Swali la mwaka: Nani alimleta Ballali nchini?

Swali la mwaka: Nani alimleta Ballali nchini?

Naomba nisikubaliane na wewe Bwana Gembe kwamba Balali alipewa kazi kwa vile alikuwa na uwezo.Naomba nikubaliane na Mwanakijiji kwamba Balali aliwekwa Bank Kuu kwa makusudi fulani.Kumbuka kwamba Balali alikuwa mwajiriwa wa World Bank.Ambacho bado kinanisumbua akili ni kwamba hivi Tanzania tulikosa watu wenye 'qualifications' za kufanya kazi Bank Kuu mpaka World Bank watuletee mtu Kama Balali?This is extremely suspicious.Ninahisi World Bank walikuwa na ajenda ya siri na ninahisi ajenda yao ni hili lililotokea.Wale wenye "idea of conspiracies" zinazoendelea nadhani wanajua kwamba World Bank,IMF au mashirika yeyote ya wakubwa hawa hawana nia ya kweli ya kutuendeleza kiuchumi.Maneno yao yanaonekana kuwa matatamu sana "to unsuspicious minds,but the truth is the opposite." Ndio maana mara nyiki tumeingizwa mkenge,na kama hatukuwa waangalifu tutaendelea kuumia.

Mwanakijiji,

Mie nina uhakika kabisa balali alipewa kazi kutokana na uwezo aliokuwa nao na wakati Ballali anakuja hapa Tanzania hakuja kama Msahuri wa Mzee Ben bali alikuja kufanya kazi ya World Bank kakita jitihada za WB kusaidia nchi zilizokuwa zinaendelea.

Ballali aliletwa na World Bank na kama kuna mtu alimshauri Mkapa ampe kazi Ballali atakuwa ni Katibu Mkuu kiongozi na yeye alifanya hivyo baada ya kupatikana vetting report kutoka kwa watu wa Usalama wa Taifa.

Nakumbuka Ballali aliitwa na Mkapa pale Magogoni siku ya Jumapili na kuambiwa ameteuliwa kuwa Gavana na hakupewa muda wa kutafakari kuhusiana na hilo ila inasemekana kuna wizi flani ulitokea pale BOT na Mkapa alikasirishwa sana na kuagiza yafanyike mabadiliko makubwa pale BOT. Sema kipindi hicho watu wa aina ya Ngurumo na Mwanakijiji, Watu wenye uwezo wa kusema yale magumu kama Kubenea walikuwa hawana meno.

Ilikuwa ni tabia ya Mkapa kumfukuza mtu yeyote yule pindi anapokosea, mtakumbuka jinsi alivyomfukuza Mattaka pale PPF. Alivyomuomba Mboma aachie ngazi baada ya kashfa ya sukari, mie nilishangaa sana Mboma kurudi na kutaka ubunge!

Mkuu Mwanakijiji kama utakumbuka wakati Mkapa akiwa pale Foreign alikuwa ni Waziri pekee ambaye alikuwa akirudisha pesa wizarani kila mwaka na alikuwa na rekodi safi sana katika utendaji na utumiaji wa pesa za umma, na hii ilisababisha Mwalimu kumkubali mapema sana tofauti na wengine waliogombea 1995 (kumbukeni kashfa flani za madini 1994).

Mzee Mkapa alibadilika sana kuanzia kifo cha mwalimu, nadhani alighafirika na kupoteza mwelekeo na kuna watu walijiingiza sana pale na kujidai walikuwa watu wa karibu na mwalimu.

The one and only person wa kulaumiwa mpaka leo ni Ruhinda!
 
After all this "debate" what then?

Upuuzi mtupu! Why cry over spilled milk? That stuff is done for, kaput, a non-issue, upuuzi etc etc. The question should be: What should I do next? Or, as it is popular in Tanzania: What should the government do next? In management speak: What do we do next? How do we think outside the box and move forward?

Whether who brought Balali in, or what town to be given to release a name etc is utter upuuzi! Mwanakijiji already knew what he was asking but maybe his intentions was to add on another meaningless topic in this forum....

Dah!!!! Mshkaji unatukata stimu. Acha watu wamkome nyani regardless whether they are along MKJJ's track
 
Hii thread imekuwa inajiruida sana mbele yangu. Kuna wakati nikiwa safarini kwenda mapumzikoni Tanzania niliwahi kukutana na jamaa mmoja aliyewahi kufanya kazi nyeti pale State Department akanituma nimfikishie salamu zake kwa Mkapa, Ballali, Anna Muganda na mama mwingine aliyekuwa na jina la kutokea Songea ambaye wakati huo alikuwa anafanya kazi Wizara ya Afya. Bwana huyu alikuwa anawajua watu hao personally kutokana na kukutana nao mara kwa mara hapo Washington DC wakati akiwa state Department nao wakiwa kwenye majukumu yao ya kawaida ambapo Mkapa alikuwa Balozi wa Tanzania hapo Marekani.

Kwa hiyo Mkapa na Ballali walikuwa wanafahamiana siku nyingi sana. Nadhani Mkapa ndiye aliyemleta rafiki yake huyo wa zamani, ingawa inasemekana kuwa wakati huo Ballali alishakuwa raia wa Marekani (sina uhakika lakini na sidhani kama tetesi hizo ni za kweli).
 
Mama wa kwanza wa zamani alimtafutia mke ballali.....
 
Ndg Mtanzania,
Anaanza na jina (M), anatokea mkoa unaoanza na jina (M), na mimi naanza na Jina (M)ajita basi nakupoa mji MUSOMA ili "M" iendelee kuwa common factor.Kubaali basi na pls pasua jipu.

Majita,

Bahati mbaya tayari nimeshapewa mji na kuukubali na kutoa jina. Nikikubali na mji wa pili nitakuwa fisadi.

Dada yenu ndiye alimtambulisha Ballali kwa Mkapa. Baada fisadi mkuu kuchukua ushauri zaidi ya unaokubalika, wenye mali wakaona huyo mama hafai na ikabidi aondoke.

Mkuu FMES kamwaga mtiririko mzima.
 
Wakuu mtujibie basi swali hilo la nani alimshauri Mkapa amchukue Balali.Ninavyoona mimi dili hilo wahusika ni Chenge,Rostam,Mkapa na Balali.
 
Nani alimleta balali nchini...Kwani balali lilikuwa boga?balali alikwea mwenyewe pipa na kujileta mwenyewe bongo.
 
Nani alimleta balali nchini...Kwani balali lilikuwa boga?balali alikwea mwenyewe pipa na kujileta mwenyewe bongo.

Mkuu naona umepotea kabisa.
Yawezekana hujui Balali mwana wa Mufindi alicho tundea taifa hili na kuzugwa kuwa kafa...nisiendelee isije ikawa nongwa.Watu bado wana machungu wanataka kujua nani aliye mpa dili Balali BoT?
 
Mkuu naona umepotea kabisa.
Yawezekana hujui Balali mwana wa Mufindi alicho tundea taifa hili na kuzugwa kuwa kafa...nisiendelee isije ikawa nongwa.Watu bado wana machungu wanataka kujua nani aliye mpa dili Balali BoT?

Ukishajua nani aliyempa balali dili BoT what next?
 
Majita,

Bahati mbaya tayari nimeshapewa mji na kuukubali na kutoa jina. Nikikubali na mji wa pili nitakuwa fisadi.

Dada yenu ndiye alimtambulisha Ballali kwa Mkapa. Baada fisadi mkuu kuchukua ushauri zaidi ya unaokubalika, wenye mali wakaona huyo mama hafai na ikabidi aondoke.

Mkuu FMES kamwaga mtiririko mzima.

Mkuu Mtanzania!!
Yaani utafanya kila nitakapo kuwa napiga kona kwenda kupata moja moto moja baridi nikizungukia uani kwa familia ya huyu dada yetu niwe natapika kwa kuyatinga.Ila kwa vile fisadi anaweza akawa yeye peke yake bila familia yake kuhusika ngoja nisitapike,ila kale ka methali sijui "......... janga hula na wa kwao bado kananisuta"
 
nimefatilia hii story hapa nafikiria Balali alitumiwa bila yeye kujua, watoto wa mjiji walijua balali ajazoea mambo ya corruption na mambo mengine ya madili ya dar, kwahiyo alikuwa a good target for the really ufisadi. Na watu waliomchezea Balali ni watu ambao wapo BOT and Mafisadi wengine wa mjini hapa
 
Mkjj pata break kidogo kwanza.

[media]http://www.youtube.com/watch?v=UXDh7OwlOOM[/media]
 
Back
Top Bottom