Swali la Morality: Je, ni lazima kuusema kila ukweli unaousikia au tutangulize mbele ‘Maslahi ya Taifa’?

Swali la Morality: Je, ni lazima kuusema kila ukweli unaousikia au tutangulize mbele ‘Maslahi ya Taifa’?

Mara kadhaa raisi amesema... MSEMAKWELI NI MPENZI WA MUNGU.....

Na moja ya ahadi za TANU (CCM baadaye) ni kusema kweli daima, fitina ni mwiko...

KWENYE HAYO HAPO JUU... the only condition ya kusema kweli ni
1. Ukweli uwe kweli
2. The fact kwamba ni ukweli, hakuna lingine la kuangalia... USEMWE TU
3. Ukweli usemwe wakati wote.... hata mahakamani, ukidanganya, na ikathibitika, WOTE TUNAFAHAMU MATOKEO YAKE
4. Ukweli hauna muda, mahali, wala anayeambiwa ukweli huo ni nani... UKWELI DAIMA

HIVYO TUSEME UKWELI, NA SIKU ZOTE UKWELI UNAUMA....
 
Haya ni maono ya mtu aliyeserve as president wa USA miaka ya 1900!

Patriotism means to stand by the country. It does not mean to stand by the president or any other public official, save exactly to the degree in which he himself stands by the country. It is patriotic to support him insofar as he efficiently serves the country. It is unpatriotic not to oppose him to the exact extent that by inefficiency or otherwise he fails in his duty to stand by the country. In either event, it is unpatriotic not to tell the truth, whether about the president or anyone else.
Theodore Roosevelt

Tukiwapa watu mamlaka ya kutuchagulia ukweli wa kuuzungumza,basi tutaumizwa!Siku zote,ukweli utakaosemwa na wapinzani hauwezi kuwapendeza watawala!
The truth is always the best answer,no matter how ugly it is!
Its better an ugly truth than a sweet lie!
 
walishasema kazi yao kuuu ni kupingapinga tu basi lakini nafikiri kuna haja ya kujitafakari sio kila kitu kuropokaropoka kuna issues nyingine ni too classified sio lazima Uzi disclose for political gain hii issue ni national matter against our enemy na wanatushangaa baadhi yetu kuwa upande wao
Mzee wa Chattle ndie bingwa wa kuropoka na kukashifu watz mmoja mmoja, makundi na hata taifa. Yeye anajiita msema kweli. Mwacheni nae na wengine wote wapewe UKWELI kwa faida ya taifa, WANAPOCHEMSHA.
 
Tatizo ni kukiamini kipimo cha madhara ya kuusema ukweli. Mara nyingi unaogopa kuusema ukweli kwa kulinda maslahi kiduchu ya taifa kuliko ungeusema, taifa likaumia kidogo lakini likapata maslahi makubwa baadae. Nafikiri jamaa ameusema ukweli na nafikiri huo ukweli utaleta manufaa kwa taifa kama taifa litajielekeza kuukubali na kusonga mbele.
 
Nimekuwa nafuatlia maandiko ya Pascal lakini huwa nashindwa kuelewa huyu jamaa akili yake na msimamo wake ni upi. Ngoja tu nimuweke kwenye ignore list. Leo atasema hiki kesho atasema kile yaani kama mtoto mdogo vile hata kumbukumbu ya alichosimamia jana hana.
 
Ni maswali mazuri Bw. Pascal Mayalla (Au mwenye njaa) Kama inavyojulikana kwetu kanda ya ziwa na kuthibitishwa na JPM!
Maswali haya kuhusu morality lazima yaulizwe kwenye jamii iliyo civilised na kupenda zaidi "nguvu ya hoja" kuliko hoja ya nguvu..
Mfano kama wanausalama wetu wa kuwakamata hovyo wapinzani kwasababu za "kitoto" au za kuuliza maswali yanayohitaji majibu yameshangaza wengi kabisa, mpaka asiyependa kutumia akili yake anajuwa tu hapa, wale wapinzani kwenye siasa na watundu wanawachezea tu polisi wetu! Wanawafanya kama "puppets", wanajuwa wakitekenya pale au kukuna huku basi hata iweje, "KIKI" toka polisi ziko njiani! Swali ni kujiuliza je wapinzani bado wanaharakati au ni vyama vya siasa vilivyokomaa na kushindiliwa na itikadi, ilani na ajenda?!
Tanzania inafaidika sana na hivyo vyama pinzani, ila bado, wapinzani wanatunyenga kwa kutokutupa faida ya ruzuku walipwazo, I wish wengekuwa smart zaidi na sera zao na kufikia wengi hasa vijijini, hapo hata walio madarakani wasingekuwa wame relax namna hii, kwa kujiachia na ma scandals lukuki (rada/nssf/atcl/epa/madini..), na sababu upinzani uko weak, ndiyo maana hata kina wa poti (nyoka mwenye makengeza) wanazidi kutawala tu! Hakuna wa kuwaondoa wale mafisadi waliotuhumiwa zaidi ya raia, kishindo cha raia kikiamuwa, hata wale waliowapa madaraka wangenywea, waliotuhumiwa kwa ufisadi sasa hivi tungesikia wako gerezani au wameachia ngazi..
 
UKWELI WOWOTE LAZIMA USEMWE NA USIPOSEMWA UTAKUJA WENYEWE TU.

KUFICHA UKWELI VILEVILE NI KUJIKOMBA.

KUHUSU POLISI, WAO WANAENDA KWA AMRI, SIDHANI KAMA WANAJIAMRISHA WENYEWE.

MWISHO BW. PASKAL WEWE NI CCM DAMU KAMA MIMI TU..
 
sio kwa kuhadithiwa kuwa anapenda challenge, ila hizo challenge ziwe ni ukosoaji wa kweli wenye nia njema,

uliweza kugundua kama ana uwezo wa kuijua nia njema na nia ovu? anavyo au wewe unavyo vipimo vya nia njema na ovu? yaani nia njema au ovu ni kwa mujibu wa nani?

Jee Wapinzani Kazi yao ni Kupinga Tuu Kila Kitu au Kukosoa Tuu Hakuna Kupongeza Hata kwa Mazuri?.
Japo kazi ya upinzani ni kupinga na kukosoa, lakini tunapokuja kwenye issues muhimu kwa maslahi ya taifa, maslahi yataifa ndio yanatangulizwa mbele,


imewahi kusemwa huko nyuma kuwa kazi ya upinzani sio kuipa sifa serikali. kazi ya upinzani ni kuikosoa inapofanya makosa. pongezi tayari hizo zimeshughulikiwa. kwa viongozi kupewa mshahara kwa kazi yao hiyo ndio pongezi yao. hii term kupinga kila kitu nahisi na wewe unaitumia vibaya pia. mimi sijamsikia mpinzani hivi karibuni akikosoa utendaji wa mkuu wa mkoa wa DSM, wala wa wizara ya ardhi. hapa labda nawe umefata mkumbo pasko. halafu ukihisi mtu kapinga si ushughulika na analolisema. kama halina tatizo si umwambie wewe umepotoka hapa lakini kupinga kama zipo hoja huwezi ukakaa kimya halafu useme umelitendea haki taifa

nahisi umekerwa na press conference ya kusema ukweli na uwazi ya TL ambayo labda unadhani inapingana na maslahi ya taifa. hapa hebu tafakari tena vizuri na taratibu.

Nixon miaka hiyo aligundulika akifanya uovu kuhusu upinzani wa kisiasa miaka hiyo. kilichofanyika wamarekani wa chama tawala na upinzani walitoa mchango mkubwa kuexpose uovu ule uliomuwajibisha Nixon. mtu wa kawaida angesema ni usaliti au kutoweka mbele maslahi ya taifa kum-unsit the incumbent president. lakini kwa kuhitaji kumaintain integrity ya kiti cha urais wote walikubaliana rais atoke
 
Paskali: hili siyo swali la morality tu, pia ni la kisheria. Kuna madhahidi fulani fulani hawakubaliki kutoa ushahidi - mathalani, Lawyer kuhusu alichoambiwa ns mteja; au Padri aluchoambiwa wakati wa kuungama, au Daktari kuhusu mgonjwa wake. Hizi ni ckear-cut, lakini kuna zingine pia japo zinapita, hutiluwa mashakanashaka: mfano ni mtu na mumewe au baba na mwanaye au nyani na ngedere. Hii ya Tundulissu kutoa siri za nchi na kuwapa maadui ushahidi wa kimahakama miaka nenda rudi, halafu kuwatonya kwamba kuna ndege yetu mahali waende wakaikamate, huu ni uhaini. He us spying on his country for the benefit if uts creditors. Swali pekee tulilonalo ni kama atanyongwa au atapata msamaha wa Rais.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maoni yangu ni kwamba inabidi tuelewe vizuri na tukubaliane, nini hasa maana ya MASLAHI YA TAIFA. shida iko hapo. kwa upande wa watawala wetu, maslahi ya taifa ni maslahi yao. maslahi ya CCM ndiyo maslahi ya taifa. Full Stop. sasa shida inaanzia hapo. Chukulia suala la Lissu na Bombadia iliyokamatwa. Hoja ya Lissu ilikuwa ni kwamba Taifa linapelekwa kwenye hatari kubwa ya kuvunja ovyo mikataba, hali ambayo itapelekea tulipishwe faini kubwa na nyingi, na hii inaathiri kwa kiasi kikubwa MASLAHI YA TAIFA. Lissu alijenga hoja yake katika kauli ya Waziri wa Sheria na Katiba, Prof. Kabudi, na Waziri wa habari nk., Dr. Mwakyembe, ambaye pia ni mwanasheria nguli. hawa walisema bungeni, baada ya hoja za Lissu kuhusu tahadhari kwa maamuzi ya serikali mintarafu mikataba, kwamba Tanzania ni Sovereign State, na kwa hiyo hatuwezi kuogopa kuvunja mikataba. Lissu alitahadharisha kwamba hii kauli ni Reckless na haina umakini wala weledi, hasa ikitoka kwa wanasheria nguli. kwa hiyo hoja ya Lissu iko wazi sana, kwamba anatetea MASLAHI YA TAIFA. Ilibidi aseme wazi kwa sababu kuna ajenda ya watawala ambayo wanaipigia kelele nyingi sana kwa kutumia vyombo vyao vyenye nguvu. sasa Tundu Lissu ni mtu mmoja tu, tena asiye na nguvu kama Dola. ilibidi apige kelele namna ile ili taifa lisikie.

Watawala katika jitihada za kumzima Lissu, kuwafanya wananchi wasimsikilize, wakampaka rangi ya kukosa uzalendo, kutojali maslahi ya taifa, na kufurahia matatizo ya nchi. hii ni propaganda ambayo wenye akili wanatarajiwa kuiona na kuiweka wazi. Aliyesababisha hasara hii kubwa kwa taifa, ndiyo huyo ambaye sasa hivi ndiye Rais wetu. ameingia kwenye mzozo mkubwa na wapinzani, kutokana na njia zake ambazo siyo za kikatiba, na kinyume cha sheria na kanuni za vyama vingi, na pia anatumia nguvu za Dola kuwabana, kuwatesa na kuwanyanyasa wapinzani. haya yote yanatakiwa kutiliwa maanani, namna nyingine tutakuwa tunacheza ngoma za wapika propaganda.

Kwa hiyo suala la Morality lina nafasi yake, lakini morality hapa ni kuwaumbua watawala, kuwaweka mbali na kile kinachoitwa MASLAHI YA TAIFA. kama kweli maslahi ya taifa yangewekwa mbele, tusingeshuhudia bomoa bomoa inayoendelea hivi sasa katika barabara ya kimara - kiluvya, kwa mtindo huu, tena kinyume na maamuzi ya mahakama.

MASLAHI YA TAIFA ni kujua ni kwa vigezo gani Magufuli alivunja mkataba ule, ukweli uwekwe wazi kabisa, siyo kuficha ficha eti kwa sababu Magufuli ni Rais. inabidi tufanye kama kule Israel, ambapo mtawala anaweza kushitakiwa wakati wowote. kumfanya mtawala kuwa nusu mungu ni kunajisi maslahi ya taifa na siyo moral.
 
Paskali: hili siyo swali la morality tu, pia ni la kisheria. Kuna madhahidi fulani fulani hawakubaliki kutoa ushahidi - mathalani, Lawyer kuhusu alichoambiwa ns mteja; au Padri aluchoambiwa wakati wa kuungama, au Daktari kuhusu mgonjwa wake. Hizi ni ckear-cut, lakini kuna zingine pia japo zinapita, hutiluwa mashakanashaka: mfano ni mtu na mumewe au baba na mwanaye au nyani na ngedere. Hii ya Tundulissu kutoa siri za nchi na kuwapa maadui ushahidi wa kimahakama miaka nenda rudi, halafu kuwatonya kwamba kuna ndege yetu mahali waende wakaikamate, huu ni uhaini. He us spying on his country for the benefit if uts creditors. Swali pekee tulilonalo ni kama atanyongwa au atapata msamaha wa Rais.

Sent using Jamii Forums mobile app

kushindwa kwa kesi ya stirling haikuwa siri. ilikuwa public information. ni maamuzi ya mahakama. uhaini ni kutaka kuangusha serikali sasa kama kusema leo kwenye mediam kwamba barabara ya mahenge haipitiki wakati wa mvua kali ni uhaini basi zisihi sana mamlaka zimshughulikie TL.

now people want TL dead. geez! he is a patriot meeeen!
 
walishasema kazi yao kuuu ni kupingapinga tu basi lakini nafikiri kuna haja ya kujitafakari sio kila kitu kuropokaropoka kuna issues nyingine ni too classified sio lazima Uzi disclose for political gain hii issue ni national matter against our enemy na wanatushangaa baadhi yetu kuwa upande wao

LISU ndio alitoa Oda Ndege ikamatwe !....kwanini hamtaki kuangalia mlipojikwaa badala yake mnalaumu mlipoangukia... Issue ya MAKINIKIA mmewaita watu kila aina ya majina nivipi nao wakitushtaki tukadaiwa maHELA
ya Fidia mtataka tena watu wawaunge mkono ikiwa sasa hivi mmeziba masikio...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Paskali: hili siyo swali la morality tu, pia ni la kisheria. Kuna madhahidi fulani fulani hawakubaliki kutoa ushahidi - mathalani, Lawyer kuhusu alichoambiwa ns mteja; au Padri aluchoambiwa wakati wa kuungama, au Daktari kuhusu mgonjwa wake. Hizi ni ckear-cut, lakini kuna zingine pia japo zinapita, hutiluwa mashakanashaka: mfano ni mtu na mumewe au baba na mwanaye au nyani na ngedere. Hii ya Tundulissu kutoa siri za nchi na kuwapa maadui ushahidi wa kimahakama miaka nenda rudi - (Sidhani kama una ushahidi na hili kwa kweli) halafu kuwatonya kwamba kuna ndege yetu mahali waende wakaikamate, - (Hili la ndege haikuwa siri Mkuu wetu amekuwa akilisema kwa kulirudia rudia sana kwenye mikutano yake) huu ni uhaini. He us spying on his country for the benefit if uts creditors. Swali pekee tulilonalo ni kama atanyongwa au atapata msamaha wa Rais.
Sent using Jamii Forums mobile app

WILLIAM MARCONI, Kitu kimoja tunasahau na hili laweza kumpa point Lisu hata mahakamani, yeye alikuwa kama msomaji tu wa Tamko la chama. Maana yake ni nini, yale ni maneno toka kwa wanachama na uongozi wote kwa ujumla. Hivyo basi Lisu katumika kama radio kusema ambayo chama kilitaka yasikike kwa jamii nzima kulingana na vyanzo vyake vya taarifa. Kwa hiyo kama ni kukamata na kumshikisha adabu mtu, ilitakiwa Kamati nzima ya uongozi ya juu ya chama husika iwekwe ndani maana lile ni tamko la chama sio la Lisu, lina baraka zote za viongozi wa chama. Kama ni uhaini umetendwa na chama kizima na si Lisu peke yake. Kumtia ndani yeye na kuwaacha wengine nadhani si sahihi sana!
 
Back
Top Bottom