Tabu ninayopata kutoka kwenye familia yangu

Tabu ninayopata kutoka kwenye familia yangu

Ningekuwa nimeachwa kule bila kuhamishwa ningekuwa mbali sana ,hivyo serikalini sio sehemu salama lolote linaweza kukuta wakati wowote

Kule ilifikia hatua nilikuwa sitoi mshahara kwa Sababu ya matumizi vyakula ,na matumizi madogo madogo nilikuwa napata kwenye kilimo na ufugaji ,nilikuwa nimeshafikia hatua ya kuwauzia mayai wakaanga chipsi

Sasa nilipohamia ni kugumu hatari ,chakula vya kuku Bei kubwa halafu kuku hawana Bei ukitaka kuwauza kwa Bei mpaka usafirishe



Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Tabu Ninayopata kutoka kwenye familia yangu -25

Tulivyorudi nyumbani nikamueleza baba mwanzo wa matatizo yote ,nikamwambia baba ngoja tu nitafute mwanamke mwingine nioe ,baba akaniambia ngoja ataongea nae

Basi baadae baba akamuita tukaanza kuongea basi akaonekana ameelewa ,baadae nikaingia ndani kunywa dawa akanipa dawa vizuri nikameza

Baadae akaniambia naomba uoe mwanamke mwingine ili akusaidie si unaona unaumwa , akaniambia kwani tokea nimekwambia hivi hujawahi kufanya maandalizi ya kutafuta mtu ,nikamwambia nilitafuta lakini bado hajanielewa ,basi akaniomba namba ya simu ya huyo Dada wakaongea kwamba ameruhusu Mimi nimuoe ,yeye atakuwa mke mkubwa halafu mwenga atakuwa mke mdogo

Baadae alivyomaliza kuongea nae akanisisitiza kwamba nihakikishe naoa ,kesho yake akawa ameondoka kurudi kazini

Baadae Mimi nikamwambia baba uyu mwanamke naona hanitaki Tena ,basi yule mke wangu alikuwa anakaa na mtoto wa shangazi yake ,Sasa uyo binti akanipigia simu akaniambia yule Dada yake siku hizi anamtu waga anakuja kulala pale nyumbani aise niliumia sana

Basi baadae baba aliondoka Mimi nikabaki pale na braza na wale watoto wa Dada yangu ,baadae nikafanya process ya kumuoa yule mwanamke ,niliona nichague mtu ambae hajasoma

Bado ndoa changa nikapata uhamisho wa kuhamia wilaya ingine uhamisho kutoka kwa RAs ,basi mke wangu alivyosikia nimeoa ndio ikawa tiketi ya kuniacha

Akawaambia kwao kwamba amenikuta nimeshaoa ndio maana ameamua kuniacha ,kumbe ile kunilazimisha kuoa alitaka apate sababu ya kuniacha

Unajua Kuna kipindi kaka yangu mtoto wa mama mkubwa alijiua kwa sababu mke wake ambae alizaa nae watoto wawili alimkataa ,japo nilikuwa nahuzunika lakini nilikuwa nishangaa ni kwa Nini braza ajiue wakati wanawake wapo wengi


Aise usiombe ikakukuta yaani hauoni another option Zaid ya hiyo ya kujiua ,

Yule mwanamke niliemuoa alikuwa single mother wa watoto watatu ,nae sijui alikuwa na mental trauma alikuwa ni mkorofi sana anapenda kugombana yaani ukimkosea kidogo tayari makofi
Sasa nikaona uyu tunaweza Kuna kuumizana tulibahatika kupata nae mtoto mmoja wa kike ,lakini baadae ilibid niachane nae

Mwaka huu nimeoa mke mwingine naomba mungu sana anijaalie nidumu na uyu,

Baadae yule mke wangu wa kwanza alinitafuta na kuniomba msamaha ilikuwa bado sijaoa uyu wa tatu lakini nikaona haina haja ya kuwa na mtu asie na msimamo

Ndio maana nikaona nioe tu mtu mwingine

Sasa tabu ninazopata kutoka kwenye familia yangu ni ;-

1 wazazi na ndugu hawaniongelei vizuri pindi ninapo oa ,mke wa kwanza waliongea Mambo mengi sana hasa mama

2-hata ukitoa msaada hawathamini siku ukiombwa na ukawa huna basi ni maneno mabaya mabaya wanakuongelea

3- mama Sasa hivi ameshazeeka lakini bado anang'ang'ania kufanya zile shughuli za uvuvi Kila siku ni kupoteza pesa ,anahitaji nimnunulie mashine lakini Mimi naona ameshachoka halafu Kuna wadogo zangu wapo chuo nikinunua hiyo mashine nitashindwa kuwasapoti

4 - nimeoa mke wa tatu ,mama alitoa maneno mabaya sana but Sina Cha kufanya Zaid ya kumshukuru mungu

Kule nilipohamishwa nilitengeneza mazingira mazuri sana lengo langu ni kufungua kampuni
Ambayo itakuwa ina deals with

1 .Agroproduction (kilimo na ufugaji )
Yaani na Lima nafuga pia nakuwa na mashine za kusanga na kukoboa halafu nafunga kwenye viroba nauza

2.viwanda vidogo vidogo kama mikate na mashine ya kuprocesa ngozi

3.usagirishaji (magari ya abiria

4.duka la dawa , zahanati na maabara

5.maduka ya jumla

6 .magari ya mizigo

Naamini nitafanikiwa kwa sababu naona kabis siwezi kubadili maisha yangu kwa kazi za kuajiriwa Tena humu serikalini kulivyo na changamoto

Ndio hivyo ndugu zangu ,naombeni ushauri wenu nifanye Nini ili niweze kufikia malengo yangu

Dunia tunayoenda nayo ni ngumu sana

Mwisho



Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
Kuhusu biashara safi sana,ila ngeshauri uanze na moja kwanza isimame,tena fungua dispensary/pharmacy maana unauzoefu nayo sana.

Ndugu zako wasikuumize kichwa,kama mabaya wacha waongee hupungukiwi kitu,ukiweza saidia mkono wako unapofika,usijiumize ndo maana hadi unachanganyikiwa.

Ushauri muhimu kuliko wote,huyo mke wako wa kwanza ni mpuuuzi ni mpuuuzi sana,nakuomba tena sana asikuone ndezi,usije ukarudiana nae,mtupe mtupe kabisa.

Ni hayo tu.
 
Nje ya box;
mkuu nahisi wewe una matatizo ndiyo maana hao wanawake wawili mmeshindwana bila sababu za msingi kuwa makini na ujirekebishe hata huyo watatu angalia sana.Yawezekana una matatizo fulani kwa vyovyote hutayazungumza hapa.
 
Pole sana .
Uko ulikohamia jitahidi utimize wajibu wako , usijipendekeze kwa watu wa kuitwa DMO au RMO watakupoteza maana kwa siku hizi vigezo hawapewi kwa kuzingatia utaratibu wa wizara ila imekuwa kama kujuana tu .

Hivyo kuna muda wanaendeshwa na mambo ya kisiasa na kijamii .

Mambo magumu ya nduguzo mbona ni mambo ya kawaida kwa sasa wewe ni mtu mzima wake watatu uliooa itoshe kusema kuwa hata kama ni mdogo wa umri ila tayari umepevuka sana hivyo naweza kusema hii dunia haina shukrani .

Usihangaike kufanya kitu kilicho nje ya uwezo wako wa mshahara na pia kilicho nje ya malengo yako .

Acha kukaa ukawaza ujinga na umbeya na unafiki wa nduguzo maana haukusaidii chochote wala hautakuonhezea cheo zaidi ni kukupa stress zaidi .

Daktari , sijaona sehemu uliposema unakunywa pombe usijaribu ila sasa daktari ukiendekeza huo ujinga wa kusikiliza nduguzo wanasema nini nakuona milembe tena sio kwenda na kurudi ila yakiwa makao yako rasmi .

Jipe raha fanya kilicho ndani ya uwezo wako achana na habari za ndugu .

Daktari ni ngumu kufanya haraka ila anza kwa kupunguza mawasiliano ya day to day na nduguzo mwisho utapuuza ujinga wao .

Usisahau umetoka familia ya kimasikini sana hivyo mawazo mgando hayajawahi kupotea kwa ndugu zetu masikini hasa kwa aliyeonesha mwanga wa kuukimbia umasikini .

Alafu najua kwenu sio wewe tu mwenye mwanga kidogo wa maisha wapo wengine baadhi hivyo punguza kupenda sifa ili labda wakuone una hela au una moyo mzuri maana haya ndiyo yatakuwa ni mwanzo wa lawama za nduguzo hasa ukikosa kuwapa msaada takiwa .

Jioni njema daktari , tafakari .
Asante kwa ushauri ,nashukuru sana

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Kuhusu biashara safi sana,ila ngeshauri uanze na moja kwanza isimame,tena fungua dispensary/pharmacy maana unauzoefu nayo sana.

Ndugu zako wasikuumize kichwa,kama mabaya wacha waongee hupungukiwi kitu,ukiweza saidia mkono wako unapofika,usijiumize ndo maana hadi unachanganyikiwa.

Ushauri muhimu kuliko wote,huyo mke wako wa kwanza ni mpuuuzi ni mpuuuzi sana,nakuomba tena sana asikuone ndezi,usije ukarudiana nae,mtupe mtupe kabisa.

Ni hayo tu.
Asante mkuu

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Nje ya box;
mkuu nahisi wewe una matatizo ndiyo maana hao wanawake wawili mmeshindwana bila sababu za msingi kuwa makini na ujirekebishe hata huyo watatu angalia sana.Yawezekana una matatizo fulani kwa vyovyote hutayazungumza hapa.
Matatizo yangu Mimi ni mpole sana ,napenda kumpa mwanamke wangu nafasi ya kufanya Mambo ,siwezi kutoa pesa ya matumiz Kila siku ,waga natoa pesa fulani laki au laki mbili anatumia ikiisha ananiambia ,mke yule wa pili alianza mtindo wa vikoba na kutuma nyumbani kwao pesa ,Sasa baadae hali yangu ya fedha ikayumba ,Mimi najua pesa nyumbani ipo kumbe hakuna kitu ,tumeachana lakin aliniachia madeni mengi sana ,ambayo nimemaliza kulipa juzi juzi tu hapa

Akinishida uyu wa Sasa hivi sioi Tena nitaish maisha yangu kivyangu

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Kuhusu biashara safi sana,ila ngeshauri uanze na moja kwanza isimame,tena fungua dispensary/pharmacy maana unauzoefu nayo sana.

Ndugu zako wasikuumize kichwa,kama mabaya wacha waongee hupungukiwi kitu,ukiweza saidia mkono wako unapofika,usijiumize ndo maana hadi unachanganyikiwa.

Ushauri muhimu kuliko wote,huyo mke wako wa kwanza ni mpuuuzi ni mpuuuzi sana,nakuomba tena sana asikuone ndezi,usije ukarudiana nae,mtupe mtupe kabisa.

Ni hayo tu.
Tatizo hizo biashara ukiwa serikalini zina majungu sana ,kule nilikuwa sifanyi lakini nikasingiziwa naiba dawa ,je nikifanya itakuwaje

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Tatizo hizo biashara ukiwa serikalini zina majungu sana ,kule nilikuwa sifanyi lakini nikasingiziwa naiba dawa ,je nikifanya itakuwaje

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
Tafuta mtu utakaye muamini umuweke, majungu kwa wabongo ni kawaida.

Usifikiri mtu atapenda mafanikio yako,gata usipofanya watapiga tu majungu.
 
Story yako inahuzunisha ila pia inamafundisho sana.Ila kilichokuja kukuangusha ni mahusiano(wanawake).Pole sana.
Wewe ni mpambanaji sanaaa.
Ushauri wangu uko ulikohamia angalia fursa ya biashara ya fani yako,Kwa sababu kupitia story yako unaifanya vizuri sana,deal with your passion.Kikubwa kuliko yote jifunze kuwa na Ibada zaidi,vita yako sio ndogo hata kidogo.Songa Mbele focus.Kuhusu mama yako msaidie tu anachotaka,opinion za ndugu zako zisikilize ila usizipe nafasi ya kutawala maamuzi yako,chagua mazuri ufate na mabaya achana nayo.

It is there opinions huwezi zuia.All the best ukafanikiwe zaidi.
Amina ,Asante

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Mimi nakushauri urudi milembe kwanza wakutibu vizuri inaonekana kama umekimbia kabla ya kumaliza tiba kamili. Sababu ya kusema hivi kutokana na maamuzi yako ya kuowa bila ya mpango na kuwa na wasiwasi wa kusemwa na ndugu. Kila jema mkuu kaza buti funga mkanda pambana na maisha.
 
Mimi nakushauri urudi milembe kwanza wakutibu vizuri inaonekana kama umekimbia kabla ya kumaliza tiba kamili. Sababu ya kusema hivi kutokana na maamuzi yako ya kuowa bila ya mpango na kuwa na wasiwasi wa kusemwa na ndugu. Kila jema mkuu kaza buti funga mkanda pambana na maisha.
Nina miaka miwili inaelekea mwaka wa tatu sijawahi kutokewa Tena na hiyo hali ,Sasa hivi nimeacha kuish kwa stress

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Tabu ninayopata kutoka kwenye familia yangu -24
Basi nesi akanichukia sana akasema lazima atanikomesha ,kumbe yule nesi alikuwa anatembea na Dmo ,basi Mimi nikashangaa dmo akaanza kunibadilika

Basi baadae nikatolewa kwenye uongozi ,lakini pia nikaanza kupitia manyanyaso hapo kituoni

Mimi nilivyoona hali inakuwa ngumu ikabidi niende kwa dmo nikamuelezea changamoto ninazo pitia ,Aise hakuna kilichobadilika

Basi baadae nikasikia nataka kuhamishwa ,Kuna jambo nilifanya mpaka Leo najutia ,Kuna dili fulani viongozi walipiga akiwemo dmo ,Mimi kwa sababu ni assassin eagle niliiba zile documents ,wakati huyo napitia hizo changamoto mke wangu akawa amekuja kujifungua, aise hali ilikuwa mbaya nilikuwa Sina hata pesa

Diwani alikuwa ananikubali sana nikamshirikisha changamoto ninazopitia pia nikamdokeza Kuna documents za wizi ,diwan akasema nimpe hizo documents

Basi bana baadae kwenye vikao huko diwani akalipua Hilo bomu duh ,hakuna rangi niliacha kuona viongozi wote walinitenga ikiwemo mkurugenzi ,mpaka mkuu wa wilaya , mwenyekiti wa halmashauri

Basi bana ikaanza kusambaa taarifa kwamba Kuna wizi nimeufanya ,kwa kuwa nilikuwa Nina zile documents nikasema poa ,hapo wakinizingua hata mahakamani nitaenda

Baadae nilivyoona Mambo yanakuwa magumu ,nilikuwa Nina ujenzi sehemu niliyotaka kufanya ufugaji wa kuku na mbuzi ile nyumba ilikuwa bado haijaisha ikabid nikope ili niweze kuimaliza hiyo nyumba ,duh hili nalo ni shimo lingine nikaingia

Baadae nikafanikiwa kuimaliza ile nyumba ,unajua nilijua kinachofuata ni kufukuzwa pale kazini hivyo nilikuwa naandaa mazingira ya sehemu ya kukaa

Sasa hivi mtoto wetu ameshakuwa mkubwa ameanza kutembea ,wife akanipigia sehemu kwamba anahitaji kuachana ,nikamuuliza shida ni Nini mke wangu aise hakunielewa

Aise niliwaza sana unajua mke wangu Mimi ndio allikuwa Kila kitu kwangu ,nilimuamini mno sema changamoto tu za umbali


Nikajaribu kutafuta msaada kwa ndugu zake lakini hakuna ambae alitoa msaada

Basi Mimi nilikuwa mtu wa kupambana nikaona nitafute mbadala kumbe akili yangu haipo sawa ,Kuna demu fulani hivi nilimtongoza asubuhi jioni nikaenda kwao kwamba nataka kumuoa muda huo huo ,Sasa wale wazee wakaniona kama sipo sawa wakaniambia Rudi kesho


Aise nilishtuka baada ya wiki nikiwa hosptali ya milembe ,kumbe nilivyorudi nyumbani usiku wake nilichanganyikiwa ,nikaanza kutupia watu mawe mwisho wa siku nilipewa rufaa kwenda milembe

Baadae nimekuja kuzinduka wazazi wangu wapo pembeni na braza pia na wife ,basi tukapewa dawa pale tukaambiwa turudi nyumbani

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
Ulikua watumia pombe??
 
Nina miaka miwili inaelekea mwaka wa tatu sijawahi kutokewa Tena na hiyo hali ,Sasa hivi nimeacha kuish kwa stress

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
Samahani mkuu nataka kuelewa vizuri unataka msaada wa ushauri wa nini??
1 Ushauri wa maisha
2 Biashara
3 Mke (ex wako)
3 Kilimo
4 Ajira binafsi au Serikalini
5 Wazee na ndugu kukusema???
 
Tabu Ninayopata kutoka kwenye familia yangu -25

Tulivyorudi nyumbani nikamueleza baba mwanzo wa matatizo yote ,nikamwambia baba ngoja tu nitafute mwanamke mwingine nioe ,baba akaniambia ngoja ataongea nae

Basi baadae baba akamuita tukaanza kuongea basi akaonekana ameelewa ,baadae nikaingia ndani kunywa dawa akanipa dawa vizuri nikameza

Baadae akaniambia naomba uoe mwanamke mwingine ili akusaidie si unaona unaumwa , akaniambia kwani tokea nimekwambia hivi hujawahi kufanya maandalizi ya kutafuta mtu ,nikamwambia nilitafuta lakini bado hajanielewa ,basi akaniomba namba ya simu ya huyo Dada wakaongea kwamba ameruhusu Mimi nimuoe ,yeye atakuwa mke mkubwa halafu mwenga atakuwa mke mdogo

Baadae alivyomaliza kuongea nae akanisisitiza kwamba nihakikishe naoa ,kesho yake akawa ameondoka kurudi kazini

Baadae Mimi nikamwambia baba uyu mwanamke naona hanitaki Tena ,basi yule mke wangu alikuwa anakaa na mtoto wa shangazi yake ,Sasa uyo binti akanipigia simu akaniambia yule Dada yake siku hizi anamtu waga anakuja kulala pale nyumbani aise niliumia sana

Basi baadae baba aliondoka Mimi nikabaki pale na braza na wale watoto wa Dada yangu ,baadae nikafanya process ya kumuoa yule mwanamke ,niliona nichague mtu ambae hajasoma

Bado ndoa changa nikapata uhamisho wa kuhamia wilaya ingine uhamisho kutoka kwa RAs ,basi mke wangu alivyosikia nimeoa ndio ikawa tiketi ya kuniacha

Akawaambia kwao kwamba amenikuta nimeshaoa ndio maana ameamua kuniacha ,kumbe ile kunilazimisha kuoa alitaka apate sababu ya kuniacha

Unajua Kuna kipindi kaka yangu mtoto wa mama mkubwa alijiua kwa sababu mke wake ambae alizaa nae watoto wawili alimkataa ,japo nilikuwa nahuzunika lakini nilikuwa nishangaa ni kwa Nini braza ajiue wakati wanawake wapo wengi


Aise usiombe ikakukuta yaani hauoni another option Zaid ya hiyo ya kujiua ,

Yule mwanamke niliemuoa alikuwa single mother wa watoto watatu ,nae sijui alikuwa na mental trauma alikuwa ni mkorofi sana anapenda kugombana yaani ukimkosea kidogo tayari makofi
Sasa nikaona uyu tunaweza Kuna kuumizana tulibahatika kupata nae mtoto mmoja wa kike ,lakini baadae ilibid niachane nae

Mwaka huu nimeoa mke mwingine naomba mungu sana anijaalie nidumu na uyu,

Baadae yule mke wangu wa kwanza alinitafuta na kuniomba msamaha ilikuwa bado sijaoa uyu wa tatu lakini nikaona haina haja ya kuwa na mtu asie na msimamo

Ndio maana nikaona nioe tu mtu mwingine

Sasa tabu ninazopata kutoka kwenye familia yangu ni ;-

1 wazazi na ndugu hawaniongelei vizuri pindi ninapo oa ,mke wa kwanza waliongea Mambo mengi sana hasa mama

2-hata ukitoa msaada hawathamini siku ukiombwa na ukawa huna basi ni maneno mabaya mabaya wanakuongelea

3- mama Sasa hivi ameshazeeka lakini bado anang'ang'ania kufanya zile shughuli za uvuvi Kila siku ni kupoteza pesa ,anahitaji nimnunulie mashine lakini Mimi naona ameshachoka halafu Kuna wadogo zangu wapo chuo nikinunua hiyo mashine nitashindwa kuwasapoti

4 - nimeoa mke wa tatu ,mama alitoa maneno mabaya sana but Sina Cha kufanya Zaid ya kumshukuru mungu

Kule nilipohamishwa nilitengeneza mazingira mazuri sana lengo langu ni kufungua kampuni
Ambayo itakuwa ina deals with

1 .Agroproduction (kilimo na ufugaji )
Yaani na Lima nafuga pia nakuwa na mashine za kusanga na kukoboa halafu nafunga kwenye viroba nauza

2.viwanda vidogo vidogo kama mikate na mashine ya kuprocesa ngozi

3.usagirishaji (magari ya abiria

4.duka la dawa , zahanati na maabara

5.maduka ya jumla

6 .magari ya mizigo

Naamini nitafanikiwa kwa sababu naona kabis siwezi kubadili maisha yangu kwa kazi za kuajiriwa Tena humu serikalini kulivyo na changamoto

Ndio hivyo ndugu zangu ,naombeni ushauri wenu nifanye Nini ili niweze kufikia malengo yangu

Dunia tunayoenda nayo ni ngumu sana

Mwisho



Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
Nduguyangu,mm mwenyewe ni Dr.kama ww hapo nanipo serikalini,,napia natokea hukohuko kanda ya ziwa,ushauri wangu mkuu,nikua kwanza pole kwa changamoto nyingi sana,kingine nikua malengo yako uliyoyaorodhesha hapo nimengi,mazuri nayenye kukukwamua kimaisha nakua mtu mwenye mafanikio,ila ningumu snaa narudia tena ningumu mno kuyatekeleza ukiwa umeajiriwa ktk hizi ajira zetu za serikali cjajua utachanga vipi karata zako hadi ufanikiwe kuwa mfanya biashara wa ku-run hizo business at the same time ukiwa muajiriwa wa serikalini kwenye changamoto lukuki,nakusihi jaribu kuacha kazi baada ya kua umepata mtaji either kwa kukopa then fanya mradi kama ulivyokua unafanya kule dar kabla hujaajilwa serikalini hapo unaweza kuadvance kabla hujawa mzee,naimani naww nikijana wa below40 tu.nawasilisha!!!!
 
Ndugu na wanawake ndo wanakurudisha nyuma

Usiwape kipaumbele maana binadamu hajawahi kuridhika hata ufanye nini..so focus on yourself
 
Back
Top Bottom