Swali la Uzalendo: What is The Magic of The Same Route? Precision Air Full Flight, ATCL Half Empty

Kumbe hadi kwenye ndege ukikaa siti za nyuma unarushwarushwa kama kwenye basi....just kidding
 

Serikali haiwezi fanya biashara
 
Time matters a lot kwenye air travel. Na hii ipo hata kwenye njia nyingine za usafiri, wenyewe huita seasons.
 
Jiulize kwa nini mtaani kwako hakuna wakala wa T-Pesa;serikali ya huyu mchunga ng'ombe mwenzako sijui lini itajua kuwa biashara haiendi hivyo wanavyotaka tuendeP

Mkileta siasa ktk hili, mwishowe ni kuleta figisu kwa sekta binafsi.
Paskali mbona unatuuliza swali hili sisi? Mwulize mwenyekiti wako maana ndiye anajua mambo ya ndege!
 
Hongereni wenzetu, mimi tangu watuondelee ndege yetu pendwa Fastjet nimerudi kwenye mabasi.

Najipandia luxury yangu safi tu maisha yanakwenda, hizo bei za ATCL hawataki wanyonge wapande hizo ndege.

Ndio maana inashangaza mtu kushupaa kwamba anaongeza ndege ilihali Watanzania wenyewe hawana uwezo wa kuzipanda, ndio nini sasa?
 
Ni hali ya biasharaya siku hiyo mkuu. Hata mimi nikishakwea ATCikawa full nikarudi na Precision hatukuwa tunazidi kumi na niliumia sana. Ni biashara kwa siku na siku hubadilika. ATC wana wateja wengi kuliko precision.
 
Hiyo Precision ikiwa tupu
 
Kaka Paskali.
Kuna wakati hata baba anapokuwa mklai kupitiliza pale home, ikitokea siku baba akapigwa na baba wa jirani, watoto wake wataenda kushangilia vyumbani kwao... Ndo kinachotkea kwa ATCL... Tukumbuke FAST JET walifanyiwa figisu.. na hata precision ile ruti ya Kigoma walishafanyiwa mbwembwe.. Tukumbuke hao wanaofanyiwa figisu wan ndugu, jamaa na marafiki... hawawezi ona ndugu, jamaa au rafiki yao anafanyiwa madudu halafu wao wakae kimya.. Watamsaidia mwenzeo kwa namna wanayoiweza.. mfano kusafiri na ndege ya mwenzao..!!! THIS IS HUMAN NATURE hasa wakijisikia mwenzao kaonewa...

La pili, uhakika wa safari na majibu ya wale wanaokatisha tiketi... Safari inaweza ikafutwa au kubadilishwa muda saa yoyote NA BILA SABABU ZA KUELEWEKA KWA WASAFIRI... Ebu niambie, huyu mdau wako Mollel, kama ingefutwa au kubadilishwa muda hiyo ndege, angefanya nini..?? kama si kuikosa shughri ya kifamilia..??

ATCL ifanye ushindani, isisaidiwe kwa kuwawekea figisu wengine... AND this should go kwa wengine pia.. TTCL, TANESCO, BANDARI, etc FIGISU na ukali usio na sababu wa baba mwenye nyumba hupelekea migomo baridi
 
Haka kajamaa sidhani kama katakuja kupata uteyuzi! Yaani kameanza tena kuponda hadharani? Sijui kwa vile kameona deal la kujipendekeza limebuma?
 
Mayala aina ya posting yako wanaita ni ya tukio na hitimisho. Kwa watu wanaojua aviation industry ambayo Mayala kaonyesha haijui watakubaliaba na mimi kuwa conclusion ya Mayala ni inconclusive. Huyu Mayala hajui hata kama ndege ya ATC kuja Dar ilikuwa na ujazo gani siku hiyo maana analinganisha na ndege ya kwenda kilimanjaro. Je kama kulikuwa na tukio Dar au tukio limekwisga Arusha hivyo kuzalisha abiria wengi kwa njia ya kurudi Dar? With due respect kaandika ili aandike na sio kama mwandushi. Of course unaona hata majibu anayopata ni hayo hayo ya matukio. Siasa! Angetuletea trend ya njia hiyo kwa siku ya kwenda kwa Airlines zote mbili na kurudi kwa zote mbili tungekuwa na njia sahihi ya kujadili. Kwa kifupi kakurupuka na sioni kama ni issue ya kujadili kimkakati ukiacha mbali waosubiri kujibu kwa hisia za kisiasa bila uelewa kama yeye Mayala. Nasubiri hoja yako nisaidie kutoa mawazo sio siasa za ccm na chadema.
 
Umeelewa ulichoandika?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…