Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?


Kweli mkuu duniani hakuna urafiki wa kweli baina ya nchi changa na mabepali huwa haitokei ni kimasirahi zaidi
 
Wameshindwa kutengeneza stealth plane..
Rejea hotuba ya Putin ya mwaka 2007 huko Ujerumani kwenye kongamano la usalama la kimataifa. Alisema hivi( tafsiri isiyo rasmi), " Russia haina ela ya kutengeneza silaha za bei kubwa kama hiyo project f35 ili ile ulinganifu wa nguvu za kijeshi duniani, baada ya kuona kuna nchi moja inatumia vibaya nguvu zake za kijeshi kuharibu ustawi wa dunia. Lakini lazima Russia ilejeshe ulinganifu huo kwa kutumia mtindo wa Asymmetry ( wanamahesabu watasaidia kufafanua hili). Kwa NATO kuleta silaha za kujilinda karibu na mipaka ya Russia kisa eti ni kujilinda dhidi ya Iran na North Korea hiyo haikubaliki, Russia itatengeneza silaha ya bei rahisi ambayo itaweza kukwepa silaha hizo za kujilinda dhidi ya NATO" mwisho wa kunukuu.

March, 2018 Putini kautangazia ulimwengu kuwa ulinganifu wa nguvu za kijeshi duniani unaelekea kurejeshwa. Silaya ya kukwepa' THAAD ' mitambo nadhani iliyosimikwa Poland na kwingineko ya US tyari Russia kashaipata. Na wamsikilize sasa. Asymmetry hiyo.

US walitengeneza stealth plane ya bei kubwa kabisa...lakini ndege hiyo performance yake ni utata...kudhibitisha hilo, US anagoma kumuuzia Turkey ndege hizo kisa tu Turkey kapanga kununua S400 za Russia...na US hawafichi wanasema hiyo mitambo ita'compromise' ndege hizo...Sasa kama Yuesi(US) alitengeneza stealth plane...kweli inakuwaje anakuwa na wasiwasi na S400!? kuna Stealth plane hapo..kweli?!.hata hivyo ni kukumbushe tu ahadi ya Putin, ya ASYMMETRY...! ahadi hiyo ameifanyia kazi pia kwa stealth plane ya US.
----
Leta hoja nyingine, mkuu kuhusu hili. Karibu.
 
Ahsante sana mkuu,
Sasa kama Urusi alikuwa na nguvu nyingi zaidi ya hizi za leo kwanini alishindwa Vita Baridi ??
Katika mantiki hii unataka kuniambia kwamba Urusi ya zamani ilikuwa na nguvu kuliko Marekani ??
Kwa uelewa wangu ni kwamba, urusi kabla ya vita baridi haikuwa na nguvu kama marekani, bali nguvu ya urusi ilikuwa inachagizwa na umoja wa ussr na ikumbukwe kuwa baada ya ussr kuvunjika urusi ilibakiwa na idadi ndogo ya watu, kwa maana hiyo idadi ya watu ilikuwa kubwa kutokana na umoja huo, baada ya vita ndipo urusi ikajikita katika kukuza rasilimali watu na kuweka mkazo katika elimu na tafiti za kisayansi.
 
Hawa waruss hawa...binafsi nawakubali sana.sababu ni watu wasioteteleka...
Mwaka 1991 Soviet union ilipokufa ghafla mataifa ya magharibi yaliona ndo wakati wa kujipenyeza Urusi....na watu wengi walijua ndo mwisho wa Urusi kama ikivyotokea kwa Ujerumani,Japan etc..
Kitu cha ajabu jinsi miaka ilivyoenda ndo kwanza wanazidi kujitenga na Western countries....kuna New World Order na Balance of power waruss wameleta duniani...
Ni nchi pekee ambayo inaweza mjibu marekani na kumkosoa ..angalia suala la Syria....kuna vitu vingi vya kusema but kwa ufupi yajayo yanafurahisha sana..
Hali ikiendelea hivi ndani ya miaka 10 ijayo Waruss na Wachina watakua wanarun show....
 
Sasa kama Urusi ndiyo kichwa cha treni mbona anahangaika sana kuzuia Ukraine, Georgia zisiingine kwenye Umoja wa Kujihami wa nchi za Magharibi (NATO) na Umoja wa Ulaya (EU) ???
 
Sasa kama Urusi ndiyo kichwa cha treni mbona anahangaika sana kuzuia Ukraine, Georgia zisiingine kwenye Umoja wa Kujihami wa nchi za Magharibi (NATO) na Umoja wa Ulaya (EU) ???

Zinapata ugumu sana katika kuingia huko. Hata kama zikiingia huko hazipati ulinzi kama katiba ya NATO ilivyo.

Nitakukumbusha tu kuwa sehemu muhimu ya katiba ya ni kuwa NCHI MOJA KATI YA ZILE ZILIZO KATIKA UMOJA WA NATO IKIVAMIWA INAMAANISHA NATO NZIMA IMEVAMIWA, KWA HIYO UMOJA HUO UTASHIRIKIANA KUIKOMBOA AU KUPIGANA NA WAVAMIZI.

Nikueleza kitu, Sakashivile (aliyekuwa Rais wa Geogie wakati inavamiwa na mrusi) alisikitishwa sana na NATO iliposhindwa kutuma hata askari mmoja wakati Urusi inaivamia Geogia. Influence ya Urusi nchini Geogia ni kubwa kuliko ya NATO, amini usiamini.

Ukraini nayo ilipovamiwa hatukuwaona askari wa NATO kwenda kupigana huko. Mpaka leo hivi ninavyokwambia sehemu ya Ukraini (Kremia) iko chini ya warusi mpaka leo, lakini NATO haijaenda kuwakomboa.

Siasa za dunia hii ni ngumu kuliko mimi na wewe tunavyofikiri. Mi si shabiki wa NATO wala URUSI, ila kuzielewa siasa za haya mataifa ni muhimu kwa vile kinachotokea huko kinatuathiri hata sisi Afrika.

Angalia dunia na waasi wa Siria walivyo mu-underate Mrusi katika maendeleo ya vita vya Siria, imesababisha vifo vya watu wengi bila hata kupata kile walichodhani ni rahisi kwa vile wanaungwa mkono na NATO (Ulaya na Marekani). Lakini hali haikuwa rahisi mpaka leo wewe ni shahidi kinachoendelea huko na upande upi umesonga mbele zaidi.

Napenda kusisitiza tena na tena kuwa mimi si mshabiki wa pande yeyote kati ya hizo mbili, ila ninachosema ni kuwa kabla nchi zetu hazijafanya maamuzi tusiwadharau mmoja kati ya mahasimu hao. Sijui nani ana nguvu kuliko mwenzio, ila wote wanaathari katika maisha yetu.
 
Mkuu mbona Georgia na Ukraine sio wanacahama wa NATO ? ninachofahamu ni kwamba nchi zote mbili zinataka kujiunga NATO lakini kwa sasa si wanachama bado.
 
Katika warusi was JF wewe ndo mrusi pekee unaejielewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…