Swali la Ugomvi: Tuseme tu Hawana Uwezo?

Swali la Ugomvi: Tuseme tu Hawana Uwezo?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Na. M. M. Mwanakijiji

View: https://youtu.be/R6TiVOZZZj4?si=iM4J0sv3gbtjSNmI
Waliitwa vijana...nakumbuka walipotumbuliwa nilisema ni ujana tu unawasumbua. Nikasema warudishwe labda wamejifunza. Tukaseme wapewe nafasi tena Alipokufa JPM hawakuficha hisia zao kuonesha hasimu kaondoka na wala kupima hekima walipozungumza. Tukawaangalia.

Mama alipowarudisha ni ikawa kama ni kuwaponya. Walionewa na sasa wamerudishwa ndani. Wote walipewa wizara walizozitaka sana na ambazo zilionekana zinaendana na uwezo wao. Lakini mara hizi zote wanapata shida kuongoza. Je, hawana uwezo?

Napendekeza wasipewe nafasi yoyote ya kuteuliwa tena sasa hivi. Wabaki wabunge tu ili wajipange na waoneshe wanaweza kuongoza bila kuwa mawaziri. Wabakie wabunge wa kawaida. Inawezekana upande mwingine Raisi Samia ameona siyo suala la uwezo bali kuwaondolea majaribu ya kutumia uwaziri kujijenga majimboni kuelekea 2025. Binafsi naamini kama hili ni kweli basi mawaziri wote wenye Nia ya kugombea mwakani wangetolewa ili wabakie wabunge. Mawaziri wawe wale ambao hawana Nia ya kugombea tena mwakani. Ila nadhani ni uwezo na kukosa hekima.

Maana kama kubebwa kuna watu wamebebwa bwana lakini kama mtu habebeki unang"ang'ania kumuweka mgongoni wa nini..mara akugonge konzi, mara teke, mara akufinye masikio, mara akung'ate halafu bado anataka kupanda mabegani. Kubebwa gani huko? Hata mtoto asipotulia kwenye mbeleko unamshusha bana kha!

Inawezekana kweli wa moja available mbili na aliyezoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi. Tukubali kuwa hawana uwezo maana kama hadi sasa bado hawajui hekima ya uongozi watajua lini? Watu wasiopima yanayotoka midomoni au matendo yao watapimiwa na nani...?

Wakubali yaishe?
 
Na. M. M. MwanakijijI

Inawezekana kweli wa moja available mbili na aliyezoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi. Tukubali kuwa hawana uwezo maana kama hadi sasa bado hawajui hekima ya uongozi watajua lini? Watu wasiopima yanayotoka midomoni au matendo yao watapimiwa na nani...?

Wakubali yaishe?
Karibu Mzee Mwenzangu, Mkuu Mzee Mwanakijiji , maana wewe ni miongoni mwa my inspiration kujiunga jf, hivyo kila nikikuona nafarijika sana, na unapokengeuka, naumia sana!.

Inawezekana ni kweli hawana uwezo, ila pia mambo kama haya ya hire and fire kila uchao, pia yanatuonyesha uwezo wa mamlaka ya uteuzi, tukisema hizi ni early signs of incompetence tutakuwa tunamuonea?, na baada ya kuzibaini hizi early signs, bado tuu 2025 tuenende...?.

Hili la kila siku kuteua na baada ya siku mbili tatu kutengua au kutumbua, kwanza nilisema ni kosa, ila nikaitetea mamlaka ya uteuzi Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda

Kisha nikauliza humu Could there be a problem with our vetting systems? These hirings and firings hazitaonekana kama signs za incompetence on part of appointing authority?

Mimi nimeshauri wakati wa kuteua, sii lazima mamlaka ya uteuzi kutoa sababu, lakini kwenye kutengua na kutumbua, iwe ni lazima kutoa sababu ili hayo makosa yaliyopelekea kutumbuliwa kwao, yatumike kama shamba darasa kwa wengine hivyo kwanza nilishauri Should We Demand More Right to Information Kwenye Teuzi za Key Posts? Ziwe Endorsed na Bunge With Security of Tenure? Mawaziri Wasiwe Wabunge?

Kisha nikapongeza Pongezi Rais Samia kwa Kutuhisania Openness and Transparency Kwenye Uteuzi, Mnaonaje Ifanyike Kwenye Utenguzi na UtumbuzI Iwe ni Haki na Sio Hisani?

P
 
Ni nadra sana kwa mtu aliyetembelea mbeleko ya baba yake maisha yake yote kuwa na uwezo.

Wapo wachache wenye uwezo lakini wengi wao ikiwa ni pamoja na hao watumbuliwa hawana uwezo!

Moja ya mambo yaliyomfanya JPM kuwa waziri mzuri ni kutokuwa na tamaa, akili yake yote ilikuwa kwenye kuifanya kazi yake hiyo kwa moyo wote na akili zote.

Sasa hawa vijana wa mbeleko wanatumia asilimia kubwa ya muda wa kazi kupanga mipango ya kufanikisha matamanio yao ya mbele na kusuka mitandao yao.

Ni vema amewatoa, waende wakafanye hayo kwa uhuru wao, hiyo kazi ya uwaziri ifanywe na wanaotaka kufanya kazi.
 
Teua tengua, teua tengua, teua, tengua, teua, tengua,teua, tengua,teua, tengua,teua, tengua, teua, tengua, teua, tengua, teua tengua, teua tengua, teua tengua, teua tengua, teua tengua, teua tengua, teua tengua, teua tengua, teua tengua, teua tengua, teua tengua, teua tengua, teua tengua, teua tengua,

Mitano inatosha🙏
 
Karibu Mzee Mwenzangu, Mkuu Mzee Mwanakijiji , maana wewe ni miongoni mwa my inspiration kujiunga jf, hivyo kila nikikuona nafarijika sana, na unapokengeuka, naumia sana!.

Inawezekana ni kweli hawana uwezo, ila pia mambo kama haya ya hire and fire kila uchao, pia yanatuonyesha uwezo wa mamlaka ya uteuzi, tukisema hizi ni early signs of incompetence tutakuwa tunamuonea?, na baada ya kuzibaini hizi early signs, bado tuu 2025 tuenende...?, niliwahi kuliulizia hili humu Could there be a problem with our vetting systems? These hirings and firings hazitaonekana kama signs za incompetence on part of appointing authority?

P
Nafikiria mama anapenda sana " second chances "..ila aliwahi kusema ukimzingua....
 
I was just reading between the lines.
Majibu yapo mule mule.
👇🏿
Wabaki wabunge tu ili wajipange na waoneshe wanaweza kuongoza bila kuwa mawaziri.

Raisi Samia ameona siyo suala la uwezo bali kuwaondolea majaribu ya kutumia uwaziri kujijenga majimboni kuelekea 2025.
Plausible deniability.

Hawakumo Serikalini-Bao la 2025
 
Nafikiri Mama alikuja na huruma na kuwarudisha akifikiri wale kutenguliwa zilikua Chuki tu za Baba lakini kwa sasa ameanza kujionea uwezo na umakini wa Baba...

Nachosikitika amechelewa sana kulitambua hili....
 
Tukubali kuwa hawana uwezo maana kama hadi sasa bado hawajui hekima ya uongozi watajua lini? Watu wasiopima yanayotoka midomoni au matendo yao watapimiwa na nani...?
Kwa ufupi ni kwamba hawana uwezo. Wamefika hapo walipo kwa sababu ya mbeleko. Ukiwataka wakuonyeshe accomplishment yao angalau hata moja kwa vipindi vyao vya uongozi, kusema ukweli hawana.
Pamoja na hilo la kukosa uwezo, lipo pia la kukosa hekima. Utendaji wao wa kazi umejikita kwenye mazingira ya awamu ya nne, ambapo kila kitu kilimuwa kinafanyika bora liende. Hakuna uwajibikaji, ufisadi ndio mtindo mmoja, watu wanachekeana tu bila kuwajibishana. Wangekuwa na hekima wangejifunza baada ya kupigwa chini na JPM (rip). Hawakujua kuwa kila zama huja na kitabu chake! Vijana namna hiyo wanakosaje intelligence ya kuji-adjust kulingana na mazingira waliyomo? Hawana uwezo, na hawana hekima.
 
Nadiriki kusema kuwa UWEZO WA KIUONGOZI ni mdogo kwao....

Unawezaje kuwa kiongozi mwenye uwezo mkubwa na ukose uangalifu wa kutotambua kuwa "kukukuru kakara za malengo makubwa siku za usoni" zitakupigisha mwereka LEO?!!

Wao si Lowassa...naye pia hakufanikiwa....

#SiempreSSH[emoji2956]
 
Back
Top Bottom