Uchaguzi 2020 Swali kwa Rais Magufuli: Hofu ya nini juu ya Vyombo vya Habari?

Uchaguzi 2020 Swali kwa Rais Magufuli: Hofu ya nini juu ya Vyombo vya Habari?

britanicca

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2015
Posts
16,295
Reaction score
33,994
Hofu yote hii ni ya nini? Mmeondoa "local chanels" kwenye ving'amuzi vyote ikiwemo Dstv l, mmebakiza TBC tu. Mmelazimisha nchi nzima itizame TBC. Hamjaridhika, sasa mmehamia kwenye radio. Mnatunga kanuni za kuzuia watu kusikiliza radio za nje? Lengo ni nini?

Yani sasa hivi Dira ya Dunia ya BBC, Meza ya duara ya DW na habari za ulimwengu za VOA hatutazisikia tena hadi kibali kutoka TCRA? Ujinga gani huu?

Halafu hizi radio za nje zinazotangaza kwa kiswahili zimesaidia sana kukuza Kiswahili kimataifa. Zilianza BBC, DW na VOA lakini leo radio zenye idhaa ya Kiswahili ni nyingi sana duniani. Radio Japan, Radio Tehran, Radio China International, Idhaa ya Kiswahili ya umoja wa mataifa, Radio France Internationale etc.

Na watanzania wengi wamepata ajira kwenye vyombo hivi vya habari. Kupitia radio hizi Kiswahili kinasikilizwa sana nchi za jirani. Nenda Burundi uone watu wanavyosikikiza matangazo ya mchana ya DW, nenda Uganda uone watu wanavyosikiliza Dira ya dunia ya BBC. Kiswahili kinakua sana. Lakini leo kwa sababu ya ubinafsi tunazuia vyombo hivyo kusikika hapa nchini. Tunataka watu wote wasikilize kuhusu reli ya SGR na Flyover za Ubungo.

Hii si sawa hata kidogo. Tunakoelekea ni pabaya sana. Dalili mojawapo ya kupoteza uhuru wa habari ni kulazimisha kila mtu asikilize mawazo yako, na kukataa kusikiliza mawazo mbadala. Tuendelee kukaa kimya hadi siku tutakayoambiwa huruhusiwi kukohoa hadi kibali cha Muhimbili. Labda ndo tutapata akili.!
 
Mbona radio zinazotangaza kwa kiswahili huko japan zinabalance story?

Nyie CCM huwa kila mkiitwa kwenye kitimoto cha midahalo ama mahojiano ya kawaida tu hata na Global TV tu, huwa mnakimbiaga...

Kwa ufupi ni kuwa, nyie CCM mnapenda kupanua midomo yenu ya udanganyifu kwa wanyonge na wasio na elimu tu huko uraiani, vijijini....

Sasa kama huwa mnaingia mitini na kukimbia kila opportunity ya kujibu hoja kinzani dhidi yenu, mnategemea story iwe balanced kwa namna gani?....

Na je, watu wasirushe matangazo yao kwa sababu tu CCM wametafutwa kwa kila njia ili wajibu hoja za upande wao lakini wanakimbia...??
 
Tena maamuzi haya yalipaswa yafanywe mapema zaidi, maana Kama wanatumia vyombo vya habari za kimataifa Bora tubaki na RTD tu hakuna namna😂🤣😂! Hakuna kucheka na nyani😠! Msioweza kuishi bila hivyo vyombo vya habari vya nje nendeni huko xilipo mzifuate!
 
Nyie CCM hata mkiitwa kwenye kitimoto cha midahalo na hata kuhojiwa tu Global TV mnakimbiaga...

Nyie CCM mnapenda kupanua midomo yenu ya kudanganya wanyonge na wasio na elimu tu huko uraiani, vijijini....

Ukiingia mitini ukikimbia kujibu hoja, unategemea story iwe balanced kwa namna IPI...??

Kwa beam balance
 
Back
Top Bottom