Tabia ya wachaga kurudi kwao Kilimanjaro kila ifikapo mwisho wa mwaka ni jambo zuri na la kuigwa na makabila mengine

King Jody

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2022
Posts
1,834
Reaction score
3,456
Niwapongeze sana wachaga kwa utaratibu wao wa kukutana kila ufikapo mwisho wa mwaka,
Sababu zao kukutana ni kama ifutavyo

1. Kukutana na kuonana live ndugu jamaa na marafiki baada ya kupotezana kwa takribani mwaka mzima kwenye harakati za utafutaji.

2. Kusherehekea kumaliza mwaka salama kwa kula nyama na kunywa mbege kwa wingi

3. Kuwapiga taff wenzao ambao hali zao kimaisha hazijatengemaa

4. Kufanya mambo ya kimila nk.

Najua yapo mengi ila leo nimetaja baadhi, kama kuna mengine unaweza kuongezea.

Mimi si mchaga lakini nawaonea wivu sana wachaga kwa tabia hii ya ushirikiano, kwani umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, Hii ni tofauti kabisa na makabila mengine.

Natamani kuwajengea wanangu haka katabia ili wakikua waishi kwa Kupendana na kushirikiana.

NB: Kama wewe ni mchaga popote ulipo hongera sana.
 
Tangu niliposafiri ndipo nimegundua huu utaratibu ni mzuri sanaa aisee

Nipo South Africa,

Nili stay kwa miaka 4 Bila kurudi nyumbani aisee nilikuwa naumwa kichwa kila siku yaani kwa mawazo na stress isitoshe kipato nilikuwa napata cha kawaida sanaa nilipoamua kujenga utaratibu wa kurudi nyumbani na kufanya Safari tena ya kurudi South Africa niliona faida zake sasa hivi haijalishi nna kiasi gani?

Kidogo au kikubwa kila baada ya miaka miwili nimejiwekea narudi nyumbani kwanza kwenda kujitafakari then nasafiri tena kuja South Africa ni utaratibu ambao una faida sana kisaikologia na vinginevyo
 
Issue sio kurudi kwenu, issue ni unarudi kwenu kufanya nini, kuna nini, utakuwa na nani na unaendaje?

Kama hujui tu, fahamu haya;
1. Wachaga wanaorudi kwao December huko kwao wamejenga miji, tena miji ya uhakika. Hivyo for real wanakwenda kwao.

2. Sehemu kubwa huwa wanakwenda kutambika pia. (Ukishaona uchagani kuna kaburi nyumbani la mzee, kuna kuchinja halafu kufa na kupona ukoo umepambana kurejea December, ijue kwa 90% kuna tambiko (ulozi/uchawi/kuloga) unless ni walokole ambao hawatafanya hayo).

3. Wachaga wanaorudi kwao December ujue wana ndugu wa karibu kama wazazi wapo huko na ndugu zao wengine wa karibu watakuja December. Ni ujamaa ideology.

4. Safari ya December kurudi uchagani ni safari ya gharama kubwa kifamilia, ni lazima mfukoni uwe vizuri au ujipange kwa muda mrefu na kujinyima vilivyo.

Mwisho kabisa, huu utamaduni hata uchagani umepungua sana, karibu 50% ya wachaga hawarudi tena makwao December ukilinganisha na miaka 20 iliyopita.
 
Issue sio kurudi kwenu, issue ni unarudi kwenu kufanya nini, kuna nini, utakuwa na nani na unaendaje?

Kama hujui tu, fahamu haya;
1. Wachaga wanaorudi kwao December huko kwao wamejenga miji, tena miji ya uhakika. Hivyo for real wanakwenda kwao.

2. Sehemu kubwa huwa wanakwenda kutambika pia. (Ukishaona uchagani kuna kaburi nyumbani la mzee, kuna kuchinja na kufa na kupona ukoo umepambana kurejea December, ijue kwa 90% kuna tambile unless ni walokole).

3. Wachaga wanaorudi kwao December ujue wana ndugu wa karibu kama wazazi wapo huko na ndugu zao wengine wa karibu watakuja December. Ni ujamaa ideology.

4. Safari ya December kurudi uchagani ni safari ya gharama kubwa kifamilia, ni lazima mfukoni uwe vizuri au ujipange kwa muda mrefu na kujinyima vilivyo.

Mwisho kabisa, huu utamaduni hata uchagani umepungua sana, karibu 50% ya wachaga hawarudi tena makwao December ukilinganisha na miaka 20 iliyopita.
 
Mkuu,
Jamii iliyo na maendeleo lazima wakumbuke nyumbani kwao ila jamii za kimaskini nikurogana na ushirikina dats why Kuna jamii hazipendi kwenda ma kwao....

Chagga's ni Moja ya highly & mosted civilized tribes in Tanzania
 
Mkuu,
Hii comment yako imemaliza Kila kitu yaan case closed 🔒🔐
 
Kwenda kusalimia ndugu na jamaa na kifurahi nao ni jambo jema.

Ila hapo kwenye kufanya Mila no 4, Kwa Waliookoka, ni MARUFUKU!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…