Tabu ninayopata kutoka kwenye familia yangu

Tabu ninayopata kutoka kwenye familia yangu

MC.jpg
 
Watanzania wajinga sana wakati unatafuta wa kukusomesha kila mmoja kimya. Sasa umepata ajira kila mjinga anaejiita ndugu anakuja kuomba msaada. Nawe kiazi una saidia wakati wewe mwenyewe una shida kibao. Ndio maana hatuwezi kwenda mbele kwasababu tuna mizigo yetu na tunabeba na ya wenzetu pia.
Eagle assassin njoo malizia huko
 
Watanzania wajinga sana wakati unatafuta wa kukusomesha kila mmoja kimya. Sasa umepata ajira kila mjinga anaejiita ndugu anakuja kuomba msaada. Nawe kiazi una saidia wakati wewe mwenyewe una shida kibao. Ndio maana hatuwezi kwenda mbele kwasababu tuna mizigo yetu na tunabeba na ya wenzetu pia.
Eagle assassin njoo malizia huko
Tabia hiyo ya kuombaomba kwa ndugu mwenye kazi ilizaliwa Kigoma, ikakulia Tabora na kwa Sasa imejichimbia umakondeni.
 
Tabu ninayopata kutoka kwenye familia yangu-17

Nilianza safari kuelekea mwanza ,lengo ilikuwa niende kujitambulisha na ikiwezekana nilipe mahali kabisa ,nilifika mwanza mida ya usiku nikatafuta gesti kwa ajili ya kupumzika ,kesho yake nikaelekea ukweni ,tulivyofika tuliongea Mambo mengi na baba mkwe ,baba mkwe akaniambia kama upo tayari kutoa mahali tuma watu ili tuweze kuelewana nao mahali mkiweza kulipia ukiweza kulipia basi utaondoka na mke

Basi niliondoka ukweni na sikuona haja ya kurudi dar bila mke ,nikaona nimpigie baba simu, japo hakunilea nilikuwa Sina chuki nae ,pia alikuwa hanilaumu kwa kushindwa kumsaidia baadhi ya shida zake ,kesho yake ikabidi kina baba waje kwa ajili ya kuelewana mahali

Walifika mpaka ukweni ,wakaelewana kulipa ngombe na izo ng'ombe tukazibadilisha kwenda kwenye fedha ,nililipia kiasi na nyingine nikahahid kulipa taratibu ,basi nikapewa mke nikarudi nae dar kuendelea na kazi

Mke wangu pia nilimtafutia sehemu ya kufanya kazi hivyo maisha yalikuwa mazuri kwa upande wa kazi lakini kwa upande wa familia hatokuwa vizuri kwani tulikosa muda wa kuwa pamoja ,ila tulijiwekea malengo tulijiwekea malengo kwa muda

Sasa tatizo la pale mbezi wale jamaa tuliokuwa tunafanya nao kazi walikuwa ni wezi mno ila nilijitahid kusimamia nikanyoosha Mambo pesa ikaanza kupatikana

Siku moja siku ya sababa nilienda uwanja wa sababa kwenda kuosha macho ,basi katika kutembea kwangu nikakuta simu ya ofa kutoka Vodacom ,simu fulani hiv kubwa iPad zilikuwa zinauzwa laki moja na kumi basi nikanunua

Wale jamaa kule kazini mbezi walivyoniona na ile simu waka organized wakaenda kwa bosi wakamdanganya kwamba ile simu inauzwa Bei kubwa sana hivyo Mimi namwibia pesa ,basi Mimi nikaona bosi anaanza kunibadilika ,Mimi ndio nilikuwa meneja nashangaa naingia kazini nakuta Kuna meneja mwingine ,basi bana Mimi nikaona hakuna kibarua Tena

Nikaenda kwenye ofisi ya bosi kuongea nae yaani bosi amenuna tu akaniuliza unanidai sh ngapi ,basi akanipa pesa zangu Mimi nikaondoka zangu



Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Mimi ni kijana nilizaliwa mwaka 88 Mwanza mjini, tuliishi kwenye nyumba ya familia ile nyumba tuliishi familia mbili babu alikuwa na wake watatu hivyo pale walekaa Bibi zangu wawili na watoto wao ambao Kila Bibi alikuwa na watoto Saba Kila mtoto alikuwa na watoto wake pia hivyo waligawana vyumba, Bibi mwingine yeye hakuzaa, japo babu alikuwa na nyumba nyingine tatu.

Kila Bibi alikuwa amepewa nyumba moja na nyumba hizi zilikuwa zimejengea mitaa tofauti, kwa kifupi maisha hayakuwa mazuri pale tuliishi kigumu gumu, uwezo wangu darasani pia haukuwa mzuri japo nilikuwa siwi wa mwisho mwaka 2000 walielewana wauze ile nyumba sisi tulienda kuishi na Bibi yetu ambae alikuwa ameacha chumba kimoja katika ile nyumba waliogawiwa, vyumba vingine walikuwa wamepangisha Kodi watoto ndio waliokuwa wanachukua yeye hakupewa kitu.

Bibi yangu alikuwa mpole sana, watoto wa kiume ndio walipanga pembeni watoto wa kike walikaa na mama yao pamoja na wajukuu wale wa kiume pia kula walikuwa wanakula pale kwa bibi ,Bibi yangu alikuwa anajishughulisha na biashara ndogo ndogo aliweza kutulisha wote na matumizi madogo madogo alikuwa anatupatia ,kwakweli maisha Yale yalikuwa yananiumiza sana yaani kulala ni tabu wajukuu wengi mna lala mpaka uvunguni nilijaribu kwenda kwa mzee wangu kukaa sababu yeye alikuwa na nyumba kubwa tu ,lakin yule mke wake akakataa Mimi kukaa pale yule mwanamke alisusia Kila kitu akasema kama Mimi nakaa pale basi yeye ataondoka.

Baba ikabidi anifukuze ila niligoma kuondoka baadae baba akaniita pembeni kwa upole akanieleza nirudi tu kwa mama yangu akaniambia hanichukii ila Sasa hivi ni ngumu kumuelewa ila nikiwa mkubwa nitakuja kumuelewa basi bwana ikabidi niondoke zangu niende kwa Bibi tuliishi hivyo hivyo kwa tabu aise ,mwaka 2002 nilimaliza darasa la Saba sikufanikiwa kufaulu Bibi nae alikuwa ameshachoka Kila siku anaumwa baadae Bibi alishindwa kabisa kuendelea kufanya biashara ikabidi apumzike huwezi amini watoto walishindwa kumtunza kabisa yule mzee.

Itaendelea
===
Muendelezo soma Tabu ninayopata kutoka kwenye familia yangu
Daaahhh,naweka kambi hapa mkuuu,inasikitisha sana!
 
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
Hii story nimeipenda Sana,
Hey don't stop aseee weka vitu
 
Back
Top Bottom