Tafakari juu ya maisha ya watu mashuhuri kama Prof. Jay na uhalali wa kuomba michango ya matibabu

Wabunge wa Chadema wakistaafu wanakuwa maskini kwa sababu mishahara na posho zao zinaishia kwenye kuchangia chama.

Ndio maana Halima Mdee na wenzake wakachukua maamuzi magumu.
Hoja hafifu

Kuchangia 10-15% ya mshahara hakumfanyi mtu kuwa masikini

Hoja hapa ni kwanini mtu aliyekuwa anavuta atleast TZS. 11,000,000/- tax free kila mwezi kwa miaka mitano mfululizo plus gratuity ya TZS. 250,000,000/- leo anageuka kuwa Matonya

Vijana mna la kujifunza hapa. Bata liende na investments
 
Umewaza vyema ila Mimi kitu sijapenda ni Ile familia kwenda redion kuomba msaada wa kuchangiwa mtu Kama Prof aisee ni aibu Sana kwa familia ni Bora wasingetangaza kuomba mchango sababu naamini Prof ana marafiki wengi Sana wenye uwezo ni legend kwenye gem amewahi kua mbunge ana marafiki wengi Sana wenye nyazifa serikalini mi naamini hawa wote wangetosha kabisa kusolve hii kesi bila kwenda kuomba msaada redion

Ivi wanamuziki wanaochipukia wenye ndoto za kufanikiwa kimuziki wakiona legend Kama Prof ameugua ameshindwa kujitibu how do they feel kwenye career yao
 
Kikubwa tumuombee kwa Mungu apone....mengine tutajadili akiwa mzima kama ni lazima kuyajadili
 
Hivi ruge na hela zote zile plus familia anayotoka ilikuwa vzr na marafiki wenye hela bado waliomba michango,na serikali ikaingilia kati, imekaaje hii?
ni upumbavu kumchangia aliye nacho,
kama nina 100k, nawezachangia kadhaa walioshindwa na matibabu ya 20k ( ambayo serikali imewaignore ) kisha kupoteza maisha
 
Hivi ruge na hela zote zile plus familia anayotoka ilikuwa vzr na marafiki wenye hela bado waliomba michango,na serikali ikaingilia kati, imekaaje hii?
Serikali kuingilia sio ishu sababu Ali play part kwa kuisaidia serikali kumotivate ajira kwa vijana hivyo ana icon ya kukumbukwa kiserikali ishu ni Ile kutangaza kuomba mchango kwa watu wa kawaida ni kujidhalilisha
 
Siri ya mtungi aijue kata...

Msione watu wapo vizuri kwa nje, maisha ya mtu ni siri yake mwenyewe...
 
Umeandika point watanzania wengi sijui ni ujinga jay amejitengenezea brand jina lake linamuuza.

Sent from my VFD 600 using JamiiForums mobile app
 
Watanzania wanashindwa kuhukumu maneno ya mtoa mada wanabaki kusema yule n jina kubwa Mara ugonjwa usikie kwa mwenzio Mara Ile n kisiasa sasa n hv.

Kwa status ya Joseph Haule n tayari tunajua yupo mbele kwa hatua ya maisha ya usanii na connection zake, siasa na connection zake na uhalisia wa maisha yake na connection zake.

Serikali ikitoa pesa Mana yake wametumia Kodi za wananchi bila kujali anachangia kidogo au kikubwa swala Ni je kwa mtanzania Kama Mimi ninaeishi maisha ya kawaida Tena Bora hatasie tunaweza kukoment JF vp wale ambao hata simu tuu anaisikia kwa jirani kwa zaidi ya miaka 10 au 20 kwa maana hata uwezo wa kutoa 50k kununua simu n shida vp akipatwa na gharama ya matibabu ya 75k kwasiku serikali itamlipia? Au serikali ishalipia wangapi wa nama hyo au ndo Ivo tunaenda kuuza Nyumba na bado mgojwa haponi tunakuwa tumekosa kotekote.

Kwakua pesa za serikali n zao la juhudi la kulipa Kodi kwa watanzania hvyo hzo n pesa za watanzania Sasa serikali kwakua imeona afya ndio msingi wa yote kwanini wasiseme matibabu n bure au ilete utaratibu wa kila pesa unayopata Basi 1% ya hyo pesa inaenda kwenye mfuko wa afya ili watanzania wote tuwe na uhakika wa afya Bora?

Kama Jay wa mitulinga anachangiwa vp kina uwoya na kupiga picha anachezea pesa akiumwa nae achangiwe?
Je wazee wetu huko vijijini na wale wengi wasiojiweza wakiumwa watasaidiwa na Nani?

Kwani Jay anaumwa Nini?.
 
Povu, wivu na roho mbaya sasa zinatoka wapi, wewe kwa akili yako ulivyosikia Jay na habari zakuchangiwa

Moyoni tu lazima kichwa chako kijiulize how kwanini anachangiwa,
 
Mchonga alikuwa Rais kwa miaka 20+ lakini alipoumwa ilibidi aombe msaada wa Serikali na inasemwa walimsubirisha muda mrefu sana
sasa prof kuwa mbunge miaka 5 ndio iwe ajabu kusaidiwa
 
Mbona Ndugai tena akiwa Spika alishindwa kujilipia mabilioni huko India?

Mbona Tundu Lisu akiwa mbunge alishindwa kujilipia Nairobi hospital?

Kinachoangaliwa ni ukubwa wa tatizo, muda wa matibabu na gharama husika.

Serikali siyo wajinga kukubali kumlipia Prof Jay.

Punguza mbege.
 
Povu, wivu na roho mbaya sasa zinatoka wapi, wewe kwa akili yako ulivyosikia Jay na habari zakuchangiwa

Moyoni tu lazima kichwa chako kijiulize how kwanini anachangiwa,
Mtu anaumwa mnahoji kuhusu hela?
Shame on you!
 
Kuumwa kwa Jay kuwe wake up call kwa serikali kuja na "universal health for all". Kuna haja ya afya kuwa agenda ya kitaifa kwa sasa.
 
Mtu anaumwa mnahoji kuhusu hela?
Shame on you!
Nani kahoji kuhusu hela tumia akili usitumie makalio kufikiri

Sio tunahoji ni vile mtu unawaza kwa hali yake ya uchumi na jinsi hali ya uchumi ya watz ambao unaweza kuta ugonjwa wao ni zaidi ya proff jay na uchumi wao ni mdogo
 
Asee nimeshangazwa sana asee watu wanahoji hela kwenye uhai wa mtu?
 
Mchonga alikuwa Rais kwa miaka 20+ lakini alipoumwa ilibidi aombe msaada wa Serikali na inasemwa walimsubirisha muda mrefu sana
sasa prof kuwa mbunge miaka 5 ndio iwe ajabu kusaidiwa
Hapa unahitaji kuthibitisha!
Mimi ni shabiki wa Mwalimu, labda ungesaidia kwa kuanza kueleza ni nani kwa wakati huo aliyekuwa na jeuri ya kumsubirisha Mwalimu kisha ndo useme, msaada upi Mwalimu aliomba kutoka serikalini.

Utanisaidia sana kumfahamu zaidi huyu mwamba ninayemshabikia, ukijazia hizo info kwenye ufahamu wangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…