Taarifa: Nimekwisha kula Kiapo (DEED POLI) na kwa msajili wa Viapo na Nyaraka (Mahakama ya Ardhi) kuanzia sasa nitakuwa naitwa DON NALIMISON

Mkuu Deogratius Nalimi Kisandu sipping uamuzi wako,lakini hili jina jipya limekaa ki-ujana zaidi/kisanii. Alafu bado vyeti vyako vya elimu vinatumia jina lako la zamani,huoni litakuletea shida huko mbeleni?
 
Huyu mtu dishi bado halijakaa vizuri. Nduguze au jf iweke utaratibu tumsaidie apatiwe matibabu zaidi la sivyo anakoelekea butimba patamhusu tena
 
Safi mzee, jina kama lina harufu ya nuksi bac ruksa kulibadilisha, mshauri na mzee wa kisarawe!!
 
Mkuu ,

Nikupongeze kwa kufuata ushauri.
 
Don Nalimison amelenga uchaguzi October, angeendelea na jina lake asingekuwa na kigezo cha kugombea nafasi yoyote ya kisiasa hivyo ujaja wa Don Nalimison akaona kubadili jina ili asiwekee kikwazo/vikwazo na hata akiwekewa kikwazo aweze kupinga kisheria.

Hakimu : Mlalamikaji una ushahidi kuwa mlalamikiwa hana sifa za kugombea nafasi yoyote ya kichama ?

Mlalamikaji : ndio, ndugu Hakimu Don Nalimison alitumikia kifungo hivyo hana sifa.

Hakimu : Mlalamikiwa una chochote cha kuieleza hii Mahakama tukufu

Don : Ndio, Kipindi nasajiliwa kuingia kwenye gereza la Butimba waliniandikisha kwa jina gani ?

Mlalamikaji : Deogratius Kisandu

Don : Kwenye hii kesi imesajiliwa kwa jina lipi ?

Mlalamikaji : Don Nalimison

Don : Nenda ukamtafute Deogratius Kisandu, Don Nalimison hajawahi kutiwa hatiani na Mahakama yoyote ndani hata nje ya nchi.

Hakimu : Kesi imehairishwa hadi ushahidi wa kesi hii utakapokamilika, Mlalamikiwa ana sifa ya kugombea nafasi yoyote pasipo pingamizi.
 
[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Hata mitume walibezwa hivi hivi,
sasa anza kutafuta wafuasi polepole
tutakusikia tu muda si mrefu na kanisa lako lenye jina refu mpaka tunachelewa maombi kwa kusoma ubao wa jina la kanisa nje.

🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣Nakufa Mimi jamni🤣🤸🤸🤸🤸🤸🤸🤸🤸
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…