City Of Lies
JF-Expert Member
- Sep 8, 2011
- 4,925
- 6,137
Hao watoto walienda kuandikishwa NHC!?Kwan NHC ambae ndo mmiliki anasemaje unaenda kumuhoji mwalimu mkuu wakat mkurugenzi wa NHC yuko si wakahoji na kutafta majibu uko
NHC ni wafanyabiashara na wameona biashara ya shule za kisasa inalipa wameamua kuhamia uko medium school
Kingereza ndio maendeleo. Nchi za Afrika wanazoongea kingereza wanamaendeleo gani ? Huko chuo kikuuu ndio mlivyofundishwab? Andiko gani linasema kingereza ni maendeleo.Mnasikitisha sana ila ni wa kuwahurumia tu.Peleka mtoto hapo Mugabe acha kelele ambazo hazisaidii,Serikali imeamua kubadili shule iwe ya kiingereza huoni ni maendeleo hayo?Kwa maana nyingine mdogo wake na huyo utampeleka hapo asome kwa kiingreza.
Mshana hujaona msg hapo juu eti kingereza ni maendeleo. Kuna wanatamani hata mtaani kiswahili kipigwe marufuku.Tulipofika shuleni leo, tumeambiwa kuwa shule inavunjwa na badala yake itabadilishwa kuwa English Medium.😂
Kuna siku tutauzwa kama tulivyo
Hapo usikute kuna mwekezaji anataka kujenga godown la ghorofa 10 kwa ajili ya kituo cha kimataifa cha biashara Ubungo.Wiki iliyopita, watoto waliporudi nyumbani walileta taarifa ya kushtua kuwa Shule ya Msingi Ubungo National Housing (NHC) inauzwa, na wazazi tunahitajika kufika shuleni leo Jumanne kwa ajili ya kikao kilichopangwa. Hali hii ilisababisha taharuki miongoni mwa wazazi. Tulipofika shuleni leo, tumeambiwa kuwa shule inavunjwa na badala yake itabadilishwa kuwa English Medium.
Hata hivyo, tulipokea taarifa hii bila barua rasmi kutoka shuleni, tena watoto ndio waliotufahamisha kuhusu mabadiliko haya. Tumefika shuleni hapa, lakini tumeambiwa Mkuu wa Shule anaumwa na hayupo, Mkuu Msaidizi anasema yupo kwenye kazi maalum, na hata Afisa Elimu na Mratibu hawapo. Hatujui hatma ya watoto wetu.
Baada ya kufika hapa leo, tumeelezwa kuchagua shule nyingine kwa ajili ya kuwatoa watoto wetu, lakini hakuna maelezo ya kutosha kuhusu kwanini shule ya Serikali inavunjwa au kwanini taarifa hii inatolewa kwa dharura. Wengine wanalazimishwa kusaini makubaliano ya kuhamisha watoto bila kujua vema maelezo ya mabadiliko haya ya ghafla.
Hii ni hali ya kusikitisha kwa wazazi na inahitaji uwazi zaidi kutoka kwa viongozi wa elimu na serikali kuhusu mustakabali wa watoto wetu kwani hivi sasa unawahamishaje watoto mwishoni mwa mwaka?
Hahahaha.Kingereza ndio maendeleo. Nchi za Afrika wanazoongea kingereza wanamaendeleo gani ? Huko chuo kikuuu ndio mlivyofundishwab? Andiko gani linasema kingereza ni maendeleo.Mnasikitisha sana ila ni wa kuwahurumia tu.
Watu wangwpi TZ wanaojua hicho kingereza wanakiongea ? Zaidi ya mashuleni hicho kingereza kinaongewa wapi ? Hio ni lugha ya makaratasi haina maendeleo yoyote. Badala ya kukuza lugha yako andelea kukuza lugha za wazungu.
Halafu kingereza mnachoongea wala wazungu hawakielewi ni bora mngekiacha tu
Unasema nini mkuu mie nilikuwa nakuea mc na mkslimani wa wazungu wa misaada. Aisee kingereza chetu wazungu wanaitikia mara tatu tatu hawakuelewi ila wabongo wanajifanya eti wanajua.Hahahaha.
Ukitaka kujua kama kiingereza tunachofundishwa sisi wabongo tunaingizwa chaka siku mtafute Mzungu halafu ibuka naye shuleni uone walimu wa kiingereza watakavyojikanyaga.
Kumbe kubadili shule na kuwa ya Kiingereza ni maendeleo???Peleka mtoto hapo Mugabe acha kelele ambazo hazisaidii,Serikali imeamua kubadili shule iwe ya kiingereza huoni ni maendeleo hayo?Kwa maana nyingine mdogo wake na huyo utampeleka hapo asome kwa kiingreza.
Labda ametoka usingizini akasoma bila kutafakari aka comment pyuuuMabadiliko huwa yanafanyika kienyeji hivyo?
Hahaha!!! China International Complex MallNdo tumefikia huku sasa kama nchi hii hali sio nzuri tunapoelekea kubaya
Hadi shure ya uma
Inamaana hapo kuna kibopa analitaka hilo eneo dah
Tuliwaambia mwamba ambae ni jiwe mtamkumbuka kwa mazuri mnabaki kujamber jamber tuNdo tumefikia huku sasa kama nchi hii hali sio nzuri tunapoelekea kubaya
Hadi shure ya uma
Inamaana hapo kuna kibopa analitaka hilo eneo dah