Tabia ya Watanzania ya kuzaa hovyo ndiyo chanzo cha umaskini. Bodaboda ana watoto sita! Hata Serikali inashindwa kupanga mipango

Tabia ya Watanzania ya kuzaa hovyo ndiyo chanzo cha umaskini. Bodaboda ana watoto sita! Hata Serikali inashindwa kupanga mipango

Hii nchi hatuna tatizo la over population na istoshe shule Bure mpaka fomusikisi!! Wacha walume ngangari tupige shoo tuijaze nchi.
Nchi inahitaji watu hatakama si wasomi watachunga na kulima hko maporini
 
Kwanini awe bodaboda? Tuanzie hapo, kwanini hafanyi kazi kiwandani alipwe milioni kuanzia, 15M mpaka 26M kwa, mwaka?
Hao, watoto sio, shida,
Chanzo ni ccm, badala, ya, kujenga, viwanda wananunua v8, moja ni milioni 400!
Viwanda vitajengwa na pvt sector,
Hii akili ya kuwaza serikali ijenge viwanda wew ukaajiriwe, kwanini usiwaze wew ujenge kiwanda kama umeona gap?
 
Waswahili ukiwakuta kwenye mada za kuwakosoa na kuwalaumu viongozi wao utasema ni watu walio siriasi sana! Wakute kwenye mada kama hizi zinazowawajibisha na wao ndipo utathibitisha kuwa wao na viongozi wao ni chupa na mfuniko tu (in case ulikuwa hujathibitisha).

Comments za humu zinamtambulisha mtanzania halisi. Imagine wengi wanamhoji mtoa mada kama watu hao wanaozaa sana wanamwomba chakula! Kweli?!

Katika mada zinahitaji utulivu wa akili na kuweka mihemko pembeni basi mojawapo ni hii, ila sasa yaliyomo...

Tuna safari ndefu sana.

Population kubwa isiyo na faida ina hasara nyingi. Kuna hasara za moja kwa moja (direct) na hasara zisizo za moja kwa moja (indirect).

Mfano wa hasara zisizo za moja kwa moja ni kuendeleza utawala wa 'hovyo'. Unadhani mtu aliye busy na stress za malezi ya watoto wengi kama shule atapata lini muda wa kufuatilia na kujua kama utawala unafaa au haufai? Ni kama waalimu tu, wapo busy na watoto muda wote hawajui kama ccm inatuhenyesha ukifika uchaguzi ni kutia tick tu kwenye karatasi za kura mle ndani kama vile wanasahihisha mitihani ya watoto, na maisha yanatupiga wote wala hawajali. NATANIA walimu.
 
Mtoa mada bado hujaona, njoo huku Sumbawanga uone kilimo Cha watoto.
Wanazidi usukumani?

Juzi dogo kaoa usukumani. Pale kwenye harusi babamkwe kapewa nafasi kutoa neno kama mzazi anawasisistiza sana bintiye na mkwewe wafyatue hadi mayai yaishe! Tulibaki midomo wazi.

Usukumani ni wanazaliana haswa, zahanati na vituo vya afya kule vipo busy 24/7
 
Umewagusa penyewe wabongo wapenda ngono.
Na kumbuka starehe ya masikini wengi ni ngono tu, pesa za kwenda kutalii hana, kupumzika mahali penye hewa safi hana, kula vizuri pesa hana, kununua vitabu apate maarifa pia pesa na akili hiyo hana.

Wameleta smartphone za bei rahisi hadi 50k unapata smartphone ila matumizi ndio hola, zaidi zaidi ni kuhamasishana ngono ngono ngono tu.
Na ukizingatia ndio starehe yake basi majibu unayapata kwa huyu masikini kua na lundo la watoto.

Kuna watoto wengi mno hawawajui baba zao hasa kipindi hiki maana mama anadinywa hovyo, baba anachovya na kusepa mahali pengi pengi wala hajui kama kuna mahali kaacha mbegu.

Pole sana Tz.
 
Uko sahihi kabisa, kuna jirani yangu hapo ni bodaboda, anaishi kwenye ibada cha mlinzi wa siye na ana watoto wengi sana mpaka nashindwa kujua humo ndani walala kivipi kwani wengine wamekuwa wakubwa. Maskini na wajinga wengi wa nchi hizi faraja yao ni katika ngono zembe na ndio maana huko uswazi utakuta vitoto vimejazana kwenye mabanda

Walidanganywa na msemo wa "kila mtoto anakuja riziki yake."
 
Duh! Umepanic.
Achana nao..fanya yako

Hiyo inatuathiri wote. Wee unafikiri asilimia kubwa ya panya rodi wanatoka wapi? Wengi wao ni watoto waliokosa malezi. Mtoto anaweza asipewe mahitaji yake ya msingi, matokeo yake wanakuwa chokoraa mtaani.
 
Wacha watu wazae vije vizazi vipya vya kuikomboa Tanzania Kama China na Nigeria. Sio kizazi hichi cha Simba na yanga pumbavu zako mwana Ccm wewe.

Shida ni aina ya watu mnaowazaa na jinsi ya kuwaandaa. Siyo kila mtoto mnayemzaa ni kifaa kwa nchi. Wengine ni mzigo kwa taifa.
 
Umaskini na kuwa na familia kubwa Haina huusiano! Serikali iweke sera nzuri za uchumi na wananchi wawajibike kufanya Kaz Kwa bidii.. Bodaboda uliyemtolea mfano kwamba anaextended family pengine kuzidi wewe mtumishi.Lakini wewe mwenye mtoto mmoja unakuta life limekupiga..
Angalia hata nchi zenye uchumi mkubwa halafu check na population zao..kifupi kuzaa ni source ya utajiri kama we mzaaji utakuwa serious na life
 
Angalia na ukubwa wa nchi. Chanzo cha umasikini Ni kurundikwa mjini wakati nchi bado ina nafasi za kutosha
945,087 sq.km 86,610,000 hectares. Kila MTU angekuwa na ardhi kusingekiwa na biashara ya kuuza kila moja angefikiria kuendelea. Tungekiwa mbali.
Tuko kwenye kikao tunafikiria kutenga kaeneo kengine kwaajili ya ifadhi ndogo ya taifa tupate cheti cha utunzaji WA mazingira!!!!
 
Enzi hizo walikuwa Kama hapa kwetu na baadhi walikuwa wameshadogea katika mawazo yako. Ama huelewi sie tuko nyuma mno kwao.pia Kama hizo ardhi zipo bado,huko katavi Kuna mapori hayajawahi limwa since creation na huko congo msituni Kuna miti haijawahi kukatwa tokea kuumbwa . Ni wewe tu huko kwao Kila mahala Kuna zege

Kwa hiyo unataka tufikie hatua hiyo ya kulamba kila kitu ndo tusituke.
Shida tuliyonayo kama taifa, asilimia kubwa ya watanzania ni wajinga. Wanakosa hata elimu ya msingi ya kujisimamia katika maisha, kutia ndani kuzaa bila mpangilio. Mtu anajikuta ana watoto 6. Hata ukimuuliza kama alikuwa na mpango wa kuwa na watoto 6. Atakujibu hajui na kumsingizia Mungu kwamba ni mipango yake.
 
Waswahili ukiwakuta kwenye mada za kuwakosoa na kuwalaumu viongozi wao utasema ni watu walio siriasi sana! Wakute kwenye mada kama hizi zinazowawajibisha na wao ndipo utathibitisha kuwa wao na viongozi wao ni chupa na mfuniko tu (in case ulikuwa hujathibitisha).

Comments za humu zinamtambulisha mtanzania halisi. Imagine wengi wanamhoji mtoa mada kama watu hao wanaozaa sana wanamwomba chakula! Kweli?!

Katika mada zinahitaji utulivu wa akili na kuweka mihemko pembeni basi mojawapo ni hii, ila sasa yaliyomo...

Tuna safari ndefu sana.

Population kubwa isiyo na faida ina hasara nyingi. Kuna hasara za moja kwa moja (direct) na hasara zisizo za moja kwa moja (indirect).

Mfano wa hasara zisizo za moja kwa moja ni kuendeleza utawala wa 'hovyo'. Unadhani mtu aliye busy na stress za malezi ya watoto wengi kama shule atapata lini muda wa kufuatilia na kujua kama utawala unafaa au haufai? Ni kama waalimu tu, wapo busy na watoto muda wote hawajui kama ccm inatuhenyesha ukifika uchaguzi ni kutia tick tu kwenye karatasi za kura mle ndani kama vile wanasahihisha mitihani ya watoto, na maisha yanatupiga wote wala hawajali. NATANIA walimu.
Tena watu wa hivi Tanzania wapo wengi waliosoma na ambao hawajasoma,hawaelewi ni kwa namna gani kutofatilia mambo basic katika nchi yanavyogharimu nchi.tuna population kubwa iliyojaa wajinga.
Yani ni kazi sijui ni nini kifanyike kwa kweli.
 
Nenda kamuombe mungu radhi!

Hakuna kiumbe wa Mungu aliezaliwa hovyo hovyo kama unavyodhani na elimu hii ya kizungu ilivyokupotosha sana!

Kila kiumbe unachokiona chini ya jua Mungu alipanga kiwepo kabla misingi ya ulimwengu kuwepo!

Tupo katika zama ambazo janga moja tu linaua mamilioni ya watu popote pale Duniani,uwepo was uzao mwingi ni maandalizi ya nature muelekeo wa ku balance ecosystem!
 
Umaskini na kuwa na familia kubwa Haina huusiano! Serikali iweke sera nzuri za uchumi na wananchi wawajibike kufanya Kaz Kwa bidii.. Bodaboda uliyemtolea mfano kwamba anaextended family pengine kuzidi wewe mtumishi.Lakini wewe mwenye mtoto mmoja unakuta life limekupiga..
Angalia hata nchi zenye uchumi mkubwa halafu check na population zao..kifupi kuzaa ni source ya utajiri kama we mzaaji utakuwa serious na life
Siyo kweli mkuu, tuache kufarijiana. Raia bora huanza kuandaliwa tangu kutungwa mimba yake. Lishe bora, malazi mazuri na elimu bora ndiyo hujenga raia mpambanaji na mwenye kipato kizuri.

Unaendesha boda, ni barmaid, machinga, n.k kipato laki 2 kwa mwezi halafu una watoto 6! Hapa lazima mlo uwe mmoja kwa siku, kulala ni sakafuni, watoto full stress tangu wadogo. Hata mazingira ya utulivu ya kujisomea hawatayapata. Matokeo yake mateja, walevi na wezi wanatokea.

Unplanned family= Poverty.
 
Back
Top Bottom