We ni tapeli na njia imeanikwa ndio maana umepopomaSasa hela si zangu nikitapeliwa inakuhusu nini?
Mbona kodi zetu zinatumika kuwalipa CCM.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
We ni tapeli na njia imeanikwa ndio maana umepopomaSasa hela si zangu nikitapeliwa inakuhusu nini?
Mbona kodi zetu zinatumika kuwalipa CCM.
Mbona ivyo nawe unacheza hii michezo auSasa hela si zangu nikitapeliwa inakuhusu nini?
Mbona kodi zetu zinatumika kuwalipa CCM.
HSasa hela si zangu nikitapeliwa inakuhusu nini?
Mbona kodi zetu zinatumika kuwalipa CCM.
Tapeli kaumbuliwa dili lake lzm awe na chukiTaperi uyo MO11
Some comments aren't important,, you may decide to skip them! Jokes exist always, but never take things seriously all the timeFunzo nzuri ila matapeli watakuja kuvuruga huu uzi.
Mfano comment no.2
Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
ASANTE KWA TAHADHARIWasalaam Wakuu.
Ijapokuwa uzi kama huu ulishetwa humu juu ya utapeli ndani ya benki, lakini haukuwa umeshiba. Nikaona niwaeleze kwa undani ili tumakinike.
Kuna wale wanaopenda kujua kama nimetapeliwa ama la, ukweli ni kuwa sijatapeliwa. Ila walikuwa wanajaribu kunitapeli.
Leo asubuhi nilienda katika moja ya benki kubwa sana hapa nchini kwa nia ya kufanya miamala miwili mitatu. Sitapenda kutaja jina la benki.
Nilipofika nikaanza kujaza slip zangu. Kuna mtu (akaja pembeni yangu kwa ajili ya kujaza slip. Sikuwa na wasiwasi, nikaendelea kujaza. Nilipomaliza nikaenda kupanga foleni. Naye bila hiyana akaja kunifata kwa nyuma.
Nikakaa kama dakika mbili, akaja mwenzake. Anajidai kumuuliza, kaka ni wapi wanapobadilisha fedha za kigeni? Mimi sijawageukia nikaendelea kusogea.
Yule aliyeulizwa naye akanigusa, "eti kaka, ni wapi wanapobadilisha fedha za Kiarabu? Maana nami ni mgeni hapa". Mimi nikawaonyesha dirisha la Bureau De Change. Wakati nageuka kuwaonyesha, huyu wa kwanza akamchapa swali lingine. Kwani ni fedha zipi za kiarabu?
Jamaa akachomoa kitita kumuonyesha. Na mimi niliona pia. Kwa juu kulikuwa na noti ya dollar 100 (genuine) ya Kimarekani. Akamuuliza ni bei gani, akasema ni Dollar 15,000.
Akamuuliza kwa hiyo nitapewa bei gani kwa fedha za Kitanzania? Jamaa akachukua simu, akaenda kwenye Calculator akaandika 1,500 mara 2300. Akamuambia Utapata kama 34,000,000 TZS.
Nenda kabadili utawekewa kwenye akaunti yako. Akasema sasa sina hata akaunti ya benki. Na nasikia huwa wanauliza kiasi hiki chote nimekipata wapi. Akamuuliza, kwani wewe umekipata wapi? Akasema mishe za madini. Akamuambia hapo pagumu.
Akanigusa tena, akaniambia wewe unamshaurije jamaa? Nikamuambia aende huko ambapo hatoulizwa. Machale yakanicheza.
Jamaa nilipogeuka akamuambia, kwani wewe unatupa Tsh ngapi ili nikakubadilishie. Akasema atatoa million 3. Akamuambia fanya tano. Jamaa akalia akasema labda nne.
Akamuambia, sawa nenda nje nakuja. Huyo jamaa akasepa. Jamaa akaniuliza, twende tukachukue hela tupate cha juu.. Nikamuambia hapana..
Tukaendelea kusogea, nilipokuwa wa pili, jamaa ni watatu. Yeye pia mkononi ana slip yake. Kwamba anahitaji kuhudumiwa. Wakati wa mbele anapewa slip aondoke, akajifanya kupokea simu. Kwa hiyo hii hela nisikuwekee tena? Ahaa, nikuwekee M-Pesa eeh? Poa. Huyo akatokomea. Nikaendelea kuhudumiwa.
Tahadhari za kuchukua:
a) Kwanza, wanakuja kwenye branch ambazo zipo busy. Watu ni wengi wanaopata huduma.
b) Wanakuangalia unapojaza slip ili kuwapa nafasi wajue kama una hela.
c) Zuia tamaa yako. Usikurupuke na kufurahia umepata dili. Wewe ndiyo dili mwenyewe, wanakutafutia namna wakupige.
d) Usiwape nafasi wakushawishi. Wana ushawishi mkubwa sana. Kuendelea kuwasikiliza, kuna 80% ya wewe kulia. Wapuuzie kabisa.
e) Wana ufahamu juu ya maswala ya kibenki. Kwa hiyo kukudanganya ni rahisi mno.
f) Ukikubali kufuatana nao, kubali kuwa hela yako imeenda. Pole sana.