Tabia ya wasajili laini kutumia vitambulisho vya watu bila wenyewe kujua kusajilia watu wengine zaidi ni hatari

Tabia ya wasajili laini kutumia vitambulisho vya watu bila wenyewe kujua kusajilia watu wengine zaidi ni hatari

MR LINKO

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2016
Posts
3,034
Reaction score
3,526
Habari wakuu natumaini mko poa wote,

Iko hivi kuna kipindi nilipoteza simu yangu ya smart pamoja na laini yani niliibiwa sasa nikakaa kama mwezi maana simu nilikuwa naona sehemu ilipo nikaamini nitaipata baadae nikaja nikakata tamaa nikaona isiwe kesi ngoja nirudishe laini zangu.

Siku nimekaa nikamuona mtu anasajili line za tigo na airtel kwa bei nzuri nikaamua kusajili upya line zangu zote zilizo potea na simu sasa hichi ndo kisa nimeamka nacho asubuhi.

Leo nikaamua kuangalia namba ambazo zimesajiliwa na kitambulisho changu cha nida namba nilizoziona mpaka nika shangaa nimekuta line ya tigo ina number 4 wakati tigo niko na line mbili. Airtell nina line moja nimekuta nina line 2 haloteli sina nimekuta nina line ya halotel kasoro voda tu ndo nimekuta iko salama.

SWALI: hawa watu huo mchezo wanao ufanya umenikera sana kumbe unawapa number ya nida akija mtu mwingine na wao wana sajili kwa kitambulisho chako.

Tena kitu ambacho sio sahihi na hili swala limeongelewa sana kuhusu kumsajilia mtu line kwa kitambulisho cha mtu kuwa ni kosa. Ningekuwa na uwezo wa kuwa shtaki sikufichi leo ninge anza process zote na nijue huyo msajili line kwanini alifanya hivyo.

N:B Penda kuangalia kama mimi yaweza kuwa una number zaidi ya 7 bila kujijua na nimepanga naenda kuzifungia line zote bila huruma kama kuna mtu alikuwa anatumia line yangu atajua hajuii.

Nawasilisha.
 
Sidhan kama namba ya nida tu inamtosha kusajili line zngine bila ww kutia kdole.

Mara nyng wakiwa wanakusajilia wanajifanya mtandao unazngua, afu wanakwambia weka tena kdole, pale ndo wanakua wanasajili line ya pili kwa kidole/nida yako.
 
Sidhan kama namba ya nida tu inamtosha kusajili line zngine bila ww kutia kdole.

Mara nyng wakiwa wanakusajilia wanajifanya mtandao unazngua, afu wanakwambia weka tena kdole, pale ndo wanakua wanasajili line ya pili kwa kidole/nida yako.
Afate huu ushauri
 
Habari wakuu natumaini mko poa wote.

Iko hivi kuna kipindi nilipoteza simu yangu ya smart pamoja na laini yani niliibiwa sasa nikakaa kama mwezi maana simu nilikuwa naona sehemu ilipo nikaamini nitaipata baadae nikaja nikakata tamaa nikaona isiwe kesi ngoja nirudishe laini zangu.
Hyo ni michezo yao ya kitambo vile anavokwambia weka gumba vzr ndo lain zinasajiliwa ivoo
 
Mm huwa naenda kufungia laini mpaka halotel kigoma wameshanizoea

•Jamaa wa ikulu siku zako zinahesabika
 
Back
Top Bottom