Tahadhari: Huyu ni tapeli wa Kujiaminisha?

Tahadhari: Huyu ni tapeli wa Kujiaminisha?

Naomba nikiri hoja yangu imelenga kuleta hoja vijana wajitume na sio kuwa ombaomba ilihali wana nguvu.
View attachment 2933415

Mwaka 2023 mwezi wa 5 nikiwa natembea maeneo ya Ubungo jirani na NBC bank alikuja kijana ambaye anaonekana kwenye video hapa na akaniambia yeye ni mwalimu amemaliza SUA na amepata kazi Songwe hivyo anaomba nimuongezee nauli ili aweze kufika. Alinifuata kwa nidhamu na kwa namna alivyokuwa akiongea (Angalia hata hii video hapa anavyojieleza kwa ustadi) niliamini kweli ni mtu mwenye elimu yake na pengine kweli hana kazi ndio amepata. Nikaona si vibaya nikijigeuza kuwa malaika wa zamu kwake ili afanikishe safari ya kwenda Songwe alipodai amepata kazi. Nikamuuliza nauli akanitajia na na akasema aka niasi kidogo kama elfu 10, nikampa, Sikumbuki ni kiasi gani ila kama sio kwenye 40,000 maana nilihakikisha nampa nauli ya kumfikisha. Akanishukuru sana akanipa na namba yake but sikuiSave kiukweli (Good enough alikuwa na smartphone)

Tarehe 10 Machi, Mwaka 2024 nikiwa kwenye gari nimetoka Mazimbu naenda mjini, nimefika na kusimama sehemu ya mataa, Mtu yuleyule niliyemsaidia nauli ya kwenda Songwe kwenye kazi, nimekutana nae tena na akagonga kioo na kuomba nisimame mbele baada ya mataa. Mawazo yangu nikajua pengine ameniona na amenikumbuka anataka kunishukuru kwa msaada niliowahi kumpa, Baada ya kuvuka mataa na kusimama kumsikiliza pengine anashukuru kwa msaada wa awali, nikashangaa analeta maombi ya aina ileile.

Bahati mbaya baada ya kumwambia siku nyingine aliondoka na wakat namuita ili nimkumbushe akawa ameondoka hakutaka hata kusikiliza. Wakati namtafakari hasa kuwaza umbali wa kutoka relini ambako amedai aliponiona ndio amenikimbilia, nikakumbuka kuwa Dashboard camera yangu ilikuwa on nikataka kuprove kweli aliniona tangu relini? nikaendelea kujiridhisha kuwa ni Muongo.

Baada ya kutembea takriban Mita 400 kutoka relini, (sehemu ambayo yeye alisema ndipo aliniona na kunikimbilia) ndipo alionekana akitembea kuelekea uelekeo ambao nilikuwa nakwenda kupitia camera ya mbele. Nilipofika usawa wake mbele kidogo ndipo alionekana kuangalia gari kupitia camera ya kulia. ndipo akaamua kuja na kuvuka upande wa abiria kama anavyoonekana kupitia camera ya nyuma. na hatimaye maelezo yake ni kama anavyoonekana kupitia camera ya kushoto japo hajaonekana vizuri.

Tujihadhari na huyu mtu ni wazi atakuwa ndio mchezo wake kujipatia pesa kwa udanganyifu na pengine kafanya hivyo mikoa mingi.

Tazama Video nilipokutana nae Morogoro


View: https://youtu.be/sd2-OcpDkv0


UPDATE ZA ZA WADAU WENGINE WALIOKUTANA NA HUYU BWANA:

Na wewe ni yuleyule, mbona picha zote mbili zimepigwa siku moja sehemu moja. Picha ya kwanza inaonesha shati alilovaa ndilo alilovaa Moro na ukuta unaoonekana Ubungo ndio unaonekana Moro. Kwa hali hii atakuwa amekuambukiza kusema uongo au nia yako ni kutuonesha unayo gari yenye kamera, kama ni hivyo hongera.
 
Na wewe ni yuleyule, mbona picha zote mbili zimepigwa siku moja sehemu moja. Picha ya kwanza inaonesha shati alilovaa ndilo alilovaa Moro na ukuta unaoonekana Ubungo ndio unaonekana Moro. Kwa hali hii atakuwa amekuambukiza kusema uongo au nia yako ni kutuonesha unayo gari yenye kamera, kama ni hivyo hongera.
Picha na video zote ni za Morogoro. Kama umeangalia vizuri hiyo picha imekuwa captured toka kwenye video hiyohiyo ya Morogoro.
 
Watu kama hawa ukitaka kiwakomoa wapeleke stand uwalipie nauli umpe tiketi. Kama muda upo hakikisha anapanda bus na kuondoka. Ukigundua ni Tapeli, Piga picha tuma hata polisi waendelee na majukumu ya kunyoosha taifa.

Tusiache kutenda mema, maana wengine kwa kufanya hivi wamewasaidia na malaika -Biblia
Polis hawa hawa
 
Miaka hiyo nipo dukan mwenge nauza nguo. Akaja mzee mtu mzima. Akasalimia then akaniambia mwanangu Mimi baba yako nina shida ya nguo unaona nilizovaa zilivyoisha na kweli amevaa matambara ya kutosha. Kabla cjamjibu akashuka chini akapiga sala flan ya kiislam huku akinisih Mungu atanibariki. Basi mi nakuonea huruma nikamfungia nguo za kutosha na viatu juu. Haijapita mwez mzee akajichanganya dukan kwangu kkoo kwa style ile ile nilimtukana akaondoka kimya kimya.
 
Utashangaa kusikia huyo jamaa nimekumbana naye Dar, Morogoro na Mbeya. Mbeya nami nikiwa napita kama mgeni, nikiwa nimepaki gari pembeni ya barabara, huku mwenyeji wangu kaniachia usukani, (mwenyeji aliingia ofisi za ardhi) mara paapu, akatokea huyo jamaa (anachagua watu). Akajifanya alikuwa anafanya kazi kama intern ofisi za ardhi Mbeya kipindi cha Lukuvi. Akasema hawajalipwa bado pesa za miezi kadhaa, hivyo anaomba msaada aisitiri familia yake. Nikasema bwana mimi miguu hata haijapoa moto na ndio nimefika tu Mbeya kwa mtu, kawaombe wenyeji wenye pesa. Aliniharibia siku. Dar vuupu, karibu na Mlimani City, story zilezile, mara mji kasoro bahari akajihusisha na SUA kusoma Master. Nikamwambia shida ukiwa tapeli unahitaji usiwe unasahau, ukisahau utakuja kukamatwa. Nilidhani Afro zangu au rangi yangu ni rahisi kunikumbuka na kunikwepa. Nikamwambia utakufa maskini.

Huyo mjamaa ukisema huna pesa, au ukashtuka, atakufanya nafsi yako ijutie. Utajiona kama shetani, kumbe yeye ni tapeli kubwa. Wako wengi matapeli wa namna hiyo.

Naomba nikiri hoja yangu imelenga kuleta hoja vijana wajitume na sio kuwa ombaomba ilihali wana nguvu.
View attachment 2933415

Mwaka 2023 mwezi wa 5 nikiwa natembea maeneo ya Ubungo jirani na NBC bank alikuja kijana ambaye anaonekana kwenye video hapa na akaniambia yeye ni mwalimu amemaliza SUA na amepata kazi Songwe hivyo anaomba nimuongezee nauli ili aweze kufika. Alinifuata kwa nidhamu na kwa namna alivyokuwa akiongea (Angalia hata hii video hapa anavyojieleza kwa ustadi) niliamini kweli ni mtu mwenye elimu yake na pengine kweli hana kazi ndio amepata. Nikaona si vibaya nikijigeuza kuwa malaika wa zamu kwake ili afanikishe safari ya kwenda Songwe alipodai amepata kazi. Nikamuuliza nauli akanitajia na na akasema aka niasi kidogo kama elfu 10, nikampa, Sikumbuki ni kiasi gani ila kama sio kwenye 40,000 maana nilihakikisha nampa nauli ya kumfikisha. Akanishukuru sana akanipa na namba yake but sikuiSave kiukweli (Good enough alikuwa na smartphone)

Tarehe 10 Machi, Mwaka 2024 nikiwa kwenye gari nimetoka Mazimbu naenda mjini, nimefika na kusimama sehemu ya mataa, Mtu yuleyule niliyemsaidia nauli ya kwenda Songwe kwenye kazi, nimekutana nae tena na akagonga kioo na kuomba nisimame mbele baada ya mataa. Mawazo yangu nikajua pengine ameniona na amenikumbuka anataka kunishukuru kwa msaada niliowahi kumpa, Baada ya kuvuka mataa na kusimama kumsikiliza pengine anashukuru kwa msaada wa awali, nikashangaa analeta maombi ya aina ileile.

Bahati mbaya baada ya kumwambia siku nyingine aliondoka na wakat namuita ili nimkumbushe akawa ameondoka hakutaka hata kusikiliza. Wakati namtafakari hasa kuwaza umbali wa kutoka relini ambako amedai aliponiona ndio amenikimbilia, nikakumbuka kuwa Dashboard camera yangu ilikuwa on nikataka kuprove kweli aliniona tangu relini? nikaendelea kujiridhisha kuwa ni Muongo.

Baada ya kutembea takriban Mita 400 kutoka relini, (sehemu ambayo yeye alisema ndipo aliniona na kunikimbilia) ndipo alionekana akitembea kuelekea uelekeo ambao nilikuwa nakwenda kupitia camera ya mbele. Nilipofika usawa wake mbele kidogo ndipo alionekana kuangalia gari kupitia camera ya kulia. ndipo akaamua kuja na kuvuka upande wa abiria kama anavyoonekana kupitia camera ya nyuma. na hatimaye maelezo yake ni kama anavyoonekana kupitia camera ya kushoto japo hajaonekana vizuri.

Tujihadhari na huyu mtu ni wazi atakuwa ndio mchezo wake kujipatia pesa kwa udanganyifu na pengine kafanya hivyo mikoa mingi.

Tazama Video nilipokutana nae Morogoro


View: https://youtu.be/sd2-OcpDkv0


UPDATE ZA ZA WADAU WENGINE WALIOKUTANA NA HUYU BWANA:
 
Watu kama hawa ndio wanaharibia wenye shida, dhiki na uhitaji hasa.

Nakumbuka mwaka 2017 nikiishi Ubungo nilitingwa sina kazi na sina hata mia mbovu MFUKONI sikuweza kuamini ilinibidi niombe kwa wasamaria hata hela ya kula njaa ilinikung'uta balaa

Akatokea mwanafunzi mmoja wa Udsm pale Mabibo hostel akanipiga tafu kwa kunipa 2k ndio nikaweza kupata chakula.

Natamani leo hii ningeweza hata kumtambua yule bro nimshukuru kwa moyo mkuu but ndio hivo tena.
Ninachoweza na mimi ni kusaidia pale ninapoweza until my last time.
 
Watu kama hawa ndio wanaharibia wenye shida, dhiki na uhitaji hasa.

Nakumbuka mwaka 2017 nikiishi Ubungo nilitingwa sina kazi na sina hata mia mbovu MFUKONI sikuweza kuamini ilinibidi niombe kwa wasamaria hata hela ya kula njaa ilinikung'uta balaa

Akatokea mwanafunzi mmoja wa Udsm pale Mabibo hostel akanipiga tafu kwa kunipa 2k ndio nikaweza kupata chakula.

Natamani leo hii ningeweza hata kumtambua yule bro nimshukuru kwa moyo mkuu but ndio hivo tena.
Ninachoweza na mimi ni kusaidia pale ninapoweza until my last time.

Mara nyingi ukitendewa wema na mtu sio rahis sana kurudisha wema kwake isipokuwa cha kufanya tenda wema kwa wengine. Jinsi unavyotamani kumpata na kumshukuru ndivyo Mungu alivyombariki na kufikisha shukrani zako kwake kupitia kwa watu wengine. Amani ya Mungu itawale kwako
 
Mimi juzi kati nilikuwa natoka tu kwenye ATM mahali, nakutana na kijana ananisimisha eti!

Kiukweli sikujishughulisha kabisa kusimama au kumsikiliza!! Maana nilijua angeniletea tu zile story za kuokota madini ya almasi, au kujifanya ana shida.
 
Nakumbuka siku moja Buguruni sheli dogo wa shule ya msingi alinifuata akaniambia anakaa G/mboto ana nauli nikampà jero baadae nikiwa bado niko hapo stendi nikamuona anaongea na mtu fulani nikamsogelea kimya kimya kumsikiliza anamwambia nini yule mtu nilikuwa nimeshahisi anampiga sound yule mtu na kweli nilimsogelea nikamsikia anadai Hela ya nauli nilimtimua yule dogo pale stendi.Mitapeli ya dizaini hii ipo mingi
Nazan hii tabia yakuomba nakujipatia pesa zabwerere inakautamu flan ivi .sasa mimi juzi tu hapa mzee mmoja kanifuata nakunipanga kijana sijala nisaidie nikaona sio kesi nikazama mfukon nikampa pesa kdg ,nimetembea hatua kama 6 nageuka nyuma nakuta anampanga tena dada mmoja nae bila hiana akazana kwene pochi akampa pesa ,chap akavuka rod akaenda kijiwe cha bodaboda nako akaanza kuwapanga sema wengi wakawa wanachomoa mpaka mmoja akajitolea kumpa chochote ndio akachomoka.nikajisemea kumbe uyu mzee mhuni nakwasiku itakuwa anakusanya maokoto yakutosha tu
 
Humu wapo sana katika sekta ya kuabisha watu wanafurahi sana ila sasa ukiwa unahitaji kazi hawakupi mtaji hawakupi.

Yaani maisha huwa ni mazuri endapo ukimkalisha nakumwambia sema ukweli usaidike naje tukijikusanya tukakufungulia kitu kidogo ujisogeze kimaisha wewe na watoto.

Humu mna ngo's nyingi ila kuwasaidia wenzenu mbaya kabisa . Hamtaki . Mtu kachanganyikiwa he needs help sio unafikoa hadi ubamrekodi yanini wewe mtoa mada unajiona halafu unajiita Amani ya Mungu huna hayaa
 
Watu kama hawa ndio wanaharibia wenye shida, dhiki na uhitaji hasa.

Nakumbuka mwaka 2017 nikiishi Ubungo nilitingwa sina kazi na sina hata mia mbovu MFUKONI sikuweza kuamini ilinibidi niombe kwa wasamaria hata hela ya kula njaa ilinikung'uta balaa

Akatokea mwanafunzi mmoja wa Udsm pale Mabibo hostel akanipiga tafu kwa kunipa 2k ndio nikaweza kupata chakula.

Natamani leo hii ningeweza hata kumtambua yule bro nimshukuru kwa moyo mkuu but ndio hivo tena.
Ninachoweza na mimi ni kusaidia pale ninapoweza until my last time.
pole sana ungekufa aisee
 
Back
Top Bottom