Tahadhali kwa wenye mamlaka: Watu wamekataa tamaa na hawaogopi tena risasi wala kukaa mahabusu au kwenda jela

Tahadhali kwa wenye mamlaka: Watu wamekataa tamaa na hawaogopi tena risasi wala kukaa mahabusu au kwenda jela

Jana niliweka uzi hapa nikionya watawala kuwa unyanyasaji ukizidi, unafanya watu wafike point of no return na wanakuwa tayari kwa lolote: kuuwawa, kuumiziwa, kufungwa jela, n.k.

Nilisema kadri watu wanavyouwawa, kuteswa, kupotezwa, n.k, wanaobaki wanajengea ujasiri na wanafikia hatua wanaona na wao hawana tena cha kupoteza na hiki ndio sasa kinakwenda kutumia. Tunakwenda kubaya.

Leo kupitia mtandao wa X, viongozi wakuu wa CHADEMA (Mbowe na Lissu) wameonyesha kuwa wako tayari kwa lolote hata kama ni kwa kupoteza uhai wao wataandamana(wamethibitisha maneno yangu)

Nilitamani sana maneno niliyoyasema mimi yangesemwa na watu wenye kuheshimika na wenye ushawishi katika jamiii, labda ujumbe ungewafikia watu wengi zaidi na ungepewa uzito.

Ni bahati mbaya watu wenye ushawishi wamechagua kukaa kimya, ila nawaambia mtawasikia wakitoa kauli baada ya mambo kuharibu.

Tunamshukuru Mzee Butiku kwa kusema aliyoyasema walau yeye katimiza wajibu wake.

Katibu Mkuu wa CCM, Dr. Nchimbi hakuwa serious katika hotuba yake ya hivi karibuni, hivyo sioni kama alikuwa na msaada wowote kwa chama chake na Taifa kwa ujumla.

Uzi husika ni huu:


Niliyoyasema ndio haya yameanza kutimia:
Leo mtashuhudia miujiza jinsi risasi zitagoma kutoka kwenye Magazine.

Mungu wetu sio Mungu Dhaifu
 
Back
Top Bottom