Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,336
- 4,731
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Mkoani Tabora leo tarehe 19 Mei, 2022.
Ria Samia yupo mkoani Tabora kwa Ziara ya kikazi kwa siku 3, tangu aanze ziara hii amefanya uzinduzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo zikiwemo barabara na pia amesisitiza katika kulinda na kutunza miundombinu, watu kuongeza thamani katika uzalishaji wa bidhaa zao na pia kuwa wabunifu na kuendeleza uchumi wa viwanda.
=======
MAKAMBA: HATUJAFANYA UWEKEZAJI, MIUNDOMBINU IMECHAKAA, GRIDI IMEZIDIWA
Changamoto kubwa ya umeme Nchini imetajwa kuwa ni kutofanyika kwa uwekezaji wa kuboresha miundombinu inayoendana na mahitaji, ndiyo maana gridi ya umeme imekuwa ikizidiwa uwezo wake wa kufanya kazi.
Waziri wa Nishati, January Makamba amesema hayo na kuongeza: “Miundombinu ni kama waya zenye urefu na unene sahihi, transfoma, vituo vya kupokea na kupoozea umeme.
“Changamoto ya umeme ipo kwa kuwa hatukufanya uwekezaji unaoendana na mahitaji kwa miaka mingi, matokeo yake mfumo wa gridi yetu umeelemewa kutokana na kuongezeka mahitaji na uchakavu.”
Hotuba ya Rais Samia uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora
Kwa kuwa leo ni siku yangu ya mwisho kwa ziara hii basi nianze kwa kushukurani kuwashukuru Mkuu wa Mkoa huu, Wakuu wa Wlaya na wananchii wa Mkoa huu wa maeneo niliyotembelea na hata ambayo sijatembelea ikiwemo viongozi wa dini kwa dua na sala na machifu wenzangu nawshukuru sana kwa kuniunga mkono tangu nimeingia hapa kwenye mkoa huu pamoja na madereva wote kwa kutuendesha kote tulipokwenda na kufika salama, pia wananchi wote wa mkoa huu nawashukuru sana kwa ukarimu mlionifanyia, wajasiliamali, wamachinga, wanawake nawashukuru kwa zawadi na ukarimu wenu.
Shughuli nilizofanya katika ziara hii zote zomeshasemwa na waziri hivyo hakuna tija ya kuzirudia ila mkoa huu wa Tabora umepiga hatua kubwa sana za kimaendeleo katika mkoa huu, nimefika maeneo mbalimbali hata kule sikonge ambako kuna barabara imejengwa na nyumba nzuri zimejengwa ambazo hazina tofauti na za mijini, hivyo hiyo ni hatua kubwa ya kimaendeleo.
Mawaziri msivunjwe maneno na watu Inawezekana kuna maneno mengi sana, lakini hampati maneno kama ninayopata mimi. Hayanivunji moyo, najenga Nchi
Mambo mengi yameshasemwa hivyo mimi nina mambo mawili, moja ni kuwa maendeleo haya ni kwa ajili yenu na hivyo ni lazima kutunza miundo mbinu hiyo, muitunze na kulinda.
Na la pili ni swala la Ajira, kwenye kila fursa ya miradi kuna kursa ya ajira hivyo mchangamkie fursa kwani mnaweza kuajiriwa kama vibarua au kujiajiri kwa kuuza maji nk, lakini pia kuna mambo mengi kama umeme nk ambayo yamesha fafanuliwa vizuri na mawaziri.
Katika ziara hii, zimebainishwa changamoto nyingi ambazo mawaziri wangu wameshazitolea ufafanuzi vizuri wameeleza kuhusu mipango ya baadaye, kwa hiyo changamoto hizo zitatatuliwa, lakini pia kuna fedha za halmashauri zinaletwa hapa nataka kusema kuwa simamieni hizo fedha zikafanye kazi vizuri kuna wanaotaka kunijaribu kuwa zipofanya kazi vizuri watapata nini sitasema hapa nini kitawakuta ila wanijaribu.
Tabora ni eneo la hifadhi, kuwepo na mipaka ya kijijini na shughuli za watu na kuwepo na hifadhi kwani tukisema tukate misitu ili kupanua maeneo ya watu tutakosa hifadhi hata kilimocha nyuki hakitakuwepo, hivyo tupunguze wingi wa mifugo isiyo na tija kwani hatutakata tena maeneo ya hifadhi hivi karibuni mpaka baadaye.
Pia kuna swalqa la mitaala kuwa haiwaandai vijana kujitegemea hivyo tunatakiwa kubadili mitaala ili vijana waweze kujitegemea na kujiajiri, nami nakubaliana na swala hili la kumtayarisha kijana aweze kukubalika kwenye ajira au kujiajiri mwenyewe na wizara inapita kuchukua maoni ya wananchi ili kuweza kukabiliana na swala hilo.
Kuna kiwanda kinajengwa Urambo cha Kuzalisha asali nami nipongeze juhudi za mkoa, na kuna fedha zinakuja hivyo asali hiyo iandikwe kuwa inazalishwa Tabora.
Swala la usalama wa chakula, niwaombe sana wana Tabora kuhifadhi sana chakula kilichopo, tumekosa mvua kwa misimu miwili hivyo tutunze chakula kilichopo maana kukosa mvua si matakwa ya mtu bali ni matakwa ya Mungu na tulivyo haribu mazingira, nimejionea kwa macho yangu njiani hali ya mazao hairidhishi ila naona viazi njiani tutunze chakula kilichopo.
Kuna hili la fedha kwenye halmashauri, fedha zinapokuja kwenyehalmashauri wananchi wajue kuwa kuna fedha zimeletwa na ni kiasi gani hakuna haja ya kuficha, matumizi chama kijue wananchi wajue ili waweze kufatilia lakini pia, waweze kujua fedha hizo zimetumikaje kama kwa kufata kanuni na sheria maana hakuna mtu anayeweza kusema fedha hizi ziende hapa zisiende hapa, kuna mabaraza ya madiwani nyinyi ndio mna mamlaka ya kuamua matumizi ya fedha maana sheria imekupeni mamlaka hivyo fedha zifuate kanuni na sheria ya jisni ya kutumia.
Kuna malalamiko ya machifu kuwa hawatambuliwi naomba muwatambue na muwashirikishe kwenye maendeleo kwani kila mtu anamila na desturi zake. Muwashirikishe katika maendeleo.
Kuna swala la Tabora Girls, kuwa nusu ya eneo lake lijengwe shule ya vipajai maalumu hilo naliacha kwenye uongozi wa hapa watajua nini cha kufanya, lakini kuna swala la mipaka ya majeshi na maeneo ya wananchi hili nalibeba nitalifanyia kazi.
Tunaposema tumeanza kukigeuza kilimo ni kwa kutoa ruzuku, na tumeanza kutoa ruzuku lakini mwaka jana hakukua na ruzuku ila mwaka huu kuna ruzuku.
Baada ya kusema haya niwashukuru wana Tabora na niseme nilikuwa na ziara nzuri sana na niwaahidi kuwa nitarudi niende kwenye wilaya ambazo sijafika, niwashukuru sana niwaage kwa kusema kazi iendelee.
Ria Samia yupo mkoani Tabora kwa Ziara ya kikazi kwa siku 3, tangu aanze ziara hii amefanya uzinduzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo zikiwemo barabara na pia amesisitiza katika kulinda na kutunza miundombinu, watu kuongeza thamani katika uzalishaji wa bidhaa zao na pia kuwa wabunifu na kuendeleza uchumi wa viwanda.
=======
MAKAMBA: HATUJAFANYA UWEKEZAJI, MIUNDOMBINU IMECHAKAA, GRIDI IMEZIDIWA
Changamoto kubwa ya umeme Nchini imetajwa kuwa ni kutofanyika kwa uwekezaji wa kuboresha miundombinu inayoendana na mahitaji, ndiyo maana gridi ya umeme imekuwa ikizidiwa uwezo wake wa kufanya kazi.
Waziri wa Nishati, January Makamba amesema hayo na kuongeza: “Miundombinu ni kama waya zenye urefu na unene sahihi, transfoma, vituo vya kupokea na kupoozea umeme.
“Changamoto ya umeme ipo kwa kuwa hatukufanya uwekezaji unaoendana na mahitaji kwa miaka mingi, matokeo yake mfumo wa gridi yetu umeelemewa kutokana na kuongezeka mahitaji na uchakavu.”
Hotuba ya Rais Samia uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora
Kwa kuwa leo ni siku yangu ya mwisho kwa ziara hii basi nianze kwa kushukurani kuwashukuru Mkuu wa Mkoa huu, Wakuu wa Wlaya na wananchii wa Mkoa huu wa maeneo niliyotembelea na hata ambayo sijatembelea ikiwemo viongozi wa dini kwa dua na sala na machifu wenzangu nawshukuru sana kwa kuniunga mkono tangu nimeingia hapa kwenye mkoa huu pamoja na madereva wote kwa kutuendesha kote tulipokwenda na kufika salama, pia wananchi wote wa mkoa huu nawashukuru sana kwa ukarimu mlionifanyia, wajasiliamali, wamachinga, wanawake nawashukuru kwa zawadi na ukarimu wenu.
Shughuli nilizofanya katika ziara hii zote zomeshasemwa na waziri hivyo hakuna tija ya kuzirudia ila mkoa huu wa Tabora umepiga hatua kubwa sana za kimaendeleo katika mkoa huu, nimefika maeneo mbalimbali hata kule sikonge ambako kuna barabara imejengwa na nyumba nzuri zimejengwa ambazo hazina tofauti na za mijini, hivyo hiyo ni hatua kubwa ya kimaendeleo.
Mawaziri msivunjwe maneno na watu Inawezekana kuna maneno mengi sana, lakini hampati maneno kama ninayopata mimi. Hayanivunji moyo, najenga Nchi
Mambo mengi yameshasemwa hivyo mimi nina mambo mawili, moja ni kuwa maendeleo haya ni kwa ajili yenu na hivyo ni lazima kutunza miundo mbinu hiyo, muitunze na kulinda.
Na la pili ni swala la Ajira, kwenye kila fursa ya miradi kuna kursa ya ajira hivyo mchangamkie fursa kwani mnaweza kuajiriwa kama vibarua au kujiajiri kwa kuuza maji nk, lakini pia kuna mambo mengi kama umeme nk ambayo yamesha fafanuliwa vizuri na mawaziri.
Katika ziara hii, zimebainishwa changamoto nyingi ambazo mawaziri wangu wameshazitolea ufafanuzi vizuri wameeleza kuhusu mipango ya baadaye, kwa hiyo changamoto hizo zitatatuliwa, lakini pia kuna fedha za halmashauri zinaletwa hapa nataka kusema kuwa simamieni hizo fedha zikafanye kazi vizuri kuna wanaotaka kunijaribu kuwa zipofanya kazi vizuri watapata nini sitasema hapa nini kitawakuta ila wanijaribu.
Tabora ni eneo la hifadhi, kuwepo na mipaka ya kijijini na shughuli za watu na kuwepo na hifadhi kwani tukisema tukate misitu ili kupanua maeneo ya watu tutakosa hifadhi hata kilimocha nyuki hakitakuwepo, hivyo tupunguze wingi wa mifugo isiyo na tija kwani hatutakata tena maeneo ya hifadhi hivi karibuni mpaka baadaye.
Pia kuna swalqa la mitaala kuwa haiwaandai vijana kujitegemea hivyo tunatakiwa kubadili mitaala ili vijana waweze kujitegemea na kujiajiri, nami nakubaliana na swala hili la kumtayarisha kijana aweze kukubalika kwenye ajira au kujiajiri mwenyewe na wizara inapita kuchukua maoni ya wananchi ili kuweza kukabiliana na swala hilo.
Kuna kiwanda kinajengwa Urambo cha Kuzalisha asali nami nipongeze juhudi za mkoa, na kuna fedha zinakuja hivyo asali hiyo iandikwe kuwa inazalishwa Tabora.
Swala la usalama wa chakula, niwaombe sana wana Tabora kuhifadhi sana chakula kilichopo, tumekosa mvua kwa misimu miwili hivyo tutunze chakula kilichopo maana kukosa mvua si matakwa ya mtu bali ni matakwa ya Mungu na tulivyo haribu mazingira, nimejionea kwa macho yangu njiani hali ya mazao hairidhishi ila naona viazi njiani tutunze chakula kilichopo.
Kuna hili la fedha kwenye halmashauri, fedha zinapokuja kwenyehalmashauri wananchi wajue kuwa kuna fedha zimeletwa na ni kiasi gani hakuna haja ya kuficha, matumizi chama kijue wananchi wajue ili waweze kufatilia lakini pia, waweze kujua fedha hizo zimetumikaje kama kwa kufata kanuni na sheria maana hakuna mtu anayeweza kusema fedha hizi ziende hapa zisiende hapa, kuna mabaraza ya madiwani nyinyi ndio mna mamlaka ya kuamua matumizi ya fedha maana sheria imekupeni mamlaka hivyo fedha zifuate kanuni na sheria ya jisni ya kutumia.
Kuna malalamiko ya machifu kuwa hawatambuliwi naomba muwatambue na muwashirikishe kwenye maendeleo kwani kila mtu anamila na desturi zake. Muwashirikishe katika maendeleo.
Kuna swala la Tabora Girls, kuwa nusu ya eneo lake lijengwe shule ya vipajai maalumu hilo naliacha kwenye uongozi wa hapa watajua nini cha kufanya, lakini kuna swala la mipaka ya majeshi na maeneo ya wananchi hili nalibeba nitalifanyia kazi.
Tunaposema tumeanza kukigeuza kilimo ni kwa kutoa ruzuku, na tumeanza kutoa ruzuku lakini mwaka jana hakukua na ruzuku ila mwaka huu kuna ruzuku.
Baada ya kusema haya niwashukuru wana Tabora na niseme nilikuwa na ziara nzuri sana na niwaahidi kuwa nitarudi niende kwenye wilaya ambazo sijafika, niwashukuru sana niwaage kwa kusema kazi iendelee.