Swali kuhusu tabia ya kususa, kugomea au kuzira: Je, si tabia za kike, si utoto?

Swali kuhusu tabia ya kususa, kugomea au kuzira: Je, si tabia za kike, si utoto?

Mkuu The Big Boss, naomba nikuhakikishie katika maisha yangu yote, sijawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa. Paskali, hanunuliki na yeyote kwa lolote kwa sababu hana price tag. Mimi ni priceless, sio CCM wa Chadema, wala Ukawa, wala Lowassa wala Magufuli, ana uwezo wa kuninunua, kwa sababu I'm not for sale, na sina any price tag!.

Naomba uniamini hili ni swali tuu, nimeuliza hawa wanaosusa, wamesusa ili wapate nini?!.

Ni swali tuu.

Paskali
😄😄😄😄😄😄😄 eti paskali hanunulik!!!!!
 
Wanabodi,

Hili mada ya swali kuhusu tabia ya kususa, kisiasa, huu mtindo wa kuzira au kususa susa, kususia kila jambo usilokubaliana nalo, sio tabia za kike hizi?, au sio tabia za kitoto?!. Mtu unasusia jambo fulani la kisiasa, ili upate nini?. Kususia jambo lolote la kisiasa bila kupiga hesabu ya what do you want to achieve na kususa huko, sio political suicide?.

The Motive Behind Kususa.
Jee ni nini the motive behind kususa jambo fulani, una susa ili uachieve nini, na baada ya kususa, jee hao wasusaji huwa wanakipata kile walichokusudia?!. Kususa jambo fulani bila malengo, sio tuu ni utoto, bali ni ujinga, kwa sababu ni sawa na kumsusia ngedere shamba la mahindi!, utayavuna mabua!.


My Take. (Maoni Yangu).
Kususia kushiriki uchaguzi sio suluhisho, huku ni kujiua kabisa kisiasa, dawa ni kujenga hoja madhubuti na kukaa mezani kuzungumza, vingine tuitumie mahakama yetu kuzifumua sheria kandamizi za uchaguzi ili zituletee uchaguzi huru na wa haki.


1. Tume yetu ya Uchaguzi NEC, japo sio inclusive lakini ni Tume Huru, licha ya kuteuliwa na rais ambaye ni Mwenyekiti wa chama kimojawapo, kwa uhuru ule ule wa Mahakama zetu ambazo majaji huteuliwa na rais huyo huyo ambaye pia humteua Mtendaji Mkuu wa Bunge letu. Kama Bunge limeweza kuwa huru kwa mfumo huu, na Mahakama ni huru, hata Tume pia ni huru, ila ionekane kuwa huru, something more needs to be done kwenye Tume Hii.
2. Sheria yetu ya uchaguzi, ina mapungufu makubwa yanayohitaji kufanyiwa marekebisho ili kutoa ushindani wa haki. Tusiilaumu Tume kwa chochote kinachotokea kwa sababu Tume inatekeleza sheria zilizopo, kama ni sheria kandamizi, ni kosa la sheria na aliyezitunga na sio kosa la mtekelezaji.
3. The political game playing field is not level, we need to create a level playing field ili kupata ushindani wa haki. Hili nalo ni tatizo la kikanuni, mfano uchaguzi wa 2020, kuna mgombea mmoja anaingia kwenye kinyanganyiro na vingora, msafara, media, na wasaidizi kibao, huku budget yake is fully footed by state, ashindane na makapuku!, unategemea nini?. Tangu tumeanza uchaguzi wa vyama vingi, kuna chama dola kinashindana na vyama makapuku!.
4. Now it's high time vyama vya siasa, vianze kutake responsibilities kwa matokeo ya utendaji wa vyama vyetu kwenye chaguzi mbalimbali, kwa kukubali kushiriki uchaguzi katika mazingira haya, na tukishindwa kihalali kwenye sanduku la kura, katika uchaguzi huru na wa haki, tukubali matokeo, na sio kutafuta visingizio.
5. Lazima tufike mahali, kwa pale ambapo uchaguzi ulikuwa huru na wa haki licha ya kasoro za hapa na pale, ambazo hazitaathiri, matokeo ya jumla ya uchaguzi huo, tujifunze kukubali matokeo na kushindwa kihalali, asiyekubali kushindwa sio mshindani. Kisha turudi nyuma kujitathmini where did we go wrong. Tulipaswa kufanya nini ili kupata ushindi katika mazingira kama haya.
Conclusion.
The bitter reality kwa wapenda demokrasia wa kweli wa mfumo wa vyama vingi nchini, mimi nikiwemo, tumeshuhudia hali hii ndio uwezo wa ushindani kwa vyama vyetu vya upinzani nchini Tanzania ndio umefikia hapa baada ya miaka 26 ya vyama vingi, naweza kusema kuwa this is the peak ya upinzani Tanzania, upinzani Tanzania, ndio imefika mwisho wake sasa!. Sasa tuanze kujiuliza, jee kama hali ni hii sana, je hali itakuwaje kwa uchaguzi wa 2020?. Kama wapinzani hawatabadili mbinu na strategies, za namna ya kushindana na CCM kwenye ushindani usio sawa kupitia sanduku la kura, then, uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, kuna hatari kubwa kwa CCM, kuyarejesha majimbo yote ya uchaguzi yaliyokuwa yanashikiliwa na upinzani, hivyo kuirudisha Tanzania kuwa ni nchi rasmi ya chama kimoja cha siasa, something which is not healthy at all to true modern democracy!.


Hongereni sana CCM kwa ushindi mtamu.
Poleni sana Chadema/Ukawa kwa kupoteza majimbo, wabunge na madiwani.


Tanzania kama taifa, tujipe pole kwa gharama kubwa za chaguzi hizi, ila tuombe sana Mungu alisaidie taifa letu kama gharama hizi za uchaguzi wa kinachoitwa demokrasia ya uchaguzi huru na wa haki, zinajumuisha, machozi, jasho na damu za Watanzania, kwa kugharimiwa na damu na roho za Watanzania, hakuna namna nyingine yoyote ya fidia kwa damu za watu na roho za watu, zaidi vya karma!'

Nawatakia Furahi Day ya Ijumaa Njema.

Wasalaam.

Paskali

Rejea za kuhusu Kususa.
Baada ya uchaguzi wa 2010, Chadema ilisusia matokeo na kujidai kuwa hawamtambui JK, ila bunge tuu lilipoanza, niliibua mjadala huu
Chadema Yakubali Yaishe! Yamtambua Rais!, Yampongeza Rais!.


Matokeo ya Chadema Kususia Hotuba ya JK na Kuapishwa kwa Pinda

Media Kususia Habari za Fulani: Jee Tanzania Tuna Independent Media Yenye Jeuri Hiyo?.

Uchaguzi wa 2015 Ukawa wakadai Lowassa ndie mshindi, hivyo wakajifanya kususa, na kutomtambua Magufuli, mimi niliwapa ushauri ufuatao
Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali ya Magufuli ni Serikali Haramu. Hukumu ya Karma ii Juu Yake!.


Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Hata kama ni kweli uliibiwa kura; Kaa kimya, Mungu ndiye akupiganie!

CUF kushiriki Uchaguzi wa Marudio Zanzibar si hiyari, Ni lazima! Vinginevyo, huo ndio mwisho wake - JamiiForums

Hatimaye CUF 'Wameridhia' Rasmi, Kushiriki Uchaguzi Wa Marudio Zanzibar!. - JamiiForums

Japo umegharimiwa kwa machozi, jasho na damu, ulikuwa huru na wa haki!. Hongera CCM, CHADEMA poleni!. Mungu saidia Tz - JamiiForums

Ujio wa Lowassa CHADEMA: Kuna kundi wamesusa, wanapanga kurejea CCM! - JamiiForums
Kuendelea kushiriki hizi chaguzi ni kuwapotezea wananchi muda wao, ukweli ni kwamba ccm imesha wadharau wananchi kupita kiwango, jambo muhimu kwa chama mfu kama ccm ni kujitafakari walipo kosea, na kubaki kuiba kura na kuidanganya dunia kuwa watanzania bado wanakipenda hicho chama ni upuuzi ulio pitiliza, Bashiru na Polepole wana uwezo mdogo sana was kisiasa.
 
Mayala wewe ndo maana ulitukanwa wazi wazi na magufuri ukashangilia. Ccm inavyofanya na dola unaona ni sawa??? Acha upambaf, watu wanauawa na kuteswa sana, mbona huhoji wala kuandika chochote?


Hivi kwanini wachangia hoja wengi hatumuelewi huyu Mayala mpaka wengine wanamwita njaa? ndugu yangu kama umesoma hoja zote alizoziweka Pasco kwenye bandiko hili basi utaona kuwa maswali yako kaweka majibu mazuri tu ambayo si ya kutunga....lakini swali la msingi linabaki palepale kuwa "Tabia ya Kususa, kuzira au kugomea" nafikiri Pasco anajua jibu lake ila anataka watu nao wachangie
 
Wanabodi,
#paskali uwe unapenda kukubaliana muda wa kutokukubaliana. Unapochukizwa na jambo onesha hatua uliyoichukua. Unaweza kununa, kupiga Keller, kuondoka, kususa3, kupiga, kuleta kizaazaa au kunyamaza. Acha kukariri ujinga. Nani amekukaririsha kuwa ukisusa jambo unakuwa mwanamke automatically? Ndiyo ninyi huwa mnaambiwa mwanaume halii. Na akilia ataitwa mwanamke. 😂😂😂😂Muulize Jenerali Ulimwengu akusaidie maswali.

Hili mada ya swali kuhusu tabia ya kususa, kisiasa, huu mtindo wa kuzira au kususa susa, kususia kila jambo usilokubaliana nalo, sio tabia za kike hizi?, au sio tabia za kitoto?!. Mtu unasusia jambo fulani la kisiasa, ili upate nini?. Kususia jambo lolote la kisiasa bila kupiga hesabu ya what do you want to achieve na kususa huko, sio political suicide?.

The Motive Behind Kususa.
Jee ni nini the motive behind kususa jambo fulani, una susa ili uachieve nini, na baada ya kususa, jee hao wasusaji huwa wanakipata kile walichokusudia?!. Kususa jambo fulani bila malengo, sio tuu ni utoto, bali ni ujinga, kwa sababu ni sawa na kumsusia ngedere shamba la mahindi!, utayavuna mabua!.


My Take. (Maoni Yangu).
Kususia kushiriki uchaguzi sio suluhisho, huku ni kujiua kabisa kisiasa, dawa ni kujenga hoja madhubuti na kukaa mezani kuzungumza, vingine tuitumie mahakama yetu kuzifumua sheria kandamizi za uchaguzi ili zituletee uchaguzi huru na wa haki.


1. Tume yetu ya Uchaguzi NEC, japo sio inclusive lakini ni Tume Huru, licha ya kuteuliwa na rais ambaye ni Mwenyekiti wa chama kimojawapo, kwa uhuru ule ule wa Mahakama zetu ambazo majaji huteuliwa na rais huyo huyo ambaye pia humteua Mtendaji Mkuu wa Bunge letu. Kama Bunge limeweza kuwa huru kwa mfumo huu, na Mahakama ni huru, hata Tume pia ni huru, ila ionekane kuwa huru, something more needs to be done kwenye Tume Hii.
2. Sheria yetu ya uchaguzi, ina mapungufu makubwa yanayohitaji kufanyiwa marekebisho ili kutoa ushindani wa haki. Tusiilaumu Tume kwa chochote kinachotokea kwa sababu Tume inatekeleza sheria zilizopo, kama ni sheria kandamizi, ni kosa la sheria na aliyezitunga na sio kosa la mtekelezaji.
3. The political game playing field is not level, we need to create a level playing field ili kupata ushindani wa haki. Hili nalo ni tatizo la kikanuni, mfano uchaguzi wa 2020, kuna mgombea mmoja anaingia kwenye kinyanganyiro na vingora, msafara, media, na wasaidizi kibao, huku budget yake is fully footed by state, ashindane na makapuku!, unategemea nini?. Tangu tumeanza uchaguzi wa vyama vingi, kuna chama dola kinashindana na vyama makapuku!.
4. Now it's high time vyama vya siasa, vianze kutake responsibilities kwa matokeo ya utendaji wa vyama vyetu kwenye chaguzi mbalimbali, kwa kukubali kushiriki uchaguzi katika mazingira haya, na tukishindwa kihalali kwenye sanduku la kura, katika uchaguzi huru na wa haki, tukubali matokeo, na sio kutafuta visingizio.
5. Lazima tufike mahali, kwa pale ambapo uchaguzi ulikuwa huru na wa haki licha ya kasoro za hapa na pale, ambazo hazitaathiri, matokeo ya jumla ya uchaguzi huo, tujifunze kukubali matokeo na kushindwa kihalali, asiyekubali kushindwa sio mshindani. Kisha turudi nyuma kujitathmini where did we go wrong. Tulipaswa kufanya nini ili kupata ushindi katika mazingira kama haya.
Conclusion.
The bitter reality kwa wapenda demokrasia wa kweli wa mfumo wa vyama vingi nchini, mimi nikiwemo, tumeshuhudia hali hii ndio uwezo wa ushindani kwa vyama vyetu vya upinzani nchini Tanzania ndio umefikia hapa baada ya miaka 26 ya vyama vingi, naweza kusema kuwa this is the peak ya upinzani Tanzania, upinzani Tanzania, ndio imefika mwisho wake sasa!. Sasa tuanze kujiuliza, jee kama hali ni hii sana, je hali itakuwaje kwa uchaguzi wa 2020?. Kama wapinzani hawatabadili mbinu na strategies, za namna ya kushindana na CCM kwenye ushindani usio sawa kupitia sanduku la kura, then, uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, kuna hatari kubwa kwa CCM, kuyarejesha majimbo yote ya uchaguzi yaliyokuwa yanashikiliwa na upinzani, hivyo kuirudisha Tanzania kuwa ni nchi rasmi ya chama kimoja cha siasa, something which is not healthy at all to true modern democracy!.


Hongereni sana CCM kwa ushindi mtamu.
Poleni sana Chadema/Ukawa kwa kupoteza majimbo, wabunge na madiwani.


Tanzania kama taifa, tujipe pole kwa gharama kubwa za chaguzi hizi, ila tuombe sana Mungu alisaidie taifa letu kama gharama hizi za uchaguzi wa kinachoitwa demokrasia ya uchaguzi huru na wa haki, zinajumuisha, machozi, jasho na damu za Watanzania, kwa kugharimiwa na damu na roho za Watanzania, hakuna namna nyingine yoyote ya fidia kwa damu za watu na roho za watu, zaidi vya karma!'

Nawatakia Furahi Day ya Ijumaa Njema.

Wasalaam.

Paskali

Rejea za kuhusu Kususa.
Baada ya uchaguzi wa 2010, Chadema ilisusia matokeo na kujidai kuwa hawamtambui JK, ila bunge tuu lilipoanza, niliibua mjadala huu
Chadema Yakubali Yaishe! Yamtambua Rais!, Yampongeza Rais!.


Matokeo ya Chadema Kususia Hotuba ya JK na Kuapishwa kwa Pinda

Media Kususia Habari za Fulani: Jee Tanzania Tuna Independent Media Yenye Jeuri Hiyo?.

Uchaguzi wa 2015 Ukawa wakadai Lowassa ndie mshindi, hivyo wakajifanya kususa, na kutomtambua Magufuli, mimi niliwapa ushauri ufuatao
Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali ya Magufuli ni Serikali Haramu. Hukumu ya Karma ii Juu Yake!.


Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Hata kama ni kweli uliibiwa kura; Kaa kimya, Mungu ndiye akupiganie!

CUF kushiriki Uchaguzi wa Marudio Zanzibar si hiyari, Ni lazima! Vinginevyo, huo ndio mwisho wake - JamiiForums

Hatimaye CUF 'Wameridhia' Rasmi, Kushiriki Uchaguzi Wa Marudio Zanzibar!. - JamiiForums

Japo umegharimiwa kwa machozi, jasho na damu, ulikuwa huru na wa haki!. Hongera CCM, CHADEMA poleni!. Mungu saidia Tz - JamiiForums

Ujio wa Lowassa CHADEMA: Kuna kundi wamesusa, wanapanga kurejea CCM! - JamiiForums
 
I personally respect your opinions but sometimes you are completely out of scope!!
Kwa mazingira wanayopitia wapinzani ni magumu mno,kwa maoni yangu,watu wenye weledi wa kufikiri na wenye kuamini kwenye demokrasia na utawala wa sheria wangeungana na upinzani na sio kubez wala kuuliza maswali ya kinafiki(rhetoric questions)
Hakuna aliyesalama na mfumo na wala tusiwachie wapinzani??.Kwa hali ilivyo huhitaji kuhadithiwa shuruba wanazopitia wapinzani.Mimi nawaheshimu sana akina Mbowe pamoja na mapungufu yao as long wote tunamapungufu!!!
Tusibeze tukifikiri sisi hayatuhusu!!!
Watu wale wenye moyo wa dhati kupigania demokrasia na maendeleo wamekatishwa tamaa jinsi walivyo vunjwa moyo na viongozi wa vyama vya upinzani kwa sarakasi za mgombea uraisi 2015.

Wengi waliobaki ni wapiga zumari na kutetea maslahi binafsi tu. Haki wanayoililia akina Mbowe ilisombwa na mafuriko ya kutengenezwa na fedha za babu Laigwanoni ile 2015.
 
Kaka Pascal naelewa sana unachosema. Mbali na lugha ya udhalilishaji uliyotumia, nimeelewa hoja yako. Kinachoendelea kinaonesha wazi kuwa CDM wamekosa mbinu mbadala. Kususa au kugoma siyo suluhisho hasa kwa Viongozi wasioelewa hata maana ya demokrasia. Siasa za nchi zilizoendelea ni tofauti kabisa na za nchi zetu hizi zisizoendelea. Kuzira au kususa kisiasa havioneshi kuitishia serikali. Ni muda wa upinzani kutumia njia nyingine zinazoweza kuwapa haki zao za msingi. Hapa ndo tujadiliane njia mbadala tofauti na njia hizi zinazotumika sasa zisizo na matunda kwa wapinzani.
Mjumbe arrowhead kweli wewe ni kichwa Mkuki.Ulimsikiliza Mbowe vizuri? Au umejump kumuunga mkono Paschal na kumcriticise kidogo km ingekuwa Bungeni ungeuka mkono hoja.
Point ya msingi Mbowe alicodemix kwa kusema namnukuu" ku retreat sio ku surrender" Hilo peke ake linatosha na amesema wanajipanga kuongeza nguvu ya Chama kwa kutumia mbinu mbadala kwanza kwasasa.Which is merely right and logical in normal common sense really in unfairly current competitive political ground.
 
Mkuu The Big Boss, naomba nikuhakikishie katika maisha yangu yote, sijawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa. Paskali, hanunuliki na yeyote kwa lolote kwa sababu hana price tag. Mimi ni priceless, sio CCM wa Chadema, wala Ukawa, wala Lowassa wala Magufuli, ana uwezo wa kuninunua, kwa sababu I'm not for sale, na sina any price tag!.

Naomba uniamini hili ni swali tuu, nimeuliza hawa wanaosusa, wamesusa ili wapate nini?!.

Ni swali tuu.

Paskali
Huoni kuwa wataokoa fedha nyingi,yaani unashiriki kitu ambacho huwezi tangazwa mshindi!
 
Mjumbe arrowhead kweli wewe ni kichwa Mkuki.Ulimsikiliza Mbowe vizuri? Au umejump kumuunga mkono Paschal na kumcriticise kidogo km ingekuwa Bungeni ungeuka mkono hoja.
Point ya msingi Mbowe alicodemix kwa kusema namnukuu" ku retreat sio ku surrender" Hilo peke ake linatosha na amesema wanajipanga kuongeza nguvu ya Chama kwa kutumia mbinu mbadala kwanza kwasasa.Which is merely right and logical in normal common sense really in unfairly current competitive political ground.
Mkuu tabia hatuipimi kwa kauli au tendo moja. Mazoea ndiyo hujenga tabia. Tabia ya kususa kwa vyama pinzani haijaanza katika chaguzi hizi ndogo, ilokuwepo hata katika chaguzi kuu zilizopita. Hoja Hapa ni kutaka kujua éndapo njia hii ya kununa ina mashiko au ndo itakuwa kumsusia ngedere shamba la mahindi. Sipingi alichokesema Mbowe, Kweli wanahitaji njia mbadala kupambana na raisi wetu ambaye hajali wala hana muda na demokrasia
 
Sasa wapinzani awajaungana na hakuna mpinzani wa kuwaunga mkono chadema kwa hivyo ukisusa ,umesusa peke yako
Kwanza mbowe angeanza kufanya ushawishi kwa wapinzani wenzake kisha wangekuwa wote kwa pamoja kama wapinzani wangetoa tamko la pamoja
Mbowe na chadema yao ni wabinafsi sana wana umimi
hivyo kususa kwao hakuta athiri jambo lolote
Wapinzani wengine wamepata uwanja wa kujitangaza
Ukiwa mwanaume wa kweli kama bobi wine unatakiwa upambane kweli kweli upinzani sio lelemama kama mbowe anavyodhani.
 
Watu wale wenye moyo wa dhati kupigania demokrasia na maendeleo wamekatishwa tamaa jinsi walivyo vunjwa moyo na viongozi wa vyama vya upinzani kwa sarakasi za mgombea uraisi 2015.

Wengi waliobaki ni wapiga zumari na kutetea maslahi binafsi tu. Haki wanayoililia akina Mbowe ilisombwa na mafuriko ya kutengenezwa na fedha za babu Laigwanoni ile 2015.
I due respect your foolish advertisements,let your foolishness prevails out of my content!!
 
Kumbe kuna tabia za kike wao wamesusia we hujakatazwa kushiriki kama tuko 10 tunapiga 100 je kwanini ashiriki we shiriki tu wala ucjali kususa kwao huna haja ya kupayuka we sema UTASHIRIKI au wasipo shieiki na wewe ushiriki wako unapotea cjui bac sawa
 
Mkuu nakuelewa sana ila ni vigumu kukubaliana na hoja yako. Huwezi kulinganisha majukumu mazito ya tume ya uchaguzi na kazi ya majaji mahakamani kuamua mashauri hata km yanagusa kiasi gani maslahi ya nchi. uchaguzi ni mchakato wa kuamua nani anastahili kushika dola, kuongoza nchi, unaamua ni nani/chama gani imepewa ridhaa ya wananchi kuunda serikali. Ni mchakato unaoamua mustakabadhi wa nchi kisiasa, kiuchumi, kidiplomasia nk Utalinganishaje haya? Mkiti huyu na wakurugenzi wake wa tume wote ni wateule wa mgombea ambaye ni mshindani ktk uchaguzi. Tunaambiwa kila siku wasimamizi wa vituo vya kupigia kura wengi ni makada wa chama tawala na ushahidi ulionyeshwa , haya hayatokei bahati mbaya. HATA KWA AKILI YA KITOTO viongoz wa tume ni watu wenye masilahi na aliyewateuwa. Na wakishapokea matokeo lazima wamweleze hali halisi km kuna anguko wtaanza kutafuta mbinu za kulifix. TETEENI MUTETEAVYO LKN INAHITAJIKI TUME HURU YA UCHAGUZI na kikubwa katiba ya Warioba inahitajika ili kuweka uwanja sawa wa kiushindani.
Pili unaposema huyo bwana ni game changer ni sawa sababu hakuna uwanja sawa na kibaya zaidi si mtu anayefuata sheria za nchi. Yeye ndiye katiba, mahakama bunge ndiye bodi ya zabuni, ndiye mamlaka ya manunuzi. Angekuwa game changer ktk misingi ya katiba ya nchi akitumia mbinu za kiushindan zilizo za haki ktk mfumo wa vyama vingi vya siasa .Mwambie arejeshe bunge mubashara na kikubwa aruhusu mikutano ya kisiasa km zamani apo ndipo utajua ni nini watanzania wanawaza. Washindani wake wote wamefungwa midomo na mikono imefungwa nyuma. Anajidai yeye pekee na chama chake. Huyo si game changer. Sifa ya kijinga.
Huyo bwana hana kasi yoyote ile, umenyamazisha wengine wote, hukosolewi huambiwi alafu mtu unasifu ana kasi. Kasi ipi? Kuuwa demokrasia, kuuwa uchumi na watu kuzidi kuwa maskini, kuteka na kutesa hii ndio kasi unayozungumzia. Uchumi umekufa, umesambaratika tunaishi ktk propaganda za kijinga
 
Bwana P nataka nikuambie kabisa km kwa sasa hutumiki basi umeamua kujitumikisha labda ukiwa na matarajio fulani, Hebu nikuulize ni nini kisaikolojia kilichokusukuma kuchagua maneno uliyotumia ktk post yako, ''tabia za kike''. Unadai huna chama, lkn ulikusudia kufikisha ujumbe gani kwa jamii dhidi ya wale unaowakosoa.
 
Wewe nadhani unatatizo la mapokeo,ndiyo mana umetumia neno eti kususa ni tabia za kike!Inamana wewe wanawake umewaweka kundi la mataahira?Acha mfumo dume,pia Acha akili za mapokeo,acha kudhalilisha mama zetu,labda kama hao wanawake uliotolea mfano ni wa ndani ya familia yako tu.Jambo la pili ambalo linaashiria wewe unatumia akili za mapokeo badala ya uyakinifu ni pale uliposema kuwa chadema wanasusa bila kutoa ufumbuzi,hii si kweli.Mbowe ameeleza kuwa wanasheria wa chama wanaendelea na hatua mbalimbali za kisheria na taratibu nyingine pia zinaendelea.Sasa wewe waliokufundisha kuongea ulichoongea mbona wamekudhalilisha?You better use your brain properly. Heri kufa na mawazo yanayoishi kuliko kuishi na mawazo yaliyokufa.Upumbavu ni ile hali ya kuujuwa ukweli,kuuona ukweli,lakini unaendelea kuamini katika uongo.
 
Wewe nadhani unatatizo la mapokeo,ndiyo mana umetumia neno eti kususa ni tabia za kike!Inamana wewe wanawake umewaweka kundi la mataahira?Acha mfumo dume,pia Acha akili za mapokeo,acha kudhalilisha mama zetu,labda kama hao wanawake uliotolea mfano ni wa ndani ya familia yako tu.Jambo la pili ambalo linaashiria wewe unatumia akili za mapokeo badala ya uyakinifu ni pale uliposema kuwa chadema wanasusa bila kutoa ufumbuzi,hii si kweli.Mbowe ameeleza kuwa wanasheria wa chama wanaendelea na hatua mbalimbali za kisheria na taratibu nyingine pia zinaendelea.Sasa wewe waliokufundisha kuongea ulichoongea mbona wamekudhalilisha?You better use your brain properly. Heri kufa na mawazo yanayoishi kuliko kuishi na mawazo yaliyokufa.Upumbavu ni ile hali ya kuujuwa ukweli,kuuona ukweli,lakini unaendelea kuamini katika uongo.
Jaimee unaamini njia zinazotumika na vyama pinzani zinaweza wapatia haki zao katika chaguzi zijazo ? Kwa kuzingatia matukio ya nyuma na njia chadema walizotumia kudai haki zao, unadhani njia hizo ni sahihi ? Ikiwemo kususia chaguzi, kutoka katika vipindi vya bunge, kutohudhuria kuapishwa kwa raisi n.k. njia hizi zimewapa manufaa gani ? Na unadhani zikiendelea zitawapa manufaa yapi ? Kwa mtazamo wako, ukivaa viatu vya mheshimiwa mbowe, ungeweza tumia njia gani tofauti na hizi ili kupata haki za kisiasa ?
 
Wanabodi,

Hili mada ya swali kuhusu tabia ya kususa, kisiasa, huu mtindo wa kuzira au kususa susa, kususia kila jambo usilokubaliana nalo, sio tabia za kike hizi?, au sio tabia za kitoto?!. Mtu unasusia jambo fulani la kisiasa, ili upate nini?. Kususia jambo lolote la kisiasa bila kupiga hesabu ya what do you want to achieve na kususa huko, sio political suicide?.
Naweza nikahisi kuwa ile kamati ilipokuita ilikupa ToR za kuandika haya Maswali yako. Na nakumbuka yule Mzee aliposema Jina lako kwa Lugha ya Kisukuma linamaanisha njaa alimaanisha alichokuwa amemaanisha. Kwa platform ile na kwa swali ulilomuuliza kujibu kuwa wewe jina lako la ukoo maana yake njaa alikufahamu vizuri. Sasa ni wakati wako wa kuitibu njaa. itibu salama
 
Back
Top Bottom