Swali la uchumi: Kwanini vikwazo vya mataifa yenye nguvu kubwa kiuchumi havifanyi kazi dhidi ya Urusi?

Swali la uchumi: Kwanini vikwazo vya mataifa yenye nguvu kubwa kiuchumi havifanyi kazi dhidi ya Urusi?

Hayo maneno yalisema na Prof Halford Mackinder (The Father of Geopolitics) kwenye chapisho lake la mwaka 1904 liitwalo The Geographical Pivot of History. Mle ndani alianzisha kitu kiitwacho The Heartland Theory, na kusema taifa lolote litakalofanikiwa kuitawala Urusi (The Heartland) ndiyo litaitawala dunia.

Kiufupi, hata Adolf Hitler anapovamia Urusi mwaka 1931 ilikuwa kwasababu aliamini katika hii falsafa, ambayo wanafalsafa wengine kama Henry Kissinger, George Kenan na Zbigniew Brezinsky waliifuata.
View attachment 2702409

NB: Ila je, hili lina ukweli wowote au yalikuwa ni mawazo tu ya wasomi wa Ulaya ???
Ingekuwa ina ukweli asilimia 100, Warusi wenyewe wanaojitawala huenda wangekuwa watawala wa hii dunia mpaka sasa.
 
Ndugu mchumi, mtaalamu mwenzako Zitto Jr anasema haipo hivyo, ulivyosema wewe hapa. Anasema kwamba miaka mitano ijayo G7 watapata mbadala wa nishati ya Urusi. Ila takwimu za kihistoria zinasema kwamba Ujerumani amekuwa akitegemea gesi, mafuta, chuma na mpira kutoka Urusi ili kuendesha uchumi wake wa viwanda tokea miaka ya 1930's na mpaka leo imepita miaka 93 bado hajapata mbadala.

Hivi inawezekana kabisa kwamba kuna siku mataifa ya magharibi hasahasa Ulaya, yataacha kutegemea rasilimali kutoka Urusi, na ile nchi ianguke kutokana na kuwa dhaifu kiuchumi, ??? Haya hapa chini ni maneno ya mchumi na mwanahistoria kutoka Yale University na Cambridge University.

View attachment 2702425
Hapana professor, takwimu na nimeattach link ya Reuters inaonyesha jinsi Ujerumani inaizidi kupunguza utegemezi wa Gas ya Russia In fact Germany inategemea gesi ya Norway kuliko ya Russia


So sielewi kivipi iwe reliant kwa gas ya Urusi wakati Kuna alternatives
 
kwa lugha rahisi hapo, tajiri ni mwenye mahindi (maana akipandisha bei au akigoma kuuza wewe mwenye milioni utahangaika sana kupata mbadala, au pengine ukipata itakua bei juu mno,

ndipo ile nadharia kwamba ulaya magharibi ni maskini (pengine kuliko afrika) inapoingia,..... leo tukisema kila mtu aishi kwa kutegemea alichonacho, basi wale wenzetu wanaweza kufa sana,

na hii ndiyo inayombeba Urusi, ana bidhaa ambazo ulaya wanazihitaji ili waendelee kuishi na uchumi wao usitetereke pakubwa,......
Mkuu embu kuwa serious basi.
 
Hayo maneno yalisema na Prof Halford Mackinder (The Father of Geopolitics) kwenye chapisho lake la mwaka 1904 liitwalo The Geographical Pivot of History. Mle ndani alianzisha kitu kiitwacho The Heartland Theory, na kusema taifa lolote litakalofanikiwa kuitawala Urusi (The Heartland) ndiyo litaitawala dunia.

Kiufupi, hata Adolf Hitler anapovamia Urusi mwaka 1931 ilikuwa kwasababu aliamini katika hii falsafa, ambayo wanafalsafa wengine kama Henry Kissinger, George Kenan na Zbigniew Brezinsky waliifuata.
View attachment 2702409

NB: Ila je, hili lina ukweli wowote au yalikuwa ni mawazo tu ya wasomi wa Ulaya ???
Ukweli wa hiyo theory unapimwa kwa impact ya yankiuchumu wa Russia duniani.Mgogoro wa Uchumi unayoikumba Ulaya nzima na USA imetokana na vikwazo vilivyowekwa na wao wenyewe dhidi ya Russia.

Issue ya vikwazo kwa Russia imepelekea kuyumba kwa uchumi wote wa Dunia,hii ni kutokana na ukweli kuwa Russia amesababisha Currency ya USA ($) kuyumba vilevile masoko ya mitaji na dhamana kwenye masoko ya USA na Europe kuyumba-hali iliyopelekea Nchi zote kuyumba kiuchumi.

Asiyelijua hili hana akili na asiyetaka kulikubali basi ubongo wake una kamasi.
 
Ndugu mchumi, mtaalamu mwenzako Zitto Jr anasema haipo hivyo, ulivyosema wewe hapa. Anasema kwamba miaka mitano ijayo G7 watapata mbadala wa nishati ya Urusi. Ila takwimu za kihistoria zinasema kwamba Ujerumani amekuwa akitegemea gesi, mafuta, chuma na mpira kutoka Urusi ili kuendesha uchumi wake wa viwanda tokea miaka ya 1930's na mpaka leo imepita miaka 93 bado hajapata mbadala.

Hivi inawezekana kabisa kwamba kuna siku mataifa ya magharibi hasahasa Ulaya, yataacha kutegemea rasilimali kutoka Urusi, na ile nchi ianguke kutokana na kuwa dhaifu kiuchumi, ??? Haya hapa chini ni maneno ya mchumi na mwanahistoria kutoka Yale University na Cambridge University.

View attachment 2702425
Issue ni kuwa kwa zaidi ya miaka 150 hakujapatikana hizo njia mbadala zitakuja kupatikana Leo?,hata wakisema wasitegemee mafuta na gasi kama njia kuu ya nishati chochote watakacho kibuni kitahitaji resources na hizo resources lazima utakwenda Russia tu.

Kwa sasa hata ukimyenga Russia ukimbilie katika Nchi zingine bado ni Yale Yale issue itakuja kwenye reserve ya hiyo Nishati Nchi nyingi zinazo hizo nishati but kwa ujazo gani?? Kabla hawajaishiwa.Vipi swala LA gharama ambalo litaongeza gharama za ualishaji Mara dufu.
 
No it's not true, ingekua pesa ni nyingi kuliko bidhaa basi kungetokea hyperinflation kama iliyotokea kipindi cha Great Economic Depression.

I would request actual data to back this fact.
Mkuu unabisha kuwa USA ha print pesa ambayo haiendani na production yake?
USA ame print USD kama njugu na kupeleka Ukraine.
 
Gharama za kuzifata huko zilipo mpaka kuzifikisha kwao ni kubwa kuliko kuzifata za Urusi....Sana Sana wameziwekea baadhi ya 'vigingi' kama adhabu mfano 'price cap' kwenye mafuta ya Urusi pekee.

Hakuna Price cap iliyofanikiwa na Crude oil imeanza kupanda tena. Labda useme ni Price cap ipi umefanikiwa mpaka sasa.
 
Mkuu unabisha kuwa USA ha print pesa ambayo haiendani na production yake?
USA ame print USD kama njugu na kupeleka Ukraine.
Mkuu The Boy Wonder amekiri kwamba pesa ya USA ni reserve currency na kwamba Kila nchi inaitumia kwenye kufanya biashara kimataifa so hata siku Moja supply ya dollar haiwezi kuzidi demand ya dollars kwenye biashara ya kimataifa.

Hata Tanzania tunaprint Hela sana ila wakati Gani inaongezwa au inapunguzwa kwenye uchumi is strictly regulated to avoid hyperinflation
 
Kinachoibakiza urusi kusimamia ni appeasement policy, hii pia ilifanyika kwa Hitler kipindi anaijenga Ujerumani kuwa taifa kubwa miaka ya 1930s.

Appeasement policy ni Ile sera ambayo unamuacha adui Yako afanye Ghasia anazotaka kwa kuepuka kuanzisha naye vita kwa kuhofia akijibu mapigo basi anaweza leta madhara makubwa hata kama utamshinda vitani.

So Urusi anasurvive sababu kwanza anakiuka masharti ya vikwazo mfano Kuna nchi Bado zinachukua gesi na mafuta kwake licha ya zuio ila Sasa mtamfanyeje? Mtamshambulia kwa Kulikua vikwazo? Ndio tunarudi kule kule kwa appeasement policy?

Kingine Urusi ana population kubwa, so ukianzisha vita naye believe me hata kama watakufa million 50 Bado tu watazalisha wanajeshi Kila siku hivyo vita haitoisha na italeta madhara makubwa kwa west.

So uwezo wa kumtandika urusi wanao ila at what cost? Anaweza akapigwa sana ila trust me nusu ya ulaya inaweza kuchakazwa kwa nuclear weapons ambayo itahitaji miaka zaidi ya 7 kusafisha radiation kwenye mazingira.

So Urusi kinachomfanya asurvive ni uwepo wa nuclear na population kubwa ila combat wise haogopeki hata kidogo no wonder Ukraine tu inamtoa jasho sembuse NATO?
Ndoto za asubuhi, kama wangekuwa na uwezo huo wangethubutu waone. Mbona nchi nyingine wanavamia iweje isiwe Urusi?! Siku hao wamagharibi wakithubutu ndio utakuwa mwisho wao. Wamejaribu vikwazo tu lakini nchi zao hazikaliki ni fujo za wenyewe kwa wenyewe kila kukicha watu wao hawaitaki nato na umoja wa ulaya...
 
Ndoto za asubuhi, kama wangekuwa na uwezo huo wangethubutu waone. Mbona nchi nyingine wanavamia iweje isiwe Urusi?! Siku hao wamagharibi wakithubutu ndio utakuwa mwisho wao. Wamejaribu vikwazo tu lakini nchi zao hazikaliki ni fujo za wenyewe kwa wenyewe kila kukicha watu wao hawaitaki nato na umoja wa ulaya...
Waivamie ya Nini wakati imeshindwa vita? Hivi Russia kuiteka Kiev imeshindikana kwa zaidi ya mwaka Sasa ndio sembuse wapambane na NATO?

Hivi Kuna Taifa lilikua na nguvu kuliko USSR? ila iliporomoka kirahisi tu ndio sembuse a weakened Russia?

Wanachohofia ni madhara ya vita tu yatakua makubwa ila sio kwamba wanaogopa kushindwa vita.
 
Waivamie ya Nini wakati imeshindwa vita? Hivi Russia kuiteka Kiev imeshindikana kwa zaidi ya mwaka Sasa ndio sembuse wapambane na NATO?

Hivi Kuna Taifa lilikua na nguvu kuliko USSR? ila iliporomoka kirahisi tu ndio sembuse a weakened Russia?

Wanachohofia ni madhara ya vita tu yatakua makubwa ila sio kwamba wanaogopa kushindwa vita.
Yetu macho tusubiri.
 
Waivamie ya Nini wakati imeshindwa vita? Hivi Russia kuiteka Kiev imeshindikana kwa zaidi ya mwaka Sasa ndio sembuse wapambane na NATO?

Hivi Kuna Taifa lilikua na nguvu kuliko USSR? ila iliporomoka kirahisi tu ndio sembuse a weakened Russia?

Wanachohofia ni madhara ya vita tu yatakua makubwa ila sio kwamba wanaogopa kushindwa vita.
Iraq hawakuogopa madhara ya kivita mkuu.
 
Ni maandalizi.
Russia alijiandaa kwa haya, Donetsk ilikaribia kujitenga mwaka 2014. Separatist chini ya makamanda kama Motorola na Givi walikaribia Kuichukua Mauripol, kabla ya kupewa order ya Kusitisha kutoka Kremlin.

Nadhani Russia ilijipima msuli wake, ikajiona haiwezi kuwasupport kama ikiwekewa vikwazo kwa wakati ule. Wamejipanga na 2022 wamerudi tena. Kwahiyo si ajabu uchumi wao kutoanguka kama ilivyotarajiwa. Westerns either hawakulijua hili au walipuuzia lakini wakati wanaweka vikwazo walitarajia internal disputes ziiangushe russia, walichosahau ni kuwa Mpaka January 2022 kupeleka jeshi Ukraine ilikuwa ni stance ya wapinzani.

Wamefanya nini? Wameuondoa uchumi wao kutoka kwenye utegemezi wa magharibi ( japo sio asilimia 100), na wakifanikiwa kuikamata Afrika basi hawatokamatika.
 
Mkuu The Boy Wonder amekiri kwamba pesa ya USA ni reserve currency na kwamba Kila nchi inaitumia kwenye kufanya biashara kimataifa so hata siku Moja supply ya dollar haiwezi kuzidi demand ya dollars kwenye biashara ya kimataifa.

Hata Tanzania tunaprint Hela sana ila wakati Gani inaongezwa au inapunguzwa kwenye uchumi is strictly regulated to avoid hyperinflation
Niliuliza swali hili maksudi kutaka kupima uaelewa wako wa mfumo mzima wa BRETTON WOODS. Ila ukanijibu kwamba haiwezekani fedha zikachapishwa nyingi kuliko bidhaa za masokoni. Ulinishangaza sana ndugu mchumi. Binafsi, nikakwambia siyo kweli na nikakuwekea Money Base (MO) ya Marekani na mahesabu yake, ila ukaendelea kubisha. Kwanini, hukuzingatia kikokotoo nilichokiweka ndugu mchumi na ukaendelea kubisha, ???

Mosi, Kiufupi ni kwamba, kadiri mataifa mengi yanavyopunguza matumizi ya dola uchumi wa Marekani na dunia nzima uko hatarini mno. Hili ni suala ambalo wengi hamjaliona tangu huu mgogoro uanze. Uvamizi wa Ukraine ni geresha tu, ila vita yenyewe ipo kwenye uwanja wa kiuchumi na inalenga kumuumiza Marekani zaidi. Marekani ana mengi ya kupoteza kuliko Urusi kwasababu, udhaifu wake mkuu uko kwenye dola (The Dollar is America only ultimate weapon).

Pili, wakati vita ya pili ya dunia inaisha Marekani ndiyo taifa lililokuwa na dhahabu yote ya dunia. Kumbuka biashara na mikopo baina ya mataifa mengine ya Marekani ilitolewa kwa dhahabu. Vita inakaribia kuisha, kila dhahabu ya duniani hapa ilikuwepo Marekani. Mwaka 1944, wakafanya kikao na kuamua kwamba kwasababu Marekani ndiyo taifa lenye dhahabu yote duniani, basi dola ndiyo iwe, The International Reserve Currency. Mataifa yakasaini, The Bretton Woods Agreement.

Tatu, dola ya Marekani mbali na kuwa chombo cha manunuzi, ikawa ni moja ya bidhaa muhimu kwenye soko la dunia ambayo inauzwa na taifa la Marekani peke yake. Hivyo ili mataifa mengine yaweze kufanya biashara za kimataifa, yalitakiwa yaende Marekani kununua dola ndiyo yafanye biashara. Utaratibu ukawa ni kwamba, taifa inabidi liuze bidhaa zake zisizopungua thamani ya dola 100 ili kupata dola kadhaa za kimarekani. Ikumbukwe Marekani, anachapisha hizi fedha kwa gharama (Seigniorage) ya dola 0.5.

Nne, mbali na hili, mataifa yakawa yanazipata hizi dola kupitia taasisi za kifedha za Marekani kwa njia ya mikopo au uwekezaji kwenye masoko ya hisa na hati-fungani za kimarekani. Hivyo soko la mitaji na dhamana la Marekani likageuka kuwa kubwa mno kupita kiasi. Utaratibu ukawa hivi: Taifa kama Uingereza, linaenda kununua dola za Marekani ili kufanya biashara ya kimataifa, ila baada ya kupata faida inazichukua hizo fedha tena na kwenye kuziwekeza nchini Marekani kwenye soko la mitaji ili Marekani azizungushe na kuwapa faida.

Hivyo fedha zinatoka Marekani na kurudi Marekani na kurudi Marekani. Marekani anachofanya ni kuwapa Makaratasi yaliyochapishwa tu. Hata kama hajapata faida, anachapisha fedha anawapa maana mnazihitaji kufanyia biashara ya kimataifa.

Tano, mchezo huu ulienda hadi kufika mwaka 1969. Mataifa ya Ulaya kama Ufaransa yakaanza kulalamika kwamba dunia nzima tunaupa ruzuku uchumi wa Marekani (The Entire World is subsidizing American Economy), jambo ambalo ni kweli. Bahati mbaya sana ikafahamika kwamba dhahabu ambayo ilikuwa imeunganishwa na fedha ya Marekani imeisha. Ufaransa chini ya Charles De Gaulle wakaanza kwenye kubebe dhahabu yao Marekani.

Hali ya Marekani ikageuka kuwa mbaya kufika mwaka 1970, na ikategemewa kwamba dola ndiyo ilikuwa inaenda kuanguka. Raisi Richard Nixon akaihakikishia dunia kwamba angefanya marekabisho kwenye mfumo mzima wa fedha wa dunia, endapo mataifa yatakubali kuendelea kutumia fedha ya Marekani, ndipo wakasaini makubaliano ya Bretton Woods II. Wewe kama mchumi, ulitakiwa uwe unayafahamu vizuri haya.

Sita, mfumo wa Bretton Woods II, ulimtaka Marekani na yeye akubali kuingiza bidhaa kutoka nchi nyingine na kwenda kuwekeza viwanda vyake nchi za nje ambako kuna gharama rahisi na mataifa mengine yakawekeza pamoja na Marekani. Haya makubaliano yaliiokoa dola ambayo ilikuwa inaenda kuanguka. Hivyo ukitaka kuelewa vizuri uchumi wa dunia unaendaje, ni lazima ufahamu kilichotokea mwaka 1965-1975.

Saba, Marekani baada ya kuona amebanwa, hana dhahabu na amekaliwa kooni na mataifa mengine akaamua kuacha kabisa mfumo wa matumizi ya dhahabu, The Gold-Standard. Akatumia mbinu ya kiakili kwamba aende kufanya makubaliano na mataifa ya kiarabu kwamba yatumie fedha ya kimarekani kwenye biashara zao zote za mafuta. Hivyo akatengeneza mfumo mpya uitwao, The Petro-Dollar System. Ambapo nishati ilikuwa ndiyo bidhaa muhimu, lakini ni lazima inunuliwe kwa fedha za kimarekani.

Mataifa ya kiarabu yakawa matajiri ndani ya muda mfupi na Marekani akawa hayagusi kabisa. Hivi unadhani wakina Mfalme Faisal wa Saudi Arabia, walivyomuwekea Marekani vikwazo vya mafuta mwaka 1973, waliitoa ile jehuri wapi, ??? Marekani alikuwa anawategemea waarabu, na wao wanamtegemea Marekani. Anahitaji mafuta ya mwarabu, lakini anahitaji zaidi dola iendelee kutumika na mataifa ya duniani.

Nane, Marekani alivyoachana na matumizi ya dhahabu, akaanza kutumia fedha makaratasi ambazo zimepewa thamani na benki kuu (Fiat Currency). Hapa ndipo akapata nguvu zaidi. Akiwa anahitaji kufadhili bajeti yake au kupata fedha ya kupambana vita baridi, alikuwa anachapisha fedha nyingi tu. Utofauti na mataifa mengine ni kwamba Marekani anachapa fedha bila kuwa na woga wa mfumuko wa bei kwasasabu fedha yake itanunuliwa tu na mataifa mengine, ambayo yatakuja tena kuwekeza Marekani. Hili ndilo lipo mpaka leo hii.

Tisa, ili kuongeza fedha kwenye soko la mitaji na fedha, benki kuu (The Federal Reserve) ikaamua kupunguza kabisa riba hadi kufika 0.6%. Ambapo mikopo kutoka kwenye mabenki ikawa ni ya bei rahisi mno hadi kwa watu wa chini kabisa. Watu wakawa wanakopa sana halafu wanawekeza fedha hizo kwenye masoko ya hisa na hati-fungani. Wamarekani wengi wakageuka kuwa matajiri, ili utajiri wako ndiyo huo ambao msingi wake ni fedha za makaratasi.

Ndiyo maana masoko ya dhamana ya Marekani yakitikisika kidogo tu, lazima uone mabenki yanafungwa na watu maelfu ya watu kuumizwa. Sasa, nikakuuliza makusudi kabisa, kwamba unadhani Marekani alivyopandisha riba (Hiking Interest Rates) kutoka 0.6% hadi kufika 6% ndani ya mwaka 2022, ni jambo la kawaida, ???

Wewe ukanijibu ni jambo la kawaida maana uchumi ndivyo ulivyo. Nikashangaa mno, imekuwaje wewe ambaye huwa una akili umembwela kama washabiki wengine wa humu ndani wasiokuwa na ufahamu wa mambo!!! Mpaka sasa sijapata majawabu.

Kumi, Mradi wa NORD-STREAM II, baina ya Urusi na Ujerumani ulikuwa ni wa matrilioni ya fedha na ulitegemewa ufanywe kupitia fedha za Ulaya na Urusi. Marekani alitaka ufanywe kupitia dola na mwishowe alivyoona mwanya akaamua kulipua kabisa mabomba ili mradi ufe kibudu. Mengi yamejificha na wengi badi hatujang'amua tu. Hii vita inalenga zaidi kumuumiza Marekani, Ukraine ni geresha tu.

NB 1: Lengo la mataifa kama Urusi, Saudi-Arabia, Uchina hata Ufaransa, yanafahamu kabisa kupambana na Marekani kijeshi ni kujitakia matatizo (Is courting death), maana Marekani ndiyo taifa lenye jeshi kubwa na linaloogopesha zaidi hapa duniani (They're armed to the teeth). Mbinu rahisi kabisa ya kumkomesha ni kucheza na mfumo wa fedha wa dunia ambako ndiko kuna udhaifu mkubwa, ili watu wapoteze imani ya kuwekeza kwenye masoko ya fedha ya Marekani.

Kama leo Marekani amenyang'anya fedha za Urusi (Foreign Reserves) ambazo aliziwekeza kule Marekani, unadhani mataifa kama Uchina ambalo limewekeza sana kwenye dola za Marekani kwa kununua deni la Marekani (Treasury Bills) ataziacha fedha zake nchini huko bila kuogopa kwamba siku yeye akivamia Taiwan atakutwa na yanayomkuta Urusi, ??? Hebu fikiri.

Mwisho kabisa, Marekani ana deni la taifa la Trillion 31 ambalo kiuhalisia limeshavuka uwezo pato lake la taifa. IMF wanasema nchi inakuwa na deni stahimilivu pale ambapo halivuki asilimia 70% ya GDP ya taifa hilo. Bahati mbaya deni la Marekani limevuka. Ila kwanini, Marekani hajapata, Default kama mataifa mengine, ???

Sababu ya kwanza ni kwamba, deni la Marekani lipo katika dola za kimarekani.
Sababu ya pili ni kwamba, kama Marekani anachapisha tu dola zake ili kufanya marejesho.

Upande mwingine, taifa la Marekani mbali ya kuwa na deni kubwa la trilioni 31, ina uhaba wa bajeti wa dola za Kimarekani Trilioni 1.15. Ila Marekani anaendelea kudunda tu kwasababu, anaweza kuchapisha fedha ili kukidhi mahitaji ya bejeti. Fedha za makaratasi zikizidi, hata nyinyi watanzania mtaenda kuzinunua tu ili muweze kufanya biashara za kimataifa.
===============================================================
BAADA YA KUELEZANA HAYO, BASI ZINGATIA HAYA YAFUATAYO:

Kipindi cha UVIKO, serikali ya Marekani ilichapisha dola za kimarekani Trilioni 1.9, ambazo hata mimi binafsi nilizipata. Hizi ni fedha nyingi mno ambazo ni makaratasi (Money Made Out of Thin Air) yaliyopewa thamani. Bahati mbaya sasa, kabla ya hizi fedha hazijaingia vizuri kwenye mzunguko, ili mataifa mengi wanunue vita vya Ukraine ikaanza.

Tangu vita ianze, Dola imepungua mzunguko kutoka 75% dunia nzima hadi kufika 59% ndani ya mwaka 2022 peke yake. Hili ni hatari mno kwa Marekani. Jambo kama hili mara ya mwisho lilitokea mwaka 2000 baada ya Tech-Bubble na September 11. Ndiyo, dola haiwezi kuanguka kirahisi maana hakuna fedha mbadala kwa sasa inayoaminika (No Alternative Reserve Currency of Similar Confidence). Asilimia 46% ya soko la dhamana na mitaji dunia nzima liko katika fedha ya Marekani na wadua wake wawekezaji wakubwa ni Japan, Uchina, UAE, Saudi-Arabia nk

Nimefurahi sana kuona bwana Econometrician ameelewa kinachoendelea. Uvamizi wa Ukraine ni geresha tu. Hatari yenye iko kwenye uchumi, maana wakubwa wameamua kuvimbishiana misuli na kukomoana. OPEC wanamvimbia Marekani kwasababu wanafahamu kwamba wao ndiyo wameshikilia karata ya mwisho ya uhai wa dola ya Kimarekani. Marekani analifahamu hili na hawezi kufanya lolote. Siku Saudi Arabia wakiacha kutumia dola kwenye biashara ya mafuta, ndiyo basi tena, The Collapse of Bretton-Woods II.

NB 2: Kama dola ya Marekani itaendelea kupungua mzunguko, basi hata nguvu yake kiuchumi na faida anazozipata kutokana na kuchapisha fedha makaratasi zitapungua. Pia haya yafuatayao yanaweza kutokea:

1. Marekani itashindwa kulipa deni lake kupitia kuchapisha fedha (Defaulting)
2. Marekani itashindwa kupata fedha za bajeti, (America has a huge budget deficit)
3. Marekani itaagiza bidhaa za nje kwa gharama mno kwasababu hatatumia fedha zake tena.
4. Marekani itakumbwa na tatizo kubwa la mfumuko wa bei usioisha (Hyper-Inflation)
5. Masoko ya hisa ya Marekani yataanguka vibaya mno na dunia nzima tutaumizwa.

Ndugu Zitto JR, kama hadi hapa hujaelewa chochote, basi sidhani kama ntakushauri chochote kile ukanielewa. Niliuliza swali kuhusu AUSTRALIA, ambalo linaendana na hali ilivyo nchini Marekani, ila ukakwepa kunijibu. Ungeyafahamu ya AUSTRALIA, basi ungefahamu ni wapi Marekani kama taifa anajikwaa hadi kufika hapa alipo, japo yeye ni taifa kubwa sana.
 
Nimetaja vipimo vitatu. Kama hutaki taja vya kwako unavyotumia mwenyewe vinavyosema Urusi ana uchumi mkubwa. Na ututajie ni ya ngapi kiuchumi duniani
Siku zote uchumi unaotokana na mikopo ni uchumi hewa si himilivu hasa ukipata tatizo la kijamii au kiuchumi. Kwa mfano ukienda benki kukopa ni kweli UNAKUWA na fedha mfukoni lakini siku mwenye fedha akizihitaji na ukawa unazo pungufu ya alizozikukopesha au ukawa umeshindwa kulipa mkopo Kwa kadri ya makubaliano atatanga mali ulizo nazo ili ziuzwe kufidia fedha zake. Kama ulikuwa na nyumba au shamba litauzwa na utabaki masikini kuliko kabla hujakopa. Gdp ya mkopo si ya kuringia. Russia ameshinda hii vita ya kiuchumi Kwa sababu alikuwa na vitu muhimu ambavyo kama nchi mukivikosa vinaleta taharuki kubwa nchini kimaisha na kiuchumi.

1.CHAKULA
Urusi ni mzalishaji mkubwa wa chakula na anategemewa na dunia nzima , Kwa hiyo wananchi wake hawakuona kupanda kwa bei ya chakula ila kupungua Kwa bei baada ya soko la nje kusuasua.

2.Mafuta
Baada ya baadhi ya nchi kususa kununua mafuta yake aliyateremsha
bei Kwa soko la ndani na nchi marafiki Kwa hiyo wananchi kupata nafuu ya maisha, pia kupata masoko mapya Kwa nchi marafiki.

3.
Gesi
Baada ya ulaya kususa kununua gesi yake na hujuma kufanyika kwenye mfumo wa kupereka gesi ulaya ,alihimalisha soko la ndani Kwa kuweka unafuu wa bei.
Hivyo ndivyo vitu muhimu vinavyogusa wengi hivyo kufanya wananchi wa kawaida kutokuona mfumuko wa bei unaoathiri maisha yao.

4.
ZANA ZA KIJESHI.
Vita inakomba Hera nyingi hasa za nje kama unategemea kila ZANA uiagize nje ya nchi kama ilivyokuwa kwetu wakati wa vita ya Kagera. Mtihani huu Urusi kaushinda Kwa kuwa na akiba kubwa ya siraha na uzalishaji unafanyika ndani ya nchi, Kwa hiyo alichofanya ni kuongeza tu uzalishaji wa siraha.

Mambo hayo hapo juu ndiyo yalifanya uchumi wa Russia usitetereke huku waliomwekea vikwazo na wenye uchumi wa madeni wakipata mdororo wa uchumi. Unajidai kula kuku Kwa fedha ya mkopo ha ha ha ....!
 
Uchumi hautenganishwi na siasa. Sera za uchumi zinatolewa na wanasiasa na uchumi unaongozwa kwa mlengo wao. Mambo ya kiuchumi kama industrialization, trade, treaties, kujenga Panama na Suez, uwepo wa Fed, gold standard na kila kitu cha kiuchumi kinaanzia kwenye siasa. Wanasiasa wana uwezo wa kuharibu au kukuza uchumi, siasa haiachi kitu kwenye nchi. Ndio maana wanapiga kura kwa wanasiasa, hawapigi kwa wakuu wa majeshi ili waongoze jeshi wanavyotaka, hawapigi kwa Chairman wa Central bank au Governor wake.

Baada ya kusababisha mfumuko wa bei kwa Magharibi, Russia imekuwa ya ngapi kiuchumi ambayo haina mfumuko?
Baada ya Waarabu kuiwekea Marekani oil embargo mwaka 1973 kama adhabu ya kuisadia Israel kwenye Yom Kippur war, Marekani ikafeli uchumi sio?
Finland mwaka jana imefungiwa gesi kabisa kabisa na Urusi, umeona wamepungukiwa nini cha ajabu?
Urusi yenyewe imepandisha interest rate mwaka jana. Na kwani hizo rasilimali za OPEC ni za Urusi? Yaani Iran, Qatar, Saudi Arabia au Kuwait waache kuuza mafuta kukuza uchumi wao wamsikilize mtu kaamua kuanzisha ugomvi?bUnategemea watu wana oil-dependet economy wazime visima ili kuikomesha Western ambao ndio wateja wao, wamsikilize Russia ambaye ni mshindani? Sababu za OPEC kusitisha kuuza rasilimali kwa West ni zipi, yani Russia wenyewe hawajasitisha sembuse OPEC.

Sababu walijiweka kwenye utegemezi wa gesi ya Urusi. Na Urusi ambavyo haina siasa za akili (jambo unalopinga kwamba tusizungumzie siasa) wameamua kuihakikishia Ulaya kwamba wao sio dependable kwenye nishati, muda wowote wanazira na kutishia kuzima mara kupunguza flow. Alternatives hata kama ni expensive zinatafutwa, subiri miaka kadhaa uone watishia gesi wataiweka wapi. Russia wanatumia gesi kama silaha, Western wanatumia uchumi kama silaha.
Je, Russia haijapata recession?

Kwani huo mwaka 2008 mabenki yalikuwa insolvent sababu ya nini au nayo ni Urusi. Urusi kwa maamuzi ya kiuchumi na kisiasa ina uwezo mdogo kuharibu uchumi wa dunia. Marekani kwa sera mbovu za siasa inaweza poromosha uchumi wa dunia, China nayo inaweza fanya jambo ikaharibu. Urusi atatumia nguvu nyingi kuharibu uchumi duniani, labda aamue naye kujiua kiuchumi.
Je data za mabenki ya Urusi zinasemaje, mabenki yao yanakua au yako insolvent.

Mbadala ila wa gharama kubwa upo, unahitaji miaka kadhaa ya kujiandaa. Hata hivyo Urusi haitoi gesi bure, kama haitaki hiyo hela basi ifunge mabomba tuione itaishije. More than 15% ya mapato yao yanategemea gesi na mafuta, wafunge kwa wengine wote waiachie China na India pekee. Wakati huo China ina mikataba na nchi kama Saudi Arabia, haiwezi chukua kiasi kikubwa zaidi kwa Russia wala haiwezi chukua kila flow kutoka kwao.
Alafu Warusi milioni 144 ambao hawana hata purchasing power ni negligible kwenye uchumi wa dunia. Urusi mwaka jana hata magari waliyonunua hayafiki nusu ya waliyonunua Brazil.

Tufanye sababu ni Russia. Sasa imekuwa ya ngapi kiuchumi baada ya kuifanya Fed ipandishe interest hadi asilimia 6?
Ni kipi Russia imepata mpaka useme imefanikiwa kiuchumi, au ni kipi Marekani imekosa.

Lini Gazprom au Rosneft imeacha kuuzia Ulaya gesi?
Ukiachana na Nord Stream 2 ambayo pipeline imelipuliwa na sidhani kama ilikuwa imekamilika, gesi inaendelea kuuzwa. Kwanini wasipate hela sasa kama bei ya soko ni nzuri.
Au ni vikwazo gani vilisema ni marufuku Russia kuuza nishati, sanasana waliweka threshold kwenye mafuta watakaonunua. Na ni nchi chache zilifanya hivyo.

Hiyo ni India. Wapi imeandikwa kwamba Urusi ikiwekewa vikwazo India ishuke kiuchumi? Yani Yanga ichukue kombe, uulize kwanini TP Mazembe haifanyi usajili.
Kama unataka ziende sawa, kwanini Russia ilivyovamia Ukraine na India haikuivamia Pakistan au China.

Alafu soko la hisa la Urusi likawa la ngapi kwa thamani ya makusanyo ya mitaji baada ya masoko ya Ulaya kuanguka?
Urusi soko lake la hisa hata masoko makubwa duniani halipo.
Na je ni mara ya kwanza masoko ya hisa Ulaya kuanguka, je mara zote yanaangushwa na Urusi?

Ni maamuzi ya kiuchumi ya nchi hizo. Au hizo phenomena zimeanza leo baada ya Urusi kuwekewa vikwazo?

Sababu kuna sarafu nyingine nyingi zenye kuwa mbadala wake kama GBP, CAD, Swiss Franc, RMB, Euro, Yen na nyinginezo. Lakini katika hizo usitarajie kuiona RUB maana haina maana kwenye exchange duniani.

Na huoni aibu kabisa unataja USD inatumika 55% duniani. Si unajua inayofuata kwa kutumika zaidi inatumika kwa asilimia ngapi?
Wakati huo Russia hizo sio level zake, imekalia kuchimba ardhi na kuuza maliasili.

Narudi palepale. Russia hakuna anayetaka kuiua kiuchumi, hivyo haijawa survival wa kitu ambacho hakipo. Kila siku ukiwa unajihisi unafuatwa na majambazi alafu unafika salama nyumbani utaamini wewe ni bingwa wa kujilinda kumbe wasiwasi wako.
Marekani iache kuua nchi ya pili mpaka ya 10 kwa GDP, iende kuua ya 11 ambayo inabadilishana na South Korea kwenye hiyo nafasi.
Yani wewe jamaa unaulizwa vizuri tu lakini unajibu kama mwanamke mjamzito.
 
Kufupi ni kwamba vikwazo vyote walivyomuwekea Urusi vimefeli vibaya mno . Na hii ni kwa sababu Putin alikuwa ameshajipanga kabla ya kuivamia Ukraine, kitu ambacho mataifa ya Magharibi yalikuwa hayakijui
Tokea mwaka 1944, baada ya kutengeneza mfumo wa Bretton-Woods hakuna taifa ambalo limewahi kuwa na uchumi mkubwa kama Marekani. Kufika mwaka 1945, Marekani ilikuwa inamiliki nusu nzima ya uchumi wa dunia. Fedha ya Marekani ikishikiliwa na dhahabu (Gold-Backed) ilikuwa ndiyo inatumiwa kwa kiwango kikubwa kwenye biashara zote za kimataifa.

Mwaka 1957, baada ya Raisi Gamal Abdel Nasser wa Misri kutaifisha mfereji wa Suez, Uingereza, Ufaransa na Israel waliunda mkakati wa kuvamia Misri ili kumtoa Nasser. Mkakati huu ulikufa kibudu baada ya Raisi wa Marekani General Dwight Eisenhower kuwachimba mkwara mzito Waingereza kwamba wangeacha kununua hati-fungani (Sovereign Bonds) za Uingereza na nyingine wangeziuza, jambo ambalo lingeangusha uchumi wa Uingereza.

Kiufupi, baada ya hili kutokea Raisi wa Ufaransa General Charles De Gaulle alilalamika na kusema kwamba "The dollar gives America an exorbitant privilege in international financial system". Akimaanisha kwamba dola inampa Marekani nguvu iliyomithirika kwenye uchumi wa dunia dhidi ya mataifa mengine. Kiufupi Marekani akikutoa kwenye mfumo wake wa kifedha, lazima uumie.

Wataalamu wanatumia vipimo (Metrics) kama GDP na PPP kupima uchumi wa dunia. Ukitumia kipimo cha GDP, nadhani Marekani ndiyo taifa lenye uchumi mkubwa zaidi duniani likifuatiwa na Uchina. Uchumi wa Marekani peke yake ni asilimia 24% ya uchumi wa dunia (Global GDP). Kiufupi ni kwamba, all financial roads lead to America.

Marekani hayuko peke yake, anashirikiana na wenzake wa kule Ulaya (European Union) na wenzake wa chama cha mabwanyenye wa dunia almaarufu kama G7. Ukichanganya uchumi wa Marekani, Ufaransa, Uingereza, Ujerumani, Italia, Canada na Japan, ambao ndiyo nchi tajiri zaidi duniani unapata asilimia 30.7% ya uchumi wa dunia (Global GDP).

Kiuhalisia, haya mataifa saba ndiyo yanayoendesha uchumi wa dunia kupitia mifumo waliyoitengeneza baada ya mwaka 1945. Viwanda vikubwa duniani ni vyao, masoko makubwa ya hisa ni yao, mabenki makubwa duniani ni yao, wao ndiyo wanaongoza katika kuzikopesha fedha nchi nyingine na wao ndiyo wanaongoza kwa kuuza huduma zaidi hapa duniani.

Maswali yangu ya kiuchumi ni haya yafuatayo:
Mosi, kwanini Urusi ambayo ni asilimia 4% tu ya uchumi wa dunia (Share in Global GDP) bado haijaanguka baada ya mataifa makubwa yanayomilikia asilimia 30.7% ya uchumiwa dunia kuwawekea vikwazo vikali ?

Pili, kwanini makampuni ya Urusi ya nishati ndiyo yameongoza duniani kwa kuuza zaidi nishati, ilhali yamewekewa vikwazi baada vikali ? Takwimu zilizotolewa na Marekani yenyewe zinasema kiujumla mashirika ya nishati ya Urusi yameuza zaidi na kupata faida kipindi hiki cha vita na vikwazo kuliko kipindi kingine chochote. Tatizo liko wapi hapa ?

Tatu, Je, tutegemee kwamba kuna siku hivi vikwazo vitafanya kazi na vitauangusha uchumi wa Urusi kama ambavyo Raisi Biden alisema mwaka 2022 kabla ya uvamizi kuanza ? Alisema kwamba uchumi wa Urusi ungeanguka ndani ya wiki chache tu, sasa ni mwaka na zaidi. Mataifa ya Magharibi yamefanikiwa au tuendelee kusubiri ?
 
Nitajibu swali lako kama ifuatavyo:

Uchumi wa Russia haujateteleka kwa sababu zifuatazo

1. Russia ni Superpower Halisi: unavyodeal na nchi kubwa kama Russia inakupasa uwe na Plan B au C. West walishindwa kutambua Stage alokuwa amefikia Russia ilikua ni stage kubwa sana. Sababu Russia alizifanya nchi za ulaya kuwa dependent kwake kwenye suala la Nishati na ili kuwakamata zaidi alijenga pipes “strems” za kusuply gas na mafuta kwa cheap price.

2. Nature of economic system: Russia ni socialist state hivo major means of production ziko under the government. Zile sector zinazobeba uchumi wa nchi bhasi kuna mkono wa Serikali. Ndomana unaona hizi Gazprom na Rosatam bado ziliendelea kufanya vizuri licha ya vikwazo.

3. Strong leadership

4. Russia ni moja ya nchi ambazo zinajitegemea kiuchumi hawa jamaa karibu 90% wanajitegemea ni asilimia ndogo sana ambazo wana import.

5. Russia wana intelejensia hatari sana ambayo inafanya kazi kwa ufanisi mkubwa (FSB).

6. Russia is Rich in natural resource ($75 trillion approximately)
Umenirudisha darasani kwa Historia na Uchumi , shukrani mkuu 👏🏾👏🏾👏🏾
 
Kufupi ni kwamba vikwazo vyote walivyomuwekea Urusi vimefeli vibaya mno . Na hii ni kwa sababu Putin alikuwa ameshajipanga kabla ya kuivamia Ukraine, kitu ambacho mataifa ya Magharibi yalikuwa hayakijui
Nimezungumza na baadhi ya wachumi humu ndani. Nikawauliza hivi ni sahihi kusema kwamba taifa ni dhaifu kiuchumi kwa kuzingatia tu, uchumi wa kifedha, Finance Economy. Bila kuzingatia uwezo wa nchi kwenye uchumi wa bidhaa, Commodity Economy, ???

Maana uchumi wa Urusi ni mdogo mno kuliko hata ule wa Italia, ila sasa madhara ya kumtenga Urusi kiuchumi na kidiplomasia yamekuwa makubwa mno na kuumiza pande zote. Hata Marekani, EU na G7 walisema kwamba wangeweka vikwazo ambavyo vingeangusha uchumi wa Urusi ndani ya wiki chache. Je, walikosea kuangalia ukubwa na nguvu zao kwenye jicho la, Finance Economy, peke yake, ???

 
Back
Top Bottom