Tabia ya wazazi kukataa wachumba kisa ukabila ikomeshwe

Tabia ya wazazi kukataa wachumba kisa ukabila ikomeshwe

Mallia

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2018
Posts
437
Reaction score
1,562
Hii tabia ya chafu ya kupeleka wenza nyumbani alafu wazazi wanamkataa mtu uliyempeleka imepelekea vijana wengi kuingia kwenye mahusiano ya ndoa na watu ambao sio machaguo yao na ndio maana ndoa za sikuhizi hazidumu, unakuta mtu ni mchaga basi kisa wazazi wake wanataka wachaga wenzao anamuacha labda binti mzuri wa kabila lingine ambae ukute wamesota wote alafu anaskiliza wazazi anachagua mtu wa kabila lake mwishiwe ndoa zinakufa

Naongea haya sababu yametokea ndani ya familia yangu , niliwahi chumbiwa na mwanaume ambae nilitoka nae mbali sana, kipindi ambacho nimemaliza chuo akaleta barua nyumbani, mwanaume ni mtu wa Dodoma mgogo, wazazi wakamkataa kabisa kisa mkoa anaotoka, wakajakunyoosha mikono juu baada ya mimi kupata ujauzito wa huyo mwanaume, wakamuita haraka na Ndoa ikafungwa haraka haraka bila kupenda na leo ni mwaka wa 11 ndoa ina amani tele

Mdogo wangu wa kiume anaefuta hivyo hivyo akapeleka mwanamke wa kabila tofauti , wakakaa kikao wakamkataa eti hilo kabila halifai kuoa mwisho wa siku akalazimishwa kuowa mtu wa nyumbani, kweli akampata na kumpeleka but si mtu ambae alikuwa moyoni ni basi tu, ndoa ikafungwa , mimba ya kwanza ikakutwa mwanamke ana VVU, kaka akachanganyikiwa, akapimwa zaidi ya mara tatu kwa miezi tofauto akakutwa yupo salama, yule mwanamke ugonjwa alipoutoa haikujulikana

Kikawekwa kikao kiamue mustakabali wa ndoa, wale wale mashangazi waliomkataa mwanamke wa kwanza ndio hao hao wakalazimisha ndoa ivunjwe eti hawataki kaka afe mapema, wakapiga majungu ndoa ikavunjwa sasa hivi wametengana, kaka kuja kushtuka yule mwanamke aliyekataliwa nyumbani kashaolewa na mtu mwingine na maisha yanaendelea vizuri tu

Juzi tena mdogo wangu wa mwisho wa kiume kapeleka taarifa za kutaka kuowa binti wa singida huko nae vile vile ni mtu ambae wanafahamiana tokea shule hadi kutafuta maisha wamesaidiana, home wamemkataa , huyu mdogo wangu wa mwisho ndio kacharuka kabisa ,kawaambia anaowa yeye hawaowi ndugu kwa hasira akaondoka hajarudi tena

Sasa kwa tabia kama hzi vijana mnaotarajia kuowa or kuolewa kuweni makini sana na ndugu , usishinikizwe na mtu kuchagua mtu wa maisha yako, mwanamke au mwanume wa maisha yako ni wewe mwenyewe unamjua,

Ukiowa mwanamke mshenzi kisa ndugu wanamtaka,jua mabalaa yatakukuta wewe hao ndugu watakuwa wanaskia tu huko japo walikuwa mstari wa mbele kukushinikiza, oa au olewa na mtu ambaye umemuelewa na amekuelewa na unajua kumdhibiti na mnaweza kuishi kwa amani na upendo, usioe kabila kama kigezo mtakuja kulia.
 
Uwaambie wazazi wako wakuletee mchumba watakayeweza kuishi nao wao.
Inaonekana wanataka watakaoweza kuishi na wazazi na sio mtu wa kuishi na watoto wao.
Poleni! Wakasema mgogo ombaomba na wezi wa ng'ombe!😆

Everyday is Saturday.............................. 😎
 
iyo ilisha wai nikuta musoma nilizaa na mdada wa kikulya tukapanga kwenda kujitambulisha kufika kwao wamenikataa kisa mm mfupi binti alizimika mazima wakampa kitisho ukilazimisha litakalo kukuta usije uka2tambua kama sisi wazazi wako binti alichukua maamuzi magumu sana
 
Hii tabia ya chafu ya kupeleka wenza nyumbani alafu wazazi wanamkataa mtu uliyempeleka imepelekea vijana wengi kuingia kwenye mahusiano ya ndoa na watu ambao sio machaguo yao na ndio maana ndoa za sikuhizi hazidumu, unakuta mtu ni mchaga basi kisa wazazi wake wanataka wachaga wenzao anamuacha labda binti mzuri wa kabila lingine ambae ukute wamesota wote alafu anaskiliza wazazi anachagua mtu wa kabila lake mwishiwe ndoa zinakufa

Naongea haya sababu yametokea ndani ya familia yangu , niliwahi chumbiwa na mwanaume ambae nilitoka nae mbali sana, kipindi ambacho nimemaliza chuo akaleta barua nyumbani, mwanaume ni mtu wa Dodoma mgogo, wazazi wakamkataa kabisa kisa mkoa anaotoka, wakajakunyoosha mikono juu baada ya mimi kupata ujauzito wa huyo mwanaume, wakamuita haraka na Ndoa ikafungwa haraka haraka bila kupenda na leo ni mwaka wa 11 ndoa ina amani tele

Mdogo wangu wa kiume anaefuta hivyo hivyo akapeleka mwanamke wa kabila tofauti , wakakaa kikao wakamkataa eti hilo kabila halifai kuoa mwisho wa siku akalazimishwa kuowa mtu wa nyumbani, kweli akampata na kumpeleka but si mtu ambae alikuwa moyoni ni basi tu, ndoa ikafungwa , mimba ya kwanza ikakutwa mwanamke ana VVU, kaka akachanganyikiwa, akapimwa zaidi ya mara tatu kwa miezi tofauto akakutwa yupo salama, yule mwanamke ugonjwa alipoutoa haikujulikana

Kikawekwa kikao kiamue mustakabali wa ndoa, wale wale mashangazi waliomkataa mwanamke wa kwanza ndio hao hao wakalazimisha ndoa ivunjwe eti hawataki kaka afe mapema, wakapiga majungu ndoa ikavunjwa sasa hivi wametengana, kaka kuja kushtuka yule mwanamke aliyekataliwa nyumbani kashaolewa na mtu mwingine na maisha yanaendelea vizuri tu

Juzi tena mdogo wangu wa mwisho wa kiume kapeleka taarifa za kutaka kuowa binti wa singida huko nae vile vile ni mtu ambae wanafahamiana tokea shule hadi kutafuta maisha wamesaidiana, home wamemkataa , huyu mdogo wangu wa mwisho ndio kacharuka kabisa ,kawaambia anaowa yeye hawaowi ndugu kwa hasira akaondoka hajarudi tena

Sasa kwa tabia kama hzi vijana mnaotarajia kuowa or kuolewa kuweni makini sana na ndugu , usishinikizwe na mtu kuchagua mtu wa maisha yako, mwanamke au mwanume wa maisha yako ni wewe mwenyewe unamjua,

Ukiowa mwanamke mshenzi kisa ndugu wanamtaka,jua mabalaa yatakukuta wewe hao ndugu watakuwa wanaskia tu huko japo walikuwa mstari wa mbele kukushinikiza, oa au olewa na mtu ambaye umemuelewa na amekuelewa na unajua kumdhibiti na mnaweza kuishi kwa amani na upendo, usioe kabila kama kigezo mtakuja kulia
Naungua mkono wazazi wanaona mbali kama ili kabila la kutoka uko milimani sio la kuoa tena ukikuta single maza ndio inakuwa promax, mzazi anajua unaenda kutafuta kifo kwa fast charging.

Sent from my 601SO using JamiiForums mobile app
 
Jirani yetu alipeleka mchumba nyumbani ni binti walikutana UDSM alikataliwa walitaka wa kabila Lao. Yule kaka alipata break down, baada ya maombi na tiba alifanikiwa kukaa sawa na kuendelea na ajira.

Alimpata wa kabila lake lakini hata siku moja hutawaona pamoja. Kanisani kila mtu anakwenda misa yake, mke ni wale wamama wa khanga kiunoni masaa 24, jamaa brother men kwa sana.
 
Jirani yetu alipeleka mchumba nyumbani ni binti walikutana UDSM alikataliwa walitaka wa kabila Lao. Yule kaka alipata break down, baada ya maombi na tiba alifanikiwa kukaa sawa na kuendelea na ajira.

Alimpata wa kabila lake lakini hata siku moja hutawaona pamoja. Kanisani kila mtu anakwenda misa yake, mke ni wale wamama wa khanga kiunoni masaa 24, jamaa brother men kwa sana.
Hahahahah kuna jamaa aliacha akaoa upya! Mwanamke alikuwa sala 5 yani jamaa bishop kuvaa vaa vipensi mwanamke akawa mtu wa risala tu! Mwishowe jamaa aliotea kigoli akakitia unyago kisha akakioa baada ya mtoto wa kwanza kuzaliwa!
 
Back
Top Bottom