Ikiwa unavuta kwanini inakusumbua mwanao kuvuta?
Mimi mzee hakuwa mnywaji wala mvutaji. Na wanae tumekua hivyo, na wanangu ingawa wadogo bado ila hawajawahi niona nimeshika pombe wala sigara.
Naamini lifestyle yangu ina ushawishi kwa wanangu
Kama itakuwa umenisoma vizuri Nyumbani kwangu sigara ni marufuku hata uwe ni rafiki yangu nakuheshimu kiasi gani ni big no.
Tukiwa kwenye vikao vyetu vya kukemea uzee hapo sigara ruksa hata Mimi naweza kuvuta kusindikiza kamnyeso.
Kumbuka Mimi si mvuta sigara wa kwenda dukani kununuwa sigara, Bali nikiwa kwenye shangwe ndio naweza kuvuta na inaishia huko, hakuna mtoto wangu yeyote anayejuwa kwamba huwa nagusa sigara.
Labda nikuweke wazi, my first born anamalizia masters yake University, huyu huwa nakaa naye tunapiga wote gambe ni adult tayari ila ni yeye mwenyewe aliamuwa kuunganisha masters baada ya first degree.
Nataka kuwa mkali sana kwa huyu wa high school kwa sababu yeye ndio mwenye bahati ya kwenda kusoma University akifanya vizuri form na kupasuwa vizuri.
Nayajuwa maisha vizuri, nimeanza maisha ya kupiga box mamtoni nikiwa Mdogo, nawajuwa age mates wangu ambao tulikuwa nao Uingereza walilipiwa ada na Wazazi wao na hawakurudi na vyeti Bongo.
Nimeuza asset zangu nyinyi ambazo nimezipata kwa machizi jasho na damu, sitaki kuona nainvest ujinga, Nina wadogo zao, nikishawatowa wao hata nikiishiwa nguvu wao ndio wa kuhakikisha wadogo zao wanapata quality education kama waliyopata wao.
Tena asiponisikiliza pesa yangu atakula last born wa kike na nitamkatia bima ya maisha yeye amalize form six aendelee kuvuta sigara vizuri.