Tabia yangu ya kutojipendekeza, kusujudia maboss na kutokuwa mfitini inanisotesha mtaani

Tabia yangu ya kutojipendekeza, kusujudia maboss na kutokuwa mfitini inanisotesha mtaani

unauliza kama umekatika kichwa, unauliza wangap kwani nikikwambia 20 utakuwa na uhakika gani ama majibu yangu utayapima vipi? kama ya kweli ama laaah

kwani dini ile we umejua ni dini gan?

Unaniuliza badala ya kunijibu nilichokuuliza katika swali langu la Kwanza kabisa?
 
Kama kawaida baada ya kumaliza chuo nikaingia mtaani kusota na maisha bahati nzuri nikapata intern kwenye moja ya taasisi za serikali zinazolipa vizuri.​

Changamoto ikawa kumbe kwenye taasisi hizi za serikali inatakiwa ufanye kazi kwa bidii bila kusahau kujipendekeza kwa boss.​
Kwa jinsi nilivyo tabia yangu ya kutopenda kujipendekeza wala kufitini wafanyakazi wenzagu mm nikawa natimiza Majukumu kama kawaida.​

Kumbe ilitakiwa niwe naenda hata kumuona boss personly angalau mara moja kwa wiki kumsalimia tu ambavyo wengine hufanya sasa mm nawaza nikamuone manager nimweleze nini Cha zaidi wakati meeting za Kila wiki tunakutana na kila mtu anawasilisha ripoti yake?.​

Basi bwana boss akaanza kulalamika ooh sina msaada kwenye office ikabidi nifuatilie kujua ninakwama wapi bassi wadau wakanitonya jipendekeze nenda hata mara moja peleka umbea wowote ule atakukubali tu.​

Asikwambie mtu hakuna kazi ngumu Kama kuwa mmbeya eneo la kazi Kama hauna tabia hiyo.​

Mm nikasema potelea mbali ilimradi natimiza Majukumu yangu na nipo qualified siwezi kujipendekeza kwenye ofsi hii nitapata kazi hata kwingine.​

Mkataba wa intern ukaisha boss Kama kawaida akaaniambia nitafute kazi sehemu nyingine.​

Mwamba nikaona siyo kesi nikaingia mtaani nikapata kazi kampuni nyingine ya kibongo aisee kule ndo ikawa balaa bila kuwa mbeya humalizi mwezi unatimuliwa boss anataka kila siku mpishane na wafanyakazi ili apate taarifa mara huyu kapeleka fulani mwizi kaiba mafuta, kifusi.​

Daah nikaona pia isiwe kesi nikaacha kazi.​
Sasa Nina mwaka nasota mtaani nimezunguka kinoma hamna kazi kila Kona patupu wadau wanashauri tafuta hata viongozi wa kisiasa ujipendekeze kazi siku hizi kujuana mm naona wananisumbua tu.​

Natafuta kazi nikiamini qualifications zangu zitanibeba lakini patupu nimeapply sehemu nyingi hata kuitwa hakuna.​

Nikatafuta mpaka sehemu za vibarua patupu. Sasa nawaza hii tabia ya kutojipendekeza nitaachaa vipi maana kubadili tabia ni ngumu kama kubadili ngozi.​


Pole sana
mimi nilifanya kazi Bulyanhulu Mines, Kazi nilipata kwa connection ya Dingi, sijui kumbe mshahara wako wa kwanza unatakiwa nusu kwa nusu na kabosi ka kabongo tu wakati kampuni ya Wacanada, wenzagu wote walifanya hivyo, na pia mara kwa mara wanamcheki ka laki hivi duuh!
Mimi nilikuwa nampotezea tu, lakini sikudumu nikachongewa upuuzi, nikapigwa bomba
nakasema mimi na kazi bongo mwisho ndio huu
 
Pole sana
mimi nilifanya kazi Bulyanhulu Mines, Kazi nilipata kwa connection ya Dingi, sijui kumbe mshahara wako wa kwanza unatakiwa nusu kwa nusu na kabosi ka kabongo tu wakati kampuni ya Wacanada, wenzagu wote walifanya hivyo, na pia mara kwa mara wanamcheki ka laki hivi duuh!
Mimi nilikuwa nampotezea tu, lakini sikudumu nikachongewa upuuzi, nikapigwa bomba
nakasema mimi na kazi bongo mwisho ndio huu
😂😂😂
 
Unaniuliza badala ya kunijibu nilichokuuliza katika swali langu la Kwanza kabisa?
Mkuu nikujibu nini kwani dini ile ni dini gani? labda nikujibu dini ile ni ndugu zetu, ni familia rafiki, ni jamaa zetu ko kuanzia ngazi ya mtu mmoja, familia,koo tunaona yanayo tokea.

bahati nzuri nilipata fanya mkoa na ofisi walipo wengi nikawa na uzoefu wa tabia zao anzia kwa jamii hadi ofisini ni uongo na unafiki mwanzo mwisho. .
una swali lingine
 
hii dini ni kweli ni ndugu zetu ila kwa kuchongeana wako vyema, anzia ngazi za familia,ukoo hadi majirani ni uongo uongo tu hadi wanaume sijui wana tatizo gani hawa jamaa.
Sio kweli ndugu.
Mimi kwenye sehemu nilizopita za kazi hao watu wa dini hiyo mnaowasema hawakuwepo au hata kama walikuwepo haivuki asilimia 5.
Lakini bado majungu na kujikomba kulikuwa kwingi kwa hao watu wa dini mnayoisifia.
Tuchukulie kwa mfano kwenye utawala wa Magufuli halafu tuangalie watu wanaojikomba kwake.
Akina Paulo makonda ni dini gani?Akina palamagamba ni dini gani?Akina Augustino Mrema ni dini gani?
Kitu ambacho hamjajua hiyo ndio asili ya Mtanzania kazi kidogo maneno mengi,wewe ukiwa mchapakazi utachukiwa na kuambiwa unataka sifa.
Nenda nchi kama Sudan kama utakutana na upuuzi kama huu.
 
Kama kawaida baada ya kumaliza chuo nikaingia mtaani kusota na maisha bahati nzuri nikapata intern kwenye moja ya taasisi za serikali zinazolipa vizuri.​

Changamoto ikawa kumbe kwenye taasisi hizi za serikali inatakiwa ufanye kazi kwa bidii bila kusahau kujipendekeza kwa boss.​
Kwa jinsi nilivyo tabia yangu ya kutopenda kujipendekeza wala kufitini wafanyakazi wenzagu mimi nikawa natimiza Majukumu kama kawaida.​

Kumbe ilitakiwa niwe naenda hata kumuona boss personly angalau mara moja kwa wiki kumsalimia tu ambavyo wengine hufanya sasa mimi nawaza nikamuone manager nimweleze nini cha zaidi wakati meeting za Kila wiki tunakutana na kila mtu anawasilisha ripoti yake?.​

Basi bwana boss akaanza kulalamika ooh sina msaada kwenye office ikabidi nifuatilie kujua ninakwama wapi bassi wadau wakanitonya jipendekeze nenda hata mara moja peleka umbea wowote ule atakukubali tu.​

Asikwambie mtu hakuna kazi ngumu Kama kuwa mmbeya eneo la kazi Kama hauna tabia hiyo.​

Mimi nikasema potelea mbali ilimradi natimiza Majukumu yangu na nipo qualified siwezi kujipendekeza kwenye ofsi hii nitapata kazi hata kwingine.​

Mkataba wa intern ukaisha boss Kama kawaida akaaniambia nitafute kazi sehemu nyingine.​

Mwamba nikaona siyo kesi nikaingia mtaani nikapata kazi kampuni nyingine ya kibongo aisee kule ndio ikawa balaa bila kuwa mbeya humalizi mwezi unatimuliwa boss anataka kila siku mpishane na wafanyakazi ili apate taarifa mara huyu kapeleka fulani mwizi kaiba mafuta, kifusi.​

Daah nikaona pia isiwe kesi nikaacha kazi.​
Sasa Nina mwaka nasota mtaani nimezunguka kinoma hamna kazi kila Kona patupu wadau wanashauri tafuta hata viongozi wa kisiasa ujipendekeze kazi siku hizi kujuana mimi naona wananisumbua tu.​

Natafuta kazi nikiamini qualifications zangu zitanibeba lakini patupu nimeapply sehemu nyingi hata kuitwa hakuna.​

Nikatafuta mpaka sehemu za vibarua patupu. Sasa nawaza hii tabia ya kutojipendekeza nitaachaa vipi maana kubadili tabia ni ngumu kama kubadili ngozi.​

Ur sucha a good person ubarikiwe sana, binafsi niko hivo maisha yangu yote. Sijawahi kuingia ofisi za mabosi kwa kujipeleka bila shida rasmi ama kuitwa never.
 
Back
Top Bottom