Tafakari yangu juu ya Wasomi-Masikini wa JF

Tafakari yangu juu ya Wasomi-Masikini wa JF

Wakili wa shetani

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2022
Posts
1,726
Reaction score
3,391
Juzi kati nilikuwa nazungumza na madogo fulani wawili kuhusu Jamiiforums. Wale madogo wakasema kuwa hawajawahi kuisikia Jamiiforums!! Nilishangaa sana, ni madogo wenye kazi na wako active kwenye mitandao ya kijamii. Yaani mtandao upo tokea mwaka 2006 hawajawahi kuusikia!!? Licha ya hayo, ukifanya search ya mambo mbalimbali ya kiswhili utakutana na links za JF. Inamaana hawajawahi kufanya hivyo!! Nikasema pengine JF si muhimu kama ambavyo members tunaichukulia.

Sasa juzi kukawa na habari ya watu kulizwa na upatu wa MTFE, nikakaa nikatafakari na kuona kuwa mtu wa JF hawezi kupigwa kirahisi na kitu kama hicho, members humu ni wasomi wanaochambua mambo kwa kina. Pia ni masikini wenye tahadhari na pesa zao na wanaopeana tahadhari hizo. Ni watu wanaoangalia mambo kwa uhalisia wake. Tafakari yangu ikanipeleka mpaka kwa madogo wale. Nikaona kuwa kwa kutoijua kwao JF wako vurnerable kwa mambo mengi sana. Kila siku tunajiuliza ponzi schemes zinapata wapi wajinga wa kuwapiga, nikagundua ni kama wale madogo.

Taarifa ni ulinzi dhidi ya mambo mengi sana. Tafakari ile ilinifanya nione kuwa JF ni muhimu kuliko tunavyoichukulia.
 
Juzi kati nilikuwa nazungumza na madogo fulani wawili kuhusu Jamiiforums. Wale madogo wakasema kuwa hawajawahi kuisikia Jamiiforums!! Nilishangaa sana, ni madogo wenye kazi na wako active kwenye mitandao ya kijamii. Yaani mtandao upo tokea mwaka 2006 hawajawahi kuusikia!!? Licha ya hayo, ukifanya search ya mambo mbalimbali ya kiswhili utakutana na links za JF. Inamaana hawajawahi kufanya hivyo!! Nikasema pengine JF si muhimu kama ambavyo members tunaichukulia.

Sasa juzi kukawa na habari ya watu kulizwa na upatu wa MTFE, nikakaa nikatafakari na kuona kuwa mtu wa JF hawezi kupigwa kirahisi na kitu kama hicho, members humu ni wasomi wanaochambua mambo kwa kina. Pia ni masikini wenye tahadhari na pesa zao na wanaopeana tahadhari hizo. Ni watu wanaoangalia mambo kwa uhalisia wake. Tafakari yangu ikanipeleka mpaka kwa madogo wale. Nikaona kuwa kwa kutoijua kwao JF wako vurnerable kwa mambo mengi sana. Kila siku tunajiuliza ponzi schemes zinapata wapi wajinga wa kuwapiga, nikagundua ni kama wale madogo.

Taarifa ni ulinzi dhidi ya mambo mengi sana. Tafakari ile ilinifanya nione kuwa JF ni muhimu kuliko tunavyoichukulia.
Kama mtu hata hajui umuhim wa taarifa ya habari ya saa2 usiku, huyo ni ngumu kuifaham jf.
 
Hakuna kitu kama hicho, hiyo ilikuwa JF ya zamani not now! Humu kuna chekechea wa siasa uchwara! Weka topic yenye kuhitaji intellectual higher mental faculties to discuss, watakuja watano kama siyo zero responses!
Unaweza kua sawa kua sasa hivi hakuna watu wenye uwezo wa kuchambua mada nzito. Ila kitu naamini JF members wake wapo na intellectual capacity nzuri kuliko huko mitandao mingine FB, Insta na Twitter.

Hao unaowaona huko wanajua humu ndani pia wana accounts zao.
 
JF kunamadini sana sema tu wapo Chekechea baadhi wanaharibu jukwaa. Ishu za Vanilla, MTFE, upatu, bank nyonya damu, DECI vimejadiliwa sana huku. Kwa mtu msomaji huku huwezi tapeliwa kidhembe hivyo. Jana naona wazee wa Vanilla wameng'ang'ania mkuu wa mkoa Kigoma awasaidie kuwaokoa na wazee wa vanilla
 
Back
Top Bottom