Swali kwa wasomi wa Jiografia na Fizikia wenye akili zao, kama ulienda shule kukariri pita mbali

Swali kwa wasomi wa Jiografia na Fizikia wenye akili zao, kama ulienda shule kukariri pita mbali

vipi nzi aliekaa juu ya bawa la hiyohiyo ndege. akitaka kuruka kutoka bawa moja kwenda lingine?.. mruko wa kuikatiza ndege inayosafiri uelekeo tofauti na nzi.

au
nzi huyo huyo akiwa hukohuko nje ya ndege akiamua kuruka uelekeo huohuo wa ndege kitambo cha mita moja kufikia anapotaka. atafanikisha lengo?


msingi wa swali nimezingatia vitu vyote vinaenda kat

tunapoambiwa na watabiri wa hali ya hewa kwamba Upepo utavuma kwa kasi ya 30km/h. huu upepo hauhusiani na hii dunia au?

iweje mabati yaezuliwe na upepo ambao haufiki hata robo ya speed ya dunia?
Hapo mbona simple tu? Jiulize kwa nini gari inayokimbia wakati wewe umekaa ndani yake ikisimama ghafla unaweza kutokea kwenye kioo cha mbele kama ipo speed sana? Jibu ni unakimbia sawasawa na speed ya hiyo gari ......sasa je kama unakimbia speed sawa na gari unawezaje kutembea taratiibu ndani ya hilo hilo gari kuhama siti moja kwenda nyingine? Au kutoka siting ya nyuma kwenda sit ya mbele taratiibu kabisa? Tena hapo tunaongea gari ambayo speed yake inabadirika badirika ......sasa dunia inaenda constant speed, vitu vyote vilivyopo ndani yake vitakimbia speed hiyo hiyo..
Hivyo basi nikitaka kuhama position moja kwenda nyingine ndani ya hii hii dunia inayokimbia lazima nianzishe speed mpya.
Ila mtu aliyepo nje ya dunia na hayupo kwenye speed yake ataniona nakimbia kuliko dunia.
Vivyo hivyo mtu akiwa ndani ya basi linalotembea na yeye anatembea halafu wewe umesimama pembeni ya barabara huwezi kumuona akitembea taratibu utaona anakimbia pamoja na basi. ( OYA SAYANSI KUIELEZA KWA KISWANGLISH NI MSALA)
 
Kuna kuta za dunia/nguzo ambazo wazungu hawataki zifikiwe, mwezi ndio husogeza maji yaan kupwa na kujaa kwa bahari kwa sababu ya utambalale, kuzama na kuibuka kwa jua upande mwingine yaani nguzo moja na nguzo nyingine na kufanya kati kati kusiguswe na mwanga wa jua
 
Nje ya mada; Una unga wa ugali, maji, sufuria, mkaa ,jiko la mkaa, mwiko wa kuongea ugali na banio. Lengo ni kupika ugali.

Umewasha jiko la mkaa kisha ukatenga sufuria la ugali, umeweka maji na unga kiasi ili uandae uji ambao ukichemka ipasavyo utaweka unga halafu kwa kutumia mwiko utasonga ugali.

Swali; Ni kwanini ukiweka unga kabla maji / uji haujachemka vizuri ugali hautaiva (utakuwa mbichi) hata kama utaongeza moto mwingi ?

Niliwahi kuuliza swali hili kwa mwalimu wangu wa physics, badala ya kunijibu alinichapa kwa madai kwamba nauliza maswali ya ajabu ajabu
Mifano mingine inayohusisha vyakula vya wanga vinavyohitaji joto maalum ili viive kwa namna inavotakiwa:

1. Kupika wali: Ukiongeza mchele kwenye maji ambayo hayajafikia kiwango cha kuchemka, mchele utakuwa mgumu kwa sababu chembechembe zake za wanga hazitakuwa na joto la kutosha kupenya ndani na kufanya mchele uwe laini. Utapata wali mbichi au mgumu hata kama utaendelea kupika kwa muda mrefu.

2. Kupika uji: Kama unga wa uji utawekwa kabla ya maji kufikia kiwango cha kuchemka, uji hautakuwa mzito ipasavyo.

Uji utabakia kuwa mwepesi na mbichi kwa sababu wanga hauna nguvu ya kuunda muundo mzito unaotarajiwa.
(kwenye hili wengi wamejikuta hawaelewi kwanini hawezi kupika uji ulioiva)

3. Kupika tambi: Tambi zikiwekwa kwenye maji yasiyo ya moto (kama hayajafika kiwango cha kuchemka), matokeo yake ni kwamba zitaiva nje lakini ndani zitabaki mbichi au zenye ugumu, hata kama utazipika kwa muda mrefu zaidi.

Kwa hivyo, katika vyakula vyote hivi, joto linalofaa la maji au mchanganyiko ni muhimu ili chembechembe za wanga ziweze kuvimba na kuiva ipasavyo. Ikiwa hatua hii itapuuzwa, chakula kinabaki na ubichi.
 
"Kama tunaambiwa Dunia inazunguka kwa kasi ya 1,674km/saa, kwanini ndege au helikopta hazipai juu, zikaganda na kusubiri sehemu inapohitaji kwenda ifike kisha itue?"

Nadhani swali limefanana hivi; kama Dunia inazunguka kasi hiyo, kwanini binaadam akiruka anatua palepale na si sehemu nyingine?

Tunasoma majibu yenu sehemu ya maoni. Karibuni
Hahahahaha
 
😄

😄 Mfano mzuri wape hii!! Tuonavyo linapochomoza mashariki kwenda magharibi ni kama tunaona kama linazama chini. Je linazungukia chini Ili liibukie tena mashariki? Jibu ni hapana! Itoshe kusema linazunguka clockwise. Hivyo dunia imesimama tuli kama plate ya saa na jua linazungukia juu ya Dunia kama mshale wa saa unavyozunguka juu ya plate ya saa yenyewe.
Wakati Joshua anapigana vita, Mungu alimwambia Joshua simamisha jua, hakumwambia asimamishe dunia.
 
"Kama tunaambiwa Dunia inazunguka kwa kasi ya 1,674km/saa, kwanini ndege au helikopta hazipai juu, zikaganda na kusubiri sehemu inapohitaji kwenda ifike kisha itue?"

Nadhani swali limefanana hivi; kama Dunia inazunguka kasi hiyo, kwanini binaadam akiruka anatua palepale na si sehemu nyingine?

Tunasoma majibu yenu sehemu ya maoni. Karibuni
Hata ndege ikiwa juu bado iko controlled na gravity ya dunia.
 
Dunia inazunguka pamoja na kilichopo juu ya ardhi, ni sawa na kusema nzi akiwa ndani ya ndege akataka kuruka kutoka siti ya nyuma kwenda siti ya mbele atashindwa kufika kwa vile ndege inakimbia kwa kasi sana, Hapana si kweli huyo nzi atafika vizuri tu sababu ndege inayembea na yeye anatembea hayupo excluded. Ndivyo ilivyo kwa helikopta hiyo uliyoitolea mfano. Ngoja wanafizikia waje wakufafanulie kitaalamu zaidi.
 
Wakati Joshua anapigana vita, Mungu alimwambia Joshua simamisha jua, hakumwambia asimamishe dunia.
Wakatoliko walimweka Galileo under house arrest kwa mawazo kama yako. Miaka miambili baadae wakaja kukiri hadharani kuwa jamaa alikua sahihi kwa kusema dunia ndio inazunguka sio jua.
 
Wakati Joshua anapigana vita, Mungu alimwambia Joshua simamisha jua, hakumwambia asimamishe dunia.
Ukitaka kujadili hoja za kisayansi Acha hivyo vitabu pembeni....
Ukishaingiza biblia na quran sayansi itakuwa ngumu kwako! Mfano vitu kama sigara au bangi vimeandikwa wapi kwenye hivyo vitabu?
 
Hakutakuwa na mabadiliko makubwa kihisia kwa abiria waliondani ya hiyo JET kwani chombo hicho kitakuwa bado ndani ya mvuto wa Dunia na hakingeweza kuathiri kitu kama wakati au nafasi kwa kiwango kikubwa.(MFANO NI ULE WA UKIWA NDANI YA LIFTI NA UKAWA UNATAKA KUPAA). Ni kama tu kuzunguka Dunia haraka zaidi kuliko ilivyo kawaida.

Labda Kwa mujibu wa nadharia za Einstein za uhusianifu, iwapo chombo hicho kingeweza kufikia kasi karibu na ile ya mwanga, kungeweza kutokea athari kama za kupinda kwa muda (time dilation), ambapo muda ungeonekana kupita polepole kwa abiria wa chombo hicho ikilinganishwa na wale walioko duniani. Lakini kwa kasi ndogo za jet, athari hizi hazitakuwa kubwa.

Kama nimfuatiliajibwa movie kama uliwahi ona series moja inaitwa
The Flash. Kuna majibu ya hili swali lako ndani ya ile series.

Sijui umepata kitu.? Ahsante
Shukrani mkuu jibu sawiha kabisa.
 
Ujinga hujaelewa geography rudi shule
Dunia inazunguka

Mfano ukichukua mpira wa miguu ukaweka sisimizi juu ya mpira kisha uzungushe mkononi sisimizi hawezi Anguka chini

Binadamu na maji yote uyaonayo ya mito na bahari ni kama kisisimizi tu kwenye tufe la dunia ndio maana hata likizunguka hatuwi kichwa chini miguu juu na kudondoka kama sisimizi tu ukiweka juu ya mpira wa miguu atabaki wima tu
Kweli kabisa. Sisimizi ukimuuliza mpira una umbo gani atasema tambarare
 
Dunia inazunguka pamoja na kilichopo juu ya ardhi, ni sawa na kusema nzi akiwa ndani ya ndege akataka kuruka kutoka siti ya nyuma kwenda siti ya mbele atashindwa kufika kwa vile ndege inakimbia kwa kasi sana, Hapana si kweli huyo nzi atafika vizuri tu sababu ndege inayembea na yeye anatembea hayupo excluded. Ndivyo ilivyo kwa helikopta hiyo uliyoitolea mfano. Ngoja wanafizikia waje wakufafanulie kitaalamu zaidi.
Kwa ufafanuzi wako kwa huo mfano mdogo umebeba majibu ya kisayansi kwa swali la mtoa hoja, kwa hiyo jibu hili limeifunga mada.
 
Back
Top Bottom