Tahadhari: Utapeli ndani ya benki

Tahadhari: Utapeli ndani ya benki

mimi humu nakuja kupoteza muda kama kijiwe cha kahawa
usichukulie mambo ya humu serious
Point mkuu. Unaweza ukaumia watu wanavyojibizana, kumbe wajitesa... Wao wanafahamiana.
 
Ni ujinga kuibiwa wakati umeenda Bank kufanya mishe zako tu......yaani huwezi jiuliza tu kuwa unapata 3m kirahisi ivyo......hata NMB Kkoo wapo kibao tu
Hawa watu ni wataalamu wa psychologia kabisa, unajua ww labda umeenda na laki yako hapo ya ada ya watoto tena umeipata kwa msoto kweli kweli, the moment unasikia 3m ya chap akili inaanza kupanga matumizi badala ya kufikiri hii fursa gani inanifuata kizembe hiv? na huwa wanaangalia na mtu kama kwako 3m ni hela ya kawaida hawawezi kuja koz wanajua hautapanic wanatafuta mtu ambaye hiyo hela hajawaza hata kuiona kwa pamoja licha ya kuimiliki
 
Hawa watu ni wataalamu wa psychologia kabisa, unajua ww labda umeenda na laki yako hapo ya ada ya watoto tena umeipata kwa msoto kweli kweli, the moment unasikia 3m ya chap akili inaanza kupanga matumizi badala ya kufikiri hii fursa gani inanifuata kizembe hiv? na huwa wanaangalia na mtu kama kwako 3m ni hela ya kawaida hawawezi kuja koz wanajua hautapanic wanatafuta mtu ambaye hiyo hela hajawaza hata kuiona kwa pamoja licha ya kuimiliki
Bado kwa mtu makini hata kama hiyo 3m kuipata au hujawahi kuishika ni uzembe mkubwa sana kukutana na mtu popote pale na yeye kuanza kuongelea kukunufaisha wewe hasa kipindi hiki cha uchumi mgumu na humjui......utaibiwa kama unatamaa tu na siyo vinginevyo
 
Bado kwa mtu makini hata kama hiyo 3m kuipata au hujawahi kuishika ni uzembe mkubwa sana kukutana na mtu popote pale na yeye kuanza kuongelea kukunufaisha wewe hasa kipindi hiki cha uchumi mgumu na humjui......utaibiwa kama unatamaa tu na siyo vinginevyo
Yeah ndo wanacho deal nacho wanaamsha tamaa za mhusika kama yupo makini mission yao itakuwa imefel kama kwa mtoa maada
 
Huu ni utapeli Wa kishamba sana.

Huwa najiuliza mtu unaingiaje tamaa Kwa pesa ambayo hujaitolea jasho mpaka unaenda kutapeliwa.

Tunduma pia nimewahi kuwaona hawa washamba, mmoja anajifanya anakupita Kwa kasi huku anaongea na simu halafu mbele anadondosha Bunda la minoti ili ushoboke, hujakaa vizuri mwenzake anakuovateki anajifanya kuziwahi hizo Pesa eti ameokota, sasa ukiwa na Tamaa za fisi kujifanya macho kuona anakushawishi umfuate ili mkagawane hizo pesa. Huko sasa ndiyo wewe unageuka Fursa.
 
Wasalaam Wakuu.

Ijapokuwa uzi kama huu ulishetwa humu juu ya utapeli ndani ya benki, lakini haukuwa umeshiba. Nikaona niwaeleze kwa undani ili tumakinike.

Kuna wale wanaopenda kujua kama nimetapeliwa ama la, ukweli ni kuwa sijatapeliwa. Ila walikuwa wanajaribu kunitapeli.

Leo asubuhi nilienda katika moja ya benki kubwa sana hapa nchini kwa nia ya kufanya miamala miwili mitatu. Sitapenda kutaja jina la benki.

Nilipofika nikaanza kujaza slip zangu. Kuna mtu (akaja pembeni yangu kwa ajili ya kujaza slip. Sikuwa na wasiwasi, nikaendelea kujaza. Nilipomaliza nikaenda kupanga foleni. Naye bila hiyana akaja kunifata kwa nyuma.

Nikakaa kama dakika mbili, akaja mwenzake. Anajidai kumuuliza, kaka ni wapi wanapobadilisha fedha za kigeni? Mimi sijawageukia nikaendelea kusogea.

Yule aliyeulizwa naye akanigusa, "eti kaka, ni wapi wanapobadilisha fedha za Kiarabu? Maana nami ni mgeni hapa". Mimi nikawaonyesha dirisha la Bureau De Change. Wakati nageuka kuwaonyesha, huyu wa kwanza akamchapa swali lingine. Kwani ni fedha zipi za kiarabu?

Jamaa akachomoa kitita kumuonyesha. Na mimi niliona pia. Kwa juu kulikuwa na noti ya dollar 100 (genuine) ya Kimarekani. Akamuuliza ni bei gani, akasema ni Dollar 15,000.

Akamuuliza kwa hiyo nitapewa bei gani kwa fedha za Kitanzania? Jamaa akachukua simu, akaenda kwenye Calculator akaandika 1,500 mara 2300. Akamuambia Utapata kama 34,000,000 TZS.

Nenda kabadili utawekewa kwenye akaunti yako. Akasema sasa sina hata akaunti ya benki. Na nasikia huwa wanauliza kiasi hiki chote nimekipata wapi. Akamuuliza, kwani wewe umekipata wapi? Akasema mishe za madini. Akamuambia hapo pagumu.

Akanigusa tena, akaniambia wewe unamshaurije jamaa? Nikamuambia aende huko ambapo hatoulizwa. Machale yakanicheza.

Jamaa nilipogeuka akamuambia, kwani wewe unatupa Tsh ngapi ili nikakubadilishie. Akasema atatoa million 3. Akamuambia fanya tano. Jamaa akalia akasema labda nne.

Akamuambia, sawa nenda nje nakuja. Huyo jamaa akasepa. Jamaa akaniuliza, twende tukachukue hela tupate cha juu.. Nikamuambia hapana..

Tukaendelea kusogea, nilipokuwa wa pili, jamaa ni watatu. Yeye pia mkononi ana slip yake. Kwamba anahitaji kuhudumiwa. Wakati wa mbele anapewa slip aondoke, akajifanya kupokea simu. Kwa hiyo hii hela nisikuwekee tena? Ahaa, nikuwekee M-Pesa eeh? Poa. Huyo akatokomea. Nikaendelea kuhudumiwa.

Tahadhari za kuchukua:
a) Kwanza, wanakuja kwenye branch ambazo zipo busy. Watu ni wengi wanaopata huduma.

b) Wanakuangalia unapojaza slip ili kuwapa nafasi wajue kama una hela.

c) Zuia tamaa yako. Usikurupuke na kufurahia umepata dili. Wewe ndiyo dili mwenyewe, wanakutafutia namna wakupige.

d) Usiwape nafasi wakushawishi. Wana ushawishi mkubwa sana. Kuendelea kuwasikiliza, kuna 80% ya wewe kulia. Wapuuzie kabisa.

e) Wana ufahamu juu ya maswala ya kibenki. Kwa hiyo kukudanganya ni rahisi mno.

f) Ukikubali kufuatana nao, kubali kuwa hela yako imeenda. Pole sana.
Tusio na Akaunti 'Benki' Uzi hautuhusu.
 
Back
Top Bottom