TAHURI: Tumuunge mkono Rais Magufuli katika vita dhidi ya Corona

TAHURI: Tumuunge mkono Rais Magufuli katika vita dhidi ya Corona

Eti wangeleta TIBA badala ya chanjo msipende kudiscus mambo ya kitaalam ki siasa zaidi VIRUS vinakufa kwa dawa gani.?
Vinakufa kwa dawa ya minyooo 😎😎😎
 
Maisha ya mwanadamu ni muhimu kuliko kitu chochote duniani ikiwemo uchumi na hizo trillioni ulizotaja.
Huwezi kuacha kukopa hela kumtibia mwanao, mkeo babako au mamako ukitamani wafe ili usidaiwe 🙄 🙄 🙄 🙄
 
Weka mambo sawa.Sio kumkomoa mtu.Watu wapo na wanaona,wanasikia nk. Siku zote nyumba ya jirani ikiungua moto,wewe unakuwa karibu na maji ili kukabiliana na moto.Ndiyo maana Watu wengi wanahitaji chanjo kwa ajili ya kujikinga.🔇
Ukiangalia mazungumzo ya watu humu kuhusu hizo chanjo asilimia kubwa wanamjadili Magufuli na kauli zake kuhusiana na hili suala la chanjo,yani kwamba hakuna chengine cha kujadili zaidi ya kumzungumzia Magufuli katika hili.

Ndio maana wengine wanakuwa hawaelewa kuwa hizo chanjo zikija ni lazima kila mtu kuchanjwa ama vp? Kuna watu huko huko Marekani ambako wanakufa sana tu na corona ila wapo ambao bado hawachanjwa hadi sasa wanasikiliza kwanza ila huku inaonekana watu hawana la kujiuliza katika hizo chanjo wanaona Magufuli ndio anataka kuzingua.
 
0079FD31-35BC-4AAF-A8CE-11990EAEC676.jpeg

Hivi kipimo kipya cha covid kinachukuliwa hivi???bora nifwe
 
Hii inaitwa 'rationalisation'. Labda kama TAHURI wangekuja na utafiti kuonyesha kuwa wamegundua dawa ambayo ni mbadala wa hiyo chanjo au bado wanaendelea nao. Lakini 'maneno matupu hayavunji mfupa'.
 
Eti wangeleta TIBA badala ya chanjo msipende kudiscus mambo ya kitaalam ki siasa zaidi VIRUS vinakufa kwa dawa gani.?
Kama wamewaza kuleta kinga wameshindwa kuleta tiba?

Mkuu, wewe ndio unaleta siasa sio huyo jamaa.
 
itazigharimu kiasi cha Dola za Marekani kati ya 7-11 kwa chanjo moja".
kwa Tanzania pekee kama Rais Magufuli ataruhusu chanjo itatugharimu Tsh104Trilioni kwa idadi ya watu wetu nchi nzima
tuseme watanzania tupo million 70. Chanjo moja iwe usd 11.
so total cost itakua 70,000,000 x 11 =770,000,000usd ambayo ni sawa na tshs 1,925,000,000,000 (trillion 1.925 kwa rate ya 2500)
sasa hiyo 104 trillion ni pamoja na derivery au? saa zingine uongo aufai.
 
Maisha ya mwanadamu ni muhimu kuliko kitu chochote duniani ikiwemo uchumi na hizo trillioni ulizotaja.
Huwezi kuacha kukopa hela kumtibia mwanao, mkeo babako au mamako ukitamani wafe ili usidaiwe 🙄 🙄 🙄 🙄
Wangapi unao wajua waliokufa kwa Corona?

Fikiri nje box mkuu.
 
Bollen ngeti ni mpumbavu fulani anayenunulika kwa pipi ya kisiasa kupingana na sayansi. Wanasayansi mko wapi kujibu na kumsaidia kiongozi anayeongoza kwa aibu tanzania?
 
"kama nia njema kwa nini wazungu wamekimbilia kutafuta chanjo badala ya tiba kamili?
Erythrocyte unaona takataka hili, eti dawa kamili! Virus huwa hawana dawa , virus are hard to treat because of the rate of mutations...... Hata hizi chanjo wanasema kama kuna mutation kubwa it can render them useless! You can slow their infection by vaccines...
 
Taasisi ya Haki za Binadamu, Tanzania Human Rights-Foundation (TAHURI) imetoa tamko la kuwataka Watanzania kuungana pamoja katika vita dhidi ya Shirika la Afya Duniani, WHO na Rais Magufuli huku likiwataka wananchi kumuunga mkono Rais wao.

Akiongea na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa taasisi hiyo Bollen Ngetti amesema;

"Tunaweza kutofautiana katika mambo mengi ya kiitikadi, kimtazamo na maono lakini katika mambo ya msingi kwa nchi kama hili la chanjo ni sharti tuungane kuwa kitu kimoja".

Aidha, Ngetti ambaye ni mwandishi wa habari nchini amesema Watanzania wasikimbilie tu athari za kiafya kwa chanjo hiyo na badala yake waangalie athari za kiuchumi.

"Tutambue kuwa dunia iko katika vitu kubwa ya kiuchumi. Kama Tahuri hatutajikita sana katika athari za kiafya za chanjo hiyo lakini tufikirie ni fedha kiasi gani chanjo hiyo itaswaga?"

"Ikumbukwe kwamba, kwa mujibu wa WHO ili nchi za ki-Afrika kupata chanjo kutoka makampuni yaliyojiorodhesha kwenye mkataba wa COVAX ambayo ni BioNTech na Moderna itazigharimu kiasi cha Dola za Marekani kati ya 7-11 kwa chanjo moja".

Ngetti ameendelea kusema, "kwa Tanzania pekee kama Rais Magufuli ataruhusu chanjo itatugharimu Tsh104Trilioni kwa idadi ya watu wetu nchi nzima. Hii ni fedha nyingi sana kwa nchi changa kama sisi".

Ngetti amefafanua kuwa fedha hizo zitatakiwa kukopwa kutoka Benki ya Dunia kwa udhamini wa ADB na itachukua miaka zaidi ya kumi kuzirejesha kwa riba ya asilimia 7.2.

Aidha, Ngetti amehoji, "kama nia njema kwa nini wazungu wamekimbilia kutafuta chanjo badala ya tiba kamili? Walijua kwa tiba utahitaji dozi chache sawa na idadi ya walioambukizwa ambao kwa sasa ni milioni 100 lakini kinga utacheza namba ya watu duniani".

"Jambo la pekee kama Taifa tunalotakiwa kufanya ni kufuata masharti ya kujikinga huku tulifanya kazi kwa bidii, huu ni upepo unaovuma na kupita, tusiondoshwe kwenye reli".

Ngetti amemaliza kwa kusema, "Magufuli si kichaa, wala hana historia ya ukichaa, anatutakia mema tusimvunje moyo. Lakini pia wataalamu wetu nao wakeshe maabara kukuna vichwa aidha kuchunguza chanjo hizo au kugundua za kwetu kama Waganda wanavyofanya"

My Take: Kwa vita hii tutashuhudia na kusikia mengi. Vita hii ya Magu na wanasayansi itaibua makubwa. Subiri tuone!
Huyo Ngetti naye ni mpuuzi au mjinga. Ni chanjo ipi ambayo Tanzania iliwahi kununua.

Chini ya mikataba ya kimataifa, nchi maskini kama Tanzania hupewa chanjo bure. Unachotakiwa ni kushirikiana na jamii ya kimataifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom