu na MI6 na CIA pale alipotaka kuiondoa Australia kwenye kambi ya mabeberu na kuifanya isifungamane na upande wowote kwenye Vita Baridi. (Hili la kumtoa Whitlam kibabe halina utofauti na lile Urusi walimfanyia Raisi Viktor Yushenko wa Ukraine)
Mifano iko mingi sana hapa duniani, endapo tutachambua bila kuweka mizania ya upendeleo. Kule Ufaransa wanatumia Francophones System na CFA Franc kutawala nchi za Afrika, ambazo zimelazimishwa zisiwe na Central Bank, na akiba yao yote ya fedha za kigeni iko mikononi mwa Ufaransa ambaye ni lazima wamwombe ruhusa ili watumie akiba yao. Hata Uturuki naye anafanya hivyohivyo kule Cyprus, Greece, Azerbaijan-Armenia, Serbia na Albania, kwa kutumia waislamu wenye asili ya kituruki kuvuruga amani na kueneza ushawishi wake.

MWISHO KABISA: Ambacho Urusi anakifanya kule Ulaya Mashariki ni kinyume na sheria za kimataifa. It's simply Illegal, defies common precepts of decency and I don't condone it. Japo ukweli ni kwamba hakuna taifa kubwa duniani ambalo halifanyi ambacho kile Urusi wanakifanya kulinda maslahi yao aidha ya kiuchumi, kiusalama na kiutamaduni hata kwa mbinu ambazo ziko kinyume na utaratibu wa sheria za kimataifa ambazo zina mzizi kwenye mkataba wa Westphalia (Treaty of Westphalia) wa mwaka 1648, uliomaliza vita mbaya ya kidini iliyopiganwa miaka 30 baina ya Waprotestanti na Wakatoliki ambao walikuwa wanavutana juu ya mambo hayahaya unayoyasema hapa (Catholic Revanchism and Imperialism).

Mkataba unasisitiza katika kuheshimu, State Sovereignty, Political Independence and Territorial Integrity hata pale ambapo taifa kubwa halikubaliani na falsafa za kisiasa na kidini za taifa dogo.

ENIWEI kwasababu tumeshaamua kuamini kwamba RUSSIA IS A BAD GUY with no legitimate security concerns and interests, na kila kinachofanywa na Wamarekani, Waingereza, Wafaransa na Wayahudi ni sahihi kwasababu ni GOOD-GUYS, basi sidhani kama hata tukifanya mjadala wa miaka 10,000 naweza kukubadilisha.

=====================================================
Ila uhalisia, ni ule ambao Professor John Mearsheimer amekuwa akiusema siku zote kwa zaidi ya miaka 40 sasa. Kwamba hakuna taifa kubwa takatifu (Benign Hegemony), kwamba liwe na mabavu halafu lisijaribiwe kutumia hayo mabavu kujipatia kila linachokitaka, aidha kijeshi au kwa namna yoyote ile.

Haya Mkuu uwe na siku njema, I rest my case!
Shukrani kwa uchambuzi wako.

Nafahamu vyema wazo kuu la uchambuzi wako kwamba mataifa makubwa huwa na sera, mikakati na matendo mbalimbali [halali na haramu kulingana na sheria za kimataifa] kwa kisingizio cha kulinda maslahi ya taifa/kitaifa. Hii hoja uliyoisema hapa nimewahi kuisema pia humu jukwaani miaka kadhaa iliyopita kwa maneno tofauti kidogo.

Pitia uchambuzi huu hapa chini:

Kwa vile mada iliyoletwa jukwaani (natambua ni ya zamani kidogo) haihusu mfumo wa uhusiano wa kimataifa wa dunia yetu kwa ujumla wake unaozingatia "maslahi ya taifa/kitaifa" bali ni mahususi kwa ajili ya Urusi/USSR, nimeamua kujikita zaidi kuizungumzia Urusi ama USSR pekee na sera au matendo yake ya kihistoria ambayo yamepelekea athari au mabadiliko makubwa katika siasa za jiografia na uhusiano wa kimataifa.

Mambo mengi uliyosema ikiwemo mifano uliyoambatanisha na hoja yako kuu (maslahi ya taifa/kitaifa) ni masuala ambayo yanahitaji mijadala mipya kabisa (separate) na tunaweza tusikubaliane katika baadhi ya masuala hayo uliyoyasema.

Lakini, kwa kiasi kikubwa nakubaliana na wewe kwenye msingi mkuu wa hoja yako kwamba mataifa makubwa, yenye ushawishi mkubwa katika masuala ya kijeshi, kisiasa na kiuchumi yamekuwa na sera, tabia au mienendo fulani ndani na nje ya mipaka yao kwa kisingizio cha kulinda maslahi ya taifa/kitaifa ambayo wakati mwingine ni kinyume na maslahi ya wengine ama sheria za kimataifa.

Kimsingi, dunia imekuwa ikiendeshwa kwa nguvu na ushawishi wa kitu kinachofahamika kama "maslahi binafsi" ili kujihakikishia survival. Hilo lipo tangu zamani [karne nyingi zilizopita] na hata ukisoma vitabu vya dini zinazoaminika hivi sana duniani, utakutana na matendo kama haya yaliyopo hivi sasa kwa jina lilelile la kulinda maslahi ya taifa ama jamii ya watu fulani walioishi zama za kale.

Nadhani hata John Mearsheimer analifahamu hilo vyema ingawa amekuwa akikosolewa vikali na wasomi wenzake wa masuala ya siasa za kimataifa kutokana na baadhi ya misimamo yake na vilevile kwa kutokuwa consistent kwenye masuala kadhaa mahususi yahusuyo geopolitics hususani za Mashariki ya Kati na issue ya Ukraine na Urusi.

Kwa kusema hayo, nafikiri mada kuu iliyowasilishwa jukwaani imepatiwa jibu/jawabu. Shukrani!
 
Hakuna anayesumbuliwa na Russia wewe sijui upo dunia gani, juzi Russia ameenda kuomba msaada wa kuunga na North Korea kuunganisha nguvu ya pamoja mana US peke yake haiwezi na hata North Korea haikutosha kaenda tena Vietnum ni russia anatapa tapa alijinata yeye ni superpower Ukrean tu imemtoa mavi sasa mwaka 3
It seems time has vindicated me.​
 
Wasichokijua Wengi Kuwa Urusi ni taifa tajiri kinishati na kiteknologia..

Bila gesi ya Urusi chi nyingi za Ulaya watu watakufa kwa baridi, mfano Italia inategemea Gesi ya Urusi kwa asilimia 80%
Muda ni mwalimu mzuri sana.​
 
Back
Top Bottom