Taarifa ya ajali: Mwana JF mwenzetu Ushimen kapata ajali mbaya na sasa yuko Muhimbili hospital

Taarifa ya ajali: Mwana JF mwenzetu Ushimen kapata ajali mbaya na sasa yuko Muhimbili hospital

Na hii ndio taarifa yake

Habari ya asubuhi wana familia.

Sisi tunaumwa, nilipata ajali mbaya tarehe 5 October na ilionekana nimepata fracture kwenye mguu, siku tatu mbela ikaonekana nimepata clavicle dissociate (mfupa wa bega ulipishana.

Na nilimuona bingwa wa mifupa tukapata matibabu (arm sling na figger of 8).

Niliendelea kupata nafuu hadi tarehe 24 ghafla nilianza kupata maumivu mapya upande wa kulia kama kichomi kikali, tulipata rufaa na sasa tupo muhimbili Sewahaji 17 room 12.

Nimetobolewa pafu baada ya kugundilika lili pata kuvia dam na uzembe ulifanyika kwa kutokugundua tatizo hilo na nikakaa na shida hiyo kwa wiki 3.

Kwakifupi hatuendelei vizuri sana lakini nashkuru Mungu naendelea kutoa damu kwenye pafu na sasa nikama inatoa usaha.

Leo kuna vipimo tutafanya pamoja na kukaa na wataalam, kama ikiwa bora zaidi tunaweza sogea kwa nchi yenye wataalamu zaidi ili tupate kupona.

Naomba mtuweke kwenye maombi n Mungu atawabariki sana.

NB: Kwenye ajali hiyo mbaya iliyohusisha madereva wawili pamoja na Ushimen! Dereva wa kwanza ambaye ndie alisababisha ajali hiyo mbaya alikufa pale pale.. Dereva wa pili aliyekuwa na Ushimen alifariki siku tatu baadae

Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumuepusha ndugu yetu na kifo.. Tumuombee nafuu ya mapema
Pole yake
 
Wakuu.

Nimepata wasaa wa kupita MNH jioni hii na nimefika alipo ndugu yetu Ushimen

Kwanza sikuwa namfahamu kwa sura/hatukuwahi kuonana ana kwa ana. Yeye pia hivyo kama mimi.

Mwaka 2020 nilibadilishana naye contact hapa hapa JF tukaweza kuwasiliana nje ya hapa, since then, sikuwahi kupoteza namba yake.

Pamoja na kutaniana humu kama kawaida yetu ila nje ya JF haikuwa haba pia kwa mawasiliano.

Leo hii nimefika kumuona kwa mara ya kwanza na yeye kuniona kwa mara ya kwanza, cha kusikitisha yeye akiwa kitandani, ni mipango ya Muumba wetu.

Nimefurahi na yeye kafurahi pia kuonana naye hasa akiwa kwenye hali yake hii.

Kama Mshana Jr alivyoeleza hapo kwenye uzi, jamaa kaumia sehemu za bega(kwa ndani, hamna mchubuko kwa nje), Pafu( hapa ndio ilipo shida kubwa kwani liliathirika na kutiririsha damu na kujaa) ambapo kwa sasa kawekewa mpira wa kutoa hiyo Damu na maji maji.

Kwenye kuwezesha hayo maji yatoke analazimika kupush kwa kupuliza Pulizo(yaani anakaza/bana mbavu) ili mapafu yabane na kufanya maji yasukumwe yatoke kupitia mpira uliounganishwa. Tumuombee.

Wale ambao mtaweza na kupenda kwenda kumjulia hali, yupo Sewahaji 17, room/kitanda 12.
 
Na hii ndio taarifa yake

Habari ya asubuhi wana familia.

Sisi tunaumwa, nilipata ajali mbaya tarehe 5 October na ilionekana nimepata fracture kwenye mguu, siku tatu mbela ikaonekana nimepata clavicle dissociate (mfupa wa bega ulipishana.

Na nilimuona bingwa wa mifupa tukapata matibabu (arm sling na figger of 8).

Niliendelea kupata nafuu hadi tarehe 24 ghafla nilianza kupata maumivu mapya upande wa kulia kama kichomi kikali, tulipata rufaa na sasa tupo muhimbili Sewahaji 17 room 12.

Nimetobolewa pafu baada ya kugundilika lili pata kuvia dam na uzembe ulifanyika kwa kutokugundua tatizo hilo na nikakaa na shida hiyo kwa wiki 3.

Kwakifupi hatuendelei vizuri sana lakini nashkuru Mungu naendelea kutoa damu kwenye pafu na sasa nikama inatoa usaha.

Leo kuna vipimo tutafanya pamoja na kukaa na wataalam, kama ikiwa bora zaidi tunaweza sogea kwa nchi yenye wataalamu zaidi ili tupate kupona.

Naomba mtuweke kwenye maombi n Mungu atawabariki sana.

NB: Kwenye ajali hiyo mbaya iliyohusisha madereva wawili pamoja na Ushimen! Dereva wa kwanza ambaye ndie alisababisha ajali hiyo mbaya alikufa pale pale.. Dereva wa pili aliyekuwa na Ushimen alifariki siku tatu baadae

Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumuepusha ndugu yetu na kifo.. Tumuombee nafuu ya mapema
Mungu aweke uponyaji kwa ndugu yetu Ushimen

Pia salutation ya kusema SISI TUNAUMWA... ni gender queer?

WanaJF mlioko Dar pls mtuwakilishe
 
Back
Top Bottom