FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 100,246
- 123,145
Tafakuri yangu leo imenikumbusha Sana Dar ya zamani 60s na 70s.
Wale wanaoikumbuka Dar na Tanzania ya zamani tukumbushane, si lazima iwe 60s na 70s, nimeweka kigezo hicho binafsi kwani ndipo zamani kwangu. Wengine mnaweza kuweka zamani yenu.
Nnaanza na Dar kwani ndipo makazi yetu miaka hiyo na sehemu zingine Tanzania ntagusia kumbukumbu zangu huko nilipopata fursa ya kupatembelea miaka hiyo.
Dar.
Nakumbuka , viwanja vya mnazi mmoja tulipoenda kutazama sinema za tarehe 3 (Aspro) kama sikosei na nyingine ilikuwa tarehe ngapi sikumbuki lakini nadhani ilikuwa ya sabuni za Omo.
Hao walikuwa wanavuta watu wengi sana wa viunga vya Kariakoo na jirani jirani miaka hiyo kujankutazam sinema za bure huku wakifanya matangazo ya biashara zao.
Hiyo ni fungua dimba nitaendelea na mengine uzi unavyoendelea.
Karibuni nanyi mlete kumbukumbu zenu za popote mlipokuwa.
Wale wanaoikumbuka Dar na Tanzania ya zamani tukumbushane, si lazima iwe 60s na 70s, nimeweka kigezo hicho binafsi kwani ndipo zamani kwangu. Wengine mnaweza kuweka zamani yenu.
Nnaanza na Dar kwani ndipo makazi yetu miaka hiyo na sehemu zingine Tanzania ntagusia kumbukumbu zangu huko nilipopata fursa ya kupatembelea miaka hiyo.
Dar.
Nakumbuka , viwanja vya mnazi mmoja tulipoenda kutazama sinema za tarehe 3 (Aspro) kama sikosei na nyingine ilikuwa tarehe ngapi sikumbuki lakini nadhani ilikuwa ya sabuni za Omo.
Hao walikuwa wanavuta watu wengi sana wa viunga vya Kariakoo na jirani jirani miaka hiyo kujankutazam sinema za bure huku wakifanya matangazo ya biashara zao.
Hiyo ni fungua dimba nitaendelea na mengine uzi unavyoendelea.
Karibuni nanyi mlete kumbukumbu zenu za popote mlipokuwa.