Tafakuri: Kuna nini nyuma ya mashambulizi haya kwa Makamba?

Yani afanye hujuma Halafu tiss wanamuangalia tu ! Mkuu labda hujui gvt coordination inavyofanya kazi kila waziri na wizara kuna nyoka maalumu wanaoripoti kwà mama direct kila kitu sasa hiyo hujuma anaifanyia wapi?


Bora hao tiss wangeripoti kwingine,mama,anayetafuta backup 2025?
 
Yani afanye hujuma Halafu tiss wanamuangalia tu ! Mkuu labda hujui gvt coordination inavyofanya kazi kila waziri na wizara kuna nyoka maalumu wanaoripoti kwà mama direct kila kitu sasa hiyo hujuma anaifanyia wapi?
Tiss hawawezi kua na Nguvu Kama kiongozi no 1 hajaona mapunguf yake na kukekemea.

Tulikua na sabaya,musiba n.k
Wamefanya maovu mengi ila kwasababu kiongozi no 1 hajakemea Basi yalionekana Ni mema TU na hao hao TISS waliufyata

Tatizo la nchi hii Ni mfumo
Maamuz makubwa ya Nchi hii yanategemea upepo wa raisi unavuma kuelekea wapi mkuu.
 
Sukuma gang walichukia sana mtu wao Kalemani alipotumbuliwa na kuteuliwa Makamba. Hiki ndicho chanzo cha chuki.

Kalemani, Msukuma, Gwajima, Kabudi, prof. Mkumbo, n.k ni nyoka wa sukuma gang
Mnakosea Sana kuleta ukanda kwenye Mambo muhimu yanayogusa watanzania wote.

Suala la umeme kukatika katika linahusu nchi nzima na sio jamii ya wasukuma Wala wamakonde au wachaga & etc.

Na sio kila anaemkosoa makamba Basi Ni msuk, pro-magufuli au anautaka uwaziri wake.
 
Mawaziri ni wanasiasa wanaosimamia sera ambao kuwepo au kutokuwepo kwao shughuli za moja kwa moja za wizara zitafanyika kama kawaida kupitia makatibu wakuu na wataalamu wao.
Kelele zote hizi ni matokeo ya siasa za kijinga na hasa hasa uchawa uliojitokeza sana siku hizi.
 
majinga machache tu yenye udini na ukabila ndo yana chuki nae. Ni mwanadamu ana makosa yake. Ila anakosolewa kwa chuki za sukumagang majinga yale
Wanaomkosoa makamba,
wengi wanamkosoa kwa hoja na kueleza wazi mapungufu yake kiutendaji.

Ila wengi wanaomtetea makamba,
wanajaribu kuhamisha mjadala na kuufanya too personal kwa kutokujibu hoja na kuegemea upande wa chuki,wivu au husda kwenye uwaziri wake.

Hivi kwani tangu Uhuru hii wizara imepata mawaziri wangapi wa nishati Kias kwamba yeye TU ndio ionekane anaonewa wivu na wenzake?

Hivi hii wizara inaingiza sh. Ngapi kwamba ionekane Ndio wizara Lulu kuliko wizara nyingine zote?

Mbona malalamiko ya makamba hatuyaskii wizara ya utalii, wizara ya madini, na wizara nyingine zenye mafungu lukuki?
 
Haileti mantiki wala maana kumlaumu Makamba kwasbb ya kukatika kwa umeme. Hoja hii ya kipuuzi lazima ijibiwe kipuuzi.

Ndiyo! Ni upuuzi kusema kwamba amakamba anakata umeme. Anaukataje? Yaani yeye kama waziri ana mamlaka ya kuukomoa umma wa watanzania wote mpk mhe rais? Kwamba akate umeme huku rais , makamu wa rais na waziri mkuu wakimuangalia tu?

Makamba akate umeme nchi nzima vyombo vya ulinzi na usalama vikimuangalia tu? Hujui kuwa umeme ni uchumi? Kwahiyo Makamba awe anaharibu uchumi halafu anatazamwa tu? Acheni porojo.
 
Tatzo la nchi hii waziri ana kauli na maamuz zaid kuliko katibu wa wizara na wengineo.

Waziri akiwa mjuaji sana na kujifanya geneous. Wizara nzima inageuka shaghala bhagala.
 
Soma comment namba 26
 
Kwani mfano mzuri sabaya kipindi Cha magu anahujumu wafanyabiashara, ananyanyasa watu

hao mawaziri wakuu, Raisi na wengineo uliowataja hawakuepo?

Mbona magu alipofariki ndio akaonekana alikua na hatia.

Ndo hivyo hivyo umeme unavokatika tunavomlaumu makamba maana ndio top kimaamuzi khs wizara husika.

Kwa nchi Hii
matokeo mazur ya wizara yanategemea utendaji mzur wa waziri husika.

Rejea kipind Cha jpm Yuko ujenzi,
Kila mtu aliona utendaji wake na wengi tuliusifia.

Juzi TU Hapa tamisemi alikuepo mchengerwa, kila mtu alimsifia.

Lukuvi kule ardhi,
Kila mtu aliiona kazi nzur aliyoifanya.

Mkuu,
Kazi nzur haijifichi, makamba kiukweli anapwaya Sana.
 
Hatumpendi. Full stop!
 
Poor you!!!
Maisha yake unayajua vzr ee?!!

Kwa hoja mfu kama hizi zenu basi ni sawa tu aendelee kujiona yuko smart kwani ni kweli yuko hatua nyiiingi mno mbele ya upeo wenu nyie.

Amekubabaisha nn na kivipi?

Kwani hapo alipo aliombewa na nani?!!!
Wewe, zaidi ya chuki kwa huyo Makamba, unakijua nn tukuombee?!!!
Kati yenu na yeye nani anatukana?!!
 
Hawezi kuonwa vizuri kwa kitendo cha kusimama juu ya JNHEP na kuanza kuporomosha kejeli na kutoa kauli za uongo uongo.
We ndo walewale tu, KEJELI ZIPI?!! KAZITOA LINI, WAPI NA KIAJE?!!!!!!
 
Bila shaka aliyekomenti hii katoroka milembe hospital?
 
Akili yako wewe mleta mada na makamba hakuna tofauti, wote ni mabwege na wababaishaji tu. Hakuna cha maana ulichomsemea, yani ni sawa na majibu yake, vyote ni porojo tu.
 
Yani afanye hujuma Halafu tiss wanamuangalia tu ! Mkuu labda hujui gvt coordination inavyofanya kazi kila waziri na wizara kuna nyoka maalumu wanaoripoti kwà mama direct kila kitu sasa hiyo hujuma anaifanyia wapi?
Hizo ripoti is nothing kama hakuna nia ya kutake action kwa mwenye mamlaka.

Kama aliyemweka anaona hizo ripoti majungu tu basi hali itabakia kama ilivyo.

Mifano ipo mingi ya aina hii.

Kuhusiana na umeme inaonekana kama anajihujumu mwenyewe maana kabla ya yeye kuwa waziri umeme haukua tatizo ila kwa sasa ni tatizo na ananekana kupigia debe wazi wazi biashara za watu.(gesi).

Kwanini asiulizwe??

Nchi sio ya mama yake, atambue hilo. Ni ya kila Mtanzania na ataulizwa maswali muda wowote ule.

Kama hataki maswali aache hiyo nafasi maana sio lazima sana awe kiongozi.
 
Mtatumia kila njia kumsafisha
ila ubovu wa makamba hasa suala la kukatika katika ovyo na mgao wa umeme hauhitaji elimu ya chuo kikuu kugundua kua jamaa Ni mbabaishaji au anatuhujumu kwa maksudi kabisa.
Wazoefu wa maisha ya hapa nchini wanajua vizuri kuwa kukatika kwa umeme hakujawahi kuisha nchi hii enzi na enzi......labda mwenzetu ulikuwa unaishi nje ya nchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…