Taarifa kutoka TRA kuhusu kubadilisha umiliki wa chombo cha moto

Taarifa kutoka TRA kuhusu kubadilisha umiliki wa chombo cha moto

Kazi yao ni kukaza ili raia aumie. Ila sio kutazama changamoto ya sheria zilizopo ambazo zinafanya raia waone kodi ni mzigo na kuzikwepa.

Tatizo hapa sio raia kukwepa kufuata taratibu za kisheria bali tatizo ni hizo taratibu za kisheria zinabinya masilahi ya raia na kumnyima haki zake.

Pumbavu sana.
 
Naomba niseme tu mnaoona hili zoezi n baya acheni upumbavu na uvivu wa kufikiri, kila kitu kulalamika tu.

Kwaiyo mnataka muuziane kinyemela tu mtaani huko na wewe unayenunua unamiliki Mali kinyume na taratibu unaona fresh tu akati kiuharisia wewe sio mmiliki halali kwa sababu hujafata taratibu.

Kama mmiliki kafariki si kuna vielelezo kama mtu kafariki? Acheni kujifanya mnataka maendeleo akati bado mna akili za kizamani kila siku mtaona maendeleo ni kero kwenu.

Waafrika tulivyo wajinga tunaamini mtu asiyefata utaratibu halali na akafanikisha jambo lake uyo ndo mjanja sasa na kila mtu atamsifia. Ujanja ni kufata taratibu
 
Mambo mengine huleta ugumu wa maisha tu bila sababu. Let's agree that there are issues can work better in Europe or America but not in Africa, at least in some decades to come. Otherwise watajikuta wanakosa hata hicho kidogo.
Tatizo msisitizo wao ni nini, kuwa watu wafuate taratibu na sheria au kuwafanyia raia extortion kupitia mfumo wa sheria za kikanjanja......?!
 
Magari yanalipiwa yaingiapo inchini.sasa Kama mmiliki wa kwanza anamuuzia mtu Kodi ya Nini tena?,wakati gari ilisha lipiwa?.Au TRA Wana anzisha double taxiation?aghhhhhhh!!!!!
TRA thinking tank yao ni zero. Ubunifu hakuna kabisa.....
 
Wrong start!
Kazi ya TRA ni kukusanya kodi sio kukagua gari. Wala sio kubuni kodi au TOZO mpya bila kupitishwa na Bunge.

Hiyo kazi ya ukaguzi kama gari ni la wizi ifanywe na polisi.
Maana yake polisi (walio na data au taarifa za magari yaliyoibiwa) ndiyo watoe clearance report kwamba gari husika sio la wizi.

Mnapotaka kila taasisi moja ifanye kazi zisizo zake mnasababisha mianya ya rushwa, uonevu, usumbufu na unnecessary red tape.

Kwamfano niko kijijini nimepatwa shida ya dharura nisimuuzie mali yangu rafiki yangu, ndugu, au jirani yake mpaka TRA wahusike! M/Kiti wa serikali ya mtaa au Wakili/Hakim hawatoshi?

TRA itafika mahali watataka wawepo kila unaponunua baiskeli, bodaboda, bajaji, nyumba, cement, matofali, mabati nk. Eti kwasababu huenda hicho kitu ni cha wizi!
Na mahari watataka wapate percentage yao......
 
Naomba niseme tu mnaoona hili zoezi n baya acheni upumbavu na uvivu wa kufikiri, kila kitu kulalamika tu.

Kwaiyo mnataka muuziane kinyemela tu mtaani huko na wewe unayenunua unamiliki Mali kinyume na taratibu unaona fresh tu akati kiuharisia wewe sio mmiliki halali kwa sababu hujafata taratibu.

Kama mmiliki kafariki si kuna vielelezo kama mtu kafariki? Acheni kujifanya mnataka maendeleo akati bado mna akili za kizamani kila siku mtaona maendeleo ni kero kwenu.

Waafrika tulivyo wajinga tunaamini mtu asiyefata utaratibu halali na akafanikisha jambo lake uyo ndo mjanja sasa na kila mtu atamsifia. Ujanja ni kufata taratibu
Wewe nae basi kuwa na uelewa. Unadhani kwamba wanaopinga hawapendi kufuata sheria?!

Tatizo hizi taratibu zinakuwa na makando makando ya upigaji ndani yake. Mamlaka zinakuwa zinabana sana raia kuwa huru na maisha kulingana mifumo ya kiuchumi ilivyo kwa sasa ambapo hela zinatoka sana kuliko zinavyoingia.
 
Nionalo kwa baadaye ikiwa mwitioo utakua mdogo, polisi watatumika kwenye hili zoezi. Ukisimamishwa unaombwa kadi na kitambulisho chako. Ukisema umeazima kwa siku moja gari inawekwa kituoni ukamlete mmiliki halali. Ugumu utakuja pale utakapokua umemuacha mmiliki dar na wewe uko uyole.

Sent from my SM-J530F using JamiiForums mobile app
Haiwezekani na itafeli maana si kila mwenye gari anaendesha yeye. Kuna magari ya mizigo, daladala, tax, magari ya kukodi, kuazima. Usumbufu utakuwa mkubwa. Kila siku itakuwa watu wanaitwa polisi kuthibitisha umiliki.
 
TRA tumekuja na utaratibu mpya, unapokuja kubadilisha umiliki wa chombo lazima mmiliki wa mwanzo awepo, mmiliki mpya (aliyeuziwa) awepo na atuonyeshe kitambulisho chake, chombo lazima kiwepo maofisa wetu wakikague kuanzia Chassis Number. Unapobadilisha umiliki wa chombo lazima zile kodi za uhamishaji wa chombo zichukuliwe, TRA tukusanye mapato.
Mnapoweka conditions wekeni pia options in case condition A haiwezekani basi X itakubalika, kwa mfano mmiliki yupo hoi hospitali, anauza gari lake ili atibiwe, je atafikaje TRA?
 
Wrong start!
Kazi ya TRA ni kukusanya kodi sio kukagua gari. Wala sio kubuni kodi au TOZO mpya bila kupitishwa na Bunge.

Hiyo kazi ya ukaguzi kama gari ni la wizi ifanywe na polisi.
Maana yake polisi (walio na data au taarifa za magari yaliyoibiwa) ndiyo watoe clearance report kwamba gari husika sio la wizi.

Mnapotaka kila taasisi moja ifanye kazi zisizo zake mnasababisha mianya ya rushwa, uonevu, usumbufu na unnecessary red tape.

Kwamfano niko kijijini nimepatwa shida ya dharura nisimuuzie mali yangu rafiki yangu, ndugu, au jirani yake mpaka TRA wahusike! M/Kiti wa serikali ya mtaa au Wakili/Hakim hawatoshi?

TRA itafika mahali watataka wawepo kila unaponunua baiskeli, bodaboda, bajaji, nyumba, cement, matofali, mabati nk. Eti kwasababu huenda hicho kitu ni cha wizi!
Unaelewa kubadili umiliki maana yake ni nini? Au umeendika ugolo wako kisa una ITEL na upo kwa kochi la shemeji yako? Kabla hujaandika kitu kwenye hoja za msingi anza kwanza kujiuliza maswali muhimu. Ujuaji kama huu ndio unafanya tuwe nyuma kimaendelo. Ngoja nikupe maelezo, unapobadili umiliki wa chombo utahitaji
1. TIN ya mmiliki wa chombo kitu ambacho ni rahisi tu kupata ambapo kwenye kadi ya gari inaonekana wazi kabisa.
2. passport ya mmiliki ambapo nayo ni rahisi kupata kupitia TIN yake.
3. barua ya kuomba kubadili umiliki nayo ni rahisi maana hakuna uthibitisho kuwa huo ndio mwandiko wa mmiliki halali.
4. Mkataba wa mauziano baina ya mnunuzi na mnunuaji, hapa pia ni rahisi maana unajiandikia tu unapitisha kwa wakili/mwanasheria.
5. Hati ya kiapo cha Umiliki wa chombo ambayo utaipata kwa mwanasheria/mahakamani ambayo nako wala hawajui kama ww ndio mmiliki hivyo ni rahisi sana kufoji.
6. Kadi OG ya chombo cha moto ambayo pia unaiweza ipata ikiwa gari imeibiwa na mwenye gari alikuwa anatunza hiyo kadi ndani ya gari.
NB haikuwa lazima mmiliki afike ofisini na hapo ndipo inafanya iwe rahis hata gari ya wizi iweze badilika umiliki.
Hivyo basi MABORESHO HAYA YATALETA UFANISI NA KUPUNGUZA WIZI, LKN PIA ITAMPUNGUZIA GHARAMA MMILIKI MPYA kuhangaika na TRA. YANAPOTOKEA MABORESHO TUWE POSITIVITY KATIKA KUHOJI NA KUCHAMBUA BADALA YA KUJIFANYA TUNA AKILI ZAIDI YA WATU WENYE UZOEFU NA HIZO IDARA MIAKA NA MIAKA.
 
Binafsi naona utaratibu ni mzuri, sababu una faida NYINGI kuliko hasara. Tatizo ni namna ya utekelezaji tu..system zao zitakuwa fair enough? Na kama kupata details za mwenye kadi itakuwa ngumu means zoezi litakuwa gumu..lakini Kwa mnunuzi details ZAKE ni rahis , na kwakweli inapendeza ukinunua UPATE kadi Yako , penye shida ni mkataba wa mwanasheria Tena mwenye kutoa EFD receipt, ...unajua Kwa MDA mrefu baadhi ya watu wali ignore ubadirishaji wa umiliki..watu wakishapeana kadi halisi basi !!! Sasa mnyololo wa kuuziana sometimes UNAWEZA Kuta ni mrefu ..YAANI tokea Kwa muuzaji wa kwanza mpaka wa mwisho ..UNAWEZA Kuta wewe ni mmiliki wa 5 huko, aliyekuuzia nae hakubadiri, nae hakubadiri pia....basi kumpata yule wa AWALI ni shida...wangesema LABDA utaratibu uanze Sasa (japo Sio rahisi kujua kama ni lini ) ..ila dhana nzima ya kubadiri umiliki ni mhimu na ni vema Sana hata kama gari ni ya 1.5ml[emoji3]
SIKU UKIUZA GARI NA ULIYEMUUZIA AKAENDA KUFANYA TUKIO LA UJAMBAZI, AU KUBEBA WAHAMIAJI HARAMU AKATELEKEZA GARI NDIO UTAJUA UMUHIMU WA KUBADILI UMILIKI WA GARI MAPEMA SANA. MARA NYINGI HATUJUI KAZI ZA WAL TUNAOWAUZIA.
 
Wakuu Someni Hii Taarifa Kutoka Mamlaka Ya Mapato Tanzania (TRA)View attachment 1968871

=====

October 8, 2021 by Global Publishers

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kumekuwepo na changamoto kubwa ya baadhi ya watu wanakuwa wamesajili vyombo vya moto lakini usajili wao ni batili, hawajasajiliwa na TRA ambapo magari yao yanakuwa yameliingiza nchini kimagendo, jambo linalopelekea magari zaidi ya moja yote yanakuwa na namba moja ya gari.

Hayo yamesemwa leo Ijumaa, Oktoba 8, 2021 na Mercy Macha ambaye ni Afisa Msimamizi wa Kodi TRA wakati akitolea ufafanuzi katika kipindi cha Front Page kinachoruka kupitia +255 Global Radio huku akiwahimiza wananchi kufuata taratibu zilizowekwa na mamlaka hiyo kubadili umiliki wa vyombo vya moto ili kuondokana na changamoto mbalimbali zinazoweza kuwakumba.

“Jukumu la TRA sio kukusanya kodi tu, hata kuelimisha pia. Kabla hujanunua gari lazima au chombo chochote cha moto, fika TRA ujue kama chombo hicho ni cha halali, hakidaiwi kodi, fuata taratibu wa kubadilisha umiliki kuja kwako.

“TRA tumekuja na utaratibu mpya, unapokuja kubadilisha umiliki wa chombo lazima mmiliki wa mwanzo awepo, mmiliki mpya (aliyeuziwa) awepo na atuonyeshe kitambulisho chake, chombo lazima kiwepo maofisa wetu wakikague kuanzia Chassis Number. Unapobadilisha umiliki wa chombo lazima zile kodi za uhamishaji wa chombo zichukuliwe, TRA tukusanye mapato.

“Gharama ya kuhamisha umiliki wa chombo cha moto ni Tsh 100,000 jumlisha asilimia 1 ya gharama ya ununuzi iliyoandikwa kwenye kwenye mkataba, na huu mkataba lazima uwe legal, usainiwe na mwanasheria na aweke risiti ya huduma aliyotoa.

“Kuna wanaopewa bajaji za mkataba, anaendesha akimaliza mkataba anakabidhiwa inakuwa ya kwake lakini hawaji kubadilisha umiliki, hawa nao tunawahimiza kuja TRA kubadilisha umiliki wa vyombo vyao.

“Kwa magari ambayo yameingizwa nchini yakiwa na msamaha wa kodi, wakati yanauzwa kuna utaratibu wa kufuatwa kuhakikisha msamaha hauhami kwenda kwa mtu mwingine, mhusika arudi TRA kufuata taratibu hizo. Usiuze chombo chako cha moto bila kuhakikisha umebadilisha umiliki, unayenunua hakikisha nawe unakuwa mmiliki halali wa chombo chako,” Mercy Macha, Afisa Msimamizi wa Kodi TRA.
View attachment 1969147
View attachment 1969149
mmiliki awepo na mnunuzi awepo, kuna tatizo. mtu kanunua gari kwenye mnada uliohusisha magari yaliyo kamatwa kwa wadaiwa sugu, wamiliki utawapata wapi?
 
Hivi Wamefanya risechi ya Kutosha kweli? Na Kama Leo Ardhi Wamesitisha Kutoa hati za makaratasi eti wanatoa hati za Electronic ambazo Toka Mwezi Wa 3 hakuna hati iliyotoka
mambo mengi Tanzania ni mwendo wa zimamoto, hakuna maandalizi, wala utafiti.
 
Niliuziwa gari na mzungu 2013 alisharudi kwao. Nampataje Leo hii 2021?
Muda wote huo ulikuwa hujabadirisha umiliki?
Mimi cha kwanza kabisa ni kubadirisha umiliki ,ili niwe na uhakika na mali yangu hapo hata barabarani unatembea kwa kujiamini
 
Mlolongo mrefu sana aisee ,mara police,mara viapo,mara hati , yaani ni mwendo wa tozo tu ndani ya nchi ya TOZONIA
 
Naona TRA wametoa ufafanuzi namna ya kubadili umiliki wa vyombo vya moto du kumbe unaweza baadaye shindwa liuza kama ulinunu bila libadili jina au jamaa akakupiga famba

WhatsApp Image 2021-10-10 at 3.29.18 PM (1).jpeg
 
Back
Top Bottom