Uchaguzi 2020 Taarifa kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi itazuia Mawakala wa Vyama kuingia na simu zao katika vituo vya kupigia kura imetushtua

Uchaguzi 2020 Taarifa kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi itazuia Mawakala wa Vyama kuingia na simu zao katika vituo vya kupigia kura imetushtua

SUALA LA SIMU KWA MAWAKALA: TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI MSIHARIBU UCHAGUZI WA WATANZANIA!

Taarifa kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi itazuia Mawakala wa Vyama kuingia na simu zao katika vituo vya kupigia kura imetushtua hata sisi viongozi wa Kanisa! Simu ina mambo mengi sana katika ulimwengu wa sasa ikiwemo kutunza kumbukumbu kwa njia mbalimbali.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi haiwezi kuwafanya mawakala kama 'tabula rasa' yaani watu wasioweza kuhifadhi kumbukumbu yo yote na hata kushindwa kuwasiliana. Mawakala wakiwa na simu wanaweza kupiga picha matokeo halisi ili kudhibiti wizi wa kura! Kitendo cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuzuia Mawakala kuingia na simu katika chumba cha kupigia kura ni sawa na kuandaa usiri utakaopelekea mazingira ya kuibiwa au kuchakachuliwa kwa kura!

Tunaitahadharisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuacha kutoa maelekezo au kutunga kanuni kwa lengo la kufanya Matokeo ya Uchaguzi Mkuu yasiheshimike na wananchi! Ili kuleta afya ni vizuri maelekezo na kanuni za Tume zikubaliwe na vyama vyote. Tume iepuke kutoa kanuni na maelekezo katika kipindi hiki kwa lengo la kuubeba upande mmoja na kuunyonga upande mwingine!

Sisi tumekwisha kutimiza wajibu wetu (Ezekieli 33:1-20).

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani
Ikilazimu, hata mawasiliano ya simu na internet hayatakuwepo.
 
SUALA LA SIMU KWA MAWAKALA: TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI MSIHARIBU UCHAGUZI WA WATANZANIA!

Taarifa kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi itazuia Mawakala wa Vyama kuingia na simu zao katika vituo vya kupigia kura imetushtua hata sisi viongozi wa Kanisa! Simu ina mambo mengi sana katika ulimwengu wa sasa ikiwemo kutunza kumbukumbu kwa njia mbalimbali.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi haiwezi kuwafanya mawakala kama 'tabula rasa' yaani watu wasioweza kuhifadhi kumbukumbu yo yote na hata kushindwa kuwasiliana. Mawakala wakiwa na simu wanaweza kupiga picha matokeo halisi ili kudhibiti wizi wa kura! Kitendo cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuzuia Mawakala kuingia na simu katika chumba cha kupigia kura ni sawa na kuandaa usiri utakaopelekea mazingira ya kuibiwa au kuchakachuliwa kwa kura!

Tunaitahadharisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuacha kutoa maelekezo au kutunga kanuni kwa lengo la kufanya Matokeo ya Uchaguzi Mkuu yasiheshimike na wananchi! Ili kuleta afya ni vizuri maelekezo na kanuni za Tume zikubaliwe na vyama vyote. Tume iepuke kutoa kanuni na maelekezo katika kipindi hiki kwa lengo la kuubeba upande mmoja na kuunyonga upande mwingine!

Sisi tumekwisha kutimiza wajibu wetu (Ezekieli 33:1-20).

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani
Goli la mkono hilo, ccm bana
 
Hiyo ni kanuni ya tume, na chama chako chadema walisaini fomu ya maadili ya uchaguzi! Na walikubali, Sasa wewe askofu mchunga siasa unapinga Kama Nani?

Viongozi wa dini Leo walikuwa ukumbi wa Mwalimu Nyerere wakati Rais anapokea gawio la billion 100!!
Wewe endelea na siasa, siku ya mwisho Mungu atakuuliza haesabu yake

Iko kwenye kanuni ipi iliyosainiwa wapi?

Wacha maneno weka hiyo kanuni ya kuzuia simu kwenye listi zilizosainiwa hapa.

Acheni utani nyie. Safari hii tumedhamiria haswa. Ama zetu ama zenu.

ICC ataamua hili battle!
 
Iko kwenye kanuni ipi iliyosainiwa wapi?

Wacha maneno weka hiyo kanuni ya kuzuia simu kwenye listi zilizosainiwa hapa.

Acheni utani nyie. Safari tumedhamiria. Ame zetu ama zenu. ICC ataamua hili battle!
Kama unazo nguvu mbona kila wakati unawaza ICC tu jitokeze tu barabarani wakunyowe kwa kisu!
 
Bado watanzania hatujatatua tatizo kabisa. Lengo tupate tume iliyo huru ambayo haina upendeleo wowote hapo ndipo tutakuwa na uchaguzi wa huru na haki.
 
Sasa Askofu kila mtu akipiga picha, then tuanze kutafuta picha ya nani ndio sahihi? Tume ina lengo zuri kwamba taarifa za matokeo ziwe na channel moja, sio kila mtu na matokeo yake itakuja kuleta taharuki na hatimae vurugu.Endelea kuchunga kondoo wa Bwana mambo mengine haya kuhusu. Usichanganye siasa na dini

Kwani hiyo picha inapigwa kutoka wp? Hata isifanane maana yake ni form ya msimamizi ndio itapigwa picha
 
Lazima chama tawala kutumia dola ili kubaki na dola!
Au mmesahau kauli ya Katibu?!
 
Siku ukitia akili kichwani utaelewa tu umuhimu wa simu ili kupambana na wizi wa maccm kwa kutumia hila mbali mbali na simu zitasaidia kuanika wizi na uhuni wao hadharani si kwa Watanzania tu bali dunia nzima.
Hoja Hafifu kabisa..
Mawakala tayari wameaminika na Vyama vyao na sidhani kama kuna uhitaji wa kua na simu kwenye vituo na sidhani kama sheria inaelekeza kufanya hivyo.
 
Hawa maaskofu wengine wa aina hii sijui wanapatikana kwa vigezo gani imagine huyo anayesema hayo ni askofu anaetegemea kuongoza kondoo zake katika njia ya kwenda mbinguni sijui anawaza nini manake kwenye kituo Kuna mawakala na hata wagombea wanaweza kuwepo Sasa suala la. Kusema mawakala wapige picha matokea sijui haoni impact yake badae kuwa kila wakala anaweza kuwa na version yake ya kura kwa kweli viongozi wetu wa dini kuweni makini kwa dhamana mlio nayo ni kubwa Sana msitake sasa waumini tuanze kugawanyika kwa kuonyesha dhahiri mna ushabiki wa kisiasa ni vyema mkahubiri amani na kuombea uchaguzi uishe salama msiwe vyanzo vya vurugu manake hata nyie mtakua wahanga
Hakuna amani bila haki, funga bakuli lako

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Wapwa

Ni ukweli usiofichika kuwa CCM ina mbinu nyingi sana za uwizi wa kura, bahati mbaya nyingi tayari zimeshajulikana. Sasa kuna baadhi ambazo hazipigiwi kelele sana lakini ni mbinu mbaya sana na wakiitumia lazima watafaulu na kutakuwa hakuna pa kulalamika. mawakala muwe makini sana kwenye hili.

1 ) Watendaji kukusanya namba na vitambulisho vya kupigia kura
Kwa takribani miezi 6 sasa maeneo mengi sana, watendaji wamekuwa wakipita nyumba kwa nyumba kukusanya taarifa za wapiga kura, mfano namba ya kitambulisho na eneo unalopigia kura, kuna siku nliuliza hapa hizi taarifa wanazokusanya zinakwenda kufanyiwa nini hakuna aliyekuwa na jibu, na hii wamekuwa wakiifanya kwa siri sana.

Walichokipanga hawa jamaa, ni kwamba mfano kituo A kina wapiga kura 250, inajulikana ya kuwa sio wapiga kura wote watakaoenda kupiga kura, kwa hiyo mfano wakipiga kura watu 130, sababu tayari wana taarifa za wapiga kura wote wa kituo A wanaweza kujua nani amepiga nani hajapiga wakisaidiana na wasimamizi ndani ya kituo, kwa hiyo ni rahisi either kuleta mamluki kumalizia idadi iliyobakia wakiwa na taarifa sahihi za wapiga kura wa kituo husika au kutafuta upenyo wa kuongeza kura nyingine ndani ya box la kura. mfano wakiongoza kura 50 * vituo 50000 watakuwa wamefanikiwa kuongeza kura zaidi ya 2000,000+ .

Sasa nini kifanyike. Hapa tutagemea zaidi WAKALA kuhakikisha anajua idadi KAMILI ya watu wote waliopiga kura ndani ya kituo chake, na sio kupata idadi kutoka kwa msimamizi wa kituo. WAKALA hakikisha muda wote unakuwa kituoni, na kila anayeingia unamuhakiki sura yake ndani ya kitambulisho na unamuhesabu ili kutokuruhusu udanganyifu wowote wa idadi ya waliopiga kura.

2 ) Majimbo yaliyopita bila kupingwa

Haya majimbo yalikuwa ni mkakati wa kuongeza kura za uraisi kwao, huku kuna uwezekano mkubwa wa kupata 100% kwa kila kituo, kwa iyo tunaomba mawakala wetu muwe makini sana na wapiga kura na idadi ya watu watakaopiga kura ndani ya vituo vyenu.


Haki huinua Taifa
 
Sasa Askofu kila mtu akipiga picha, then tuanze kutafuta picha ya nani ndio sahihi? Tume ina lengo zuri kwamba taarifa za matokeo ziwe na channel moja, sio kila mtu na matokeo yake itakuja kuleta taharuki na hatimae vurugu.Endelea kuchunga kondoo wa Bwana mambo mengine haya kuhusu. Usichanganye siasa na dini
Kwani hata kukiwa na picha elfu 1 za tukio lile lile kuna ubaya gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maagizo yoyote ya Mahera yasiyo na msingi wa kisheria yapuuzwe na kudhauliwa.

Hili halimo katika sheria, lipuuzwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Napeleka makalioni kwako,wewe ukidhani napeleka wapi sheikh?
 
Back
Top Bottom