Nashukuru kwa kunialika kwenye mjadala huu,
Proved, japokuwa nimechelewa kujiunga. Majukumu mengine [yaliyo nje ya platform hii] yanachangia kutopatikana humu mara kwa mara.
Awali kabla ya yote, kuna suala moja la msingi sana ambalo kwa maoni yangu haliko sawa kuhusiana na mjadala wenyewe uliopo mezani.
Hoja au mada ina kichwa cha habari kinachosema: "Swali la uchumi: Kwanini vikwazo vya mataifa yenye nguvu kubwa kiuchumi havifanyi kazi dhidi ya Urusi?"
Hiyo title pekeyake ina-demand ama inahitaji set of valid statements zinazozipa justification hoja kuu iliyomo katika title husika kwa sababu title imebeba hoja nyingine kubwa tu ambayo ni conclusion ya mjadala mwingine huru. Hoja ambayo inapaswa kusapotiwa na premises ama hoja zingine ndogondogo ili kuithibitisha. Nimeipitia mada nzima kuanzia title, introduction na context ya mjadala kwa ujumla wake. Kwa bahati mbaya, sijaziona hizo premises ambazo zinaakisi hoja iliyopo katika title ya mada ama mjadala mzima.
Ninachozungumzia ni
uthabiti ama
validity ya mjadala. Nitafafanua!
Hoja yoyote inayouliza "Kwanini" ama "Why" kwa kiingereza ni hoja ambayo inatumia conclusion ya hoja nyingine ambayo tayari imethibitika kuwa ni kweli (True), ili kuzibaini sababu ama reasons za kuwepo kwa huo ukweli (Truth). Ukiuliza "Kwanini kitu fulani hakifanyi kazi dhidi ya fulani?" maana yake ni kuwa hoja ama swali hilo limetumia conclusion "kutofanya kazi" kutoka katika hoja nyingine/zingine huru kujengea hoja ya "Kwanini" iliyopo mezani ambayo ndiyo mleta mada ameiwasilisha.
Ili statement "havifanyi kazi" iliyomo katika title ya mada iwe sahihi ama valid, inahitaji kusapotiwa na mtiririko wa premises, reasons, evidence, facts ama data zilizotokana na tafiti mbalimbali ili kufikia conclusion niliyoisema ya "kutofanya kazi" kisha ndipo tuingie sasa katika hoja mpya ya "Kwanini havifanyi kazi" iliyopo mezani, kitu ambacho sijakiona katika context ya mada/mjadala.
Mfano mwingine rahisi:
Kuna utofauti mkubwa kati ya general question kama "Umeenda shule leo?" na swali kama "Kwanini umeenda shule leo?".
Swali la pili hapo lenye "Kwanini" ni sahihi ama valid endapo tu conclusion "kwenda shule" inaweza kuthibitika kuwa ni kweli kwa ushahidi wa akiwemo anayeulizwa na muuliza swali mwenyewe. Kama kuna possibility yoyote ile kuwa huyo anayeulizwa hilo swali hajaenda shule siku hiyo, basi swali zima linakosa mantiki, hivyo swali sahihi linalopaswa kuulizwa kwanza pengine ni lile la kwanza.
Mfano mwingine ni kutoka katika mada yenyewe:
Swali la pili limeuliza kitu kama hiki; "Kwanini makampuni ya Urusi ya nishati ndiyo yameongoza duniani kwa kuuza zaidi nishati, ilhali yamewekewa vikwazo vikali?". Hapo kuna conclusion "kuongoza duniani" inayotokana na hoja ambayo haijaambatanishwa na facts wala data zozote zile zenye kuthibitisha statement hiyo. Swali dogo tu: takwimu sahihi za mauzo ya nishati ziko wapi?
Kwa kifupi ni kwamba, title ya mada imebeba hoja nyingine huru ambayo haina uthibitisho ukizingatia maudhui ya mada ama mjadala mzima. Vilevile, maudhui ya mjadala hayajakidhi mahitaji yenye kuyapa usahihi maswali yote yaliyowasilishwa mwishoni. Mada imejikita zaidi kuelezea superiority ya western countries kiuchumi bila ya kutupa facts zenye kusapoti title iliyowasilishwa pamoja na maswali matatu ya mwishoni ambayo ndiyo mjadala uliopo mezani.
Baada ya kusema hayo, nitaendelea kupitia michango ya wadau wengine kisha nitachangia zaidi pale ambapo nitapata muda wa kufanya hivyo. Haya ndiyo maoni yangu kwa sasa. Asante!