Swali: Hivi kwa sisi wazazi ukisikia mtoto wako wa kiume anavuta sigara, unamkanyaje?

Wewe unashabikia yanga unataka mwanao afanye nini
Anyway Kuna jamaa namfahamu anafanya kazi NMB wilaya frani,ni very smart ila anakula chigga,kiukweli hua namdharau mnoooo
Sasa sigara na wee kimdharau inahusu nn? Km yuko smart na kazi zina muendea, anapungukiwa nn? Si unaumia mwenyewe ukute hata hajui km una mdharau, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Wabongo bhana, wanavhekeshaaa mnoo.
 
Bora huyo analala na dada wa kazi, huyo ni rijali japo siyo tabia njema. Ungesikia analala na kijana mwenziye ungezimia
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ila watuu khaaah.
 
Tabia za foolish age hizo, Mzazi usipokaza kipindi hicho ndiyo unaweza poteza Mtoto, maana ndiyo umri wa makundi!!
Ningefahamu umri wa huyo kijana wake ningechangia.
 
Dr Matola PhD, mbona formula ya Ubaba iko wazi kabisa, "as long you are under my roof,na Sheria za Baba ndiyo zitakua final kwenye mgogoro wowote ule! Na atakae jaribu kupinga maelekezo, Vikwazo vya kiuuchumi vinamuhusu ikiwepo na mpingaji ajitafutie mji wa kufanya mambo yake kwa uhuru!!
 
It's really challenging kumfukuza mtoto nyumbani ambaye hajamaliza hata kidato cha Sita.

By the way ni jambo lakumuonya tu.

Kama Baba asipokusikia ni kumhandle polepole
 
Safi sana[emoji106]
 
It's really challenging kumfukuza mtoto nyumbani ambaye hajamaliza hata kidato cha Sita.

By the way ni jambo lakumuonya tu.

Kama Baba asipokusikia ni kumhandle polepole
Wwe kuna mitoto mingine hata Mzazi aseme vp pamoja na kutumia viongozi wa Dini lakini toto halisikii, ndiyo kwanza kila siku unaitwa police au Serekali za mita na kwa Mjumbe kesha haribu huko! Mtoto wa kusikia hata hutumii nguvu kubwa kumuekewesha na akakuelewa!!
 
Mimi nimeanza kuvuta sigara form 2 au 3 nna faham njia gani ukitumia unaweza muweka mwanao na sigara na vilevi kibongo bongo kuvuta sigara, tumbaku, ganja ni swala la asili na wala halihusiani na ukosefu wa maadili ni kama unavoona kila mchina unaekutana nae anavuta sigara lakini sio kwamba hawana maadili au hawa perform vizuri majukum yao,
Sigara sio nzuri ina madhara kama ilivyo pombe tu
Hizi ni baadhi ya sababu zinazopelekea watu wengi kuanza kuvuta sigara:-

1. Stress za mapenzi
2. Upweke
3. Makundi
4. Mambo ya genetics ( yani hapa kitu inakujaga tu mtu anajikuta anamapenzi na nicotine anakua karithi icho kitu kama watu wanavyorithi umalaya[emoji16])
5. Kutokuwa na hofu ya mungu
6. Movies na video mbali mbali za musiki
7. Kupenda kujaribu jaribu mambo ( hii ipo kwa watoto wengi wakiume na ndo maana 95% ya wanaume washawah kujaribu mchezo wakuvuta sigara either karatas au kuokota vishungi

Huwezi kumzuia kwa kumtajia madhara au kwa kuwa mkali HAIPO IYO ataongeza mbinu za kujificha apo sasa fegi ndo inakua tamu vibaya mno yani unaenda kuitafutia utulivu si mnajua kitu cha wizi kinavokuwa kitamu

Chakufanya we muulize anatumia sigara gani mnunulie kama box 10 uwe unampa avute tu kila muda ukimuona tu ye si anajifanya gari moshi
 
Heshima nyingi kwako mkuu
 
Aaa mambo yangu ayo nicotine na caffeine kwakweli hivi vitu navipenda kutumia kwa pamoja.
 
Nyumbani kwangu ni no smoking zone, iko hivyo miaka yote hata uwe rafiki yangu sigara Nyumbani kwangu ni marufuku utavutia nje au subiri tukifika pub hata Mimi naweza kupiga ile ya kusindikizia kamnyweso.
Ikiwa unavuta kwanini inakusumbua mwanao kuvuta?

Mimi mzee hakuwa mnywaji wala mvutaji. Na wanae tumekua hivyo, na wanangu ingawa wadogo bado ila hawajawahi niona nimeshika pombe wala sigara.

Naamini lifestyle yangu ina ushawishi kwa wanangu
 
Vizuri sana[emoji122]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kuna wakati ni lazima usimame kama mkuu wa familia
Sasa ukuu sio kushika bakora na kumtandika kisa tabia yake iliyopotoka jiulize ana miaka 2 au amevuka miaka 18 ?

Ndio maana nikakwambia zungumza nae mtoto wako kwa upole Jenga ukaribu nae msikilize kwa umakini acha kujifanya bwana jela, tabia zake zimechangiwa na tabia zako jichunguze wewe kwanza ni tabia zipi ulizonazo zilizopelekea mtoto wako kuingia kwenye tabia usiyoipenda baada ya kujua hilo jisahihishe au muulize yeye ni nini kinampelekea kua na tabia usizozipenda nasisitiza acha ubabe zungumza kwa upole Mzee kua mpole ukijifanya mbabe utakua unakoleza KUNI na kuzichochea atakua smoker mara 2 ya unavyomuona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…