Taarifa ya Kusitisha huduma za Athuman Kapuya Foundation

Taarifa ya Kusitisha huduma za Athuman Kapuya Foundation

Dkt. Gwajima D

Minister
Joined
Nov 28, 2015
Posts
966
Reaction score
6,019
Wasaalam.

IMG-20240604-WA0076.jpg

4 Juni, 2024, Dodoma.
________________

Athuman Kapuya Foundation ni shirika lililosajiliwa mwaka 2021 ambapo, kwa kipindi chote limetekeleza matakwa ya kisheria ya uwasilishaji wa taarifa na kulipa ada.

Kwa mujibu wa usajili wao malengo waliyotekeleza na kupelekea hatua kuchukuliwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe Paul Chacha ni kinyume na Katiba waliyosajili na kinyume na Sheria ya Usajili wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali (Non-Government Organizations) (NGOs) ambayo imeweka bayana utekelezaji wa NGOs unatakiwa kuendana na mila na desturi za Taifa la Tanzania na sio vinginevyo.

Kutokana na upungufu huo, Ofisi ya Msajili kupitia Bodi ya uratibu wa Mashirika hayo tayari imesimamisha utendaji kazi wa shirika hilo kote nchini kupisha uchunguzi na hatua zaidi. Baada ya uchunguzi kukamilika wahusika watachukuliwa hatua zote stahiki kwa mujibu wa sheria.

Nachukua nafasi hii kumpongeza Mhe. Paul Chacha, Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa uratibu mzuri wa Mashirika yanayofanya kazi katika mkoa wake na kwa hatua alizochukua kama mamlaka kamili ya usimamizi wa shughuli za serikali ikiwemo wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake na makundi maalumu kupitia sera ya ugatuaji madaraka kwenda Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Uratibu huu makini ndiyo umepelekea kuibuliwa kwa madhaifu ya shirika hilo.

Hivyo, natoa wito kwa mamlaka zote za tawala za mikoa na mamlaka za serikali za mitaa kuendelea kuimarisha uratibu na ufuatiliaji na kuchukua hatua stahiki kwenye maeneo yao kwa mujibu wa sheria pale wanapoona kuna kukiukwa kwa sheria husika.

MWISHO.

Pia soma: Vitabu vinavyohamasisha mapenzi ya jinsia moja vyakamatwa Tabora
 
Mheshiwa, hatua hii ni njema na inastahili kabisa kuchukuliwa kwa nia ya kulinda utaifa wetu. Nipende tu kutoa wito, isiishie kwa hao tu. Kuna wale ambao wameshaathirika na jambo hili. Hao mashoga walioko mitaani, kama wizara mnachukua hatua gani? Yaani imefikia mahala wananchi wanajichukulia sheria mikononi, kwa vile tu wanaona kifanywacho ni aibu kwao na kwa taifa, lakini kama taifa, halichukui hatua stahiki.

Mfikirie yule aliyekatwa masikio huko Zanzibar na kisha kutelekezwa msituni, mfikirie yule askali ambaye alituhumiwa huko Zanzibar etc. Watu hao na wengine ambao kwa namna moja au nyingine wanajulikana, lakini hakuna hatua madhubuti za kuwadhibi. Inawezekana mnachukua hatua kimya kimya, lakini unfortunately matokeo ya hatua hizo hatuyaoni huku SITE. Hebu mfikirie yule Meneja wa Lamada aliyetajwa na akina Mwakyembe na kwmba amepongezwa kwa kuifanya hotel yake kuwa sehemu salama ya mashoga kufikia..!! Serikali imechukua hatua gani..!!??

YAANI WASIOJULIKANA WANAHITAJIKA HUKU NA SIO HUKO WALIKO..!!!!
 
Mheshiwa, hatua hii ni njema na inastahili kabisa kuchukuliwa kwa nia ya kulinda utaifa wetu. Nipende tu kutoa wito, isiishie

YAANI WASIOJULIKANA WANAHITAJIKA HUKU NA SIO HUKO WALIKO..!!!!
Mheshimiwa ukizingatia mamlaka ulizonazo nakuomba uliangalie swala ya wastaafu wazee wa kule tabora Kaliua ambao mpka sasa hawajalipwa pesa zao wanazungushwa tu. Kama itakupendeza naweza kutoa details zaidi privately. Ahsante
 
Hamjaeleza mnachunguza tuhuma zipi?
Ingia google andika Athumani Kapuya Foundation utaona kuna video ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe Paul Matiko Chacha akichambua yaliyojiri. Nimetoa kwa ufupi tu kuwa, tunaungana na Mkuu wa Mkoa kwenye taarifa yake na hatua alizochukua na sisi tunaendelea mbele kitaifa kupitia bodi ya usajili.
 
Kwanini mnasubiri mpaka tatizo liibuliwe hakuna mkakati wa luzuia kabla ya kutokea?
Watu wenye kutaka kufanya jambo tofauti mbona Wana mbinu nyingi na wengi wanadhibitiwa na wengine wanapenya lakini wanashikwa kama hivi. Mbona hata vibaka wanadhibitiwa na Polisi kata wengine wanapenya? Magonjwa yanadhibitiwa wengine wanaugua.

Wakiugua wengine wanapewa dawa zilezile mwingine anapona mwingine haponi. Hata kukamatwa Kwa Hawa ni ishara ya mifumo kufanya kazi. Tushirikiane maisha haya ni mapambano mwanzo mwisho....
 
Aisee hatari sana madame,
Haya Maswala yafuatiliwe kwa umakini maana kuna watu hua wanaficha taarifa na ushahidi kwa Rushwa na vitisho,
Maana kupitia hizo NGOs zao wanapata mafungu kutoka kwa wafadhili Washenzi kuendesha harakati za hovyo wakijificha kwenye kivuli cha Wahisani!
Kama Taifa tuwe makini!
Ahsante Sana kwa angalizo
 
Mheshiwa, hatua hii ni njema na inastahili kabisa kuchukuliwa kwa nia ya kulinda utaifa wetu. Nipende tu kutoa wito, isiishie kwa hao tu. Kuna wale ambao wameshaathirika na jambo hili. Hao mashoga walioko mitaani, kama wizara mnachukua hatua gani? Yaani imefikia mahala wananchi wanajichukulia sheria mikononi, kwa vile tu wanaona kifanywacho ni aibu kwao na kwa taifa, lakini kama taifa, halichukui hatua stahiki.

Mfikirie yule aliyekatwa masikio huko Zanzibar na kisha kutelekezwa msituni, mfikirie yule askali ambaye alituhumiwa huko Zanzibar etc. Watu hao na wengine ambao kwa namna moja au nyingine wanajulikana, lakini hakuna hatua madhubuti za kuwadhibi. Inawezekana mnachukua hatua kimya kimya, lakini unfortunately matokeo ya hatua hizo hatuyaoni huku SITE. Hebu mfikirie yule Meneja wa Lamada aliyetajwa na akina Mwakyembe na kwmba amepongezwa kwa kuifanya hotel yake kuwa sehemu salama ya mashoga kufikia..!! Serikali imechukua hatua gani..!!??

YAANI WASIOJULIKANA WANAHITAJIKA HUKU NA SIO HUKO WALIKO..!!!!
Ahsante kwa maoni nimekusoma
 
Back
Top Bottom