Tabia ya Watanzania ya kuzaa hovyo ndiyo chanzo cha umaskini. Bodaboda ana watoto sita! Hata Serikali inashindwa kupanga mipango

Tabia ya Watanzania ya kuzaa hovyo ndiyo chanzo cha umaskini. Bodaboda ana watoto sita! Hata Serikali inashindwa kupanga mipango

Acheni uvivu fanyeni kazi na familia zenu mtazimudu bila kutegemea serikali.Ila mkiwa wavivu mtalalamikia kuzaa ovyo na umaskini hautapungua bila kuchukua hatua stahiki za kufanya kazi kwa bidii na kuheshimu uumbaji wa Mwenyezi Mungu.

Hizo zama za kufanya kazi sana, bila kuwa na mipango ya maisha zilipitwa na wakati.
Mkizishikilia sana mtakufa masikini
 
Kwa mwendo huu hakuna rais atakayeweza kuumaliza umaskini wa nchi hii.

Ili twende sawa nitoe tafsiri ya umaskini kwa mujibu wa IMF:- umaskini ni hali ya kukosa huduma za afya/maji, chakula, elimu na mahala pazuri pa malazi (nyumba bora).

Kwa tafsiri hii, na kwa uzazi holela wa hapa nchini, ni lini kila mtanzania atakuwa na uwezo wa kuwa na nyumba bora, uwezo wa kupata huduma za afya aitakayo kwa bima ama fedha yake, uwezo wa kupata milo 3 bila shida yoyote?

Unakuta bodaboda ana watoto 6? Mama ntilie, machinga na barmaid eti nao wana familia kubwa? Nchi hii tunaenda wapi? Watu waelimishwe kuwa, siyo kila mtu lazima azae. Watoto siyo asset kwamba utakopea mkopo.

Serikali ikijenga shule ama zahanati, miaka 2 tu zimezidiwa na idadi ya watu. Hata madawati yanakuwa tatizo kila mwaka kwasbb watanzania wanafyatua watoto mno. Hakuna kitu kinawezekana bila family planning.

Dkt. Slaa alipokuwa balozi Sweden alisema "Tanzania na Sweden zilikuwa na idadi sawa ya watu mwaka 1961 (milioni 9 kila moja). Hivi sasa Sweden ina watu 15M, wakati Tanzania ina watu 60+M". Hii ni hatari.

Kwa ujinga huu wa kuzaa hovyo umaskini hautatuachia. Watu milioni 60, walipa Kodi 2M !!!

Itungwe sheria, mtu akitaka kuzaa aweke milioni 10M benki kama dhamana ya malezi bora ya mtoto.

Vinginevyo, shika, peleka akafungwe.
ulishawalisha??
 
Masikini hujisifia ngono huku wakisema wenye hela ni tia maji tia maji kwa upande huo, sasa kimbembe huyu masikini (ambaye ki uhalisia sio masikini wa nguvu, ila ni maskini wa Ubongo na fikra) anapo fikisha watt saba waanze kuparangana ndio utamwonea huruma.
 
Trump ana 5......tajiri la kutupwa. Halafu boda ana 6.

George Bush anaye momoja tu, wewe wa kwa Mtogole unao 6.

Obama ana 2 tu....wewe kinyozi unao 8.

Bill Clinton anaye mmoja tu ...wewe muuza nyanyaunao 20
Hao ni Wale official ambao wewe unawajua. Laiti kama ungekuwa una ukaribu nao kama huo ulionao na hao bodaboda Hadi ukajua idadi za watoto walionao, ungekuja kufuta hii siledi
 
Kama hawajakufuata kukuambia uwasaidie kuwalelea watoto wa basi waache hangaika na yako
 
Mi huku nilipo wanaomba hadi sukari, unga mara mboga yaani shida hadi njiti za kiberiti, huwa najiuliza sana wamezaa watoto wengi wa nini sasa hata kuwahudumia ni shida
Bora hao wanaomba, huku wanaiba mpk ndala msikitini
 
Mkuu hayo ndo mawazo yaliyotufikisha hapa tulipo. Kuishi kwa bahati nasibu. Bro maisha ni kupanga na kupanga ni kuchagua.
Sasa una uhakika gani kwamba huyo mwenye watoto wengi alipanga na alichagua? Hatuwezi kulingana vyanzo vya kutafuta furaha na hamasa katika maisha. Kimsingi kila mtu ashinde mechi zake.. unless alikufata kukuomba umsaidie kupanga chumba kingine kimoja kwaajili ya kuwaweka watoto wake walale, otherwise kila mtu ashinde mechi zake.
 
Wanazidi usukumani?

Juzi dogo kaoa usukumani. Pale kwenye harusi babamkwe kapewa nafasi kutoa neno kama mzazi anawasisistiza sana bintiye na mkwewe wafyatue hadi mayai yaishe! Tulibaki midomo wazi.

Usukumani ni wanazaliana haswa, zahanati na vituo vya afya kule vipo busy 24/7
Huko sumbawanga, mpanda, mlele, mpimbwe sijui Tanganyika wasukuma wamejaa na ndio wanazaliana sana kuliko wafipa
Acheni kabisa
 
Tuseme masikini anapenda ngono kuliko tajiri. Mawazo yake yote ni ngono na sio uchumi. Bara la Afrika masikini wapo wengi sana ndio maana ongezeko la watu ni kubwa.
 
Back
Top Bottom