Swali kwa Jaji Mkuu: Je, ni haki kwa kina Rostam Aziz kutozwa faini badala ya kifungo lakini kina Mbarikiwa kupewa kifungo badala ya faini?

Swali kwa Jaji Mkuu: Je, ni haki kwa kina Rostam Aziz kutozwa faini badala ya kifungo lakini kina Mbarikiwa kupewa kifungo badala ya faini?

Issue ya Kibwetere ni tofauti na ya Mbarikiwa. Ukweli toka tumekuwa na huyu Jaji mkuu hadhi ya mahakama ni kama imeshuka sana,na ukute ndo sababu hata wenzie wanapinga kuongezewa muda kinyume na kanuni za utumishi.
Ni kipindi chake huyu tumeshuhudia mahakama zikitumika kisiasa mnoo. Pengine ndo sababu alikaimu muda mrefu kabla ya kuthibitishwa kuwa CJ tofauti na watangulizi wake.
Unachanganya mambo!! Suala la Prof Juma kuendelea kuwa Mkuu wa Mhimili wa Mahakama ni kitu tofauti na huyo mwehu wenu mnamuita "Mbarikiwa".

Mimi nasema TUIPONGEZE Serikali kwa inachofanya KUDHIBITI hizi madhehebu za kishenzi za akina Mwakilesile maana hata akina Kibwetere au Mackenzie walianza hivi hivi.
 
Aziz anatoka sero anacheka kabisa huku anapiga picha kwa mapozi ya video.

Rostan Aziz aliposema bongo hakuna mahakama bali kikundi cha upigaji tu aliambiwa aombe msamaha ila alisema ukweli.
 
"Individual prophylaxis operation" ndiyo nimeijua leo. Yaani mtu anapewa "operation" ili kuzuia magonjwa, ushaona wapi hiyo? Ni oxymoron kama "fighting for peace".
 
Acha urongo! Mpaka Ruto anaingia madarakani Rostam alikuwa hajaanza kufanya biashara na Kenya.
Sikiliza dada yangu kiwanda kilizinduliwa muda mfupi baada ya Rostam kurudi. Kwanini mwendazake asingekizindua kiwanda ?
 
Unaongelea kiwanda gani, kilichozinduliwa lini, na wapi?
Hujui kitu wewe, unaropoka tu. Kwanza Akram alihukumiwa siyo kwamba aliachiliwa hivi hivi. Kitendo cha kukubali kusaini plea bargain ni kukubali makosa
 
"Individual prophylaxis operation" ndiyo nimeijua leo. Yaani mtu anapewa "operation" ili kuzuia magonjwa, ushaona wapi hiyo? Ni oxymoron kama "fighting for peace".

Elimika:. Chanjo ni operesheni inayomlenga mtu mmoja mmoja kwa ajili ya kuzuia magonjwa ya kibayolojia ("Individual prophylactic operation"). Kutibu maji ya bomba yanayotoka mto Ruvu na kuingia Dar ni operesheni inayowalenga umma kwa ajili ya kuzuia magonjwa ya mlipuko ("mass prophylactic operation").

Kwa kutumia mantiki hiyo hiyo tunaweza kukubaliana kuhusu kuwepo operesheni ya kuzuia magonjwa ya kiusalama, katika ngazi ya mtu mmoja mmoja, yaani "Individual prophylactic operation". Kwa kutumia mantiki hiyo hiyo unaweza kukubaliana kuhusu kuwepo operesheni ya kuzuia magonjwa ya kiusalama katika ngazi ya kimakundi, yaani "mass prophylactic operation".

Katika operesheni za kiusalama, tunapoongelea "Individual prophylactic operation" tunamaanisha "operation" ya kumdhoofisha mtu ambaye tayari tumempa hadhi ya kuwa "tishio la kiusalama." Ni "operaion" ya kumwondolea nguvu indirectly ili asiendelee kuwa tishio.

Mfano, kama wewe tumekutafsiri kama tishio, tutafuatilia mwenendo wako wote. Tukijua umeandika barua ya kuomba kazi mahali, tuseme kwenye kampuni ya Dangote, sisi tunapeleka barua rasmi kwa Dangote yenye dokezo la kiusalama kusema kwamba, "Mwombaji wa kazi XYZ aliyeleta maombi kwenu tunamchunguza kwa tuhuma za ugaidi, kwa hiyo kuweni makini msije makaajiri gaidi."

Hakuna mwajiri angependa kujitumbukuiza kwenye matatizo kama hayo. Kwa njia hiyo, huweza kupata ajira kwake. Kwa kukosa ajira hutapata nguvu ya kifedha. Kwa kukosa nguvu ya kifedha hutaweza kuendeleza kile ambacho sisi tumeshakiita "tishio.'

Pia tunaweza kuchukua hatua ya kukuchafua kijamii. Tutapita kwenye mtaa wako unakoishi na kusambaza taarifa kila kijiwe, kwamba, "Huyu jirani yenu anayeitwa XYZ ni shoga, kwa hiyo kuweni makini naye asije akawalawiti watoto wenu wa kiume." Mara unashangaa kila jirani anakunyima ushirikiano, hata bila kukwambia sababu.

Mfano huu wa pili ni mbinu ya propaganha chafu. Mara nyingi inatumia mkakati unaoitwa "fallacy of association." Kwenye siasa, mbinu hii hutumiwa na kamati za fitina. James Mbatia aliwahi kuwa mhanga wa fitina za aina hii, kwa kupakwa matope ya kwamba yeye ni "shoga" kisa aliwahi kuonekana akiwa katika gari moja la mtu ambaye ni shoga.

Hii ndiyo maana ya "Individual prophylactic operation" niliyoikusudia. Mifano hii miwili inatosha kukufungua macho. Hivyo sasa utaelewa ninaposema kwamba kitendo cha kuua mtoto wa Mchungaji Mbarikiwa kilikuwa ni "Individual prophylaxis operation." Ukifiwa na mtoto wako, ratiba zako zote zinabadilika, uchumi wako unayumba, kisaikolojia unatikisika, na kelele zako dhidi ya watawala zinatulia kwa muda.

Tanzania tulikuwa hatutumii mbinu hii mpaka hivi karibuni baada ya kupatikana kwa baadhi ya wakuu wa vyombo vya usalama wasioamini katika ukuu wa tunu ya uhai wa watu wasio na hatia.
 
View attachment 2766809
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma

Mheshimiwa Jaji Mkuu,

Tarehe 29 Septemba 2023, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mbeya, Paul Ntumo, alimhukumu kifungo cha miaka mitatu na siku 14 jela, Mchungaji anayeitwa Mbarikiwa Dickson Mwakipesile (39), baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kuendesha huduma ya kikosi kazi cha Injili kabla ya kupata usajili kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kama sheria ya vyama vya kijamii inavyotaka.

Hukumu hiyo ilitolewa chini ya kifungu cha 25(1) cha sheria ya vyama vya kijamii. Kifungu kinaipa mahakama mamlaka ya kutoa adhabu mojawapo kati ya tatu. Kuna:
  1. Ama adhabu ya kulipa faini, kwa makosa yenye ukubwa wa kiwango cha chini (minor offenses),
  2. Au adhabu ya kifungo, kwa makosa yenye ukubwa wa kati (intermediate offenses),
  3. Au adhabu zote mbili kwa pamoja, kwa makosa yenye ukubwa wa kiwango cha juu (aggravated offenses).
Kwa mujibu wa busara ya Mahakama ya Hakmu Mkazi wa Mbeya, kitendo cha kuendesha kanisa kabla ya kupata usajili ni "interdmediate offense" na hivyo kuamua kutoa adhabu ya kifungo kwa Mwakipesile.

Mchungaji Mwakipesile amekuwa anaituhumu serikali kwamba inawaona wanachi kama nyani au kenge. Yeye ni baba mzazi wa Sifa Bujune, Muimbaji wa Injili anayetuhumiwa kusambaza uongo kutokana na Wimbo wake wa “Mnatuona Nyani tu”,


View: https://youtu.be/JSVmJqUmbHg

Wakati huo huo, kumbukumbu zinaonyesha kwamba, Akram Aziz, mdogo wake Ristam Aziz, alikabiliwa na kesi ya mashtaka 75 ya uhujumu uchumi kwa kukutwa na nyara za Serikali, silaha za aina mbali mbali na risasi zake (tazama Kkiambatanisho hapa chini).

Kesi yake iliendeshwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, chini ya Sheria ya Kanuni za Adhabu inayotaja yenye mfumo wa adhabu sawa na mfumo wa adhabu uliomo kwenye sheria ya vyama vya kijamii uliotajwa hapo juu. Mwishowe mahakama iliona kwamba Akram alifanya "minor offense." Hivyo Akram akatozwa faini, badala ya kupewa adhabu ya kifungo.


View: https://youtu.be/-FWpqOItZrI

Hali hii ya kutotabirika kwa maamuzi ya mahakama kuhusu utaratibu wa kutamka adhabu kunazitia doa mahakama za Tanzania, ambazo utendaji kazi wake unasimamiwa na Jaji Mkuu. Na tatizo liko hivi:

  1. Mahakama inayomheshimu jangili na kumtweza mchungaji au shehe ni mahakama ya hovyo sana.
  2. Mahakama inayomheshimu mwarabu na kumtweza Mbantu wa Mbeya haina haki ya kuitwa mahakama.
  3. Mahakama inayowatukuza wenye mali na kuwakandamiza makabwela sio mahakama kamwe.
  4. Mahakama inayotukuza watu wenye mamlaka ya kisasa na kutwatweza wanyonge inakuwa na watendaji ambao wana tatizo la ombwe la kimaadili.
  5. Kwa ujumla, mahakama inayokumbatia kanuni ya umachiveli, isemavyo kwamba "matokeo mazuri yanaweza kuhalalisha mbinu yoyote, hata kama ni mbinu haramu," haitakiwi katika Tanzania ya Nyerere.
Hivyo, tunapenda kutoa mapendekezo yafuatayo kwa vigogo wa nchi hii, na hasa wale wenye mapenzi mema, na wanaojali kwa mawazo, kwa maneno na kwa vitendo, zile tunu kuu za taifa hili linaloitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania:

1. Mheshimwa Jaji Mkuu achukue hatua za kulinda heshima ya Mhimili muhimu unaoitwa Mahakama kwa kuchukua hatua stahiki za kufuta uhiari wa kimamlaka (discretionary powers) walio nao mahakikmu na majaji katika hatua ya kutamka adhabu, kwa kuhakikisha sheria zote zinazotaja adhabu zinatoa vigezo vya kutofautisha kinaganaga kati ya aina zifuatazo za adhabu za kimahakama:

(a) Makosa yenye ukubwa wa kiwango cha ukomo wa chini (minor offenses) yanayostahili adhabu ya kulipa faini kama yakithibitishwa;​
(b) Makosa yenye ukubwa wa kiwango cha kati (intermediate offenses) yanayostahili adhabu ya kifungo kama yakithibitishwa; na​
(c) Makosa yenye ukubwa wa kiwango cha juu (aggravated offenses) yanayostahili adhabu zote mbili kwa pamoja kama yakithibitishwa.​
(d) Makosa yenye ukubwba wa kiwango cha ukomo wa juu kabisa (heinous offenses) yanayostahili adhabu ya kifo kama yakithibitishwa.​

2. Mheshimiwa Rais Samia atumie mamlaka yake kama Mkuu wa cnhi kufuta mara moha adhabu aliyopewa Mchungaji Mwakipesile ili kuzuia matope yanayoweza kumrukia mabegani mwake.

3. Rais Samia amwagize Waziri wa Mambo ya ndani, Mhandisi Hamad Masauni, kumpa Mchungaji Mwakipesile usajili aliouomba, maana, utafiti wetu unaonyesha kwamba, hatua zote zinazotakiwa kisheria tayari Mwakipesile amezifuata. Kanuni za utwala wa sheria na misingi ya Katiba ya nchi kuhusu uhuru wa kuabudu ifuatwe.

4. Kamati za Ulinzi na Usalama mkoani mbeya zipanguliwe na kupangwa upya. Zinapanga na kutekeleza operation zenye sura ya uhalifu dhidi ya ubinadami. "Individual prophylaxis operation" iliyofanyika kwa ajili ya kumdhoofisha Mchungaji Mbarikiwa kwa kuua mtoto wake ni mfano hai.

Tunawasilisha.

Mama Amon
Mkurugenzi Mtendaji Mkuu
Dawati la Utafiti la Mama Amon (DUMA)
"Sumbawanga Town"
S.L.P. P/Bag
Sumbawanga
30 Sep 2023


============KIAMBATANSHO KUHUSU KESI YA MDOGO WAKE ROSTAM AZIZI==================

MUHTASARI WA KESI YA MDOGO WAKE BILIONEA ROSTAM AZIZ​


View attachment 2766818

Mnamo 30 Oktoba 30 2018, saa 7 mchana maeneo ya Msasani, Jijini Dar, Akram Aziz, mdogo wake Rostam Aziz, alikamatwa na vyombo vya dola akiwa na nyara mbalimbali za serikali zikiwemo Pembe za ndovu. Tazama vielelezo vya picha hapa chini.

Ilithibika kuwa Akram (Iqram) ni jangili wa muda mrefu na upekuzi uliofanyika nyumbani kwake ulibaini kuwa Akram anamiliki silaha nyingi kinyume cha sheria, pamoja na mihuri mingi bandia ya taasisi za serikali ambapo alikutwa na “vibali feki” vya uwindaji vingi sana.

Ilifahamika kuwa amekuwa ni “Mastermind” wa ujangili nchini kwa muda mrefu sana na ndiye kinara wa mauaji ya tembo na wanyama wengine kwenye mbuga zetu.

Taarifa za uhakika zilisema kuwa mtandao huo wa ujangili ulikuwa unasimamiwa na Kaka yake Rostam Aziz pamoja na baadhi ya viongozi wengine wa vyama vya siasa na serikali katika awamu zilizopita. Hatimye Akram alitiwa hatiani na kupewa adhabu ya kulipa faili badala ya kifungo. Picha zifuatazo ni baadhi ya silaha alizokamatwa nazo:

View attachment 2766815

View attachment 2766816

View attachment 2766817

Maelekezo kutoka juu.

Eananchi hawapaswi kujitambua wala kudai haki zao. Tanzania ni uhaini kuwakosoa watawala.

Yapo makanisa na huduma za kiroho nyingi sana hawana usajili na wanaendesha huduma zao namna hiyo.

Madikteta waoga huishia pabaya sana. Sonona itawafuata maisha yao yote labda watubu
 
Umevamia fani isiyo yako. Katika operesheni za kiusalama, tunapoongelea "Individual prophylactic operation" tunamaanisha "operation" ya kumdhoofisha mtu ambaye tayari tumempa hadhi ya kuwa "tishio la kiusalama." Ni "operaion" ya kumwondolea nguvu indirectly ili asiendelee kuwa tishio.

Mfano, kama wewe tumekutafsiri kama tishio, tutafuatilia mwenendo wako wote. Tukijua umeandika barua ya kuomba kazi mahali, tuseme kwenye kampuni ya Dangote, sisi tunapeleka barua rasmi kwa Dangote yenye dokezo la kiusalama kusema kwamba, "Mwombaji wa kazi XYZ aliyeleta maombi kwenu tunamchunguza kwa tuhuma za ugaidi, kwa hiyo kuweni makini msije makaajiri gaidi."

Hakuna mwajiri angependa kujitumbukuiza kwenye matatizo kama hayo. Kwa njia hiyo, huweza kupata ajira kwake. Kwa kukosa ajira hutapata nguvu ya kifedha. Kwa kukosa nguvu ya kifedha hutaweza kuendeleza kile ambacho sisi tumeshakiita "tishio.'

Pia tunaweza kuchukua hatua ya kukuchafua kijamii. Tutapita kwenye mtaa wako unakoishi na kusambaza taarifa kila kijiwe, kwamba, "Huyu jirani yenu anayeitwa XYZ ni shoga, kwa hiyo kuweni makini naye asije akawalawiti watoto wenu wa kiume." Mara unashangaa kila jirani anakunyima ushirikiano, hata bila kukwambia sababu.

Mfano huu wa pili ni mbinu ya propaganha chafu. Mara nyingi inatumia mkakati unaoitwa "fallacy of association." Kwenye siasa, mbinu hii hutumiwa na kamati za fitina. James Mbatia aliwahi kuwa mhanga wa fitina za aina hii, kwa kupakwa matope ya kwamba yeye ni "shoga" kisa aliwahi kuonekana akiwa katika gari moja la mtu ambaye ni shoga.

Hii ndiyo maana ya "Individual prophylactic operation" niliyoikusudia. Mifano hii miwili inatosha kukufungua macho. Hivyo sasa utaelewa ninaposema kwamba kitendo cha kuua mtoto wa Mchungaji Mbarikiwa kilikuwa ni "Individual prophylaxis operation." Ukifiwa na mtoto wako, ratiba zako zote zinabadilika, uchumi wako unayumba, kisaikolojia unatikisika, na kelele zako dhidi ya watawala zinatulia kwa muda.

Tanzania tulikuwa hatutumii mbinu hii mpaka hivi karibuni baada ya kupata wakuu wa vyombo vya usalama wasioamini katika ukuu wa tunu ya uhai wa watu wasio na hatia.
Mimi nimetafsiri literally kwa Kiingereza. Basi hii phrase itakuwa made in Tz lingo sbb haileti maana kwa Kiingereza cha kawaida. Mama Amon wee kumbe ni usalama wa taifa?
 

Hata sijaelewa umeongea nini! Lakini, chini ya ibara ya 27 na 28 ya Katiba ya Tanzania (1977) kila mtu na wato wote ni walinzi wa usalama wa Taifa. Jisomee:

1696250323248.png


Kwa maarifa zaidi jisomee vitabu vifuatavyo (attached) kuhusu maana ya maneno "Ulinzi wa Taifa" yanayosomeka kwenye ibara ya 28 ya Katiba ya Tanzania (1977):

1. David Omand (2010), Securing the State (New York:OUP)

2. David Omand (2020), How Spies think: Ten Lessons in Intelligence (Penguin Books Ltd)
 

Attachments

Sawa. Huu msemo “Individual prophylaxis operation” wapi chanzo chake? Google phrase search nimeambulia sifuri.

Mara ya kwanza niliusikia kutoka kwenye kinywa cha mwalimu wangu wa masuala ya statecraft, Peter Nyamanchi Tyienyi. Sasa ni mrehemu. Lakini, ufafanuzi ufuatao utakufaa.

Elimika:. Chanjo ni operesheni inayomlenga mtu mmoja mmoja kwa ajili ya kuzuia magonjwa ya kibayolojia ("Individual prophylactic operation"). Kutibu maji ya bomba yanayotoka mto Ruvu na kuingia Dar ni operesheni inayowalenga umma kwa ajili ya kuzuia magonjwa ya mlipuko ("mass prophylactic operation").

Kwa kutumia mantiki hiyo hiyo tunaweza kukubaliana kuhusu kuwepo operesheni ya kuzuia magonjwa ya kiusalama, katika ngazi ya mtu mmoja mmoja, yaani "Individual prophylactic operation". Kwa kutumia mantiki hiyo hiyo unaweza kukubaliana kuhusu kuwepo operesheni ya kuzuia magonjwa ya kiusalama katika ngazi ya kimakundi, yaani "mass prophylactic operation".
 
Sheria huwa haina jicho linalofanana. Unapoona sheria haitoi adhabu moja basi ujue hapo macho yanaweza kutofautiana. Sababu ziko nyingi kila mtu anaweza kuwa na yake.
 
Sheria huwa haina jicho linalofanana. Unapoona sheria haitoi adhabu moja basi ujue hapo macho yanaweza kutofautiana. Sababu ziko nyingi kila mtu anaweza kuwa na yake.

Lakini kazi ya sheria ni kuisaidia jamii kujua kesho kutatokea nini, yaani kutabirika kwa maisha ya watu, au tuseme predictability. Unasemaje kuhusu sifa hii muhimu inayopswa kuwa sifa mojawapo ya sheria zote duniani?
 
Back
Top Bottom