Tahadhari ya utapeli mpya Dar kwa sasa

Benk kuna Utaratibu wa kupitia account zote zilizo Dormant Kwa miezi zaid ya 12 kuna next of Kin wanawasiliana naye kujua taarifa zake ! Nimefanya I know! Tatizo liko Mpesa na Tigo pesa wanakausha na mpunga wako b
Hela zote za kwenye simu au benki huwa zinarudishwa Benki Kuu, hakuna hela ya mtu aliyekufa inaliwa na Kampuni za simu au benki
 
Niliozwa mke kumbe alikuwa mke wa mtu, siku tumelala saa sita usiku eti mjumbe na mume mwenzangu wamekuja kunifumania! Eti akanisamehe ila mke kamchukua, dili la pande mbili, nilikooa eti yule ni yatima hapa si kwao walipanga tu kwa muda.
 
Unatapeliwaje mara nying hvo mkuu...una elimu gani
 
mbona mimi hakunambia hayo
View attachment 2040296
Atakuliza
Ni tapeli na mhuni, na kuna mahali alishafukuzwa kazi...ofisi kubwa tu siwezi kuitaja
 
Pole mzee. Siku zote ukishaona unapewa deal tamu sana kiasi kwamba udenda unaanza kukutoka unatakiwa ushtuke kuwa unapigwa mda si mrefu.

Wazungu wanasema "When the deal is too good, think twice."
Tatizo letu wabongo tunapenda vitu vya dezo. Yaani unataka uuziwe Iphone ya sh. milioni 1 kwa sh. laki 2. Yalishawahi kunikuta haya. Nimekoma.
 
Kuna dereva wa TANROSDS alinunua simu used. Aisee polisi walimla zaidi ya 2 m. Walikua wanajua fika huyu hawezi kukosa 2 m, hata Kama Hana anakopesheka.
Simu ya laki tano unainunua kwa laki unusu, kweli. Hata Kama amekwama vipi mwambie nduguze wakamkwamue.
 
hii ya simu watu wanalizwa sana kwa kweli ni bora serikali ingeliingilia kati swala hili
 
hii ya simu watu wanalizwa sana kwa kweli ni bora serikali ingeliingilia kati swala hili
Halafu hauziwi mtu aliyechoka.
Wana Target mtu mwenye nazo na mwenye heshima zake, mwenye uwoga wa kulala lockup. Maana kituo unachopelekwa Ni kile kilichojaa vibaka wenye vidonda vinavyonuka, lockup iliyotapakaa mikojo chini maana vibaka na mateja wanakojoa popote.
Kuna jamaa walimuingiza Buguruni kwa Hali aliyoikuta mle ndani alitoa rushwa fasta pamoja na kwamba walimbambikia kosa.
 
siku nakuja kudakwa jamaa alikuwa ana daftari zima la kesi za simu means kama atazidaka zote lazma alambe hata ka ist kakupunguzia uchovu
 
Kuna kijana mtaani kwangu,Ni wakala wa m-pesa na kusajili line,

Kamsajilia mtu kwa kitambulisho chake,kaenda kufanya uhalifu,

Hapa ameuza nyumba yake kwa Bei ya kutupa amalize kesi,

Kaiuza juzi tu aisee
 
Jamaa kajiingiza kwenye mercury huko, akikusimulia jinsi atakavyopata 500milioni unajiuliza hivi huyu anadhani pesa inakuja kirahisi hivi? Mwambie sasa unaenda kupigwa uone atavyokudharau..
Atapigwa atachakaa matapeli wana story tamu sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…