Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Either of the two bado ni shida tu hiyo.Tatizo msisitizo wao ni nini, kuwa watu wafuate taratibu na sheria au kuwafanyia raia extortion kupitia mfumo wa sheria za kikanjanja......?!
Tumeishaaa!
Kichomiz:Wameongeza tozo na usumbufu uliotukuka
Saint Ivuga:Hence: watu hawatauziana na tra Watakosa mapato
Hawa majamaa wamesomea wapi!?
Udsm ndio inaleta majitu kama haya au degree za chupli chupli?
Yaani jitu linaongea kiurahisi tu halijali yaani
*152*00#Ivi kuna namna ya kujua kama unadaiwa mtandaoni...msaada kwa anae fahamu
Zoezi litafanikiwa kwa mbindeExtrovert:
Zoezi litafanikiwa au tutarajie kuporomoka kwa mapato ?
Mie naona watu wataacha magari nyumbani na kupungua kwa mapato kupitia mafuta. Ila wachache watakomaa na kudeal na matrafiki kwa kuwapa buku 2Zoezi litafanikiwa kwa mbinde
Kwa shida shida saanaZoezi litafanikiwa kwa mbinde
Yani kwa tabu na njaa matatizoKwa shida shida saana
Si wote wafanyao sharati hupata UKIMWI siku hiyo hiyo, lakini baadaye unaingia, anaanza kutumia ARV!Unaongelea bongo hii hii au wapi?Zaidi ya miaka 10 nafanya hivyo afu fresh kabisa.
Download app ya GePG utapata kila aina ya bili za serikaliIvi kuna namna ya kujua kama unadaiwa mtandaoni...msaada kwa anae fahamu
Ndio ujinga wenyewe huo.Sasa Kama Mmiliki Wa Awali Yuko Mbali au amefariki Ts means Hawawezi Kufanya Transfer?
Wakuu Someni Hii Taarifa Kutoka Mamlaka Ya Mapato Tanzania (TRA)View attachment 1968871
=====
October 8, 2021 by Global Publishers
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kumekuwepo na changamoto kubwa ya baadhi ya watu wanakuwa wamesajili vyombo vya moto lakini usajili wao ni batili, hawajasajiliwa na TRA ambapo magari yao yanakuwa yameliingiza nchini kimagendo, jambo linalopelekea magari zaidi ya moja yote yanakuwa na namba moja ya gari.
Hayo yamesemwa leo Ijumaa, Oktoba 8, 2021 na Mercy Macha ambaye ni Afisa Msimamizi wa Kodi TRA wakati akitolea ufafanuzi katika kipindi cha Front Page kinachoruka kupitia +255 Global Radio huku akiwahimiza wananchi kufuata taratibu zilizowekwa na mamlaka hiyo kubadili umiliki wa vyombo vya moto ili kuondokana na changamoto mbalimbali zinazoweza kuwakumba.
“Jukumu la TRA sio kukusanya kodi tu, hata kuelimisha pia. Kabla hujanunua gari lazima au chombo chochote cha moto, fika TRA ujue kama chombo hicho ni cha halali, hakidaiwi kodi, fuata taratibu wa kubadilisha umiliki kuja kwako.
“TRA tumekuja na utaratibu mpya, unapokuja kubadilisha umiliki wa chombo lazima mmiliki wa mwanzo awepo, mmiliki mpya (aliyeuziwa) awepo na atuonyeshe kitambulisho chake, chombo lazima kiwepo maofisa wetu wakikague kuanzia Chassis Number. Unapobadilisha umiliki wa chombo lazima zile kodi za uhamishaji wa chombo zichukuliwe, TRA tukusanye mapato.
“Gharama ya kuhamisha umiliki wa chombo cha moto ni Tsh 100,000 jumlisha asilimia 1 ya gharama ya ununuzi iliyoandikwa kwenye kwenye mkataba, na huu mkataba lazima uwe legal, usainiwe na mwanasheria na aweke risiti ya huduma aliyotoa.
“Kuna wanaopewa bajaji za mkataba, anaendesha akimaliza mkataba anakabidhiwa inakuwa ya kwake lakini hawaji kubadilisha umiliki, hawa nao tunawahimiza kuja TRA kubadilisha umiliki wa vyombo vyao.
“Kwa magari ambayo yameingizwa nchini yakiwa na msamaha wa kodi, wakati yanauzwa kuna utaratibu wa kufuatwa kuhakikisha msamaha hauhami kwenda kwa mtu mwingine, mhusika arudi TRA kufuata taratibu hizo. Usiuze chombo chako cha moto bila kuhakikisha umebadilisha umiliki, unayenunua hakikisha nawe unakuwa mmiliki halali wa chombo chako,” Mercy Macha, Afisa Msimamizi wa Kodi TRA.
View attachment 1969147
Kwa nini tunalipia kadi 50,000 .. ? Huu ni udhamba mkubwa. Kwanza hatuhitaji hiyo kadi0Wakuu Someni Hii Taarifa Kutoka Mamlaka Ya Mapato Tanzania (TRA)View attachment 1968871
=====
October 8, 2021 by Global Publishers
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kumekuwepo na changamoto kubwa ya baadhi ya watu wanakuwa wamesajili vyombo vya moto lakini usajili wao ni batili, hawajasajiliwa na TRA ambapo magari yao yanakuwa yameliingiza nchini kimagendo, jambo linalopelekea magari zaidi ya moja yote yanakuwa na namba moja ya gari.
Hayo yamesemwa leo Ijumaa, Oktoba 8, 2021 na Mercy Macha ambaye ni Afisa Msimamizi wa Kodi TRA wakati akitolea ufafanuzi katika kipindi cha Front Page kinachoruka kupitia +255 Global Radio huku akiwahimiza wananchi kufuata taratibu zilizowekwa na mamlaka hiyo kubadili umiliki wa vyombo vya moto ili kuondokana na changamoto mbalimbali zinazoweza kuwakumba.
“Jukumu la TRA sio kukusanya kodi tu, hata kuelimisha pia. Kabla hujanunua gari lazima au chombo chochote cha moto, fika TRA ujue kama chombo hicho ni cha halali, hakidaiwi kodi, fuata taratibu wa kubadilisha umiliki kuja kwako.
“TRA tumekuja na utaratibu mpya, unapokuja kubadilisha umiliki wa chombo lazima mmiliki wa mwanzo awepo, mmiliki mpya (aliyeuziwa) awepo na atuonyeshe kitambulisho chake, chombo lazima kiwepo maofisa wetu wakikague kuanzia Chassis Number. Unapobadilisha umiliki wa chombo lazima zile kodi za uhamishaji wa chombo zichukuliwe, TRA tukusanye mapato.
“Gharama ya kuhamisha umiliki wa chombo cha moto ni Tsh 100,000 jumlisha asilimia 1 ya gharama ya ununuzi iliyoandikwa kwenye kwenye mkataba, na huu mkataba lazima uwe legal, usainiwe na mwanasheria na aweke risiti ya huduma aliyotoa.
“Kuna wanaopewa bajaji za mkataba, anaendesha akimaliza mkataba anakabidhiwa inakuwa ya kwake lakini hawaji kubadilisha umiliki, hawa nao tunawahimiza kuja TRA kubadilisha umiliki wa vyombo vyao.
“Kwa magari ambayo yameingizwa nchini yakiwa na msamaha wa kodi, wakati yanauzwa kuna utaratibu wa kufuatwa kuhakikisha msamaha hauhami kwenda kwa mtu mwingine, mhusika arudi TRA kufuata taratibu hizo. Usiuze chombo chako cha moto bila kuhakikisha umebadilisha umiliki, unayenunua hakikisha nawe unakuwa mmiliki halali wa chombo chako,” Mercy Macha, Afisa Msimamizi wa Kodi TRA.
View attachment 1969147
View attachment 1969149