Tabia ya kuomba hela halafu ukishatumiwa husemi imefika au kutoa shukrani sio nzuri

Tabia ya kuomba hela halafu ukishatumiwa husemi imefika au kutoa shukrani sio nzuri

Tatizo mnakera mno ,unakuta mtu namba yako anaifahamu , majina yako unayotumia anayajua yote
Bado akituma hata dk kadhaa hazijapita anauliza umepata? Agrrr mnakera

Hela ya mtu haisubiri wewe upate matatizo. Akikupa ujue amedivert mipango, ameona jambo lako ni muhimu. Shukuru hata kwa Hilo.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo mnakera mno ,unakuta mtu namba yako anaifahamu , majina yako unayotumia anayajua yote
Bado akituma hata dk kadhaa hazijapita anauliza umepata? Agrrr mnakera
Utetezi wa kitoto sana huu.

Kwa mantiki hii unaweza kupoteza fedha nyingi sana kwa uzembe, nakusimulia kisa kimoja utajifunza umuhimu wa kumjulisha mtumaji kwamba pesa imefika.

Siku moja nikiwa nafanya transaction ya laki 3 kwenda kwa jamaa yangu aninunulie kitu flani hapo kwa Makonda, tulisha chat WhatsApp tukakubaliana fresh, sasa wakati nataka kutuma nikampigia simu, yeye tayari yuko K/Koo anasubiri pesa iingie atoe, nikamuuliza nitume namba ipi maana ana namba nyingi na zote zimesajiliwa akanitajia.
Nikatuma, kumbe kwa bahati mbaya ile namba ilikua imepotea ina mwezi mzima na hajairudisha sasa alisahau kuniambia, nimetuma pesa nimekaa nusu saa nikampigia kujua kama ameshanunua mzigo anasema bado hajapata muamala, nikascreenshot ile msg nikatuma WhatsApp lakini kwake haijafika, sasa tumelumbana sana baada ya muda akabaini namba niliyotuma pesa ilishapotea.

Kwahiyo nikaenda Tigo pesa kushughulikia pesa irudi sikutaka kusubiri yale masaa 24 kutokana na kubanwa na shida niliyokuwa nayo.
Sasa kwa mfano ningekaa kimya je huyo jamaa angeendelea kusubiri kwa muda gani? Pamoja na kwamba jina lilitoka jina lake.

Muungwana ukitumiwa pesa toa mrejesho, maana mtu anaweza kutuma kupitia wakala sasa yuko dukani anasubiri umjibu we unakausha, na kuna wakati mwingine miamala huwa inafeli sasa kutoa mrejesho ni muhimu. Hicho ni kitendo cha uungwana tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hatufundishi watoto kushukuru wanaposaidiwa. Wakiwa watu wazima hivyo hivyo, hawashukuru kwa kitu chochote. Kila kitu wanaona ni haki yao tu. Siyo kwako tu. Inatokea mara nyingi sana. Hata wanaojiita wasomi ni hivyo hivyo. It is sad.
Ni kweli mtoto unampa kitu anapokea na kuondoka kama vile bata anayedonoa, tabia mbovu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni tabia mbaya ya wazazi ambayo tunarithisha watoto na wao kurithisha watoto wao. Mtoto hawezi kuzaliwa akijua kushukuru. Ni lazima afundishwe.
Ndiyo hivyo kutofundishwa kushukuru, nyumbani tu watoto wakimaliza kula chakula lazima wamshukuru mpishi kwa chakula, na chochote anachopewa lazima atoe asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuwafundishe watoto kushukuru, akijua thamani ya neno asante hatasahau hata akija kuwa mkubwa. Matatizo mengine tunatengeneza wenyewe, unampa pipi mfundishe kushukuru, mwombe akupe nawe sema asante.

Lakini pia, tusipende kuwa on the receiving end.
 
We ukishatuma kazi yako imeisha, unataka uambiwe imefika kwani hujahakiki namba au hujapokea ujumbe kuwa ‘imethibitishwa’... hela yenyewe shingapi basi..!!

Ukipewa usisahau, ukitoa toa bila kukumbuka... usingoje shukrani.
 
"Ukitoa sahau, Ukipokea usiache kukumbuka"

Fid q.


"Tenda wema nenda zako usingojee shukrani"


Wahenga.
 
Back
Top Bottom